Academic weapon, weapon of propaganda, ugonjwa wa uongo ambao wazungu wameuleta Tanzania

Academic weapon, weapon of propaganda, ugonjwa wa uongo ambao wazungu wameuleta Tanzania

Leslie Mbena

JF-Expert Member
Joined
Nov 24, 2019
Posts
207
Reaction score
677
Leo 17:55hrs 06/09/2020

Wazungu walituletea Nuclear weapon ikaua wajapan kule Hiroshima na Nagasaki, Majiji Makubwa mfano wa Tokyo, Majiji ya Hiroshima na Nagasaki yaliteketea ndani ya dakika, dunia ikapoteza mainjia wa daraja la juu, wasomi wa daraja la sita, Maguru wa elimu, Academician wenye academic theory, academic knowledge, academic experience, academic exposure,

Wataalam wenye kuandika journals na makala ambazo Unaweza kunukuu kupata ctitic, Academic Terrorist ambao wako tayari kwa mjadala wowote mahali popote na mtu yeyote, watu ambao waliweza kufanya ugunduzi na kuibadili dunia katika Sayansi, kizazi cha watu awa waerevu kabisa duniani kilimalizwa na bomu la Nyuklia, ilikuwa huzuni kwa dunia kupoteza Maguru wa kiuchumi, kisayansi, kisheria na kiuongozi,

Leo wazungu wametuletea biological weapon ya kirusi cha corona, Watanzania tumeishinda hii vita ya corona lakini tumeletewa vita nyingine inaitwa Ugonjwa wa Uongo "Academic weapon" nayo iko hivi mzungu anachukua jambo la Tanzania anampa Mwanasheria Tundu Lissu aje kulizungumza, Tundu Lissu ni Celebrated Lawyer hapa Tanzania atalichukua jambo hilo na kulileta Tanzania, atampa Zitto Kabwe ambaye ni Mchumi, atatuficha kiuchumi atalizungumza kiuhasibu mbele ya Watanzania, Hii ndio inaitwa Academic Weapon, Ugonjwa wa Uongo.

- Tundu Lissu, Zitto Kabwe, Bernard Membe wanasema Ununuzi wa Ndege hauna faida! (kiuhasibu)

Watasema ununuzi wa ndege kubwa kumi, Boeing, Airbus na Bomberdier unamsaidiaje Mwananchi kule kijijini, kiuhasibu (Accounting) kweli Mwanakijiji hapandi ndege ila kiuchumi(Economically) Mwanakijiji anapanda ndege kila siku kwa maana Juice yake ya Maembe itauzwa kwenye ndege, juice yake ya machenza na machungwa itauzwa kwenye ndege, korosho yake ya Mtwara, Lindi na Kibaha itauzwa kwenye ndege, itamrudishia faida baada ya kuiuza,

Kusema Air Tanzania inaleta hasara kwa ununuzi wa ndege kama asemavyo Zitto Kabwe, Tundu Lissu, Freeman Mbowe na Benard Membe ni uongo mkubwa, ukisema Air Tanzania inaleta hasara hii unazungumza kiuhasibu (Accounting) ambapo utachukua Purchasing price utatoa Expenses mfano Bilioni 1 utatoa Milioni 800 ukipata Milioni 200 watasema ni hasara lakini kiuchumi (Economically) Air Tanzania inaleta faida kubwa kwa Tanzania, Watalii wanaletwa na ndege zetu za Air Tanzania, tumeona Tanapa wametoa gawio la bilioni 650 kwa Serikali na hizi hela zimetokana na Watalii wanaoletwa na ndege zetu,

Ndugu zangu wa Matombo, Morogoro wanapanda ndege kila siku kwa huduma za Kijamii wanazopata toka Serikalini, dawa inayopatikana kwenye hospitali imetokana na Watalii wanaoletwa na ndege zetu kulipia kodi ya shilingi bilioni 10 Serikalini kila Mwaka, Ndugu zetu wa Tawa, Kiloka na Mkuyuni Mkoani Morogoro watapata dawa, watapata huduma za Kijamii kwa kodi inayoletwa na Watalii, lakini hili ni la kiuchumi, badala ya kulieleza kiuchumi Zitto Kabwe ataelezea kiuhasibu kuwa ununuzi wa ndege hauna faida,

-Mishahara kutopanda kwa Watumishi wa Umma.

