ACT: Tunaitaka Serikali ya JMT, kuacha utowaji wa Leseni kwa eneo la Fungu Mbaraka na Bahari Kuu upande wa Zanzibar

ACT: Tunaitaka Serikali ya JMT, kuacha utowaji wa Leseni kwa eneo la Fungu Mbaraka na Bahari Kuu upande wa Zanzibar

Kwa hiyo muungano wenye faida ni kuimeza Zanzibar hivi nyinyi watanganyika mbona hamjielewi mbona MNA rasilimali nyingi tuu za kukutoweni katika umaskin hamtosheki mpaka kile kidogo cheti mukinganganie??
Kuwa na rasilimali nyingi sio sababu ya kugawa rasilimali kwa asiye kuwa nacho.
 
Kwa mujibu wa ibara ya pili ya katiba ya JMT, eneo la JMT ni eneo lote la iliyokuwa Tanganyika na eneo lote la iliyokuwa Jamhuri ya watu wa Zanzibar!.

Ardhi yote ni mali ya Watanzania chini ya udhamini wa rais wa JMT, ila Rais wa JMT kabla hajalihawanya eneo la Zanzibar, atajadiliana kwanza na rais wa Zanzibar, visiwa vyote vya bahari ya Hindi mkabala na Tanzania ikiwemo Zanzibar na Pemba ni mali ya JMT.
P
Kwenda wewe chuki zenu bite kwanza rejea katika uhalali wa huo unaoitwa muungano Kisha ndio uje kwenye hivyo vifunga hakuna ushahidi popote unaoonesha wazanzibar waliridhia muungano huu wa kimagumaashi
 
Ndio kabisa kwa ukaribu wa coastline ya bara na Zanzibar, bara wana strong claim ya kisiwa kushinda Zanzibar.

Halafu wazanzibari mnafurahisha sana hivi unadhani kuna mtu atakują kujenga refinery ya LNG tena Zanzibar, wakati bara inajengwa.

Hiki ndio kitakachotokea hata sehemu za Zanzibar zikibainika zina commercial wells, refinery inatafanyika bara, serikali ya bara itawatoza hela kwa sababu mafuta sio maswala ya muungano.

Sasa kwa akili zenu huko mbele mtasema sisi nchi moja kwanini mtutoze kutumia refinery baada ya kuona mapato mtakayopata ni kiduchu.

Akili za viongozi wa ACT ni fupi sana, akitokea mtu wa kuuvunja huo muungano ndio akili zao zitakaa sawa.
Rejea historia muungano ulianza lini Kisha jiulize kabla hapo wazanzibar hawakuishi??
 
Ibara ya kwanza ya Katiba ya JMT inasema “1. Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano".
Ibara ya pili ya katiba ya JMT inasema
2.-(1) Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanzania Bara na eneo lote la Tanzania Zanzibar, na ni pamoja na sehemu yake ya bahari ambayo Tanzania inapakana nayo.

Hivyo Zanzibar haina eneo, haina mipaka, Fungu Mbaraka ni eneo la JMT.
P
Utakufa na chuki zako ZANZIBAR haitotawaliwa na watanganyika subir Zanzibar yenye mamlaks kamili inakuja izo ibara zote zipo kimagumaashi na yote hayo yaliwekwa waz katika bunge la katiba
 
Ndio kabisa kwa ukaribu wa coastline ya bara na Zanzibar, bara wana strong claim ya kisiwa kushinda Zanzibar.

Halafu wazanzibari mnafurahisha sana hivi unadhani kuna mtu atakują kujenga refinery ya LNG tena Zanzibar, wakati bara inajengwa.

Hiki ndio kitakachotokea hata sehemu za Zanzibar zikibainika zina commercial wells, refinery inatafanyika bara, serikali ya bara itawatoza hela kwa sababu mafuta sio maswala ya muungano.

Sasa kwa akili zenu huko mbele mtasema sisi nchi moja kwanini mtutoze kutumia refinery baada ya kuona mapato mtakayopata ni kiduchu.

