Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,872
- 34,363
KATIKA hali isiyo ya kawaida mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Ramadhani Kalinywa (35-40) mkazi wa Mlandizi amefariki dunia wakati akichimba kaburi la rafiki yake aliyetambulika kwa jina moja la Rajabu.
Mkasa huo uliotokea Mlandizi Kibaha Pwani juzi, wakati marehemu Kalinywa akiwa na wenzake watatu wakichimba kaburi hilo.
Akisimulia mkasa huo, mmoja wa waombolezaji, mkazi wa eneo hilo aliyejitambulisha kwa jina la Bw. Shaabani Mguta, alisema siku ya tukio marehemu Kalinywa akiwa na wenzake watatu aliowataja kwa majina ya Bw. Bosco Bosco, Bw. Mohamed Juma maarufu kwa jina la 'Mtanzania' na Bw. Juma Mabunduki, walipewa jukumu la kuchimba kaburi hilo baada marehemu Rajabu kufariki.
Kabla ya kuanza kazi hiyo, waliomba pesa za kununulia gongo ili wanywe kwanza kabla ya kuanza kazi hiyo kwa maelezo kwamba marehemu kabla ya kifo chake, aliwaachia wosia kwamba akifa, watakaochimba kaburi lake, lazima wanywe kwanza pombe hiyo.
Ombi hilo lilikataliwa na waombolezaji, ndipo walipoamua kuchangishana wao na kupata sh. 9,000 zilizowawezesha kununua lita tano za gongo.
"Walifika eneo la msiba na kueleza kwamba marehemu rafiki yao (Rajabu) aliwaachia wosia kwamba akifa, kaburi lichimbwe na rafiki zake wa karibu na wote wawe wamekunywa gongo," alisema Bw. Mguta.
Alisema marehemu Rajabu kabla ya kifo chake, alikuwa rafiki wa karibu wa marehemu Kalinywa na walishirikiana katika mambo mengi ikiwa pamoja na kunywa.
Mwombolezaji mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Bw. Hamis Koroboto aliliambia Majira kuwa kabla ya marafiki hao wa marehemu kwenda kuchimba kaburi, aliwaomba wanywe chai na kiporo cha ubwabwa kwanza lakini walikataa jambo hilo.
"Walikuwa wakipokezana, anayetoka shimo anakwenda kuchukua gongo na kunywa huku akisubiri zamu ya kuingia tena kuendelea kuchimba," alisema Bw. Kiroboto.
Alisema baada ya kukamilisha shughuli hiyo
marehemu Kalinywa alikuwa wa kwanza kutoka na kujipumzisha juu ya kaburi lililokuwa pembeni yake.
Baadaye wenzake walitoka na kujipumzisha kando na kutuma taarifa msibani kuwa kaburi limekamilika hivyo mwili wa marehemu Rajab uletwe kuzikwa.
Alisema waombolezaji walipofika na mwili huo makaburini walikumbwa mshangao kukuta wachimba kaburi wote watatu wamelala fofofo na hawajitambui.
"Tulipigwa butwaa ndipo tulijaribu kuwanyanyua kujua kilichowasibu, hatukuamini Kalinywa alikuwa amekufa na wenzake walikuwa taabani wakipumua kwa mbali," alisema Bw. Kiroboto.
Alisema walichoamua ni kumzika kwanza marehemu Rajab na baada ya hapo waliuchukua mwili wa marehemu Kalinywa kuurejesha nyumbani kwa Rajabu kuanza msiba mpya.
"Wakati tukizika wengine waliendelea kupewa huduma ya kwanza, kwa bahati nzuri walizinduka. Baada ya mazishi tulibeba mwili wa marehemu Kalinywa kurudisha nyumbani" alisema.
Mmoja wa waombolezaji waliobaki nyumbani kwa marehemu Rajabu aliyejitambulisha kwa jina la Mzee Mcharazo, alisema baada ya waombolezaji hao kufika wakiwa na machela iliyochukua mwili wa Kalinywa, watu walitaharuki huku baadhi ya akina mama wakijaribu kukimbia kuhofia kulikoni kilichojiri makaburini hadi kurudi na mwili wa marehemu nyumbani.
Habari zaidi kutoka kwa jamaa wa marehemu Kalinywa zilieleza kwamba baada ya mwili huo kuwekwa kwa muda nyumbani kwa msibani hapo ulipelekwa kijijini jirani cha Marangaranga Mzenga alikokuwa akiishi marehemu Kalinywa.
