Adolf Hitler na ndoto ya kuitawala dunia

Adolf Hitler na ndoto ya kuitawala dunia

Hitler alitaka kugeuza meza kuua influence ya Uingereza na Washirika wake na kujiweka yeye na washirika wake Hasa Italy then Japan.

That's why aliwashambulia wote waliokuwa pro UK.

Japan walikuwa na vision yao ya Pacific walikuja kushirikiana na Hitler kwa sababu ya kuwa na adui mmoja. Russia, French na US. Kwa Manchuria, Indonesia na Pacific kwa mfuatano.

Acha kusoma vitu shallow Shallow,
Ugomvi wa Uingereza na Ujerumani umeanza hata kabla ya Hitler kuwepo. Alichokifanya Hitler ni mwendelezo wa ndoto za wakina Chancellor Otto Von Bismarck na The Kaiser.

Tatizo la zile vita za dunia lilikuwa siyo Hitler, Kaiser Wilhelm, Mussolini, General Franco au Ufashisti. Tatizo lilikuwa ni mfumo wa Siasa na Kiuchumi ambao ndiyo uliigawa dunia na kupeleka machafuko huko Barani Ulaya.

Professor Frantz Fanon anasema hivi,
"World War One was a terrible miscalculation of the imperialist powers" hivyo chanzo cha matatizo yote yale Ulaya ni Imperialism tu. (Uchumi, Uchumi, Uchumi)

Ukisoma vizuri Historia utagundua vitu vichache tu, ambavyo wewe hapa hujaviweka aidha kwa maksudi au kutokujua:

Mosi,
Mnamo Karne ya 19 hadi 20 mfumo wa Uchumi wa dunia ulikuw ni Ubepari. Ndugu zangu wajamaa wanasema Imperialism. Sasa katika Imperialism kuna kitu wanazuoni wanakiita The Basic Feature of the mode of Production.

The Export of Capital and Maximization of Profit were the Basic Features of Imperialism. Hivyo ili mataifa ya Ulaya yaweze kuishi na kutajirika ni lazima yapeleke mitaji yao nje ya mabara ya Ulaya na kuuza.

Sambamba na hilo,
Ili utajirike haraka ulihitaji Area for Investment, Cheap Labor na Unchallenged Market. Hapa taifa linajenga kitu kinachoitwa Colonial Economy. Hivyo taifa lenye viwanda lifanikiwe kuishi katika dunia ni lazima liwe na makoloni.

Ujerumani alikuwa na makoloni,
Baada ya vita wakamnyang'anganya uchumi wake ukadorora ndiyo wakina Adolf Hitler wakatokea. (Hitler was not the cause of the crises, but the effect of a failed economic system that defined world politics in the 20 Century)

Hata asingetokea Hitler nakuhakikishia The World was already doomed to war. Wangetokea wendawazimu wengine tu kwasababu Tatizo la Imperiali lilikuwa halijatibiwa na The Versailles Peace Treaty na The League of Nations.

NB: Hitler asingetokea basi vita y Pili ya Dunia ingepiganwa baina ya Mabepari wa Ulaya na Wakomunisti wa Urusi.

Lazima ukumbuke kwamba Wakina Trotsky, Lenin na Stalin wote walikuwa na mpango wa kusambaza ukomunisti dunia nzima kwa njia ya vita (Soma Speech ya Hitler siku anatangaza vita dhidi ya Urusi). Ilibaki kidogo sana Ujerumani, Italia na Uhispania wawe Wakomunisti lakini wafashisti wakawawahi.

NB: Hii ni historia ya form two bwana.
Vipi umeshasahau ???
Teh teh teh teh
 
Naona umetoka Jukwaa la siasa sikukujibu, umenifuata huku. Naona sasa unatafuta sana kujibiwa na mimi. Haya ngoa nikijibu kitaalamu tu:

Mosi,
Hakuna Super power isiyokuwa na ushawishi katika siasa, uchumi na tamadumi za mataifa mengine duniani. Umelitazama hili katika mawazo butu mnoo: Nchi kubwa kama Marekani haiihitaji kutawala mipaka yote ya dunia ili tuseme linatawala dunia,...kwenye sayansi ya siasa kuna kitu wanakiita Hegemonic Power.