Akili za viongozi wa ACT ni fupi sana, akitokea mtu wa kuuvunja huo muungano ndio akili zao zitakaa sawa.
Kasome katiba ya muungano, mafuta ni swala la muungano.
 
hakuna ushahidi popote unaoonesha wazanzibar waliridhia muungano huu wa kimagumaashi
Mkuu dega , japo ni kweli Zanzibar haikuridhia muungano kwa ratification, lakini imeridhia by performance!.

Muungano ni kama ndoa, kabla ya watu kuoana lazima kuwe na ridhaa, consent, kumuingilia mtu bila consent ni kumbaka, ni kosa la jinai.

Mwanamke akibakwa lazima apige kelele na ku resist issiingie, mwanamke akibakwa huku ametulia, hapigi kelele, ndio kwanza ana panua ili iingie vizuri kwa ulaini, asichubuke na asiumie!, halafu baada ya ubakaji huo, mwanamke huyo akaendela kuishi kinyumba na mbakaji wake huku akitimiza majukumu yote ya ndao, atahesabika ame ridhia na hiyo ni ndoa halali!.

Kwenye ndoa ya muungano wa Tanzania, Tanganyika ndio iliridhia na kufanya ratification process, Zanzibar haukuridhia, lakini imo ndani ya ndoa ikitimiza majukumu yote ya ndoa, hivyo imeridhia by performance!.
Karibu darasa la bure
P
 
Ama haya madai kwamba OMO hana hoja, huenda huelewi anachosema na hivyo huoni ndani. Huyu anatoa hoja za kisheria na sio za kisiasa.
Namsikiliza sana, hoja zake si za kisheria ni za chuki tu! Kwa mfano, anasema Tanganyika inaonea au kuinyonya Zanzibar kiuchumi. Hakuna hata siku moja ameonyesha hilo. Siku aliyojaribu kusema ni pale alipotoa hoja ya ''kugawana misaada 50%' hapo ndipo nilimdharau sana! sorry
Haina kwasababu ndo makubaliano ya muungano.
Makubaliano ya Muungano hayakusema Tanganyika ifutike. Hebu rudi usome ! au muulize OMO
Hapa ndo umechanganya mambo na ni kwasababu hujui. Nikukumbushe tu kwamba katika hiyo orodha uliyiandika kuna mambo tayari ni ya muungano.
Tunazungumzia yale ya mkataba wa Muungano! yapo 11. Nitajie moja tu ambalo nimelisema la Muungano.

Jitahidi kujifunza.
Ninajifunza kila siku. Siku hizi hatusikii upuuzi wa '' tutavunja muungano''.
Watanganyika wanasema hata leo hewala!
Mchango gani unaousemea. Na wakisema yameongezwa kinyemela hawajakosea kwani wanazungumzia muungano ambao ni mkataba wa kisheria.
Zanzibar haina mchango katika JMT kwa mujibu wa Gavana wa Bank kuu kwa miaka zaidi ya 45.
Zanzibar inapewa 10% ya Bajeti yake kutoka Tanganyika
Hailipi mikopo inayokuja kwa jina la JMT
Haina Bajeti kubwa kama Ulinzi, mambo ya ndani , nje, n.k.
Orodha ni kubwa inaendelea

Btw Hata Wabunge pale Dodoma wanalipwa na kodi za Watanganyika
nakusubiri
 
Namsikiliza sana, hoja zake si za kisheria ni za chuki tu! Kwa mfano, anasema Tanganyika inaonea au kuinyonya Zanzibar kiuchumi. Hakuna hata siku moja ameonyesha hilo. Siku aliyojaribu kusema ni pale alipotoa hoja ya ''kugawana misaada 50%' hapo ndipo nilimdharau sana! sorry
Hivi anaposema Tanganyika inaionea Zanzibar ni muongo au ni wewe unajitia upofu na uziwi? Hivi inapokuja, kwa mfano, misaada kwa Tanzania halafu Zanzibar isipewe chochote sio kuionea?!

