Acha tabia hizi uepushe magonjwa tabia

Acha tabia hizi uepushe magonjwa tabia

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363
ACHA TABIA HIZI UEPUSHE MAGONJWA KAMA

(Sukari,presha,vidonda vya

tumbo,upungufu wa nguvu za kiume,matatizo ya uzazi na kansa)


ULAFI

Kwa kawaida, mtu anapokula vyakula ambavyo havina virutubisho vya kutosha na vyenye sukari au

chumvi nyingi, hula kupita kiasi bila kujijua. Ndani ya saa 6, mtu huyu anaweza kula vyakula

vidogovidogo vingi kama vile soda, biskuti, mihogo au chipsi za kukaanga, ice cream, koni, n.k.

Ulaji wa namna hii haufai kama vile ambavyo haufai ulaji wa vyakula vilivyoondolewa virutubisho wakati wa utengenezaji, kama vile unga wa mahindi mweupe, ngano nyeupe, n.k. Mtu anapokula vyakula hivi, uchomaji wake wa mafuta mwilini huwa mgumu na hivyo mafuta kurundikana mwilini na kuwa chanzo cha unene na ugonjwa wa kisukari.


KUJISHINDISHA NA NJAA


Kama hauko katika funga, hutakiwi kushinda na njaa. Kinachotokea wakati wa kula baada ya kushinda na njaa kutwa nzima ni kula chakula kingi kwa wakati mmoja ambacho hakiwezi kuyeyushwa chote na mafuta yake kutumika kama nishati ya mwili. Matokeo yake mafuta hujihifadhi mwilini na kusababisha unene. Kuepuka hali hii, kula kwa wakati na kwa kiasi kidogo.

KULA USICHOKIJUA


Watu wengi hawana uelewa wa kutosha wa vyakula wanavyokula kama vina faida au madhara yoyote katika miili yao, hasa wale wanaokula kwenye migahawa. Kujua sifa ya kila chakula

unachokula ni jambo muhimu sana. Ni vizuri kujua mahitaji ya mwili wako ili kula chakula ambacho hakitabaki mwilini kama ziada, hasa kwa upande wa vyakula vyenye mafuta na sukari nyingi.

Ulaji wa vyakula vilivyotengenezwa kwa unga mweupe, kama vile mikate, ugali na ulaji wa vyakula vya sukari nyingi, kama vile soda na vinywaji vingine baridi, kunachangia kuongezeka kwa mafuta mwilini hivyo kusababisha unene na ugonjwa wa kisukari.

4. UKOSEFU WA MAZOEZI

Miili yetu imeumbwa kujishughulisha. Ndiyo maana utaona pale unapoamka na kujisikia mchovu, ukishaanza kufanya kazi unajisikia vizuri. Kujishughulisha kwa kufanya mazoezi kunasaidia

kuyeyusha chakula na mafuta na kuyatumia kama nishati ya mwili.
Kiafya unatakiwa kufanya mazoezi dk 20 kila siku.

5.KUTOFUNGUA KINYWA ASUBUHI


Usidhani kuwa tumbo ndilo linalokwambia halina kitu hivyo linahitaji chakula, bali ni ubongo ndiyo unaotoa taarifa ya chakula. Ni vyema ukahakikisha unafungua kinywa asubuhi ili kuulisha ubongo

wako uweze kufanyakazi yake sawasawa. kunywa maji ya uvuguvugu au matunda kabla ya kunywa chai utakuwa mweye afya na kuepuka vidonda vya tumbo.

6. KUTOKUNYWA MAJIYA KUTOSHA.


Ili chembe hai za ubongo na viungo vingine vya mwili vifanye kazi sawasawa, ikiwemo ngozi, unahitaji maji. Ili mwili uyeyushe mafuta unayokula kutokana na chakula, unahitaji kiasi cha glasi

nane za maji kila siku (kikiwa ndiyo kiwango cha chini kabisa).
Faida za maji mwilini ni nyingi. Maji siyo tu yanakata kiu yako, bali pia yanasaidia kuondoa sumu

mwilini na kukupunguzia njaa ya mara kwa mara. Vinywaji vingine kama vile soda na kahawa, siyo

vinasaidia kukata kiu, bali vinachangia ukaukaji wa maji mwilini. Usitii kiu yako kwa kujidanganya kunywa soda
 
Mkuu MziziMkavu, asante kwa kuendelea kutujuza kila mara pasi na kuchoka.Umebarikiwa mkono utoao kuliko ule upokeao.Mwenyezi Mungu akuzidishie afya na nguvu.
 
