Access Bank Tanzania yauzwa, sasa kujulikana kama 'Selcom Microfinance Bank'

Access Bank Tanzania yauzwa, sasa kujulikana kama 'Selcom Microfinance Bank'

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Benki ya 'Access Microfinance Bank Tanzania (AMBT)' yenye makao makuu imeuzwa kwa kampuni ya kitanzania ya Selcom kama mwanahisa mkubwa zaidi na sasa itajulikana kama 'Selcom Microfinance Bank'. Uwekezaji wa Selcom unaifanya benki hiyo kufikisha mtaji wa zaidi ya Sh 8.6 bilioni.
Kampuni ya Selcom Tanzania ilianzishwa mwaka 2001 kwaajili ya kusambaza vocha za malipo kabla za kampuni ya Celtel(sasa Airtel). Kwasasa Selcom inamiliki mtandao mkubwa zaidi wa mashine za malipo(POS) zinazokadiriwa kufikia ishirini na tano elfu na kuziunganisha zaidi ya benki 40 kwenye 'mobile banking' na wafanyabiashara zaidi ya 100,000 kwenye 'SelcomPay'

Access Bank Selcom.jpg
 
Benki ya 'Access Microfinance Bank Tanzania (AMBT)' yenye makao makuu yake nchini Nigeria imeuzwa kwa kampuni ya kitanzania ya Selcom kama mwanahisa mkubwa zaidi na sasa itajulikana kama 'Selcom Microfinance Bank'. Uwekezaji wa Selcom unaifanya benki hiyo kufikisha mtaji wa zaidi ya Sh 8.6 bilioni...
Access bank (T) Limited kabla haijawa Access Microfinance Bank haijawah kuwana uhusiano na Access Bank ya Nigeria japo wanafanya biashara pia Nigeria kwa jina jingine as walikuta hilolinatumika.Majority share holder alikua Access Holding ya ujeruman na structure ya shareholding ilikua hivi

AccessBank Tanzania Stock Ownership

RankName of OwnerPercentage Ownership
1AccessHolding66.11
2International Finance Corporation13.06
3MicroVest9.04
4KfW6.73
5African Development Bank5.06
Total100.00
 
Mmiliki wa access bank kutoka Nigeria alifariki miezi kadhaa iliyopita kwenye ajali ya helicopter akiwa na mke na mtoto wake wa kiume.Ameacha binti pekee very sad, naona anguko la hii benki Africa lipo karibuni
 
Mmiliki wa access bank kutoka Nigeria alifariki miezi kadhaa iliyopita kwenye ajali ya helicopter akiwa na mke na mtoto wake wa kiume.Ameacha binti pekee very sad,naona anguko la hii benki Africa lipo karibuni
Kwa HIO mfano tufe MIMI, wewe na mtoto wetu wa kiume, mtoto wetu wa kike abakie?
 
Benki ya 'Access Microfinance Bank Tanzania (AMBT)' yenye makao makuu yake nchini Nigeria imeuzwa kwa kampuni ya kitanzania ya Selcom kama mwanahisa mkubwa zaidi na sasa itajulikana kama 'Selcom Microfinance Bank'. Uwekezaji wa Selcom unaifanya benki hiyo kufikisha mtaji wa zaidi ya Sh 8.6 bilioni.
Kampuni ya Selcom Tanzania ilianzishwa mwaka 2001 kwaajili ya kusambaza vocha za malipo kabla za kampuni ya Celtel(sasa Airtel). Kwasasa Selcom inamiliki mtandao mkubwa zaidi wa mashine za malipo(POS) zinazokadiriwa kufikia ishirini na tano elfu na kuziunganisha zaidi ya benki 40 kwenye 'mobile banking' na wafanyabiashara zaidi ya 100,000 kwenye 'SelcomPay'

Mwezi February mwaka huu benki ya Access ilimpoteza mojawapo ya mmliki wake na CEO, Herbert Wigwe ambaye aliinunua benki hiyo mwaka 2002 baada ya benki kuu ya Nigeria kuchelewesha mchakato kutokana na umri wao mdogo na mwanzilishi mwenza, Aigboje Aig-Imoukhuede lakini waliweza kufanya kubwa benki ya nne kwa ukubwa Nigeria mwaka 2017 kutoka benki ndogo na dhaifu, mwaka 2018 waliungana na mshindani wake Diamond Bank na kuifanya kuwa benki kubwa zaidi nchini Nigeria na Wigwe alikuwa kwenye utekelezaji wa kuingia barani Asia kabla ya kifo chake.
Access ya Herbert Wigwe na hii oya oya ya wa mama ntilie ni vitu viwili tofauti.
 
Mmiliki wa access bank kutoka Nigeria alifariki miezi kadhaa iliyopita kwenye ajali ya helicopter akiwa na mke na mtoto wake wa kiume.Ameacha binti pekee very sad,naona anguko la hii benki Africa lipo karibuni
Haujui unachokisema, Access Bank PLC wanaingia Tanzania mwaka huu
 
Kitambo sana tulikulaga za uso
Ile benki iliyokuwa inaitwa meridian biao, vipesa vyetu vilipotea mpaka leo ikawa historia
Nikafungua pia ac benki ya Green land bank nayo ikatokeaga mauzauza

Ova
 
Mpaka 2014 walikua na mtaji wa 100b ambao ulikidhi requirement ya BOT kuwa commercial bank ...hapo katikati sijui nn kiliwakuta nimeshangaa mno kusoma mtaji wa 8.5B
Tofautisha kati ya core capital ya benki na Assets. Currently benki ina assets zaidi ya 80 billion na ndio kipimo cha ukubwa wa benki.
 
Mmiliki wa access bank kutoka Nigeria alifariki miezi kadhaa iliyopita kwenye ajali ya helicopter akiwa na mke na mtoto wake wa kiume.Ameacha binti pekee very sad, naona anguko la hii benki Africa lipo karibuni
Access Tanzania Haina uhusiano wowote na Access Nigeria. Access Tanzania imetokea ujerumani na mmiliki mkubwa alikua ni Access holding ya Berlin
AccessBank Tanzania Stock Ownership
Rank Name of Owner Percentage Ownership
1 AccessHolding
66.11
2 International Finance Corporation
13.06
3 MicroVest
9.04
4 KfW
6.73
5 African Development Bank
5.06
Total
100.00
 
Back
Top Bottom