LGE2024 ACT-Wazalendo: Waliowaengua wagombea wa upinzani wachukuliwe hatua

LGE2024 ACT-Wazalendo: Waliowaengua wagombea wa upinzani wachukuliwe hatua

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

the guardian 17

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
395
Reaction score
570
Chama cha ACTwazalendo kimetoa wito kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa, kusimamia maelekezo yake kuhusu rufani za wagombea ili kuhakikisha kuwa wagombea wa chama hicho waliotenguliwa katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji, na Vitongoji wanarejeshwa mara moja.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, Ado Shaibu Novemba 13, 2024, inasisitiza kuwa TAMISEMI isimamie maelekezo yake kikamilifu kwani katika mchakato huo kumeshuhudiwa Wasimamizi wa Uchaguzi wakidharau maelekezo mahsusi ya kikanuni.

Soma: LGE2024 ACT Wazalendo: Kuna hujuma kubwa imepangwa dhidi ya wagombea wetu

“Ikumbukwe kuwa mnamo tarehe 09 Novemba, 2024 Kiongozi wa Chama chetu alitoa rai kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuingilia kuhakikisha kuwa wagombea wa vyama vya upinzani walioenguliwa wanarejeshwa. Rai hii ilitokana na ukweli kuwa wagombea wetu walienguliwa kwa sababu za kisiasa na siyo sababu za kikanuni”, imeeleza taarifa hiyo.

Chama hicho kinasisitiza kuwa wanataka kuona hatua za haraka zinachukuliwa dhidi ya watendaji ambao wamehusika katika kuwanyima wagombea wao haki ya kushiriki kwenye uchaguzi huu kwa kuwaengua.

“Tunataka kuona hatua za kinidhamu zikichukuliwa kwa watendaji wote wa TAMISEMI waliowaengua wagombea wetu kwa uonevu na ubaguzi. Haitoshi tu wagombea kurejeshwa bali lazima kuwepo na uwajibikaji”,

20241114_061738.jpg
 
Kuwaengua wagombea ni maelekezo ya CCM na serikali yàke, sasa wàtajiçhuliaje hatua wenyewe? Sanasana watapewa asante kwa kutekeleza maagizo ya chàma.
Wa kuchukuwa hàtua ni wao ACT Wazalendo.
 
Chama cha @ACTwazalendo kimetoa wito kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa, kusimamia maelekezo yake kuhusu rufani za wagombea ili kuhakikisha kuwa wagombea wa chama hicho waliotenguliwa katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji, na Vitongoji wanarejeshwa mara moja.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo, @AdoShaibu Novemba 13, 2024, inasisitiza kuwa TAMISEMI isimamie maelekezo yake kikamilifu kwani katika mchakato huo kumeshuhudiwa Wasimamizi wa Uchaguzi wakidharau maelekezo mahsusi ya kikanuni.

Soma: LGE2024 ACT Wazalendo: Kuna hujuma kubwa imepangwa dhidi ya wagombea wetu

“Ikumbukwe kuwa mnamo tarehe 09 Novemba, 2024 Kiongozi wa Chama chetu alitoa rai kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuingilia kuhakikisha kuwa wagombea wa vyama vya upinzani walioenguliwa wanarejeshwa. Rai hii ilitokana na ukweli kuwa wagombea wetu walienguliwa kwa sababu za kisiasa na siyo sababu za kikanuni”, imeeleza taarifa hiyo.

Chama hicho kinasisitiza kuwa wanataka kuona hatua za haraka zinachukuliwa dhidi ya watendaji ambao wamehusika katika kuwanyima wagombea wao haki ya kushiriki kwenye uchaguzi huu kwa kuwaengua.

“Tunataka kuona hatua za kinidhamu zikichukuliwa kwa watendaji wote wa TAMISEMI waliowaengua wagombea wetu kwa uonevu na ubaguzi. Haitoshi tu wagombea kurejeshwa bali lazima kuwepo na uwajibikaji”,

View attachment 3151769
Ni kweli isiishie kwenye majibu rahisi kwamba watanzania hawana elimu, kwanini maswali yanatengenezwa kwa muundo wa kimitego mitego, (in a crooked manner)
 
Back
Top Bottom