Acheni Ushamba, Hakuna gari za kike wala za kiume

Acheni Ushamba, Hakuna gari za kike wala za kiume

Ulivyoweka utafikiri bongo nchi tajiri kweli, kumbe kanchi kenyewe masikini wa kutupwa watu wanashindia mlo mmoja na dollar 1 ni sawa na Tshs 2000 na soon itafika 3000..kuweni na uhalisia sio maisha ya artifial..hapa , mbaya zaidi ni third world country na akili za wananchi wake ndio kama zako.
Hili la umaskini haliwezi kuondoa uhalisia wa jambo kama gauni ni vazi la kike
litabaki kuwa la kike tu hata kama unaishi Pangoni.
 
Kuna gari za kike na za kiume. Hata yule mtengenezaji wa magari anajua kabisa hili gari nalitengezeza maalumu kwa soko fulani. Kuna magari yanatengenezwa kwa ajili ya wenye pesa nyingi. Kwa hiyo usishangae kuona kuna magari ya kike. Mfano redds ni bia iliyotengenezwa maalumu kwa wanawake. Ingawa wapo wanaume wanakunywa. Pia yapo magari yametengenezwa kwa ajili ya akina mama ila wanaume wanaendesha
 
Hahaha wabongo bana!! kwahiyo kila gari ndogo ni ya kike na kila gari kubwa ni ya kiume!! Mfumo dume hadi kwenye magari
 
Gari zenye mwonekano wa kiume na wakike hivi vijigari tudogo ni vyawanawake mwanaume kuendesha hiyo huna tofauti na kujipaka lipstick uwe na mwonekano wa like wakati ni wakiume
 
kwangu mimi naona bora magari makubwa ndo yanamfaa sana mwanaume. je!kuna raha gani kuendesha kigari kidogo alafu kafupi, ukikaa kwenye foleni alafu scania ipo imesimama pembeni yako, ukicheki pembeni tu, unagundua ukubwa wa gari lako ni sawa na tairi la scania; tairi la scania likikata kona kama vile inakuja kwako lazima akili icorrupt muda huohuo.

Watu kama wewe wanazaliwa kwa mwaka Mara moja umenena big up
 
Jerrymsigwa mimi sina gari kwakweli naomba tu kuwa mkweli katika hili

Kama huna gari ice cream na wazungu wapi na mm kukaa ulaya cyo kuwa wewe mwerevu sana ni ushambaa uliokujaa Niko nyumbani najenga taifa langu wewe kula butter kwa kutuma picha za wazungu huku hata nyumbani kwenu umeshindwa hata kupiga rangi ya nyumba ya familia yenu unasema uko ulaya shame on you!
 
Last edited by a moderator:
ila IST yakike kabisa ile.. hata taa /macho yake yanafanana na sepenga vile vle
 
Ahahaha,aisee humu kuna watu wamepanic ile mbaya,na inawezekana mleta post yumo njiani kununua,ila anasikilizia mood za watu kwanza.

Inawezekana watu tukawa tunaenda kwenye point moja kwa moja kwamba ya kike lazima iandikwe.
Hivi nani hajui kama kuna Baiskeli za kike na kiume,na nani hajui kama kuna Pikipiki za kike na kiume.Na zote hazijaandikwa kwamba is for Male or Female.
Ni sawa na mwanaume kuendesha gari ya pink au kuvaa nguo ya pink,lazima uwe kituko.Lakini je nani kasema kwamba Pink ni rangi za kike au wapi pameandikwa.
Cha kuzingatia hapa ni kwamba nimfumo ambao sie wenyewe tumeamua iwe hivyo,nandio ulivyo.
Na wale mliotoka kidogo miji ya watu ulaya ni kwamba mwanaume ukivaa nguo ya Pink usishangae ukaona unapata salama nyingi sana,ukisalimiwa na wenyeji huku wewe hata hujui kinachoendelea na kujiona kwamba umekirimiwa sana na wageni kumbe wao wanaujumbe mwingine na wewe unaujumbe mwingine kimavazi.

Na jinsi dunia inavyoenda kwa kasi,basi wewe nenda kesho Kariakoo,Kaangalie chupi,halafu uniambie kama kuna chupi zimeandikwa za kike au za kiume.Ila kitakachokufanya ujue hii chupi ya kike na kiume ni Shape yake tu.Sasa kwenye Gari is the same.
Ukweli sipendi kubeza hili,lakini Vitz na wenzie zimekaa kidada,sio siri.
Sasa kama mnasubiri kila kitu kiandikwe haya tuendeleeni

Watu kama wewe ni adimu sana humu ndani asante
 
Gari zenye mwonekano wa kiume na wakike hivi vijigari tudogo ni vyawanawake mwanaume kuendesha hiyo huna tofauti na kujipaka lipstick uwe na mwonekano wa like wakati ni wakiume

Tukisimama mimi na wewe kuna uwezekano mkubwa ukabadili kauli yako maana unaweza kujikuta unakua wa kike kimuonekano.
 
Kama huna gari ice cream na wazungu wapi na mm kukaa ulaya cyo kuwa wewe mwerevu sana ni ushambaa uliokujaa Niko nyumbani najenga taifa langu wewe kula butter kwa kutuma picha za wazungu huku hata nyumbani kwenu umeshindwa hata kupiga rangi ya nyumba ya familia yenu unasema uko ulaya shame on you!

Unatoka kwenye mada unaingia kwenye michambo. Wa hivi ndio waleeeeee!!
 
Kuna gari za kike na za kiume. Hata yule mtengenezaji wa magari anajua kabisa hili gari nalitengezeza maalumu kwa soko fulani. Kuna magari yanatengenezwa kwa ajili ya wenye pesa nyingi. Kwa hiyo usishangae kuona kuna magari ya kike. Mfano redds ni bia iliyotengenezwa maalumu kwa wanawake. Ingawa wapo wanaume wanakunywa. Pia yapo magari yametengenezwa kwa ajili ya akina mama ila wanaume wanaendesha

Hapo kwenye Redds umeua
 
IST ni ya wanawake kabisa. Wanaume wanakataa tu kwa sababu wamenunua tayari. Waachieni wenyewe wanahangaika usafiri, nyie mmeng'ang'ania gari zao msibishe.
 
Kwa muda mrefu sasa nimekuwa naona mada humu JF zikiwa zinaponda magari,kwamba magari kama Toyota Passo,Vitz,IST,Starlet,na n.k ni magari ya kike.

Naomba wote wanaoamini kuwa kuna magari ya kike watoe ushahidi,ni wapi ambako chombo cha moto kimeandikwa kuwa:

A Vehicle Special for female au for male?

Acheni Ushamba nyie watanzania ambao hamjui lolote ktk Dunia hii yenye mambo mengi na mazito.

Tanzania isiyotengeneza hata sindano eti wananchi wake wanadharau magari yanayotengenezwa nje na kuya Classify kuwa hili ni la kike na lile ni la kiume,huu ni ujuha wa hali ya juu.

Watanzania ambao hata kula yao ni shida kwa siku eti nao wanabagua magari,kwa lipi?

Ukienda,Japan,US,UK,Germany,Sweden na popote duniani ambako wanatengeneza magari,hawawezi kukuambia kuwa hili ni gari la kile na lile ni la kiume.

Siku zote maskini ni mtu anayejiona ni bora kuliko wote japokuwa hana lolote,Sasa wewe umehangaika ukapata vipesa vyako unanunua gari anakuja mjinga anakuambia ni la kike,wapi imeandikwa kuwa ni la kike,Ujinga uliokithiri.

We utakuwa una IST, si bure.....
 
Back
Top Bottom