Nacho amini mimi ni kwamba Barbra alienda kushiriki huo mkutano kwa niaba ya klabu anayoiongoza kisha aliomba kupiga picha na viongozi wao kama sehemu ya ukumbusho.
Hakuna ukaribu wala kitu chochote ambacho kimempeleka kwa lengo la connection kwa hao viongozi kwasababu hao viongozi wa timu/vilabu vyote na wanasimamia sheria za mpira. Kama ni connection basi ni connection kwa ajili yake binafsi (nafasi ya kazi) na sio connection kwaajili ya timu
Note: kungekuwa na ujamaa au hiyo connection hiyo ingekuwepo, tusingesikia Simba imezuiwa mashabiki wake kuingia uwanjani. Wangeachwa kama ilivyokuwa zamani kabla ya huyo kiongozi mpya kuingia madarakani
Nimekuelewa.
Kwanza umekubali kwamba Bi Gonzalez ameenda kusimamia maslahi ya Simba katika ''platform'' za soka la kimataifa. (Naamini ni sera ya klabu yake kujipenyeza kwenye ''ulingo wa soka kimataifa'' kwa kutumia fursa mbalimbali zinazojitoleza).
Pili, ni kweli huenda Bi Barbra anatumia fursa anazozipata akiwa kama C.E.O wa Simba kujijenga yeye mwenyewe kwa ajili ya kesho yake. Na hili si kosa hata kidogo.
Kwa maoni yangu, naamini kwamba kila anayepata fursa moja na aitumie vizuri ili kuandaa fursa nyingine siku zijazo.
1. Barbra aliitumia MeTL kujijenga na hatimaye ikampa fursa nyingine pale Simba S.C. (Then Simba to her next step...)
2. Manara ameitumia Simba S.C kupata mikataba na ubalozi wa makampuni mbalimbali ya biashara...
3. Antonio Nugaz ameitumia Clouds Media kupata dili lake Yanga S.C
4. Hassan Bumbuli ''anapaswa kuitumia nafasi yake pale Yanga'' kuandaa fursa zingine mahala pengine....
5. ''Yeye'' apatae dili Barrick na aitumie hiyo fursa ili kesho apate dili Vodacom
6. ''Yule'' apatae dili GSM na alitumie hilo dili ili kesho apate dili ''Yapi Merkezi''
Ndio maisha yanavyokwenda.
Tukumbuke kwamba hizi taasisi zipo kwa miaka mingi, watu wanakuja na kuondoka. Barbra hatokaa Simba S.C milele, ni sahihi kabisa akitumia vizuri ''benefits'' za kuwa mtendaji mkuu wa Simba kwa ajili ya ''future'' ya Simba na ya kwake mwenyewe.
Kule Clouds wana msemo wao wanasema ''
Tunakufungulia Dunia....''
Kuhusu suala la mashabiki, tangu mwanzo mimi nilikua naamini kwamba Simba S.C walikua wanapata ''unfair advantage over other clubs''.
Kwa utaratibu wa sasa, kwamba timu zote zisicheze na mashabiki naamini kuwa ''haki kwa wote'' ndio imetendeka.
Katika hili, naamini utaratibu utakua ni uleule hata katika mechi za nyumbani za timu ya Namungo.
Hivyo basi, hapa sioni ''jitihada'' za Barbra, au Simba S.C zingewezaje kubadili hili.
Mashindano yanapaswa kufanyika katika mazingira sawia. Hapo mwanzo sawia hii haikuwapo, na sasa hivi ipo.
Mwisho wa maoni yangu juu ya hili.
Karibu