Swala la kutoa maoni ya kugawana misaada ya 50% kwako ni la kudharau? Kwake halikuwa la kudharau; alikuwa anamaanisha.
Makubaliano ya Muungano hayakusema Tanganyika ifutike. Hebu rudi usome ! au muulize OMO
Hapa nawe nenda karudie tena. Hapa ndo imeandikwa kinagaubaga kwamba kutakuwa na JMT na Zanzibar. Huenda unazungumza kwa kubahatisha. Hoja hazitolewi kwa kubahatisha.
Tunazungumzia yale ya mkataba wa Muungano! yapo 11. Nitajie moja tu ambalo nimelisema la Muungano.
Huenda unasahau unayoandika. Nimetoa maoni baada ya hoja yako kwamba "mambo ambayo Zanzibar hawataki yawe ya muungano .." halafu ukayaorodhesha. Mimi nimekuambia hayo unayoandika mengine tayari ni ya muungano, ingawa sikukushtua lkn moja wapo ni la Elimu ya juu ambalo ni la muungano. Au ulikuwa unasinzia? Mimi nilikuwa najadili hoja/andiko lako na sikuzungumzia kitu kingine. Rejea tena maandiko yako halafu lete hoja.
Ninajifunza kila siku. Siku hizi hatusikii upuuzi wa '' tutavunja muungano''.
Watanganyika wanasema hata leo hewala!
Kusema ni kitu kimoja na kutekeleza ni kitu kingine. Haionekani kwamba unajifunza. Kile unchokiita upuuzi wa "tutavunja muungano" wala huwa hayasemwi. Na hayasemwi kwasababu Tanganyika, siku zote, unapozungumza swala la kuuvunja muungano inakuvunja wewe. Kinachosemwa, labda, ni haya kwa mfano: "muungano/Tanganyika u/inainyonya Zanzibar". Weka kumbukumbu zako sawasawa.
Zanzibar haina mchango katika JMT kwa mujibu wa Gavana wa Bank kuu kwa miaka zaidi ya 45.
Huyo Gavana alishawahi kukuambia pia kuwa BOT haiilipi Zanzibar mgao wa mapato yanayotoka BOT? Kama angekuwa muungwana angelisema na hili. Nenda kamuulize upate maelezo.
Zanzibar inapewa 10% ya Bajeti yake kutoka Tanganyika
Huu ni uongo wa mchana kuzimu hakuna nyota. Akili za kuambiwa changanya na zako.
Hailipi mikopo inayokuja kwa jina la JMT
Ivi upo? Akope JMT halafu ikallipe Zanzibar? Hivi umeandika mwenyewe hili au umeandikiwa ukiwa mwenyewe hupo?
Btw Hata Wabunge pale Dodoma wanalipwa na kodi za Watanganyika
nakusubiri
Mkuu nikukumbushe tu kwamba bunge ni la JMT na linaendeshwa na JMT kutokana na mapato ya JMT yanayopatikana kutoka vyanzo mbali vikiwemo kodi na ushuru, faida ya BOT na vingine. Hivi vyote vinalipwa na Watanzania na wengine wanaopaswa kulipa.

Karibu tena.
 
Hivi anaposema Tanganyika inaionea Zanzibar ni muongo au ni wewe unajitia upofu na uziwi?
Tanganyika ina watu milioni 60, Zanzibar ina 1.2 na kati yao nusu wanaishi Tanganyika.
Eneo na Uchumi wa Tanganyika huwezi kuweka katika mizani.
Mkoa mpya wa Simiyu ni mKubwa kuliko Zanzibar kwa kila kitu

Makusanyo ya kodi Zanzibar kwa 2023 ilikuwa Bilioni 58 kwa mwezi.
Kiasi hicho ni kampuni 3 tu za Tanganyika.