Habari ya majukumu ndugu! Naomba kuwashirikisha jambo hili kwa msaada zaidi. Je, inakuwaje mama anajifungua vizuri kabisa halafu baada ya dakika chache mtoto anafariki? Hali hii inajirudia kila anapo jifungua. Naombeni msaada wenu.
 
Habari ya majukumu ndugu! Naomba kuwashirikisha jambo hili kwa msaada zaidi. Je, inakuwaje mama anajifungua vizuri kabisa halafu baada ya dakika chache mtoto anafariki? Hali hii inajirudia kila anapo jifungua. Naombeni msaada wenu.
anzisha thread!
 
ACHA TABIA HIZI UEPUSHE MAGONJWA TABIA KAMA

(Sukari,presha,vidonda vya

tumbo,upungufu wa nguvu za kiume,matatizo ya uzazi na kansa)
ULAFI


Kwa kawaida, mtu anapokula vyakula ambavyo havina virutubisho vya kutosha na vyenye sukari au

chumvi nyingi, hula kupita kiasi bila kujijua. Ndani ya saa 6, mtu huyu anaweza kula vyakula

vidogovidogo vingi kama vile soda, biskuti, mihogo au chipsi za kukaanga, ice cream, koni, n.k.

Ulaji wa namna hii haufai kama vile ambavyo haufai ulaji wa vyakula vilivyoondolewa virutubisho wakati wa utengenezaji, kama vile unga wa mahindi mweupe, ngano nyeupe, n.k. Mtu anapokula vyakula hivi, uchomaji wake wa mafuta mwilini huwa mgumu na hivyo mafuta kurundikana mwilini na kuwa chanzo cha unene na ugonjwa wa kisukari.


KUJISHINDISHA NA NJAA

Kama hauko katika funga, hutakiwi kushinda na njaa. Kinachotokea wakati wa kula baada ya kushinda na njaa kutwa nzima ni kula chakula kingi kwa wakati mmoja ambacho hakiwezi kuyeyushwa chote na mafuta yake kutumika kama nishati ya mwili. Matokeo yake mafuta hujihifadhi mwilini na kusababisha unene. Kuepuka hali hii, kula kwa wakati na kwa kiasi kidogo.

KULA USICHOKIJUA


Watu wengi hawana uelewa wa kutosha wa vyakula wanavyokula kama vina faida au madhara yoyote katika miili yao, hasa wale wanaokula kwenye migahawa. Kujua sifa ya kila chakula

unachokula ni jambo muhimu sana. Ni vizuri kujua mahitaji ya mwili wako ili kula chakula ambacho hakitabaki mwilini kama ziada, hasa kwa upande wa vyakula vyenye mafuta na sukari nyingi.

Ulaji wa vyakula vilivyotengenezwa kwa unga mweupe, kama vile mikate, ugali na ulaji wa vyakula vya sukari nyingi, kama vile soda na vinywaji vingine baridi, kunachangia kuongezeka kwa mafuta mwilini hivyo kusababisha unene na ugonjwa wa kisukari.
4. UKOSEFU WA MAZOEZI


Miili yetu imeumbwa kujishughulisha. Ndiyo maana utaona pale unapoamka na kujisikia mchovu, ukishaanza kufanya kazi unajisikia vizuri. Kujishughulisha kwa kufanya mazoezi kunasaidia

kuyeyusha chakula na mafuta na kuyatumia kama nishati ya mwili.
Kiafya unatakiwa kufanya mazoezi dk 20 kila siku.

5.KUTOFUNGUA KINYWA ASUBUHI


Usidhani kuwa tumbo ndilo linalokwambia halina kitu hivyo linahitaji chakula, bali ni ubongo ndiyo unaotoa taarifa ya chakula. Ni vyema ukahakikisha unafungua kinywa asubuhi ili kuulisha ubongo

wako uweze kufanyakazi yake sawasawa. kunywa maji ya uvuguvugu au matunda kabla ya kunywa chai utakuwa mweye afya na kuepuka vidonda vya tumbo.

6. KUTOKUNYWA MAJI

Ili chembe hai za ubongo na viungo vingine vya mwili vifanye kazi sawasawa, ikiwemo ngozi, unahitaji maji. Ili mwili uyeyushe mafuta unayokula kutokana na chakula, unahitaji kiasi cha glasi

nane za maji kila siku (kikiwa ndiyo kiwango cha chini kabisa).
Faida za maji mwilini ni nyingi. Maji siyo tu yanakata kiu yako, bali pia yanasaidia kuondoa sumu

mwilini na kukupunguzia njaa ya mara kwa mara. Vinywaji vingine kama vile soda na kahawa, siyo

vinasaidia kukata kiu, bali vinachangia ukaukaji wa maji mwilini. Usitii kiu yako kwa kujidanganya kunywa soda
 
Back
Top Bottom