Kamanda wa Polisi MKoa wa Pwani, Bw. Henry Salewi alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo alisema amepata taarifa hizo na jeshi lake linaendelea kufuatilia kupata taarifa zaidi.
Mkasa huo uliotokea Mlandizi Kibaha Pwani juzi, wakati marehemu Kalinywa akiwa na wenzake watatu wakichimba kaburi hilo.
Akisimulia mkasa huo, mmoja wa waombolezaji, mkazi wa eneo hilo aliyejitambulisha kwa jina la Bw. Shaabani Mguta, alisema siku ya tukio marehemu Kalinywa akiwa na wenzake watatu aliowataja kwa majina ya Bw. Bosco Bosco, Bw. Mohamed Juma maarufu kwa jina la 'Mtanzania' na Bw. Juma Mabunduki, walipewa jukumu la kuchimba kaburi hilo baada marehemu Rajabu kufariki.
Kabla ya kuanza kazi hiyo, waliomba pesa za kununulia gongo ili wanywe kwanza kabla ya kuanza kazi hiyo kwa maelezo kwamba marehemu kabla ya kifo chake, aliwaachia wosia kwamba akifa, watakaochimba kaburi lake, lazima wanywe kwanza pombe hiyo.
Ombi hilo lilikataliwa na waombolezaji, ndipo walipoamua kuchangishana wao na kupata sh. 9,000 zilizowawezesha kununua lita tano za gongo.
"Walifika eneo la msiba na kueleza kwamba marehemu rafiki yao (Rajabu) aliwaachia wosia kwamba akifa, kaburi lichimbwe na rafiki zake wa karibu na wote wawe wamekunywa gongo," alisema Bw. Mguta.
Alisema marehemu Rajabu kabla ya kifo chake, alikuwa rafiki wa karibu wa marehemu Kalinywa na walishirikiana katika mambo mengi ikiwa pamoja na kunywa.
Mwombolezaji mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Bw. Hamis Koroboto aliliambia Majira kuwa kabla ya marafiki hao wa marehemu kwenda kuchimba kaburi, aliwaomba wanywe chai na kiporo cha ubwabwa kwanza lakini walikataa jambo hilo.
"Walikuwa wakipokezana, anayetoka shimo anakwenda kuchukua gongo na kunywa huku akisubiri zamu ya kuingia tena kuendelea kuchimba," alisema Bw. Kiroboto.
Alisema baada ya kukamilisha shughuli hiyo
marehemu Kalinywa alikuwa wa kwanza kutoka na kujipumzisha juu ya kaburi lililokuwa pembeni yake.
Baadaye wenzake walitoka na kujipumzisha kando na kutuma taarifa msibani kuwa kaburi limekamilika hivyo mwili wa marehemu Rajab uletwe kuzikwa.
Alisema waombolezaji walipofika na mwili huo makaburini walikumbwa mshangao kukuta wachimba kaburi wote watatu wamelala fofofo na hawajitambui.
"Tulipigwa butwaa ndipo tulijaribu kuwanyanyua kujua kilichowasibu, hatukuamini Kalinywa alikuwa amekufa na wenzake walikuwa taabani wakipumua kwa mbali," alisema Bw. Kiroboto.
Alisema walichoamua ni kumzika kwanza marehemu Rajab na baada ya hapo waliuchukua mwili wa marehemu Kalinywa kuurejesha nyumbani kwa Rajabu kuanza msiba mpya.
"Wakati tukizika wengine waliendelea kupewa huduma ya kwanza, kwa bahati nzuri walizinduka. Baada ya mazishi tulibeba mwili wa marehemu Kalinywa kurudisha nyumbani" alisema.
Mmoja wa waombolezaji waliobaki nyumbani kwa marehemu Rajabu aliyejitambulisha kwa jina la Mzee Mcharazo, alisema baada ya waombolezaji hao kufika wakiwa na machela iliyochukua mwili wa Kalinywa, watu walitaharuki huku baadhi ya akina mama wakijaribu kukimbia kuhofia kulikoni kilichojiri makaburini hadi kurudi na mwili wa marehemu nyumbani.
Habari zaidi kutoka kwa jamaa wa marehemu Kalinywa zilieleza kwamba baada ya mwili huo kuwekwa kwa muda nyumbani kwa msibani hapo ulipelekwa kijijini jirani cha Marangaranga Mzenga alikokuwa akiishi marehemu Kalinywa.
Kamanda wa Polisi MKoa wa Pwani, Bw. Henry Salewi alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo alisema amepata taarifa hizo na jeshi lake linaendelea kufuatilia kupata taarifa zaidi.