Hivi inapokuja, kwa mfano, misaada kwa Tanzania halafu Zanzibar isipewe chochote sio kuionea?!
Misaada inayopewa ni fadhila. Fikiria kwamba kuna misaada ya Trillioni 1, kwa mujibu wa OMO zigawanywe Bilioni 500 kila upande. Hivi hapa kuna fikra kweli ! Lakini pia Misaada ni Fadhila kwasababu hizi;
1. Zanzibar inapewa 10% ya Bajeti yake kwa kinachoitwa ''GBS'' kutoka Tanganyika. Muulize Mh. Saada Mkuya
2. Zanzibar haina gharama za Bajeti katika Wizara ya Ulinzi, Mambo ya ndani, Mambo ya nje, Muungano na Taasisi zote za Muungano. Maeneo hayo yanagharamiwa na Bajeti ya Tanganyika inayoitwa Tanzania.
3. Watumishi wa JMT Zbar ina 21 wanalipwa mishahara, mafao na pensheni kutoka Bajeti ya Tanganyika.
4. Tanganyika imeajiri Wazanzibar wengi kuliko SMZ ''Uzanzibar'' inawalipa hata kwa nafasi zisizo Muungano.
5. Nusu ya Wazanzibar wanaooishi Tanganyika wanatumia resource za Tanganyika Bure! elimu na Afya
6. Wabunge wa Zbar wanapewa fedha za mfuko wa Jimbo kutoka Bajeti ya Tanganyika
7. Wabunge wa Zbar Dodoma ni wengi kukliko 50 wa Baraza la wawakilishi, wanalipwa na Tanganyika
8. Balozi za Tanzania zinahudumiwa na Bajeti ya Tanganyika
9. Tanganyika ndio nchi iliyotoa fursa za Biashara na ajira za informal sector kwa Zbar kukiko pengine
10. Wbar wakiwemo wa ACT walipata elimu Bure Tanganyika wakati wa Nyerere , na hata leo HESLB inadhamini Wazanzibar wengi kuliko ZHESL. Nionyeshe nchi nyingine inayotoa udhamini kuliko Tanganyika
11. Hata umeme ! umeme Zanzibar inapewa Bure!

Orodha inaendelea, nikuulize misaada inayoletwa (fira za kimasikini sana) unaweza kufidia hayo hapo juu

Swala la kutoa maoni ya kugawana misaada ya 50% kwako ni la kudharau? Kwake halikuwa la kudharau; alikuwa anamaanisha.
Ni hoja ya kipuuzi !nimejibu hapo juu. Watu laki 6 wagawane sawa na watu milioni 60.
Yes laki 6 kwasababu lakini 6 wengine wanaishia Tanganyika kwa gharama za Tanganyika
Hapa ndo imeandikwa kinagaubaga kwamba kutakuwa na JMT na Zanzibar. Huenda unazungumza kwa kubahatisha.
Muungano ulikuwa April 26 1964. Jina Tanzania lilikuja November 1, 1964
Mkataba wa Muungano haukutaja Tanzania kwasababu haikuwepo. Umeelewa?
Hoja hazitolewi kwa kubahatisha.
Mkataba wa Muungano ulitaja Republic of Tanganyika and Republic of Zanzibar. April 26 ,1964
Umeelewa!
Mimi nimekuambia hayo unayoandika mengine tayari ni ya muungano, ingawa sikukushtua lkn moja wapo ni la Elimu ya juu ambalo ni la muungano.
Elimu ya Juu si kati ya 11 ya Mkataba wa Muungano.
In fact waliozua hoja ni Wazanzibar wakisema imeingizwa kinyemela mwaka 1971.

Ni kweli ndio maana tunahoji kwanini kuwe na Wizara ya Elimu ya Juu Tanzania na Elimu ya Juu Zanzibar?
Jibu ni rahisi, ili Zanzibar waweze kunufaika na fursa zinazotokana na Tanganyika!
Haionekani kwamba unajifunza. Kile unchokiita upuuzi wa "tutavunja muungano" wala huwa hayasemwi.
Tulioishi nyakati hizo, Wazanzibar wakitaka kitu wanasema ''msipofanya abcd'' tunavunja Muungano!

Watanganyika walikuwa kimya na wengine hawakujua Zbar wanapewa fursa gani.

Siku hizi Watanganyika wameamka, wanasema '' hata leo hewala''
Nikuulize Zawadini , Tanganyika itapoteza nini Zanzibar ikiondoka kwenye muungano!
Huyo Gavana alishawahi kukuambia pia kuwa BOT haiilipi Zanzibar mgao wa mapato yanayotoka BOT?
Zanzibar ilipewa 4.5% , Samia ameongeza hadi 9 % kwa ushahidi wa Mwenezi wa CCM Zanzibar Bw. Mbeto.

