Synthesizer
Platinum Member
- Feb 15, 2010
- 12,699
- 22,598
Bunge limtoa adhabu ya juu kabisa kwa kile kinachoonwa ni dharau ya Mpina kwa Spika wa Bunge. Na kwa kifupi sana, bila kutoa maelezo kamati ya maadili imetamka kwamba Bashe hakusema uongo, ikimaanisha kwamba ushahidi alioutoa Bashe, ambao uko wazi sana ni jinsi gani Bashe alidanganya, unaonwa kuwa ni uongo.
Mtu yeyeote mwenye akili timamu atajua ni nini kinachoendelea hapa, na wabungewote wenye akili timamu hawakutaka kumdadili Mpina, kwa kuwa wanajua nini kiko nyuma ya pazia juu ya suala hili la sukari - kulinda wale waliopo juu, ambao waliamua kutumia biashara ya sukari kujifaidisha wao na famiia zao. Kuna baadhi ya Wabunge hata walisema wao wanamwachia Mungu, kwa sababu anaona kila kitu wanachofanya. Kauli ya kumwachia Mungu jambo hili ilipotolewa wabunge wengi waliinamisha vichwa vyao chini kwa aibu na "remorse".
Kwa hiyo basi, hii inamaanisha nini kwa sisi wananchi ambao tunaliona hili kuwa Bunge letu? Kwanza kabisa, ni kwamba Bunge hili limetukana sisi wananchi, limeonyesha wazi haliko na wananchi, bali liko pale kutumikia watu fulani katika ubinafsi na ufisadi wao, katika hujuma yao dhidi ya nchi hii. Pili ni kwamba wananchi tumedharauliwa sana, na hata zaidi wale waliomchagua Mpina kama Mbunge wao. Bunge limeamua kwa makusudi kuwadharau, dharau mbaya kuliko ile Mpina anayosema aliifanya kwa Spika.
Na niwaambie wazi, Spika wa Bunge anatumika tu, na hata kuna tetesi kuwa amekubali kutumiwa kwa sababu ya ahadi anazopewa. Ni mtu wa kuhurumiwa sana. Alitumika wakati wa awamu iliyopita, na anatumika katika awamu hii.
Mwisho niseme wazi, Bunge na serikali wanapaswa kutambua kwamba haya mambo yana mwisho wake, na mwisho wanaotulazimisha wazalendo halisi wa nchi hii tuutafute, hautakuwa mzuri kwao. Hilo ni dhahiri kabisa.
Mtu yeyeote mwenye akili timamu atajua ni nini kinachoendelea hapa, na wabungewote wenye akili timamu hawakutaka kumdadili Mpina, kwa kuwa wanajua nini kiko nyuma ya pazia juu ya suala hili la sukari - kulinda wale waliopo juu, ambao waliamua kutumia biashara ya sukari kujifaidisha wao na famiia zao. Kuna baadhi ya Wabunge hata walisema wao wanamwachia Mungu, kwa sababu anaona kila kitu wanachofanya. Kauli ya kumwachia Mungu jambo hili ilipotolewa wabunge wengi waliinamisha vichwa vyao chini kwa aibu na "remorse".
Kwa hiyo basi, hii inamaanisha nini kwa sisi wananchi ambao tunaliona hili kuwa Bunge letu? Kwanza kabisa, ni kwamba Bunge hili limetukana sisi wananchi, limeonyesha wazi haliko na wananchi, bali liko pale kutumikia watu fulani katika ubinafsi na ufisadi wao, katika hujuma yao dhidi ya nchi hii. Pili ni kwamba wananchi tumedharauliwa sana, na hata zaidi wale waliomchagua Mpina kama Mbunge wao. Bunge limeamua kwa makusudi kuwadharau, dharau mbaya kuliko ile Mpina anayosema aliifanya kwa Spika.
Na niwaambie wazi, Spika wa Bunge anatumika tu, na hata kuna tetesi kuwa amekubali kutumiwa kwa sababu ya ahadi anazopewa. Ni mtu wa kuhurumiwa sana. Alitumika wakati wa awamu iliyopita, na anatumika katika awamu hii.
Mwisho niseme wazi, Bunge na serikali wanapaswa kutambua kwamba haya mambo yana mwisho wake, na mwisho wanaotulazimisha wazalendo halisi wa nchi hii tuutafute, hautakuwa mzuri kwao. Hilo ni dhahiri kabisa.