Ambapo taifa moja kubwa halitawali taifa jingine moja kwa moja bali kwa kupitia ushawishi. Mfano mzuri tu, Dola la Rumi halikuwa na mipaka dunia yote lakini lilikuwa na maamuzi mazito kiuchumi, kibiashara na kitamaduni kwa karibia mataifa mengi sana duniani. Hapa naongelea Civilised Nations of Europe, Asia, Africa and Central Asia.

Kipindi cha vita Baridi Kulikuwa na kitu kinaitwa Structural Theory of The Balance of Power. Dunia nzima iligawanywa katika kambi mbili kuu. Ile ya Wakilomunisti chini ya Urusi na Ile wabeapari chini ya Wamarekani.

Warusi na Warekani hawakufika Tanzania lakini maamuzi ya Moscow au Washington yalikuwa yanaathiri maisha yetu kiuchumi, kisiasa na kitamaduni. (This is purely hegemonial influence)

Pili,
Kama unajua kabisa Hitler alitaka kuunganisha Ulaya kama Dola la Mrumi basi nilitegemea kwamba ungejua kwamba Ulaya iliyo chini ya The Third Reich ndiyo ingetawala dunia.

Ni lazima ujue kwamba kama Hitler angempiga Urusi kwenye The Great Patriotic War 1941-1945 basi leo hii yeye angetawala dunia kwasababu kusingekuwa na mtu wa kumpinga kimaamuzi hapa duniani.

Kitabu cha The Rise and Fall of the Third Reich kiliandikwa na maprofessa wa Marekani ambao walipewa ruhusu kupitia nyaraka zaidi ya 30000 za Wanazi zinasema kwamba Hitler aliwadanganya Wajapani wajiunge naye na akawa anawaza baada ya kupiga Ulaya avamie Japan au The Empire of the rising sun.

Hebu pitia vizuri mambo kabla ya kuleta ubishi mkuu.

Tatu,
Umeshau ukweli wa muhimu sana ambao unathibitisha kwamba Hitler alitaka kutawala dunia. Ukweli ni kwamba mnamo karne ya 20 hasa kuanzia miaka ya 1945 hadi kufikia 1845. Mataifa ya Ulaya yalikuwa na Uchumi wa Makoloni....

Hitler angeyapiga mataifa yote ya Ulaya na yakakubali kukaa chini yake basi ni lazima angerithi na makoloni yote ya duniani.

Haya nikupe mfano mzuri tu,
Baada ya Vita ya Kwanza ya dunia kuisha Ujerumani alipewa adhabu kule Ufaransa kupitia mkutano wa Versailles Peace Treaty ambapo moja ya adhabu ilikuwa kunyanganywa makolono yake yote duniani.

Hivyo nilitegemea kwamba wewe ungefahamu kwamba Hitler angewapiga Waingereza, Wafarasansa, Wabelgiji, Wareno na Wamarekani huko Ulaya ni dhahiri kabisa angetawala dunia nzima kwasababu angerithi na makoloni yao.

Haya sasa,
Kipindi hicho cha vita ya kwanza na ya pili ya dunia. Muunganiko wa falme za Uingereza au The British Empire pekee alikuwa ana miliki Asilimia 20% ya Ardhi ya dunia, kuanzia Africa, Amerika na Asia. Hivyo kama Hitler angemshinda Muingereza pekee basi angejichukulia nchi kama Canada, India, Pakistan, Ghana, Tanganyika,Kenya, Uganda, Zimbabwe, Misri, Malawi, Zambia na Vijisiwa vingi hapa duniani.

Wewe unahisi huku siyo kutawala dunia ???

Haya angempiga Mfaransa pekee kabisaa,
Angejinyakulia Algeria, Vietnam,Burma, Central African Republic na mengineyo uyatafute.

Angempiga Ubelgiji pekee,
Angerithi koloni la Congo DRC.
Kifupi angepiga Ulaya yote ile basi angetawala Makoloni ya Afrika yote.