Imekuwa desturi Watumishi wa Umma kupandishiwa mishahara kila Mwaka huku bidhaa nazo zikipanda bei,ni sawa na kutwanga Maji kwenye kinu,Katika awamu hii ya tano,tukizungumzia kiuchumi,mishahara imepanda kwa kila Mwananchi wa Tanzania,mfano Katika Elimu bure kama ulikuwa unalipa shilingi 15,000 sasa hivi haulipi ada yoyote,Shule ya Msingi bure,Shule ya Sekondari bure,je Mishahara haijapanda kwa kila Mwananchi!? Na kwako wewe Mfanyakazi,pay as you earn yako Rais John Magufuli kaipunguza toka 13% hadi 9% Je mshahara bado haujapanda kwako!?

-Ujenzi wa Reli ya Umeme(SGR).

Tundu Lissu,Zitto Kabwe,Benard Membe watazunguka kusema ya kwamba Ujenzi wa Reli ya Umeme hauna faida kwa Watanzania,lakini watazungumzia jambo hilo kiuhasibu na kuficha kulizungumzia jambo hilo kiuchumi,Sasa kiuchumi Ujenzi wa reli ya Umeme ina faida kwa kila Mwananchi,ukisema reli ya SGR haina faida unazungumza kiuhasibu(Accounting) lakini kiuchumi(Economically) Ujenzi wa reli una faida,kiuchumi maana hata kabla ya kuanza kutumika usafiri wa treni ya Umeme,

Katika kipindi hiki cha Ujenzi wa reli hiyo tayari gharama za Ujenzi itakuwa imejilipa kupitia makusanyo ya kodi mbalimbali,ndugu zangu wa Ngererenge mtaniunga mkono,kwa siku Mfanyakazi analipwa shilingi elfu kumi,saa saba mchana anakwenda kula kwa Mama ntilie,Mama ntilie mchele kanunua dukani,Mwenye duka anaendelea na biashara kwa sababu ya Mama ntilie atalipa kodi kwenye kununua mchele na atalipa Mwenye fremu anapouzia na atanunya luku pia,Je Ujenzi wa reli ya Umeme hauna faida bado!?

-Tundu Lissu anasema atapunguza corporate tax toka 30% hadi 10%

Tundu Lissu is a celebrated lawyer but to me he is an academic toddler who is practising political masterbation,hivi leo tunakusanya Mara kodi mara mbili ya Awamu ya nne na bado haitoshi yeye anataka aje aondoe Kodi,sasa atakuja kufidia wapi au ataleta trillion 11 zake alizopewa na Wazungu uko Ubelgiji,na akizileta atawalipa nini hao wazungu!?

Tundu Lissu bado anawadanganya Watanzania kuwa atapunguza makato ya mkopo wa Wanafunzi wa Chuo, loan recovery kutoka 13% hadi 3% hivi anania gani na kizazi kijacho!? Je anataka kizazi hicho kikose mkopo kwa sababu waliochukua Mwaka 2000 hadi Mwaka 2020 hawajalipa hata nusu ya mkopo!

-Tundu Lissu anasema atafutilia mbali vitambulisho vya Wamachinga.

Vitambulisho vya Wamachinga kwa shilingi 20,000 na kuuza popote nchini Tanzania bila kusumbuliwa,leo nkiwa pale Millennium towers, Kijitonyama naona vijana wauza matunda kwenye matenga wapo na baiskeli zao, nasubiri kuingia ndani ndio nikasikiliza story mbili tatu. Mmoja anasema, "Kukaa sehemu kama hii ilikuwa ndoto, leo nauza machungwa yangu hapa hakuna hata polisi wa kunichukulia vitu vyangu, zamani ilikuwa karandinga linapita na kusomba kila kitu, mtaji wote wanauchukua"

