Pre GE2025 Ado Shaibu: Atakayehamia ACT Wazalendo ataruhusiwa kugombea Urais

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Katibu Mkuu wa chama cha ACT Wazalendo, Ado Shaibu amesema chama hicho kitampa nafasi mtu yeyote atakayehamia kuweza kugombea nafasi ya Urais.

Ado amesema taratibu za chama hicho zinasema mtu akishakuwa mwanachama anaruhusiwa kutangaza nia na taratibu zingine za usaili zikifanyika na zikampitisha basi ataweza kuwa Mgombea Urais.

"Mimi nina imani hata sasa kwa wapiganaji wengi wakifanya uchambuzi wa jukwaa mbadala katika mapambano bila shaka jibu litakuwa ACT Wazalendo tutawapa nafasi ya kugombea Urais, urais ni haki ya mwanachama kila mwanachama anaruhusiwa kutangaza nia" amesema Ado

Your browser is not able to display this video.
 
Wao hawana Mgombea?
Basi Wamkaribishe Mwenyekiti wa Zamani Mh Freeman
 
MBOWE atajiunga ACT Wazalendo , ndio akili zenu za CCM B zinavyowadanganya? Miaka yote hamjaandaa mgombea urais mnasubiri CHADEMA ipasuke, mtangoja milele nyie watu dhalimu na waovu
 
kumbe rahisi hivi basi kesho najiunga nipeni hiyo tiketi ya uraisi
 
Kumekucha
 
Chenga ya mwili hiyo! Lowasa aliokuwa na mfuko wa kununua hiyo nafasi, TL anao? Isije ikawa kama ule wimbo wa mwanameka ee...au wimbo wa solemba solemba...
 
Zitto akiwa Chadema alikuwa akilalamika kunywa nafasi ya kugombea urais, Ila kwenye chama alichoanzisha mwenyewe anashindwa kugombea.
Hayo ni maajabu nane ya dunia.
Alihama CDM na sasa inaonekana anatengeza mazingira ili yule mtunza nidhamu wa cdm aje agombee na aipaishe ACT Wazalendo.. ndiko tunako elekea huko kwa kweli...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…