Absalom Kibanda, usitumie kutekwa, kuteswa kwa mavuno toka kwa wanasiasa

Absalom Kibanda, usitumie kutekwa, kuteswa kwa mavuno toka kwa wanasiasa

Manu.

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2014
Posts
689
Reaction score
180
Wanajamvi, Salaam.

Leo nakuja kwenu jamvini baada ya kukerwa na tabia ya Mwenyekekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania Absalom Kibanda kutumia kuteswa na kutekwa kwake kama biashara. Amekuwa anaongea kwa ndimi mbili.

Mara ya kwanza alizungumzia kutekwa kwake kwa namna ambayo ingefanya jamii itafsiri kana kwamba Mwajiri wake wa zamani Gazeti la Tz Daima kupitia wamiliki wake ndio walihusika.

Alipohamia New Habari Cooperation akaishambulia Chadema mpaka tukaaminishwa kuwa huenda Chadema walihusika. Aliwahi kumtaja moja kwa moja Bw. Ludovick Joseph kama mmoja waliomteka.

Huyu Ludovick alikuwa kada wa Chadema katika kesi kigaidi ilipikwa pamoja na mwandishi uchwara Denis Msacky ambayo ilimlenga mkurugenzi wa Ulinzi na usalama wa Chadema Wilfred Lwakatare, ambayo inasemekana Zitto Kabwe pamaoja na Chama cha Mapinduzi wakiwa wabia muhimu.

Kwa sasa vita ya urais ndani ya CCM imepamba moto. Kibanda ni mhariri mkuu wa gazeti la Mtanzania. Hili gazeti lina kazi maalum ya kumpamba Eddo na kuchafua wenzake.

Juzi Kibanda ameibuka na tuhuma mpya kabisaa, Anamtuhumu mgombea urais mmoja kama mhusika wa tukio la kutekwa na kuteswa kwake. Huyu mgombea urais anatokea mikoa ya kusini, mwandani wa familia ya mkuu wa kaya. Chaguo la mama wa taifa.

Kwa kuwa huyu ndiye mpinzani mkuu wa Eddo, ni dhahiri kuwa Kibanda kwa maagizo ya waajiri na pia kwa utashi wake binafsi, amekubali kutumia kutekwa na kuteswa kwake kama Chanzo kipya cha mavuno.

Yupi mtekaji na mtesaji halisi wa Kibanda, ikiwa na yeye mwathirika amekubali kuuza utu wake kama bidhaa?
 
Kibanda nimemfuatilia kwa muda wa miezi miwili tu amenishangaza sana ,the guy is so damn opportunistic,coward na hana misimamo nahisi hata wale waliomtesa walikua sahihi inawezekana alikula hela yao akawazingua !!yaani hata Leo hii akipewa hela anaweza kukurupuka tu na kusema Slaa au Mbowe ndo walinitesa !!
 
Kibanda nahisi alijiteka ili apige fedha time hizi maridhawa kwake
 
Yawezekana hamjui hata mhusika so anarukaruka tu.

Ukiwafuatilia waandishi wengi wana njaa ya kutisha hivyo wanaendaenda tu kama kuku aliyekatwa kichwa.

Ukitaka kuamini mtafute kesho na dau la maana halafu umwambie amtaje unayemtaka wewe then sikilizia kama atashindwa.

Waandishi wanaotandikwa bongo ni wale viherehere wanaoongozwa na remote za wanasiasa.
 
Waandish wetu sometime hawajitambui! Siri ya kutekwa na kuteswa anaijua mwenyewe labda na kv!
 
Ona na wewe umeleta propoganda zako ili ujaze saver.

Duh!! ndugu umeuvua ubongo wako na sasa umeuacha uchi, kiuhalisia mleta mada ametoa taarifa sahihi kutokana na uchunguzi wake juu ya nini huyu Kibanda huwa anatamka sasa wewe kwa mahaba uliyonayo kwa Lowasa unavamiana kujibu pasipo kuchanganua nini habari inamaanisha.
 
Yawezekana hamjui hata mhusika so anarukaruka tu.

Ukiwafuatilia waandishi wengi wana njaa ya kutisha hivyo wanaendaenda tu kama kuku aliyekatwa kichwa.

Ukitaka kuamini mtafute kesho na dau la maana halafu umwambie amtaje unayemtaka wewe then sikilizia kama atashindwa.

Waandishi wanaotandikwa bongo ni wale viherehere wanaoongozwa na remote za wanasiasa.

Mkuu, napata picha.
 
Mkuu hata mimi nilibaki namshangaa kibanda,kusema ukweli nilikuwa namheshimu sana kibanda ila kutumika kiasi kile kimemshushia credibility sana.
 
Kuna uwezekano Mkubwa kuwa Mwenyekiti mmoja wa CHAMA kinachojinadi kuwa ni cha kidemokrasia chenye makao yake huko Uchagani ndio muhusika wa kutekwa kwa KIBANDA.
 
Mbona alishamtajaga siku nyingi aliyemteka na kumtesa kuwa ni muajiri wake wa awali yaani wamiliki wa gazeti la Tanzania daima. tafuta kuna thread humu ikiwa pamoja na video inajieleza kila kitu.
 
Jamani wakati wa uchguzi huu wahariri wanasaka mahera kuna mwenzako mmoja wa gazeti tofauti na lake karamba milioni 90 si unajua cha mgema huliwa na mlevi!
 
Kibanda yeye anakwenda kwa wakati kwa kuangalia wapi atapata mteremko kama ngarawa
 
Kuna uwezekano Mkubwa kuwa Mwenyekiti mmoja wa CHAMA kinachojinadi kuwa ni cha kidemokrasia chenye makao yake huko Uchagani ndio muhusika wa kutekwa kwa KIBANDA.

Wewe ulishadharaulika kipindi kirefu sana hapa jukwaani,huna jipya
 
Jamani wakati wa uchguzi huu wahariri wanasaka mahera kuna mwenzako mmoja wa gazeti tofauti na lake karamba milioni 90 si unajua cha mgema huliwa na mlevi!

Waandishi kanjanja wanaishi kwa kutegemea matukio
 
Back
Top Bottom