ACT Wazalendo: Mkuu wa Mkoa wa Dar awajibishwe haraka kulinda utu wa Wananchi

ACT Wazalendo: Mkuu wa Mkoa wa Dar awajibishwe haraka kulinda utu wa Wananchi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM AWAJIBISHWE HARAKA KULINDA UTU WA WANANCHI

Chama cha ACT Wazalendo kinalaani vikali kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Ndg. Albert Chalamila inayowataka wanawake kujifungua nyumbani kwa kutumia visu na mikasi endapo watakosa fedha za kulipia huduma hospitalini. Kauli hii inashambulia haki za msingi za wananchi kupata huduma bora za afya, hasa huduma za uzazi zilizoahidiwa kutolewa bure.

Kusoma alichokisema Mkuu wa Mkoa ~ RC Chalamila asema mjamzito anayegoma kununua gloves akajifungulie nyumbani. Hafai kuendelea kubaki madarakani

Kauli ya Mkuu wa Mkoa akiwa katika ziara Wilaya ya Temeke, inayosema kwamba mwanamke anayekosa fedha za kujifungua hospitalini ajifungue nyumbani kwa kutumia visu na mikasi. Si tu kwamba ni kinyume na maadili ya kiuongozi, sera ya utoaji wa huduma za bure kwa wajawazito bali ni yanaweka rehani maisha ya mama na mtoto.

Kauli hii ni mwendelezo wa matamko ya Chamilika yasiyo ya kiuongozi, yenye kejeli pindi wananchi wanapokuta naye kueleza matatizo yao au changamoto na huduma.

Tukio hili linadhihirisha kile ambacho Watanzania wengi wanapitia kwenye mfumo wa afya wa sasa unaotegemea uwezo wa kifedha badala ya huduma kwa wote na hivyo kuhatarisha maisha ya wananchi masikini hasa wanawake, watoto na wazee.

Ikiwa kauli hiyo ya kutaka wanawake wasio na uwezo wa kifedha wajifungulie nyumbani haifanywi rasmi kuwa msimamo wa Serikali ya Chama cha Mapinduzi, tunatoa wito wa kuchukuliwa hatua zifuatazo:

Tunamtaka Rais Samia kumwajibisha haraka Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa kauli zake zisizo za kiuongozi ambazo zinakiuka misingi ya utoaji haki na huduma za afya kwa wajawazito na watoto.

Tunaitaka Serikali kutekeleza kwa vitendo ahadi yake ya kuhakikisha huduma za uzazi zinapatikana bila gharama, kama ilivyoainishwa katika sera ya afya ya taifa.

Serikali iharakishe utekelezaji wa mfumo wa kuwaunganisha watanzania na Hifadhi ya Jamii na kutoa bima ya afya kwa wote ili kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma za afya bila ubaguzi wa kifedha.

ACT Wazalendo inaendelea kusimama kidete kuhakikisha kuwa huduma za afya si bidhaa ya kibiashara, bali ni haki inayopaswa kutolewa kwa kila mwananchi kwa heshima na utu.

Dkt. Elizabeth Benedict Sanga
Waziri Kivuli wa Afya
ACT Wazalendo
26 Januari, 2024
 
MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM AWAJIBISHWE HARAKA KULINDA UTU WA WANANCHI

Chama cha ACT Wazalendo kinalaani vikali kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Ndg. Albert Chalamila inayowataka wanawake kujifungua nyumbani kwa kutumia visu na mikasi endapo watakosa fedha za kulipia huduma hospitalini. Kauli hii inashambulia haki za msingi za wananchi kupata huduma bora za afya, hasa huduma za uzazi zilizoahidiwa kutolewa bure.

Kauli ya Mkuu wa Mkoa akiwa katika ziara Wilaya ya Temeke, inayosema kwamba mwanamke anayekosa fedha za kujifungua hospitalini ajifungue nyumbani kwa kutumia visu na mikasi. Si tu kwamba ni kinyume na maadili ya kiuongozi, sera ya utoaji wa huduma za bure kwa wajawazito bali ni yanaweka rehani maisha ya mama na mtoto.

Kauli hii ni mwendelezo wa matamko ya Chamilika yasiyo ya kiuongozi, yenye kejeli pindi wananchi wanapokuta naye kueleza matatizo yao au changamoto na huduma.

Tukio hili linadhihirisha kile ambacho Watanzania wengi wanapitia kwenye mfumo wa afya wa sasa unaotegemea uwezo wa kifedha badala ya huduma kwa wote na hivyo kuhatarisha maisha ya wananchi masikini hasa wanawake, watoto na wazee.

Ikiwa kauli hiyo ya kutaka wanawake wasio na uwezo wa kifedha wajifungulie nyumabani haifanywi rasmi kuwa msimamo wa Serikali ya Chama cha Mapinduzi, tunatoa wito wa kuchukuliwa hatua zifuatazo:

Tunamtaka Rais Samia kumwajibisha haraka Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa kauli zake zisizo za kiuongozi ambazo zinakiuka misingi ya utoaji haki na huduma za afya kwa wajawazito na watoto.