Kumbuka BoT ni Uchumi wa Tanganyika, wanachopewa ni zawadi kwasababu hawana mchango wowote katika ukuaji wa BoT! Wana mtaji lakini tu hawakukuza. In fact ni nafuu kuwalipa gharama za mtaji kuliko kuwapa 9% kwasababu ni gharama kwa Tanganyika

Gavana Ndulu (R.I.P) alisimama mbele ya Umma na kueleza bila siri. Mara ya Mwisho Zanzibar ilichangia Muungano ikiwemo ukuaji wa BoT miaka 45! iliyopita
Mkuu nikukumbushe tu kwamba bunge ni la JMT na linaendeshwa na JMT kutokana na mapato ya JMT yanayopatikana kutoka vyanzo mbali vikiwemo kodi na ushuru, faida ya BOT na vingine. Hivi vyote vinalipwa na Watanzania na wengine wanaopaswa kulipa.
Kwa Taarifa 98% ya mambo ndani ya Bunge ni ya Tanganyika ikiwemo Bajeti.

Wabunge wa Zanzibar wapo tu , hawana sababu zozote za kuwepo.

Bajeti zinazowahusu W'bar : Ulinzi, Mambo ya ndani, Nje, na Muungano. Baada ya hapo wanatakiwa waondoke wapunguze mzigo wa posho.

Inawa wahusu nini kujadili Tamisemi, Utalii, Elimu, Afya, Madini, n.k.

Kodi za Zanzibar hata zile za TRA hazivuki Bahari zinabaki huko.
Hata ushuru wa VISA za Watalii zinabaki huko lakini Wafanyakazi wa Uhamiaji wanalipwa na Tanganyika

Tuonyeshe kutoka Bajeti ya Zanzibar wapi inaonyesha mchango katika JMT
Tuonyeshe Taasisi gani inatoza ushuru au kodi Zanzibar na kuleta Tanganyika.

Nimekaa pale
 
[3
Tanganyika ina watu milioni 60, Zanzibar ina 1.2 na kati yao nusu wanaishi Tanganyika.
Eneo na Uchumi wa Tanganyika huwezi kuweka katika mizani.
Mkoa mpya wa Simiyu ni mKubwa kuliko Zanzibar kwa kila kitu

Haya uliyooredhesha yote ni majukumu ya JMT. Zanzibar inahusikaje? Ya Ngoswe mwachie Ngoswe
Muungano ulikuwa April 26 1964. Jina Tanzania lilikuja November 1, 1964
Mkataba wa Muungano haukutaja Tanzania kwasababu haikuwepo. Umeelewa?
Ni kweli. Ni serikali ya muungano iliyoelekeza kutafutwa jina la nchi hiyo hilo lilioko kwenye ni kubwa. Serikali hiyo ilikuwa chini ya Nyerere. Umeelewa hilo
Makusanyo ya kodi Zanzibar kwa 2023 ilikuwa Bilioni 58 kwa mwezi.
Kiasi hicho ni kampuni 3 tu za Tanganyika.
Nilitarajia utajibu, mimi niliuliza swali.M
Tanganyika ina watu milioni 60, Zanzibar ina 1.2 na kati yao nusu wanaishi Tanganyika.
Eneo na Uchumi wa Tanganyika huwezi kuweka katika mizani.
Mkoa mpya wa Simiyu ni mKubwa kuliko Zanzibar kwa kila kitu

