The answer is simple, "death penalty haina maana".
Tafakari mifano hii:
1. Mtu akiuwa tunataka nasi tumtendee hivyo, yaani tit for tat (jino kwa jino, jicho kwa jicho). Hii ni tafsiri potofu make ni tabia ya kinyama tu kulipiza kuuwa kwa kuuwa, kubaka kwa kubaka. Matokeo yake vifo, ubakaji utaongezeka badala kupungua.
2. Kwa vile kuuwana ni unyama, imetokea mara kadhaa ajira ya kunyonga watu kukosa waajiriwa hasa nchi kama malawi watu hurundikana gerezani wanyongaji hawaonekani. Je wanaoshabikia adhabu hii wapo tayari kwa tenda hii?
3. Adhabu hii ni feki, make kwa kuhofia kutia saini ya kuidhinisha kifo, tangu utawala wa Mkapa, hapa tz hajanyongwa mtu. Ni Nyerere na Mwinyi tu walioidhinisha.
4. Watu wengi hushabikia adhabu hii kwa vile hawahusiki moja kwa moja kama kutia saini na kutia kitanzi shingo ya mtuhumiwa. Mifano michache hapo juu inaonesha ugumu wa jambo hili.
5. Kwa mujibu wa maendeleo na ustaarabu wa kisasa uliotukuka, Haki ya Kuishi kwa Binadamu (Right to life) haiwezi kunyang'anywa na yeyote, regardless kosa lililofanyika. Ndo maana marais wengi wenye kuheshimu hili hawaweki saini.
Hitimisho:Tutumie njia mbadala za kuwafanya wakosaji watumikie adhabu zao huku wakizalisha mali katika magereza ili tukuze uchumi badala ya kushabikia visasi vya kuuwana na kulawitiana.