Sasa mtu mwenye yoyote makini ni lazima angeangalia madhara makubwa ya Hitler kutawala Ulaya pekee basi angetawala nusu ya dunia na Utajiri wake, kitu amacho kingemfanya atawale dunia nzima.

Nne,
Kuna kiti wanakiita The Mother Heart Theory,
Iliandikwa na mwanasayansi wa Siasa wa Uingereza ainyeitwa Sir Harlford McKinder, ambaye anasema Yeyote atakeyevunja nguvu ya Urusi basi atatawala karibia bara lote la Asia.
Huyu ndiye mwalimu wa Siasa wa Henry Kissinger. (The notorious cold Warrior)

Hujiulizi kwanini Hitler alitumia nguvu sana kuvamia Urusi na Uingereza ?? Wao ndiyo walikuwa na rasilimali nyingi sana duniani.

Urusi ingeanguka basi wakati ule basi Hitler angepata rasilimali nyingi sana za kuweza kuvamia Marekani na makoloni ya Afrika.

NB:Ndiyo maana asilimia 80% ya silaha zote za Wanazi zilitumika Urusi. Jiulize kwanini hakuzitumia Ulaya amalize kazo tu ??

Tano,
Usidanganyike na kilichoandikwa kwenye vitabu, jifunze kupima vitu kwa mapana zaidi. Hitler alikuwa ni mdanganyifu na mwenye mbinu mbaya sanaa na ovu.

NB:Kama angekuwa na nia ya kuifanya Ujerumani Super Power barani Ulaya, basi ni dhahiri kwamba angeheshimu Mkataba wa Molotov-Ribbentrop Pact wa mwaka 1949 ambao walikubaliana na Urusi kwamba hatavamia kwenda Mashariki kwa Poland. Kumbe ni mwongo na anaanda kitu kinaitwa The March to the East.

Mfano mwingine,
Kama Hitler alikuwa hana mpango wa kutawala dunia basi APPEASEMENT POLICY ya Waziri Mkuu wa Uingereza Neville Chamberlain ingefanikiwa kwa asilimia 100%. Wajerumani walivamia The Rhine Land, wakavamia Czechoslovakia, Uhispania na dunia ikasema tuwape kwasababu wataishia hapo. Hitler anataka kutawala hapo tu..

Nakuuliza sasa,
Je, Hitler aliishia hapo ambapo alikubaliana kwenye makaratasi na wenzake ???


Sita,
Ujerumani kama angevamia Japana wakati ule basi ni lazima angejipatia Uchina, Taiwan na Korea zote mbili ambazo zilikuwa ni sehemu muhimu kwa Ufalme wa Japan.

Hivyo basi,
Angetawala dunia yote kwa mkakati wa kusema "Shoot the head and the body will fall"

Saba,
Umesahau tena fact za muhimu.
Ujerumani ilikuwa Super Power tangu kipindi cha Prussia hadi kufikoa kwenye Franco-Prussian War of 1871. Kiufupi yeye ndiye alikuwa ni taifa lenye nguvu sana duniani hadi kufikia mwaka 1914. Miaka miwili ya vita ya kwanza ya dunia Ujerumani alishashinda vita na Muingereza alishajipanga kusalimu Amri.

Blunder la Arthur Zimmerman waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani ndilo lilifanya Marekani aingie vitani. Wazayuni wakipigia debu sana vita iendelee.

Hivyo hoja yako hapa haina mashiko kabisa na nyepesi sanaaaaaaaa.............

Nane,
Nithibitishie kwamba Hitler angeshinda vita basi angeyaacha Makoloni yote ya Mahasimu wake na kitutangazia uhuru....

Nithibitishie kwamba Hitler angeshinda vita basia asingetamani kumvamia Marekani kwa kutumia Japan na Mexico kama alivyopanga kuitumia Mexico kwenye vita ya kwanza ya dunia. Akiwaahidi Mexico kwamba wakimvamia Marekani basi angewarudishia majimbo yao ya Texas, California na Nevada.

NB: Soma The Zimmerman Telegram

Mkuu nakushauri ufanye utafiti kabla ya kukurupula kujibu hizi hoja hapa.......