Tunaitaka Serikali kutekeleza kwa vitendo ahadi yake ya kuhakikisha huduma za uzazi zinapatikana bila gharama, kama ilivyoainishwa katika sera ya afya ya taifa.

Serikali iharakishe utekelezaji wa mfumo wa kuwaunganisha watanzania na Hifadhi ya Jamii na kutoa bima ya afya kwa wote ili kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma za afya bila ubaguzi wa kifedha.

ACT Wazalendo inaendelea kusimama kidete kuhakikisha kuwa huduma za afya si bidhaa ya kibiashara, bali ni haki inayopaswa kutolewa kwa kila mwananchi kwa heshima na utu.

Dkt. Elizabeth Benedict Sanga
Waziri Kivuli wa Afya
ACT Wazalendo
26 Januari, 2024
Chalamila ni mtu mmoja wa hovyo kabisa
 
Chalamila ni mshamba mmoja ambaye akipata madaraka huwa hakawii KUKENGEUKA. Kwanza kwa background yake ni mtu anazaliwa kijiji cha Malangali. Akapata kubahatika kusoma Chuo Kikuu na kuingia CCM.

Tulimuona matamko yake ya kifedhuli akiwa RC Mbeya na Mwanza na kisha akawekwa bench na Samia.

Baadaye kuna watu wakamuombea tena kwa Samia, akarudi kama RC Kagera kisha Dar.

Alipokuwa bench alianza kufulia na kupauka hadi kuanza kurekodi nyimbo za Injili na kuzisambaza kama akina Gosbert Goodluck au Boni Mwaitege.

Anajisahau sana kwa kauli za KIFEDHULI lakini siku yake yaja
 
Kiti ya kujifungulia hazina hata bei sijui alifikiri nini yaani kutuma Tsh 50,000 kwa mgonjwa mambo mengine yaende kaona tabu mbona watu tunatoa zaidi ya hizo mtu akikwambia matatizo yake..
 
MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM AWAJIBISHWE HARAKA KULINDA UTU WA WANANCHI

Chama cha ACT Wazalendo kinalaani vikali kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Ndg. Albert Chalamila inayowataka wanawake kujifungua nyumbani kwa kutumia visu na mikasi endapo watakosa fedha za kulipia huduma hospitalini. Kauli hii inashambulia haki za msingi za wananchi kupata huduma bora za afya, hasa huduma za uzazi zilizoahidiwa kutolewa bure.

Kusoma alichokisema Mkuu wa Mkoa ~ RC Chalamila asema mjamzito anayegoma kununua gloves akajifungulie nyumbani. Hafai kuendelea kubaki madarakani

Kauli ya Mkuu wa Mkoa akiwa katika ziara Wilaya ya Temeke, inayosema kwamba mwanamke anayekosa fedha za kujifungua hospitalini ajifungue nyumbani kwa kutumia visu na mikasi. Si tu kwamba ni kinyume na maadili ya kiuongozi, sera ya utoaji wa huduma za bure kwa wajawazito bali ni yanaweka rehani maisha ya mama na mtoto.

Kauli hii ni mwendelezo wa matamko ya Chamilika yasiyo ya kiuongozi, yenye kejeli pindi wananchi wanapokuta naye kueleza matatizo yao au changamoto na huduma.

Tukio hili linadhihirisha kile ambacho Watanzania wengi wanapitia kwenye mfumo wa afya wa sasa unaotegemea uwezo wa kifedha badala ya huduma kwa wote na hivyo kuhatarisha maisha ya wananchi masikini hasa wanawake, watoto na wazee.

Ikiwa kauli hiyo ya kutaka wanawake wasio na uwezo wa kifedha wajifungulie nyumabani haifanywi rasmi kuwa msimamo wa Serikali ya Chama cha Mapinduzi, tunatoa wito wa kuchukuliwa hatua zifuatazo:

Tunamtaka Rais Samia kumwajibisha haraka Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa kauli zake zisizo za kiuongozi ambazo zinakiuka misingi ya utoaji haki na huduma za afya kwa wajawazito na watoto.

Tunaitaka Serikali kutekeleza kwa vitendo ahadi yake ya kuhakikisha huduma za uzazi zinapatikana bila gharama, kama ilivyoainishwa katika sera ya afya ya taifa.

Serikali iharakishe utekelezaji wa mfumo wa kuwaunganisha watanzania na Hifadhi ya Jamii na kutoa bima ya afya kwa wote ili kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma za afya bila ubaguzi wa kifedha.

ACT Wazalendo inaendelea kusimama kidete kuhakikisha kuwa huduma za afya si bidhaa ya kibiashara, bali ni haki inayopaswa kutolewa kwa kila mwananchi kwa heshima na utu.

Dkt. Elizabeth Benedict Sanga
Waziri Kivuli wa Afya
ACT Wazalendo
26 Januari, 2024
Naku baliana nao
 
Kiti ya kujifungulia hazina hata bei sijui alifikiri nini yaani kutuma Tsh 50,000 kwa mgonjwa mambo mengine yaende kaona tabu mbona watu tunatoa zaidi ya hizo mtu akikwambia matatizo yake..
Screenshot_20250126-223355.jpg
 
Back
Top Bottom