Zitto Kabwe,Tundu Lissu,Benard Membe hawakubaliani na kufanya biashara popote, yaani kwao inaweza kuwa kero kubwa sana lakini kwa Rais John Pombe Magufuli na tabaka la chini ni bonge moja la mtaji na faida kwa kila Mwananchi,John Pombe Magufuli has five years more,thus Wamachinga also have five years more,Ambavyo Rais John Magufuli anayo Miaka mitano mingine vivyo hivyo Wamachinga wanayo Miaka mingine mitano ya kufanikiwa kibiashara,kiuchumi kitambulisho cha 20,000 ukigawanya kwa siku 365 unapata senti 54,kwa hiyo Machinga analipa senti 54 kila siku ambayo ni sawa anauza bure bila kukatwa kodi,lakini kwa Serikali ikiwa na Machinga 1,000,000 ukizidisha 54 unapata Milioni 54 kila siku,Hii ni win win situation,Machinga anapata unafuu na Serikali inapata faida,

lakini Tundu Lissu Mwanasheria ataongea kiuhasibu kuwa atafuta vitambulisho hivyo Wakati kiuchumi senti 54 wanayolipa Wamachinga kila siku ni shilingi mili 54 kwa siku kama kutakuwa na Wamachinga Milioni 1,Sasa unajiuliza mtu anayetaka kupunguza kodi corporate tax toka 30% hadi 10% na kupunguza malipo ya mkopo wa Chuo toka 13% hadi 3% hiyo hela ya kufidia ataitoa wapi kama atapunguza kodi toka 30% hadi 10%!?

Tundu Lissu akiongea kisheria anasema Ujenzi wa Bwawa la Umeme la Julius Nyerere katika mto Rufiji hauna faida eti yapo Mabwawa ya Umeme ya Hale,Nyumba ya mungu na Mtera,lakini kiuchumi Bwawa la Umeme la megawatt 2115 analojenga Rais John Magufuli lina faida kubwa ambayo itakuja moja kwa moja kwa tabaka la chini,Bwawa la Umeme analojenga Rais John Magufuli likiisha litashusha bei ya Umeme,

Kama unatumia luku ya 30,000 kwa mwezi sasa utatumia luku ya shilingi 15,000 tu,hii ni faida kwa kila Mwananchi,na pia faida kwa Serikali kuondokana na kukipa mabilioni ya pesa kila mwezi kwa Umeme wa kukodi ambao umetuletea kashfa nyingi za Ufisadi kama Richmond na Escrow ambazo zilisababisha nchi ikaingia kwenye Umeme wa mgao na Taifa kuingia gizani,Je bei ya Umeme ikishuka bado Bwawa la Umeme analojenga Rais John Pombe Magufuli halitakuwa na maana!?

Nimalizie kwa kusema hapo zamani tulikuwa na critical thinking kwa sababu darasani tulikuwa tunaulizwa why Vasci da Gama came to Africa? na sio when Vasci da Gama came to Africa? Kwa kuulizwa why tulitumia critical thinking kudiscuss hata maswali manne tulitumia masaa mawili kuyajibu,lakini siku hizi wanafunzi badala ya kuulizwa why wanaulizwa when?

Katika kujibu swali tunatumia approach nne za kitaaluma ambazo ni legal theory, Management theory,Accounting theory na Economic theory,na Guru wa kitaaluma au mbobezi yeyote kitaaluma lazima awe na academic theory,academic knowledge, academic experience,academic exposure ambayo itamfanya aweze kuandika journal na watu wananukuu kwa ajili ya kupata elimu,ukiwa na hivi vyote basi utakuwa umefikia kiwango cha elimu ya sita baada ya Phd na uprofesa basi utakuwa ni Academis Terrorist ambaye tayari kwa mjadala wowote,mahali popote na Wakati wowote,

Nimalizie kwa kusema John Pombe Magufuli ni Guru la kitaaluma licha ya Uguru katika taaluma ya Sayansi,bado anaiendesha nchi kana Guru la kiuchumi kwa kurejea nadharia nilizozieleza hapo juu,watu wanaompinga kama Zitto Kabwe,Tundu Lissu na Benard Membe wao wanaficha kumpinga kiuchumi wanakwenda kumpinga kiuhasibu kitu ambacho hakina hoja sana,

Mfano,Rais John Pombe Magufuli aliwapiga wazungu wa Acacia kwa namba,aliwaambia walipe kodi billion of dollars,Tundu Lissu akaja kumpinga Rais John Pombe Magufuli kisheria akasema hajafuata Sheria,Zitto Kabwe akaja kumpinga Rais John Pombe Magufuli kiuhasibu akasema hajafuata taratibu za kiuhasibu,

Benard Membe akaja kumpinga Rais John Pombe Magufuli kimanagement akasema hajafuata ethics za Management lakini Rais John Pombe Magufuli alikuwa sahihi kiuchumi,na kwa hili alilishinda baada ya kuwashinda Acacia kiutendaji,Kisheria,kiuhasibu na kiuchumi,kwa hili Rais John Pombe Magufuli anastahili Tuzo ya kuwa Guru wa kiuchumi na tuzo ya Academic Terrorist.

