Afande Sele: Spika aombe Mirembe wapeleke mabasi yao Bungeni wachukue vichaa wao, waliopo Milembe wana msongo wa mawazo

Afande Sele: Spika aombe Mirembe wapeleke mabasi yao Bungeni wachukue vichaa wao, waliopo Milembe wana msongo wa mawazo

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Mwanamuziki mkongwe wa bongo wa muziki wa kizazi kipya maarufu kama Afande Sele amemuomba spika wa Bunge, Tulia Ackson awaombe hospitali ya Mirembe iliyopo mjini Dodoma wapeleke usafiri bungeni na kuchukua watu wao akidai waliopo Mirembe ni wazima ila wana msongo wa mawazo wa maisha magumu uliosababishwa na watu waliopo Bungeni.

Afande kasema kichaa wa kwanza ni waliopo bungeni akitolea mfano jinsi viongozi wa Serikali wanavyoacha gari linaunguruma ilhali wenyewe wapo kwenye vikao bila kujali kiasi cha mafuta kinachotumika na kuharibika mapema.

Amesema wahusika wameajiriwa na Serikali, wanalipwa na wengine wamesomeshwa na Serikali hiyohiyo. Afande amesema Serikali sio jitu kubwa linalogawa mahela bila sababu bali ni watu wanaohangaika na kuteseka kupitia kodi zao.

Seleman Msindi amesema unaweza kujiona uko 'Smart' kumbe kipa kashaacha goli kitambo

 
Mirembe**

Nilidhani atasema zile sarakasi ni ukichaa.!
 
Mkuu yani hiyo ID yako huwa inanikumbusha moja ya scene inayo vunja mbavu kutoka kwa Reddington

 
Afande alivua nguo jukwaani, kumbe sio ukichaa bali msongo wa mawazo!

Kama supika ataridhia hili, basi dereva wa hilo basi awe yeye Sele.
 
Back
Top Bottom