Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,336
- 4,731
TAARIAFA KWA UMMA
Ndugu waandishi wa Habari. Awali ya yote hatuna budi kumshukuru Mwenye ezi Mungu, Muumba wa mbingu na ardhi kwa kutujaalia tukawa katika hali ya uzima wa Afya na muda huu kujumuika pamoja hapa. Ingawa tumewaita muda mfupi uliopita, lakini bado mmejali na kuitikia wito wetu huu na kuja hapa ili kutusikiliza na kutupelekea taarifa zetu hizi kwa umma wa Wazanzibari na wapenda demokrasia ulimwenguni.
Ndugu waandishi wa habari, kama mnavyojua kwamba leo ndio siku ya mwisho ya Uchukuaji na Urejeshaji wa Fomu za kuomba kuteuliwa katika nafasi za Urais wa Zanzibar, Uwakilishi na Udiwani kwenye Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC). Wagombea wetu wa nafasi hizo tayari wamerudisha fomu zao.
Kilichotufanya tuwaite ni kwamba tunazo taarifa za kuaminika za mipango na njama ovu zilizoandaliwa na kuratibiwa kwa pamoja kati ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) na katika baadhi ya maeneo kuwahusisha maofisa waandamizi wa Serikali katika taasisi mbali mbali. Njama hizo ni za kuwawekea pingamizi wagombea wetu katika majimbo ambayo CCM wana uhakika hawawezi kushinda, lengo likiwa ni kuwaondoa wagombea wetu katika Uchaguzi kama ambavyo wamefanya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). Mapingamizi hayo ni katika majimbo yote kumi na nane (18) ya Pemba, lakini hasa mkakati wao na njama zao wakizitilia mkazo kwa wagombea wafuatao:-
1. Abubakar Khamis Bakary – Jimbo la Pandani
2. Said Ali Mbarouk - Jimbo la Gando
3. Omar Ali Shehe - Jimbo la Chake Chake
4. Seif Khamis Mohamed - Jimbo la Mkoani
5. Hija Hassan Hija - Jimbo la Kiwani
6. Subeti Khamis Faki - Jimbo la Micheweni
7. Hamad Masoud Hamad - Jimbo la Ole
Kwa upande wa Unguja, mpango huo pia umepangwa kutekelezwa katika Wilaya ya Kaskazini A, Wilaya ya Magharibi A na B na wilaya ya Mjini, laki hasa mkakati wao na njama zao wakizitilia mkazo kwa wagombea wafuatao:-
1. Nassor Ahmed Mazrui - Jimbo la Mwera
2. Juma Duni Haji - Jimbo la Mtoni
3. Nassor Ali Amour - Jimbo la Chumbuni
4. Ismail Jussa Ladhu - Jimbo la Malindi
5. Abdillah Jihad Hassan - Jimbo la Mwanakwerekwe
6. Hassan Jani Massoud - Jimbo la Nungwi
7. Dr. Haji Ali Mbarouk - Jimbo la Tumbatu
8. Haji Mwadini Makame - Jimbo la Kijini
Ndugu waandishi wa Habari, katika mpango huo tunazo taarifa za kuaminika katika Jimbo la Chumbuni za kumtumia Ndugu Khamis Jabu Mohamed ambaye amefukuzwa katika chama chetu kwa kumkabidhi fomu ya Uwakilishi wa Jimbo la Chumbuni ili kumuondoa Mgombea wetu halali, Ndugu Nassor Ali Amour.
Ndugu waandishi wa Habari, tunawataka Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), kuacha mara moja kupanga mipango hii miovu ya kutaka kuingiza nchi katika machafuko yasiyokuwa ya lazima kwa kuendelea kutumika na kukibeba Chama Cha Mapinduzi wakijua fika kwamba kwa wakati tulionao CCM hakisaidiliki tena kwani wananchi wameshakikataa na uthibitisho wa hilo ni Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ambapo walishindwa kwa aibu.
Hitimisho
Ndugu, Waandishi wa Habari tunaitahadharisha Tume ya Uchaguzi Zanzibar kwa kutaka kuwaondosha wagombea wetu kwa mipango na makosa ya kutengeneza. Tunaitaka Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kwanza wajitathmini wao, ikiwa Tume nzima ya Uchaguzi inayoongozwa na Jaji Mkuu mstaafu wa Zanzibar, na Makamishna ambao wengine ni Majaji wa Mahakama Kuu, kufanya makosa ya kutokuwepo kwa sehemu nzima ya TAMKO LA UTHIBITISHO WA WADHAMINI katika fomu ya uteuzi wa Uwakilishi (na kulazimika kutoa nakala za photocopy leo baada ya Chama chetu cha ACT Wazalendo kuwatanabahisha suala hilo kwa barua jana), wanawezaje kuja kuwaondosha wagombea wetu kwa hujuma au makosa ya kutengeneza?
Tunaitaka Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) ifanye kazi kwa mujibu wa taratibu na sheria za Uchaguzi bila ya kumbeba na kumpendelea yoyote yule na kuheshimu maamuzi ya wananchi kwa kuwapa kile walichokichagua. Hatutakubali wala kuvumilia njama zozote zile ovu zinazoratibiwa kuona zinawaondosha wagombea wetu
Nassor Ahmed Mazrui
Naibu Katibu Mkuu, ACT-Wazalendo
Zanzibar
09/09/2020.