CC: Consigliere, zitto junior, Red Giant
Asante Kunijibu, unajua nakukubali uko mbobezi kweli kweli. Ubarikiwe mwaka 2018. Shida yako uko too bookish and narrow analytical

Majibu yako ni matokeo ya Mpishi ya Anti Hitlers.

Nashangaa unaamini German hawana haki ya kupigania u Super Power.

Nikupe story Kwanza.

Nikiwa chuo miaka 10 iliyopita Mwalimu wangu aliuuza swali kila Mwanafunzi aseme nchi gani itakuwa next Superpower baada ya US.

Mimi nilisema German. Wengine wengi Russia. Yeye Mwalimu akasema China.

Nirudi kwenye mada.

Sababu za World war 2. Ni German kutaka kuwa Super power haraka..

Hitler alivutiwa na Roman empire ndo sababu hata utawala wake akauita third Reich.

First Reich ikiwa ni Roman Empire.
Second Reich Ukiwa German Empire ya Enzi za Bismarck.
Third Reich ni Yake German ya Hitler.

Sasa jiulize Je. First Reich na Second Reich zilitawala Dunia. Jibu common ni hapana tawala hizi nilikuwa na Nguvu kuwa kwa wakati wao..

Kwa ndoto hiyo vita ilikuwa haiepukiki kwani vikwazo vikubwa kuipata Third Reich ilikuwa ni influence ya Uingereza, Us na Russia.

Hivyo alizishambulia nchi hizo lengo likiwa kupindua na kuweka vibaraka wake.

Hii ni kama US ilivyofanya Japan, Korea na nk. Kwani US wanatawala Japan. Lah... Walimufanya Hirohito puppet WAP hadi akakana Yeye si Mungu.

Waliokuwa na Vision ya kutawala kikoloni ni Wajapan.

Waingereza ndo Wachawi wa Wajeruman. All the time wanabifu la Millennium. Si unaona baada ya German kuwa na influence zaidi yao wanakimbi EU.

Team German tunajua ikianguka US influence yote ya West inakuwa Mapegani mwa German.

Kisha mtiti wa Stalingrad unarudiwa. Hahaha

Nisemehe kwa kuweka kasitory.
 
Acha kusoma vitu shallow Shallow,
Ugomvi wa Uingereza na Ujerumani umeanza hata kabla ya Hitler kuwepo. Alichokifanya Hitler ni mwendelezo wa ndoto za wakina Chancellor Otto Von Bismarck na The Kaiser.

Tatizo la zile vita za dunia lilikuwa siyo Hitler, Kaiser Wilhelm, Mussolini, General Franco au Ufashisti. Tatizo lilikuwa ni mfumo wa Siasa na Kiuchumi ambao ndiyo uliigawa dunia na kupeleka machafuko huko Barani Ulaya.

Professor Frantz Fanon anasema hivi,
"World War One was a terrible miscalculation of the imperialist powers" hivyo chanzo cha matatizo yote yale Ulaya ni Imperialism tu. (Uchumi, Uchumi, Uchumi)

Ukisoma vizuri Historia utagundua vitu vichache tu, ambavyo wewe hapa hujaviweka aidha kwa maksudi au kutokujua:

Mosi,
Mnamo Karne ya 19 hadi 20 mfumo wa Uchumi wa dunia ulikuw ni Ubepari. Ndugu zangu wajamaa wanasema Imperialism. Sasa katika Imperialism kuna kitu wanazuoni wanakiita The Basic Feature of the mode of Production.

The Export of Capital and Maximization of Profit were the Basic Features of Imperialism. Hivyo ili mataifa ya Ulaya yaweze kuishi na kutajirika ni lazima yapeleke mitaji yao nje ya mabara ya Ulaya na kuuza.

Sambamba na hilo,
Ili utajirike haraka ulihitaji Area for Investment, Cheap Labor na Unchallenged Market. Hapa taifa linajenga kitu kinachoitwa Colonial Economy. Hivyo taifa lenye viwanda lifanikiwe kuishi katika dunia ni lazima liwe na makoloni.

