AFCON: Mambo yamebadilika?

AFCON: Mambo yamebadilika?

Miaka hiyo ya nyuma kama ni kutocheza vizuri, unaona ni timu moja au mbili ila nyingine kubwa zinacheza mpira. Ila mwaka huu wakubwa wote naona kama wanachechemea. Labda tuone gemu zinazofuata.

Ila hoja ya masilahi natofautiana na wewe. Huku national team huwa ni posho tu na huwa hawachukulii kama national team ni sehemu ya kujipatia hela. Hamna mchezaji asiyependa kuimbwa na wakwao. Hata huyo Salah kuna gemu kadhaa muhimu huwa analia wakishindwa. Hivyo hoja ya kutokufanya vizuri kisa masilahi haina mashiko. Labda ungesema mfumo pamoja na wachezaji wanaowazunguka wakiwa national team, sawa.
Wachezaji wa timu za ulaya hawajitumi kuepuka majeruhi. Pesa wanazolipwa ni ndogo ukilinganisha na wanazolipwa ulaya. Afrika habari za uzalendo ni illusion tu kuanzia kwa viongozi, raia mpaka diasporas
 
Sasa unalinganisha ufaransa na afrika. Uko mifumo ya nchi ipo organized hauwezi kulinganisha hali ya ufaransa na huku. Uko hata raia wanaona kodi yao inatumika vozuri wanaona wanathaminiwa ni rahisi kujitolea hapa juzi juzi tu madogo wamerudi na milioni 180 wameishia kupewa 20k kila mmoja halafu next tournament unawaambia wawe wazalendo kweli.!
 
Sasa unalinganisha ufaransa na afrika. Uko mifumo ya nchi ipo organized hauwezi kulinganisha hali ya ufaransa na huku. Uko hata raia wanaona kodi yao inatumika vozuri wanaona wanathaminiwa ni rahisi kujitolea hapa juzi juzi tu madogo wamerudi na milioni 180 wameishia kupewa 20k kila mmoja halafu next tournament unawaambia wawe wazalendo kweli.!
Siyo Ulaya tu hata Afrika
George Wea wakati anacheza alikuwa anajitolea kulipia tiketi ili isafiri, hivi Sadio Mane atahitaji alipwe kiasi gani timu ya taifa?
 
Mkubwa alietegemewa na akapenya mpaka sasa ni senegal pekee, wengine wote wamekaliwa kooni.

Na vile ni mechi 3 tu aisee tutashuuudia vigogo wengi wakiyaaga mashindano.
 
Kila kitu kizuri kilikua zamani! hapa ndio hua nachoka
Hahahaha halafu ukitaka evidence hakuna 😂😂😂
Ukitazama mpira wao kwenye marudio ulikuwa wa ovyo tu 😂😂 ila kutana na wazee wanavyousifia sasa 😂😂😂😂
 
Siyo Ulaya tu hata Afrika
George Wea wakati anacheza alikuwa anajitolea kulipia tiketi ili isafiri, hivi Sadio Mane atahitaji alipwe kiasi gani timu ya taifa?
Ishu sio kutoa pesa ishu ni jitihada zao uwanjani. Pesa mtu anaweza kutoa tu kwa lengo la kujilinda na kupata watetezi pale ambapo jitihada zao uwanjani zitatiliwa mashaka. Hivi jitihada za mbappe ufaransa unaweza kulinganisha na jitihada za mo salah egypt. Mpira anaoupiga anguisa akiwa napoli unaweza kulinganisha na akiwa cameroon? Miaka michache iliyopita walikua na tabia ya kujifanya majeruhi ukifika muda wa afcon baada ya kushtukiwa sasa hivi wanakuja tu kucheza kuepuka lawama uko kwenye ligi wanazocheza hawayataki haya mashindano, rais wa napoli alishawahi kuiponda afcon
 
Hahahaha halafu ukitaka evidence hakuna [emoji23][emoji23][emoji23]
Ukitazama mpira wao kwenye marudio ulikuwa wa ovyo tu [emoji23][emoji23] ila kutana na wazee wanavyousifia sasa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Afcon ya zamani ilikua tamu sana ukilinganisha na hizi za miaka ya karibuni. Tafuta marudio ya mechi za afcon moja hivi kameruni walikua wanavaa jezi hazina mikono. Ingawa nilikua bado mdogo lakini nakumbuka ulipigwa mpira mkubwa sana kwenye ile michuano
 
Ishu sio kutoa pesa ishu ni jitihada zao uwanjani. Pesa mtu anaweza kutoa tu kwa lengo la kujilinda na kupata watetezi pale ambapo jitihada zao uwanjani zitatiliwa mashaka. Hivi jitihada za mbappe ufaransa unaweza kulinganisha na jitihada za mo salah egypt. Mpira anaoupiga anguisa akiwa napoli unaweza kulinganisha na akiwa cameroon? Miaka michache iliyopita walikua na tabia ya kujifanya majeruhi ukifika muda wa afcon baada ya kushtukiwa sasa hivi wanakuja tu kucheza kuepuka lawama uko kwenye ligi wanazocheza hawayataki haya mashindano, rais wa napoli alishawahi kuiponda afcon
Ndiyo maana nilisema tangu mwanzo kucheza timu ya taifa ni uzalendo zaidi kuliko malipo. Jitihada za Mbappe timu ya taifa siyo kwa sababu analipwa posho kubwa sana, haifiki hata robo ya kile anacholipwa PSG
 
Back
Top Bottom