LGE2024 ACT Wazalendo: Wagombea wetu 51,423 wameenguliwa katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

LGE2024 ACT Wazalendo: Wagombea wetu 51,423 wameenguliwa katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2024-11-11 at 17.03.12_ff13e59d.jpg
Chama cha ACT Wazalendo kinatoa Taarifa kwa Umma kuwa wagombea wake 51423 katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji wameenguliwa kwa sababu ya udhamini wa chama ngazi ya Kata. Wagombea wetu waliogongewa mihuri ya Kata ambayo ndio ngazi ya udhamini ya ACT Wazalendo wameenguliwa katika Wilaya za Temeke, Mkuranga, Kibiti, Rufiji, Majimbo mengi ya Mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na maeneo mengine mengi.

ACT Wazalendo ilimjulisha rasmi Waziri wa TAMISEMI ambaye ndiye Msimamizi Mkuu wa Uchaguzi huu kupitia barua ya Katibu Mkuu ya tarehe 20 Oktoba 2024 yenye Kumbukumbu Namba ACT/HQ/OFKM/011/VOL.III/256. Barua yetu ilifuatia barua ya Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ya tarehe 14 Oktoba 2024 yenye Kumb. Namba CCB.126/215/01/85 ambayo ilielekeza kuwa vyama vya siasa vitaamua vyenyewe ngazi za udhamini za wagombea. Kwa masikitiko makubwa, kwenye baadhi ya maeneo, kupitia mapingamizi yaliyowekwa na wagombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) dhidi ya wagombea wetu, Wasimamizi Wasaidizi wamewaengua wagombea wetu kwenye baadhi ya maeneo hayo kwa kigezo cha kudhaminiwa na ngazi kata.

Ni jambo la kustaajabisha kuwa katika nchi moja, wapo baadhi ya wagombea wetu wameteuliwa kwa kudhaminiwa na ngazi ya kata lakini wengine wengi wametenguliwa. Waziri Mchengerwa amekubali vipi maelekezo yake kupuuzwa?
WITO WETU:

Tunamtaka Waziri wa TAMISEMI Ndugu Mohamed Mchengerwa kutoka hadharani na kuwataka Wasimamizi wa Uchaguzi kuwarejesha wagombea wetu wote walioenguliwa kwa kigezo hiki kwani kuenguliwa kwao ni dharau ya dhahiri kwake kama Mamlaka ya Uchaguzi. Uvumilivu wetu una kikomo.
Rai hii imewasilishwa pia kwa maandishi kwa barua ya Katibu Mkuu jana tarehe 10 Novemba 2024.
Imetolewa na;

Rahma Mwita,
Msemaji wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, ACT Wazalendo. Novemba 11, 2024
 
Kwa ukubwa wa chama hiki, hali ndiyo hiyo 2024.

Je kwa ushahidi huo, 2025 hali itakuwaje ikiwa vyama vikubwa na wananchi wa Tanzania hawatachukua hatua sahihi na stahiki kwa muda huu wa sasa 2024 ?

Mozambique uchaguzi wa Oktoba 2024 ulifanyiwa uchafuzi mkubwa na kupelekea :

 
hivi tanzania ina vijiji mitaa na vitongoji vingapi? mbona wengi sana waliotajwa?
 
Mkome hiyo ni laana ya kushangilia kifo cha Magufuli.
Mtanyooka tu
 
Katibu uenezi, itikadi na elimu wa chama dola kongwe aionya TAMISEMI:

 
Kwa ukubwa wa chama hiki, hali ndiyo hiyo 2024.

Je kwa ushahidi huo, 2025 hali itakuwaje ikiwa vyama vikubwa na wananchi wa Tanzania hawatachukua hatua sahihi na stahiki kwa muda huu wa sasa 2024 ?

Mozambique uchaguzi wa Oktoba 2024 ulifanyiwa uchafuzi mkubwa na kupelekea :

Vyama vinajitahidi sana....wananchi wote wanatakiwa wa chip in...
 
Back
Top Bottom