Adui wa mwanamke ni mwanamke nimeamini

Adui wa mwanamke ni mwanamke nimeamini

hitler2006

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2014
Posts
489
Reaction score
454
Yanayoendelea katika sakata la ubakaji na ulawiti la clip iliyosambaa mitandaoni yanatafakarisha inawezekanaje haya kutokea katika nchi ambayo kiongozi ni mwanamke, Waziri wa ulinzi mwanamke, Spika wa bunge mwanamke, RPC wa mkoa husika lilikotokea tukio mwanamke

Lakini kinachoshangaza zaidi ni ukimya wa viongozi wote wa wanawake wawe wanasiasa, wanataaluma kama wanahabari na wanasheria.

Kama jamii hatupaswi kuhalalisha na kufumbia macho, matukio kama haya ambayo yanaondoa heshima na kutudunisha kimaadili lakini pia ni lazima jamii isimamie utawala wa sheria na usawa mbele ya sheria kwa mustakabali wa umoja na amani ya jamii yetu

Lakini pia tukumbushane kulea watoto katika maadili yanayomkumbusha mtoto wa kiume kumlinda, kumuheshimu mtoto wa kike maana ni mama au dada huyo

Tukumbushane women are the custodian of life they must be protected.

Over
 
The way forward ni ipi sasa?tuache mambo yalivyo au
 
Sawa sawa na Anna Tibaijuka anavyojigamba mshambulia mama Samia kila siku
 
Ni vigumu kutokua na matatizo ilihali unaishi katika jamii iliyojaa matatizo ni kweli nina matatizo hasa na wanawake wasio na ujasiri wa kupaza sauti wanawake wenzao wanapodhulumiwa,kama na wewe ni mmoja wao wao hata wewe pia ni tatizo...UTTOH 2002
 
Majority ya watanzania ni illiterate yani hawana upeo wa mambo mengi ndo sababu
Wakiongozwa na alieshika hatamu juu kabisa.

Yupo radhi atoe sifa na pesa kwa magoli yanga na simba lakini si kutoa kauli kwa kitendo cha kudhalilishwa binti mdogo.
 
Back
Top Bottom