Makusanyo ya kodi Zanzibar kwa 2023 ilikuwa Bilioni 58 kwa mwezi.
Kiasi hicho ni kampuni 3 tu za Tanganyika.
Sasa ikiwa hivyo ndo ina haki ya kuonewa? Nawe kwa Utanganyika wako unaona kuna haki ya kuwaonea wengine kwasababu wao ni kidogo?
Misaada inayopewa ni fadhila. Fikiria kwamba kuna misaada ya Trillioni 1, kwa mujibu wa OMO zigawanywe Bilioni 500 kila upande. Hivi hapa kuna fikra kweli ! Lakini pia Misaada ni Fadhila kwasababu hizi;
1. Zanzibar inapewa 10% ya Bajeti yake kwa kinachoitwa ''GBS'' kutoka Tanganyika. Muulize Mh. Saada Mkuya
Orodha hii ndefu yote inaihusu JMT na Zanzibar haipaswi kubeba garama ambazo haiihusu.
Ni hoja ya kipuuzi !nimejibu hapo juu. Watu laki 6 wagawane sawa na watu milioni 60.
Yes laki 6 kwasababu lakini 6 wengine wanaishia Tanganyika kwa gharama za Tanganyika
Huenda umesahau kwamba sensa huwa inahesabu watu walioamkia sehemu husika siku ya sensa. Lakini wacha iwe hivyo. Kwa kuwa kwao kidogo ndo kunahalalisha wao kuonewa na kunyonywa haki zao. Bila shaka jawabu ni "hapana" hivyo anayo haki ya kulisemea hilo.
Muungano ulikuwa April 26 1964. Jina Tanzania lilikuja November 1, 1964
Mkataba wa Muungano haukutaja Tanzania kwasababu haikuwepo. Umeelewa?
Umesema kweli. Ulichokisahau ni kwamba baada ya hiyo Aprili, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (JMTZ), Nyerere - Mtanganyika - alitangaza kutafutwa kwa jina litakalokuwa fupi, na hivyo jina Tanzania likapitishwa na hukohuko Tanganyika, wala Zanzibar haikuhusika kwani haikuwa mamlaka yake.
Mkataba wa Muungano ulitaja Republic of Tanganyika and Republic of Zanzibar. April 26 ,1964
Umeelewa!
Hili nimelieleza hapo juu.
Elimu ya Juu si kati ya 11 ya Mkataba wa Muungano.
In fact waliozua hoja ni Wazanzibar wakisema imeingizwa kinyemela mwaka 1971.

Ni kweli ndio maana tunahoji kwanini kuwe na Wizara ya Elimu ya Juu Tanzania na Elimu ya Juu Zanzibar?
Jibu ni rahisi, ili Zanzibar waweze kunufaika na fursa zinazotokana na Tanganyika!
Nililisema hili kwa sababu ya madai yako ya Wazanzibari kukataa elimu ya juu kuwa ya muungano, nami nikakuambia unazungumza mambo ambayo tayari ni ya muungano. Ni kweli pia kuwa Wazanzibari wanasema elimu ya juu imeingizwa katika orodha ya mambo ya muunganono, kinyemela, kibabe, kihuni n.k Kwani nasema uongo ndugu yangu?
Tulioishi nyakati hizo, Wazanzibar wakitaka kitu wanasema ''msipofanya abcd'' tunavunja Muungano!

Watanganyika walikuwa kimya na wengine hawakujua Zbar wanapewa fursa gani.
Naona hapa unasema uongo. Nikujulishe tu kwamba moja ya sababu ya kuuliwa Karume ni pale aliposema "muungano mwisho Chumbe" ingawa huenda kuna na sababu nyingine, kwahivyo Watanganyika hawajawahi kuwa kimya kuhusu muungano. Weka kumbukumbu sawa.
Nikuulize @Zawadini , Tanganyika itapoteza nini Zanzibar ikiondoka kwenye muungano!
Nami naomba nikujibu kwa swali. Zanzibar itakosa nini ikiondoka kwenye muungano? Ukijibu hili swali nitakuwa na nafasi nzuri ya kukujibu.
Zanzibar ilipewa 4.5% , Samia ameongeza hadi 9 % kwa ushahidi wa Mwenezi wa CCM Zanzibar Bw. Mbeto.