Ujerumani alikuwa na makoloni,
Baada ya vita wakamnyang'anganya uchumi wake ukadorora ndiyo wakina Adolf Hitler wakatokea. (Hitler was not the cause of the crises, but the effect of a failed economic system that defined world politics in the 20 Century)

Hata asingetokea Hitler nakuhakikishia The World was already doomed to war. Wangetokea wendawazimu wengine tu kwasababu Tatizo la Imperiali lilikuwa halijatibiwa na The Versailles Peace Treaty na The League of Nations.

NB: Hitler asingetokea basi vita y Pili ya Dunia ingepiganwa baina ya Mabepari wa Ulaya na Wakomunisti wa Urusi.

Lazima ukumbuke kwamba Wakina Trotsky, Lenin na Stalin wote walikuwa na mpango wa kusambaza ukomunisti dunia nzima kwa njia ya vita (Soma Speech ya Hitler siku anatangaza vita dhidi ya Urusi). Ilibaki kidogo sana Ujerumani, Italia na Uhispania wawe Wakomunisti lakini wafashisti wakawawahi.

NB: Hii ni historia ya form two bwana.
Vipi umeshasahau ???
Teh teh teh teh
Kitu unasahau.

Ukiyachambua mataifa makuu katika WWii. Yaani German, Us UK na Japan. Ukiyatazama moja moja ukatoa miungano na urafiki.

Hakuna taifa nilikuwa na uwezo kwenda vitani na german peke yake kwa Mwezi mmoja bila kuanguswa.

German ndo ilikua taifa kuu kiuchumi na kitekinolojia shida ilikuwa halina ushawishi kidiplomasia.

Hivyo sababu za kiuchumi ni dhaifu sana.

Sababu kuu ni ideology ya kutaka ukuu kidunia.

Nakwambia Russia ingeangushwa kama si US Na UK.
 
Kitu unasahau.

Ukiyachambua mataifa makuu katika WWii. Yaani German, Us UK na Japan. Ukiyatazama moja moja ukatoa miungano na urafiki.

Hakuna taifa nilikuwa na uwezo kwenda vitani na german peke yake kwa Mwezi mmoja bila kuanguswa.

German ndo ilikua taifa kuu kiuchumi na kitekinolojia shida ilikuwa halina ushawishi kidiplomasia.

Hivyo sababu za kiuchumi ni dhaifu sana.

Sababu kuu ni ideology ya kutaka ukuu kidunia.

Nakwambia Russia ingeangushwa kama si US Na UK.

Sababu ya kiuchumi ni dhaifu ???
Kweli kabisa na wewe umejiaminisha hili ???
Teh teh teh, now i see the problem........

Umeamini kabisa kwamba Ideology tuu ndiyo ilisababisha Ujerumani kutaka kutawala yote dunia na kuanzisha vita za dunia ???

Uwe na siku njema mkuu......
 
