Adhabu ya viboko shuleni bado ni halali katika nchi angalau 64. Tanzania inang'ara kwa kutozuia viboko

Adhabu ya viboko shuleni bado ni halali katika nchi angalau 64. Tanzania inang'ara kwa kutozuia viboko

Nyani Ngabu na Kiranga kwa Marekani mfumo wa 'mateso' ya viboko kwa wanafunzi upo vipi? Ni 'adhabu' zipi hutolewa?

Sky Eclat na Rebeca 83 mfumo wa 'mateso' ya viboko kwa Uingereza upo vipi? Ni 'adhabu' gani hutolewa?
Marekani ni nchi yenye majimbo 50, hapo sijahesabu territories, na kila jimbo linaweza kuwa na wilaya (counties, boroughs, parishes) nyingi sana. Texas ina wilaya 254 nafikiri ndiyo inaongoza.

Na kila wilaya inaweza kuwa na "wilaya za kishule" tofauti.

Na kila state inaweza kuwa na sheria tofauti, na kila wilaya inaweza kuwa na sheria tofauti, na kila wilaya ya kishule inaweza kuwa na sheria tofauti.

Kwa hiyo hili ni jambo linalokwenda tofauti, angalau kwa jimbo.

Kwa habari zaidi, anzia kwenye wiki ya hili jambo hapa chini

 
Matajiri na wanasiasa wanapeleka watoto wao shule bora ambazo hakuna mambo ya viboko. Watoto wa maskini ndiyo wanapigwa stiki na kuwa watu wazima waogawaoga.
Mkuu wewe unategemea mtoto anayesoma fedha schools,shule ambazo mzazi analipa 10+M mtoto asiwe na nidhamu? Ni muda upi mtoto atamisbehave? Karo yenyewe ni adhabu tosha kwa mzazi na mtoto,

Hebu niambie kwa shule zetu ambazo mtoto inabidi awahi shule asafishe mazingira na shughuli ndogo ndogo za shule azifanye, Leo hii umwambie no sticks hapo si hakuna kitu kitafanyika shuleni,kwanza mtoto mwenyewe asipomuona Mwalimu darasani anashangilia maana hana cha kupoteza,

Nimekuwa Mwalimu for years now lakini naamini mtoto Wa shule za kata hawezi kuwa na nidhamu au kuelekea pale anapoelekezwa bila viboko,nikiwa zamu Mara nyingi watoto wananiona Mimi mpole,zamu Yangu huwa najaribu kufuata haki za watoto eti kuchapa ni dhuruma dhidi ya mtoto na hakika sipendezwi na uchapaji mtoto lakini nakuambia siku Hiyo utakuta watoto wanafika shule saa mbili,unategemea usafi Wa mazingira wafanye walimu?

Ni ngumu mno ,hizo shule mnazosema kuwa hawachapwi watoto,kwanza mtoto hafanyi usafi Wa mazingira,kuna wafuaji Wa nguo zao,ni computerized schools ambapo Mara nyingi mtoto haandiki notes na pia karo zao ni kubwa,sasa ni muda upi Mwalimu atapata nafasi ya kutoa adhabu ?

Waambieni hao watetezi Wa watoto mashuleni huku hali ni ngumu,kuni za kupikia uji Wa shule zinaletwa na mtoto,usafi Wa mazingira unategemea mtoto,maji kwa ajili ya usafi vyooni yanaletwa na mtoto,sasa kama hakuna bakora unadhani haya yataletwa na nani?


Kwa sisi wakiristo tunaamini kuwa

Mithali 23:13

Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.
 
Kwa hawa watoto wa siku hizi kama hutaki adhabu ya viboko mfundishe mwanao nyumbani kwako.

Mnalea watoto vibaya sana halafu, wakifika shule wanatukana walimu, wanawakunjia ngumi walimu, wanapiga wenzao, hawaandiki darasani, hawasomi, WAKIFELI LAWAMA MNAWATUPIA WALIMU.