Nikiishia hapa,Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854

-Bachelor of Business Administration in International Business.
-Master's in Leadership and Management.

-Research; Assessing Effects of Micro-Financing on Poverty Reduction.
 
Kama wajumbe tu wasio na elimu walikupiga spana na ulikuwa hujawaeleza huu ushudu ulioandika hapa, hebu rudi kawaeleze haya uliyoandika halafu uje utupe mrejesho.
 
Leo 17:55hrs 06/09/2020

Wazungu walituletea Nuclear weapon ikaua wajapan kule Hiroshima na Nagasaki,Majiji Makubwa mfano wa Tokyo,Majiji ya Hiroshima na Nagasaki yaliteketea ndani ya dakika,dunia ikapoteza mainjia wa daraja la juu,wasomi wa daraja la sita,Maguru wa elimu,Academician wenye academic theory,academic knowledge,academic experience,academic exposure...
Wewe ni mwana ccm mwezangu ila huna akili na umesoma vyuo vya kata sijui Mzumbe sijui St Augustine nina uhakika ulifeli form six ndio ukaenda vyuo hivyo vya kata

Kama sio hilo wewe ni kapuku na maskini wa kutupwa na hoe hae wazazi wako hawakuwa na uwezo kukupeleka shule vyuo vya nje

Leo mnaitwa mataga hapa JF,
Mlijaribu kugombea ubunge wakawapiga chini kwa uwezo wenu mdogo wa kufikiri

Ccm kama chama chetu ni taasisi imara,wewe na wapumbavu wenzako mnafikiria mkisifia mtapata bahati ya kuingia ccm

Kumbuka huyo pole pole na Bashiru ni bahati tu kuingia ccm kutokana na utawala wa Magufuli

Ccm ina wenyewe

Angalia Mama Maria Nyerere jana alisimamia msimamo kuwa yeye amelazimishwa kuongeza watu waonekane wengi

Mtu kama Silinde Magufuli akitoka ndio mwisho wake ccm

Wewe kumbaru na zero brain unaweka namba ya simu kusubiri huruma ya chama

Wewe si mwana ccm ni tumbo njaa

Mawazo ya kufikiri ccm ni kusifia ni miaka hii mitano

Ccm haipo hivyo,ccm kushinda ni mikakati na ukaribu na wajumbe

Nguvu ya lowasaa au membe haikuwa vita bali mikakati imara

Wewe ni ngumbaru,Hufai kuwa ccm
 
Leo 17:55hrs 06/09/2020

Wazungu walituletea Nuclear weapon ikaua wajapan kule Hiroshima na Nagasaki, Majiji Makubwa mfano wa Tokyo, Majiji ya Hiroshima na Nagasaki yaliteketea ndani ya dakika, dunia ikapoteza mainjia wa daraja la juu, wasomi wa daraja la sita, Maguru wa elimu, Academician wenye academic theory, academic knowledge, academic experience, academic exposure...

Matendo yenu ya kuwaumiza watz kwa miaka 5 huku mkiushughulikia upinzani kumbe jibu mmelipata. Hao wazungu ndo wamekuambieni .uuweni sekta binafsi,kazeni vyuma,bambikieni watu kesi,zulumuni wakulima wa korosho,mle rambirambi za watu,msiwape watumishi haki zao,mmue diplomasia,muue Jumuiya ya afrika mashariki,mmue demokrasia.

Kuhusu corona Kati ya waafrika na wazungu Nani wamekufa zaidi.Hizi siasa zenu ilitakiwa miaka ya 1930 enzi za ujima. Mmevuna mlichopanda wananchi awali ndege ndege hazigusi masikini ndo kundi kubwa.

Kumsingia mzungu juu ya matatizo yako ni utopolo kwinyo hao wazungu hawapo Asia,hawapo uarabuni?
 