Kiongozi wa Chama cha Kisoshalisti kilichojulikana kama ‘NAZI’, Adolf Hitler (1889-1945) alikuwa mmoja wa madikteta dhalimu na wenye nguvu kuwahi kutokea katika karne ya 20.
Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia mbabe huyo aliamka kwa nguvu kupitia chama hicho cha Wafanyakazi wa Ujerumani na kuchukua udhibiti wa Serikali ya Ujerumani mwaka 1933.
Hitler aliamuru uanzishwaji wa kambi za mateso dhidi ya Wayahudi na makundi ya watu wengine, huku akiamini kuwa kufanya hivyo ilikuwa chachu na tishio tosha dhidi ya ukuu wa himaya ya Aryani, na hatimaye kusababisha vifo vya zaidi ya Wayahudi wapatao milioni Sita.
Mashambulizi ya Ujerumani dhidi ya nchi ya Poland mwaka 1939 ndiyo yaliyoanzisha Vita Kuu ya Pili ya Dunia ambapo mpaka kufikia mwaka 1941 Ujerumani iliteka sehemu kubwa ya ardhi ya Ulaya na Afrika Kaskazini.
Ili kuepuka kukamatwa kwa kukwepa utumishi katika jeshi la Austria-Hungary, Adolf Hitler aliondoka kutoka Vienna na kuelekea Munich Mei 1913 lakini baadaye alilazimika kurejea.
Taarifa za kihistoria zinasema kuwa kiongozi huyo wa Nazi alijiunga na Jeshi la Bavaria na kuanza kufanya kazi za kujitolea, ambapo mwaka uliofuata alishiriki kikamilifu katika Vita ya Kwanza ya Dunia akiwa mstari wa mbele upande wa Magharibi ambako uzoefu wake katika vita na mapambano uliathiri mawazo, fikra na mitazamo yake yote baada ya hapo.
Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, Hitler alichukua udhibiti wa chama hicho cha Wafanyakazi wa Ujerumani kama kiongozi, hivyo alidhani kingemwezesha kushika dola ya Ujerumani punde si punde.
Aliposhindwa kwenye jaribio la mapinduzi la mwaka 1923, yeye na wenzake walikamatwa na kufungwa jela na baada ya kutokajela alijitahidi kukijenga chama hicho na kuanza mikakati ya kukamata dola kwa njia zilizo halali.
Hitler alikusudia kufanya mageuzi na kuendesha sera za kibaguzi, ambazo zingetoa nafasi ya kutosha kwa Wajerumani kuweza kuishi katika himaya kubwa duniani.
Kwanza alitabiri ingekuwa rahisi kuiteka Czechoslovakia, na kufuatiwa na Ufaransa ambayo ilikuwa kizingiti kigumu kwa wakati huo na hatimaye kumalizia na nchi ya Uingereza.
Kwa mujibu wa mikakati ya Adolf Hitler, vita ya tatu ingefuata juu ya uvamizi dhidi ya Jumuiya ya Kisovieti ambayo kwake ulikuwa ni mtihani ambao alipanga afaulu kwa kufikiri vita ingepiganwa kwa haraka na kwa urahisi.
Kwa fikra zake za kuipiga Urusi, hii ingempa utajiri wa malighafi za kutosha hususan mafuta ambayo yangemwezesha kuandaa mkakati wa maandalizi ya vita ya nne dhidi ya Marekani.
Vita hiyo ingekuwa rahisi tu kwake endapo Ujerumani ingeweza kuwa na ndege ziwezazo kusafiri masafa marefu pamoja na meli za kivita na kwa upande mwingine ndege za kutosha na jeshi la maji kubwa na imara lingemwezesha kumkabili adui kokote aliko bila umbali kuwa kikwazo.
Mara baada ya Hitler kuingia madarakani mwaka 1933, maandalizi ya Ujerumani kijeshi yalianza kufanyika, hivyo mkazo na mkakati wa muda mfupi ulikuwa kutengeneza silaha kwa ajili ya vita dhidi ya mataifa ya Magharibi, na mkakati wa muda mrefu ulikuwa juu ya uzalishaji wa silaha nzito kwa ajili ya vita dhidi ya Marekani.
Mnamo mwaka 1938, Hitler aliachana na mpango wa uvamizi wa kijeshi dhidi ya Czechoslovakia na kuangalia zaidi makubaliano ya amani na kiongozi wa nchi hiyo, ambayo yalifanyika mjini Munich na hilo lilikuwa kosa lake baya na kubwa kuwahi kulifanya.