MFUNDISHE MWANAO NIDHAMU TOKA NYUMBANI, UKISHINDWA TUACHIE TUMNYOOSHE AU BAKI NAE NYUMBANI.
Adhabu sio fimbo tu,ziko adhabu zenye manufaa nyingi tu,kulima bustabi,kupiga deki,kusafisha mazingira ya shule nk
 
Mimi mwalimu naheshimu haki za binadamu sichapi mwanafunzi, simfokei , nafundisha kwa mujibu wa ratiba tu , natoa zoezi kwa mujibu wa miongozo ya wizara , asome asisome afanye mazoezi asifanye Mimi hainihusu , najali Sana salary na biashara zangu mtaani ,
 
Mtoto wa kitanzania anayesoma shule ya kata aliyekulia katikati ya nyumba za singeli au katika jamii iliyopinda huko Tarime uache kumchapa???

Unafikiri kwanini watoto wakienda jeshini wanakuwa na nidhamu sana na ukorofi na ujinga unaisha?

Watoto wachapwe lakini wasipigwe, kuna tofauti ya kuchapa na kupigwa.

Wakiume wachapwe matako, wakike wachapwe mikono lakini kwa idadi sahihi iliyoainishwa.

Hata Biblia inasema usimnyime mtoto viboko.

Muhimu ni usimpige Kofi, ngumi, mateke etc.
 
Nyie wazazi wa siku hizi ndio wapumbavu na kina junia wenu..

Mnaharibu watoto wala msisingizie walimu
 
Hivi njia pekee ya kunyoosha nidhamu ya mtoto ni kwa kumchapa? Mbona zipo njia nyingi tu, kama mzazi hatekelezi nafasi yake vyema muite mzungumze mjue namna mnamsaidia mtoto maana sio wazazi wote ni wqzazi. Kumbuka unasomea ualimu ili kuwa walimu na walezi bora wa watoto ila hakuna shule ya kufundisha kuwa mzazi.

Tusiishie tu kuwalaumu watoto wa sasahivi maana wanafanana na wazazi wa sasa hivi, sasa iweje kosa la mzazi kuzembea kwenye malezi umpe mtoto?

Malezi ni jambo pana sana na halina mbabe, ndio maana kuna watoto wa hao hao walimu wameshindikana, kuna watoto wa wachungaji ni wavuta bangi nk. Hebu tuwe na upendo na utu kwa hawa watoto, wanahitaji upendo kuliko hivyo viboko.
Wewe ni mwalimu, umewahi kutana na mzazi anayekuja shuleni kuongea na walimu baada ya mtoto wake kuadhibiwa?

Watoto wetu tunawalea vibaya sana na wanakuwa watu wa ajabu sana, hakuna kitu wanaogopa zaidi ya kiboko. Na wasipoguswa mwalimu asiyechapa anadharaulika na hasikilizwi.
 
Una mawazo ya kijima kweli kweli. Wewe ni mwalimu? Kama wewe ni mwalimu basi ni janga la Taifa letu. Nawahurumia sana wanafunzi wanaopita kwenye mikono yako. Halafu unaonekana una taizo kubwa sana la lack of exposure. Akili zako ni kama za mwendazake.
Baki na mwanao nyumbani, mawazo ya kijima ni bora kuliko kumlea mtoto wako kama yai na akaja kusumbua walimu shuleni, na hao watoto wenu ndiyo wanaharibu watoto wengine shule sababu watoto wana tabia ya kuiga wenzao.

Mimi ni mwalimu ,na nina exposure kuliko wewe, nimekaa shule miaka mitatu kujifunza jinsi ya kulea mwanafunzi kwa kila umri, Mtoto wa kiafrika anayelelewa kizungu ni janga zaidi kuliko mimi kuwa janga.

Leeni watoto wenu vizuri au baki nao muwafundishe nyumbani kwenu.
 
Kwa hawa watoto wa siku hizi kama hutaki adhabu ya viboko mfundishe mwanao nyumbani kwako.

Mnalea watoto vibaya sana halafu, wakifika shule wanatukana walimu, wanawakunjia ngumi walimu, wanapiga wenzao, hawaandiki darasani, hawasomi, WAKIFELI LAWAMA MNAWATUPIA WALIMU.