Watz wenye kumudu kupanda ndege hata milioni moja awafiki, wengi choka mbaya hata chai tu wengi walishasahau kunywa
 
Hiyo masters yako haikusaidii hata hiyo degree wanasomaga wale waliopata vi DD
Ana masters bado ana mawazo ya ujima Kama boss wake awajui chochote kuhusu modern world sisi si kisiwa tuwe na maendeleo kwa kujitenga
 
Hiyo masters yako haikusaidii hata hiyo degree wanasomaga wale waliopata vi DD
Na Research Title akachagua ambayo hata mwanafunzi wa darasa la sita anaweza kuvijibu kwenye Elimu ya kujitegemea.
 
Leo 17:55hrs 06/09/2020

Wazungu walituletea Nuclear weapon ikaua wajapan kule Hiroshima na Nagasaki, Majiji Makubwa mfano wa Tokyo, Majiji ya Hiroshima na Nagasaki yaliteketea ndani ya dakika, dunia ikapoteza mainjia wa daraja la juu, wasomi wa daraja la sita, Maguru wa elimu, Academician wenye academic theory, academic knowledge, academic experience, academic exposure...
Hii imeandikwa na mtu wa masters from UD?
Ati Tokyo ilipigwa nuclear? Hiroshima na Nagasaki zilipigwa atomic.

Ati corona ni propoganga ya wazungu?

Mungu tuepishe!
 
Asante sana studio kwa kukusaidia tu..Nyanoko.

#MaendeleoHayanaChama.
 
Leo 17:55hrs 06/09/2020

Wazungu walituletea Nuclear weapon ikaua wajapan kule Hiroshima na Nagasaki, Majiji Makubwa mfano wa Tokyo, Majiji ya Hiroshima na Nagasaki yaliteketea ndani ya dakika, dunia ikapoteza mainjia wa daraja la juu, wasomi wa daraja la sita, Maguru wa elimu, Academician wenye academic theory, academic knowledge, academic experience, academic exposure...
Wadai hizo 400 trillions ndio utawajua mabeberu ni watu au wanyama..mbona mmesanda
 
Brother me sina msimamo kisiasa au si mshabiki kabisa.

But

Njaa ikimuuma mtoto anachokihitaji ni chakula na si kuona umejenga,unamagari,unamabiashara etc. Mtoto hawapendi usitekeleze majukumu yako mfano mambo ya msosi.

Ni wakati sasa watoto wanahitaji chakula.
 
Nilivyomaliza kusoma halafu ukaandika kiwango chako cha elimu umefanya nione hizo digrii ulizoorodhesha kuwa umesomea hazijakubadilisha kifikra. Kweli kabisa kwa elimu hiyo ndo matokeo unayoweza kuyaona.

Hivi kuongezewa mshahara maana yake ni kupunguza PAYE ambayo umeitaja kwa asilimia zake. Hivi hizo asilimia ni flat kwa madaraja yote au kima cha chini? Kuzuia mfumuko wa bei ndo kuongeza mshahara? Na masters yako kabis hukusoma tofauti ya kipato na neno mshahara?


Unataka kutua,inisha kuwa umesoma hadi masters hujui mshahara unapokuwa unaongezeka unamnufaishaje muhusika pindi akianza kulipwa pensheni yake hili nalo hulijui kabisa na una masters ktk leadership and management kesho unakuwa CEO ndo utawaminisha walio chini yako?


Pili umesoma international relation sijui nini kweli wazungu ndo wameleta korona?


Tatu bei ya umeme ilishuka lini? Kutoka sh ngapi kwa unit hadi kifikia sh ngapi?


Japo haijaruhusiwa kuhoji,unajua ni wafanyabiashara wangapi wenye mitaji mikubwa wanawatumia wamachinga kuweka bidhaa barabarani ili kukwepa kodi? Nina uchungu na hiki ila basi tu.


Ningeendelea kukusaidia utambue elimu yako haijakusaidia ila niishie tu kwa kukuelezea Tatizo lililopo hapa nchini sio kodi kama unavyoitaja ila mfumo wa ulipaji kodi na aina za kodi.


Hata hivo kwa vile una mihemko ya kisiasa hutaona uhalisia wa unachopingana nacho. Malizia na hili hakuna hicho unachoita academic weapon labda kwako unavyohadaa watu humu ndo uiite academic weapon kwa wale ambao hawana taaluma ya kupambanua mambo.

Hata hivo naomba nikushauri usitangaze credential zako iwapo unajua kabisa unachoandika hakitarajiwi kutoka kwa mtu ambaye in really ana hizo credentials kama mwanataaluma.
 
Back
Top Bottom