Alipoamua kuigeukia Ufaransa na Uingereza, Hitler hakuweza kuishawishi Serikali ya Poland kujiunga na kuwa sehemu ya himaya ya Ujerumani kwa njia za amani ili kuhakikisha hali ya utulivu inakuwapo katika mashariki ya Ulaya, hivyo alichukua uamuzi wa kuivamia na kuiharibu Poland kabla ya kuanza kuzikabili nchi za Magharibi.
Uvamizi wa nchi ya Poland ulikusudiwa kufanyika ifikapo Septemba 1, 1939 lakini ili kufanikisha azma yake hiyo na ushindi wa haraka juu ya Poland kwa kuvunja kila aina ya kikwazo mbele yake, alikusudia kuiingiza Ujerumani katika makubaliano na Urusi ili mwisho wa siku iwe rahisi kwake kuzivamia nchi za Magharibi bila pingamizi lolote baada ya Poland.
Hali kadhalika, Hitler alikusudia kufanya uvamizi dhidi ya mataifa ya Magharibi katika msimu wa baridi mwishoni mwa mwaka 1939, lakini hali mbaya ya hewa ilikuwa ni kikwazo kikubwa ambacho kingeathiri jeshi lake la anga, kwa hiyo aliamua kuahirisha mpango huo na kuhamishia uvamizi huo ifikapo mwanzoni mwa mwaka 1940 katika majira ya joto.
Kutokana na ushauri alioupata kutoka kwa Kamanda Mkuu wa Vikosi vya Wanamaji, Admiral Erich Raeder, juu ya kuivamia na kuiteka Norway ili kuwezesha upatikanaji wa njia rahisi kwa jeshi lake la maji katika Bahari ya Atlantiki kuelekea Kaskazini, aliivamia Norway Aprili 1940.
Baada ya kupokea ushauri tena kutoka kwa Kamanda Mkuu, Erich Von Manstein, lengo la uvamizi kuanzia Kaskazini lilibadilishwa na kuamua kupanga mashambulizi kuelekea nchi zilizoko Kusini mwa Ulaya kwa lengo la kuzuia misaada ya kijeshi kutoka majeshi washirika (allied forces) kuelekea nchi za Ubelgiji na Uholanzi.
Mkakati mpya wa Hitler kwa mara ya kwanza ulionekana kufanya kazi wakati jeshi la Ujerumani lilipofanikiwa kuvunja mstari wa ulinzi wa jeshi la Kifaransa na kufanikiwa ndani ya siku kumi kufika kwenye mkondo wa pwani nyuma ya vikosi vya majeshi washirika.
Baada ya kuonekana wazi kuwa majeshi washirika yaliyokwama yanaweza kutoroka kipigo cha jeshi la Ujerumani, mwelekeo wa silaha na jeshi la Ujerumani ulibadilika tena, lakini jeshi hilo lilikwishachelewa kuweza kuzuia na kufanya mashambulizi dhidi ya askari wa maeshi washirika kwa sababu kikosi maalum cha jeshi la Uingereza na wanajeshi wa Ufaransa walifanikiwa kuokolewa na kutoroka.
Pigo lililotokea mapema Juni 1940 lililosababisha anguko kwa mstari wa mwisho wa ulinzi wa jeshi la Ufaransa, lilikuwa ni ushindi kamili uliompa Hitler furaha na shangwe huku akijua anapata msaada wa kutosha kutoka kwa makamanda na majemedari wake wa kivita, ambao kila mara alikuwa akiwapandisha vyeo na kuwapa namna nyingine za rushwa kama sehemu ya kuwapa motisha ya kuendelea na mapambano.
Taarifa zinasema kuwa kwa sababu ilionekana kama vita hii ilikuwa imeisha baada ya Ujerumani kuiteka Ufaransa, Hitler alianza kupanga mipango mingine kwa ajili ya vita dhidi ya Marekani na Umoja wa Kisovieti.
Julai 11, 1940 Hitler alitoa amri kuanza kwa ujenzi wa jeshi la maji ikiwamo ujenzi wa meli za kivita na ilipofika Julai 31, 1940 baada ya mkakati wa kutaka kuvamia Umoja wa Kisovieti katika msimu wa baridi wa 1940, kutokana na ushauri wa wanajeshi wake, Hitler aliamua kuishambulia Urusi katika majira ya joto mwishoni mwa mwaka 1941.