MFUNDISHE MWANAO NIDHAMU TOKA NYUMBANI, UKISHINDWA TUACHIE TUMNYOOSHE AU BAKI NAE NYUMBANI.
Na vice versa is true wapo walimu baadhi nao wapo wanaotumia fimbo ili wafanye ngono na watoto na wengine kumalizia hasira za matatizo yao ya ndoa nyumbani. Ukiona mwalimu anachapa sana lazma nyumbani ana matatizo, unakuta mwalimu ana matatizo ya ndoa au ya kiuchumi na hata ya kisaikolojia hasira anamalizia kwa watoto. Adhabu ya viboko ya viboko kwa watoto(below 18yrs) shuleni iendelee lakini iwe na udhibiti kama sheria inavyoolekeza siyo mwalimu kujiamulia idadi ya viboko la sivyo child abuse hususani sexual abuse itatumika hapo.
 
Mimi mwalimu naheshimu haki za binadamu sichapi mwanafunzi, simfokei , nafundisha kwa mujibu wa ratiba tu , natoa zoezi kwa mujibu wa miongozo ya wizara , asome asisome afanye mazoezi asifanye Mimi hainihusu , najali Sana salary na biashara zangu mtaani ,
[emoji1787][emoji1787]mwalimu ukiwaza hivi kama wazazi wajinga na walioshindikana enzi zao wanavyowaza,utapata dhambi kwa Mungu na mtoto huyu baadae atakuja kukulaani sana kwanini ulimuachia akafanya anavyotaka.

jana ilizuka mada kijiweni,kuna mwalimu alikuwa anafanya kama wewe,hapigi mtoto wa mtu,ila akitoa kazi wanaofanya anawanakili sehemu,akarudia kama mara kadhaa akapata wanafunzi wake kadhaa wa kweli,waliobaki akawaamuru wawe wanatona nje akiingia.
mkuu wa shule nayeye akiwakuta nje anapita tu na kuwasalimia,baada ya kama mwezi hivi wakaanza kuulizana hatma yao[emoji23][emoji23].wakaona hapa tunapigwa fimbo kali kuliko fimbo zenyewe.
 
Na vice versa is true wapo walimu baadhi nao wapo wanaotumia fimbo ili wafanye ngono na watoto na wengine kumalizia hasira za matatizo yao ya ndoa nyumbani. Ukiona mwalimu anachapa sana lazma nyumbani ana matatizo, unakuta mwalimu ana matatizo ya ndoa au ya kiuchumi na hata ya kisaikolojia hasira anamalizia kwa watoto. Adhabu ya viboko ya viboko kwa watoto(below 18yrs) shuleni iendelee lakini iwe na udhibiti kama sheria inavyoolekeza siyo mwalimu kujiamulia idadi ya viboko la sivyo child abuse hususani sexual abuse itatumika hapo.
tuache sheria itadeal na watu wa namna hii.

muhimu jitahidi kumfanya mwanao kuwa na tabia malaya,mabayo itamwezesha kuishi na kila mtu.
hata mwalimu mwenye matatizo kwake hapigi mtoto mtiifu,si ndio!!!!!

unalea litoto kama yai,wataliua huko nje.wengine hawapendi ujinga.kama sio waalimu basi polisi.
 
Adhabu ya viboko kwa Watoto wetu wa kiafrika inafundisha Ila labda serikali ingetoa muongozo mwisho vingapi na wachapwe wapi.

Nikiwa Secondary Kuna teacher Alinichapa viboko Non stop, bila idadi. Nilivimba mikono wiki nzima kula siwezi ama kushika kitu chochote. Mikono ilikuwa inaganda Kama ya roboti, Yule teacher Hadi leo ninakinyongo nae.
Pole sana hata miye kuna mwalimu nna hasira naye hadi leo more than 20yrs..Serikali ilishatoa sheria na mwongozo zamanìiiii lakini haifuatwi mfano viboko mwisho ni vitatu na mwalimu wa kiume haruhusiwi kumchapa mwanafunzi wa kike, na kila adhabu ya viboko lazma mwalimu mkuu aidhinishe kwa maandishi nk nk lakini hakuna kinachofuatwa ni holela holela hadi walimu wachapaji wanatumia kama gia ya kubaka mabinti.
 
Back
Top Bottom