Ndugu waandishi wa Habari. Awali ya yote hatuna budi kumshukuru Mwenye ezi Mungu, Muumba wa mbingu na ardhi kwa kutujaalia tukawa katika hali ya uzima wa Afya na muda huu kujumuika pamoja hapa. Ingawa tumewaita muda mfupi uliopita, lakini bado mmejali na kuitikia wito wetu huu na kuja hapa ili kutusikiliza na kutupelekea taarifa zetu hizi kwa umma wa Wazanzibari na wapenda demokrasia ulimwenguni.
Ndugu waandishi wa habari, kama mnavyojua kwamba leo ndio siku ya mwisho ya Uchukuaji na Urejeshaji wa Fomu za kuomba kuteuliwa katika nafasi za Urais wa Zanzibar, Uwakilishi na Udiwani kwenye Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC). Wagombea wetu wa nafasi hizo tayari wamerudisha fomu zao.
Kilichotufanya tuwaite ni kwamba tunazo taarifa za kuaminika za mipango na njama ovu zilizoandaliwa na kuratibiwa kwa pamoja kati ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) na katika baadhi ya maeneo kuwahusisha maofisa waandamizi wa Serikali katika taasisi mbali mbali. Njama hizo ni za kuwawekea pingamizi wagombea wetu katika majimbo ambayo CCM wana uhakika hawawezi kushinda, lengo likiwa ni kuwaondoa wagombea wetu katika Uchaguzi kama ambavyo wamefanya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). Mapingamizi hayo ni katika majimbo yote kumi na nane (18) ya Pemba, lakini hasa mkakati wao na njama zao wakizitilia mkazo kwa wagombea wafuatao:-
1. Abubakar Khamis Bakary – Jimbo la Pandani
2. Said Ali Mbarouk - Jimbo la Gando
3. Omar Ali Shehe - Jimbo la Chake Chake
4. Seif Khamis Mohamed - Jimbo la Mkoani
5. Hija Hassan Hija - Jimbo la Kiwani
6. Subeti Khamis Faki - Jimbo la Micheweni
7. Hamad Masoud Hamad - Jimbo la Ole
Kwa upande wa Unguja, mpango huo pia umepangwa kutekelezwa katika Wilaya ya Kaskazini A, Wilaya ya Magharibi A na B na wilaya ya Mjini, laki hasa mkakati wao na njama zao wakizitilia mkazo kwa wagombea wafuatao:-
1. Nassor Ahmed Mazrui - Jimbo la Mwera
2. Juma Duni Haji - Jimbo la Mtoni
3. Nassor Ali Amour - Jimbo la Chumbuni
4. Ismail Jussa Ladhu - Jimbo la Malindi
5. Abdillah Jihad Hassan - Jimbo la Mwanakwerekwe
6. Hassan Jani Massoud - Jimbo la Nungwi
7. Dr. Haji Ali Mbarouk - Jimbo la Tumbatu
8. Haji Mwadini Makame - Jimbo la Kijini
Ndugu waandishi wa Habari, katika mpango huo tunazo taarifa za kuaminika katika Jimbo la Chumbuni za kumtumia Ndugu Khamis Jabu Mohamed ambaye amefukuzwa katika chama chetu kwa kumkabidhi fomu ya Uwakilishi wa Jimbo la Chumbuni ili kumuondoa Mgombea wetu halali, Ndugu Nassor Ali Amour.
Ndugu waandishi wa Habari, tunawataka Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), kuacha mara moja kupanga mipango hii miovu ya kutaka kuingiza nchi katika machafuko yasiyokuwa ya lazima kwa kuendelea kutumika na kukibeba Chama Cha Mapinduzi wakijua fika kwamba kwa wakati tulionao CCM hakisaidiliki tena kwani wananchi wameshakikataa na uthibitisho wa hilo ni Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ambapo walishindwa kwa aibu.
Hitimisho
Ndugu, Waandishi wa Habari tunaitahadharisha Tume ya Uchaguzi Zanzibar kwa kutaka kuwaondosha wagombea wetu kwa mipango na makosa ya kutengeneza. Tunaitaka Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kwanza wajitathmini wao, ikiwa Tume nzima ya Uchaguzi inayoongozwa na Jaji Mkuu mstaafu wa Zanzibar, na Makamishna ambao wengine ni Majaji wa Mahakama Kuu, kufanya makosa ya kutokuwepo kwa sehemu nzima ya TAMKO LA UTHIBITISHO WA WADHAMINI katika fomu ya uteuzi wa Uwakilishi (na kulazimika kutoa nakala za photocopy leo baada ya Chama chetu cha ACT Wazalendo kuwatanabahisha suala hilo kwa barua jana), wanawezaje kuja kuwaondosha wagombea wetu kwa hujuma au makosa ya kutengeneza?
Tunaitaka Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) ifanye kazi kwa mujibu wa taratibu na sheria za Uchaguzi bila ya kumbeba na kumpendelea yoyote yule na kuheshimu maamuzi ya wananchi kwa kuwapa kile walichokichagua. Hatutakubali wala kuvumilia njama zozote zile ovu zinazoratibiwa kuona zinawaondosha wagombea wetu
Nassor Ahmed Mazrui
Naibu Katibu Mkuu, ACT-Wazalendo
Zanzibar
09/09/2020.