Wakati Uingereza ikikataa kukubali kushindwa na kusalimu amri, Hitler alipanga kuchanganya hatua tatu ambazo zingehakikisha Uingereza inasalimu amri: kwanza kabisa, jeshi la anga la Ujerumani lingefanya uvamizi na kuharibu uwezo wa Uingereza kujitetea; pili Uingereza ingevamiwa ardhini iwapo kama isingejisalimisha, na tatu ushindi ambao ungepatikana dhidi ya Urusi ungeondoa uwezekano wa Uingereza kupata msaada wowote ule kutoka Urusi, hivyo kuangamia zaidi na kumaliza hatari yoyote dhidi ya Japan, ambayo ingehamasika kusafiri katika Bahari ya Pasifiki na kuivamia Marekani upande wa Magharibi.
Kwa upande mwingine Hitler alitaka Japan kujiunga katika vita na Uingereza na kuahidi kujiunga na Japan katika vita dhidi ya Marekani kama Tokyo ingeona umuhimu juu ya hilo, na hii ingekuwa njia nyingine kwa Ujerumani kupata kuimarisha jeshi la maji dhidi ya Marekani.
Kwenye kampeni dhidi ya eneo la Balkan, kiongozi huyo mbabe wa enzi hizo alikusudia kupata alichoamini kuwa ngome ya upande wa Kusini iliyokuwa katika hali tete, lakini hata hivyo aliona operesheni kubwa ya jeshi la anga katika eneo la Balkani ingekuwa ya gharama ya juu sana kutokana na ugumu wa eneo lenyewe na hivyo kutokusudia kufanya operesheni kama hiyo tena.
Ikumbukwe kuwa uvamizi wa Ujerumani dhidi ya Umoja wa Kisovieti ulianza Juni 22, 1941 ambapo hapo mwanzo uvamizi huo ulionekana kwenda kama ilivyopangwa, lakini ghafla kila kitu kilianza kwenda vibaya – vipigo vya kwanza ambavyo vilikusudia kuangusha Umoja wa Kisovieti ndani ya wiki chache havikuleta matokeo yaliyokusudiwa na hayakuweza kuwa na athari katika nchi hiyo, hivyo baada ya hapo, swali daima lilikuwa kwa Ujerumani ni sekta ipi nyeti na muhimu ishambuliwe ili kuidhoofisha Urusi na sekta gani iachwe.
Katika hali hiyo, Hitler alijikuta mara kwa mara akitofautiana na majenerali wake walioko mstari wa mbele katika kuamua mustakabali wa vita na baada ya vita kuonekana ikiielemea na kuigeukia Ujerumani hali ya kutofautiana kati ya makamanda wa Hitler ilizidi kuongezeka.
Wakati jeshi la Ujerumani likiendelea kurudi nyuma, Hitler alikuwa daima na wasiwasi kuhusu hasara waliyokuwa wakiendelea kuipata ya watu, hali kadhalika ya uharibifu wa vifaa vyake vya kijeshi kwa hiyo baadhi ya majemedari kama Erwin Rommel na Walther Model, mara kwa mara walikuwa wanapingana na amri ya Hitler kwa kurudi nyuma wakati majenerali wengine walikuwa wakirudishwa nyumbani kukusanya kiinua mgongo chao cha kila mwezi na kustaafu kwa kutofautiana na amri za kiongozi wao ingawa wengine walikuwa wakiendelea na kazi zao.
Hitler alifikiri kwamba kushindwa kwa Ujerumani katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia kulitokana na anguko lililotokea katika ardhi ya nyumbani mbele na kwa hivyo kudhani kuwa uanzishwaji wa sera za kidikteta na mauaji ya kukusudiwa ya Wayahudi, ulikuwa uhakika wa ushindi wa vita dhidi ya majeshi washirika, na safari hii Hitler alipoona hana jinsi na majeshi washirika yameshaingia mjini Berlin huku yakiongozwa na Jeshi Jekundu la Urusi, Hitler alijaa hofu ya kisasi ambacho Warusi wangetoa dhidi ya Wajerumani, hivyo aliamua kumuoa mke wake na wote kwa pamoja kuamua kujiua muda mfupi kabla ya jeshi la Urusi kuwasili.
Acheni kupotosha Dunia kuwa kambi za mateso zilifunguliwa kuwatesa wayahudi tu, yeye alizifungua kuwafunga wale ambao walionekana kuwa hawana msaada kwa maana ya kufanya kazi , ubunifu katika tecnolojia nk hata wajerumani waliokuwa legelege waliteswa
 
Back
Top Bottom