Kumbuka BoT ni Uchumi wa Tanganyika, wanachopewa ni zawadi kwasababu hawana mchango wowote katika ukuaji wa BoT! Wana mtaji lakini tu hawakukuza. In fact ni nafuu kuwalipa gharama za mtaji kuliko kuwapa 9% kwasababu ni gharama kwa Tanganyika

Gavana Ndulu (R.I.P) alisimama mbele ya Umma na kueleza bila siri. Mara ya Mwisho Zanzibar ilichangia Muungano ikiwemo ukuaji wa BoT miaka 45! iliyopita
Mimi nilikuuliza "huyo gavana alishawahi kukuambia ni lini Zanzibar ilipewa mgao wa mapato kutoka BOT? Mimi nataka jawabu ya hilo swali.

Zanzibar ilipewa 4.5% na nani na kwa misingi gani? Hivi unajua chi
Kwa Taarifa 98% ya mambo ndani ya Bunge ni ya Tanganyika ikiwemo Bajeti.

Wabunge wa Zanzibar wapo tu , hawana sababu zozote za kuwepo.

Bajeti zinazowahusu W'bar : Ulinzi, Mambo ya ndani, Nje, na Muungano. Baada ya hapo wanatakiwa waondoke wapunguze mzigo wa posho.

Inawa wahusu nini kujadili Tamisemi, Utalii, Elimu, Afya, Madini, n.k.

Kodi za Zanzibar hata zile za TRA hazivuki Bahari zinabaki huko.
Hata ushuru wa VISA za Watalii zinabaki huko lakini Wafanyakazi wa Uhamiaji wanalipwa na Tanganyika

Tuonyeshe kutoka Bajeti ya Zanzibar wapi inaonyesha mchango katika JMT
Tuonyeshe Taasisi gani inatoza ushuru au kodi Zanzibar na kuleta Tanganyika
mbuko la hiyo 4.5 ni nini? Ungejua usingeandika haya!
Bunge ni la Jamhuri ya muungano. Kwa makubaliano na Katiba JMT itasimamia mambo yote muungano na mambo yote yasiyo ya muungano kwa upande wa Tanganyika/Tanzania Bara, kwahivyo Watanzania wote wanahusika bila kujali wanatokea wapi. Haya mingine ni maoni yako ambayo ni kinyume na Katiba.

Wafanyakazi wa uhamiaji wanalipwa na JMT na haijawhi na haitotokea, muda wote wa uai wa muungano, kulipwa na Tanganyika. Hili unapaswa kulijua..

Mchango wa Zanzibar ktk JMT unatokana na michango , ikiwemo ile ya BOT na mingine. Nikuombe tena ukawaulize hao waliokuambia kwamba Zanzibar hailipi.. Waulize hivi "Hivi ni lini tokea muungano huu umeanzishwa imepewa mgao wake kutoka BOT?

Karibu tena.
 
Namsikiliza sana, hoja zake si za kisheria ni za chuki tu! Kwa mfano, anasema Tanganyika inaonea au kuinyonya Zanzibar kiuchumi. Hakuna hata siku moja ameonyesha hilo. Siku aliyojaribu kusema ni pale alipotoa hoja ya ''kugawana misaada 50%' hapo ndipo nilimdharau sana! sorry

Makubaliano ya Muungano hayakusema Tanganyika ifutike. Hebu rudi usome ! au muulize OMO

Tunazungumzia yale ya mkataba wa Muungano! yapo 11. Nitajie moja tu ambalo nimelisema la Muungano.


Ninajifunza kila siku. Siku hizi hatusikii upuuzi wa '' tutavunja muungano''.
Watanganyika wanasema hata leo hewala!

Zanzibar haina mchango katika JMT kwa mujibu wa Gavana wa Bank kuu kwa miaka zaidi ya 45.
Zanzibar inapewa 10% ya Bajeti yake kutoka Tanganyika
Hailipi mikopo inayokuja kwa jina la JMT
Haina Bajeti kubwa kama Ulinzi, mambo ya ndani , nje, n.k.
Orodha ni kubwa inaendelea

Btw Hata Wabunge pale Dodoma wanalipwa na kodi za Watanganyika
nakusubiri
Tanganyika ina chanzo gani cha Kodi au hizo tozo za halmashauri zenu ?
Kabla hujaanza kunijibu pitia kwanza Articles of Union ili usije kupuyanga
 
Back
Top Bottom