Katika ziara yangu niliyoifanya mwaka jana wilayani mbinga niliandika thread juu ya madudu aliyoyafanya afisa elimu msingi wilaya ya Mbinga bwana David Mathias Mkali kuiba fedha za halmashauri yeye na msaidizi wake afisa elimu vifaa na takwimu bwana Kapinga.
Ile thread niliyoiandika hapa jf kwamba afisa huyo na swaiba wake bwana Kapinga walikuwa wanashirikiana kuchangisha fedha kwa wazazi na kuzitumia kwa matumizi yao binafsi walistahili kufukuzwa kazi wote wawili.
Lakini cha ajabu afisa elimu huyo wa msingi amepewa demotion na ameenda kuripoti shule ya msingi Burundi kata ya Matiri wilaya ya Mbinga kama mwalimu wa kawaida. Hiyo adhabu haitoshi kwani ameiba fedha nyingi na alistahili kufukuzwa yeye na mwizi mwenzake Kapinga wa ofisi ya vifaa na takwimu.
Inakuwaje afisa mwizi aliyekuwa anaingiza fedha kwenye akaunti za shule halafu jioni anawapigia simu walimu wakuu kuzitoa fedha hizo zote na kumpelekea bar yeye na swaiba wake Kapinga, amefanya hivyo kwa shule nyingi tu.
Anawasainisha waratibu posho ya kikao laki saba halafu anawapa bahasha yenye shilingi elfu 35 anawaambia wakafungulie mbele ya safari, atakayelalamika anamvua madaraka, waratibu wengi wamevuliwa madaraka kwa vitendo vyao vya kudai haki zao.
Adhabu aliyopewa huyo afisa elimu msingi ni ndogo na hakuna sababu yoyote ya kumwacha Kapinga pale ofisi ya vifaa na takwimu wakati kuna ushahidi wa wazi kwamba wote ni wezi.
Tunaishukuru JamiiForums, pamekuwa mahali ambapo madudu mengi ya viongozi yanaanikwa hapa na wanaotuhumiwa wanafanyiwa uchunguzi na hatua zinachukuliwa dhidi yao. Kashfa ya escrow zilianzia hapa , kashfa za ajira za Uhamiaji na scandal nyingi tu.
Ile thread niliyoiandika hapa jf kwamba afisa huyo na swaiba wake bwana Kapinga walikuwa wanashirikiana kuchangisha fedha kwa wazazi na kuzitumia kwa matumizi yao binafsi walistahili kufukuzwa kazi wote wawili.
Lakini cha ajabu afisa elimu huyo wa msingi amepewa demotion na ameenda kuripoti shule ya msingi Burundi kata ya Matiri wilaya ya Mbinga kama mwalimu wa kawaida. Hiyo adhabu haitoshi kwani ameiba fedha nyingi na alistahili kufukuzwa yeye na mwizi mwenzake Kapinga wa ofisi ya vifaa na takwimu.
Inakuwaje afisa mwizi aliyekuwa anaingiza fedha kwenye akaunti za shule halafu jioni anawapigia simu walimu wakuu kuzitoa fedha hizo zote na kumpelekea bar yeye na swaiba wake Kapinga, amefanya hivyo kwa shule nyingi tu.
Anawasainisha waratibu posho ya kikao laki saba halafu anawapa bahasha yenye shilingi elfu 35 anawaambia wakafungulie mbele ya safari, atakayelalamika anamvua madaraka, waratibu wengi wamevuliwa madaraka kwa vitendo vyao vya kudai haki zao.
Adhabu aliyopewa huyo afisa elimu msingi ni ndogo na hakuna sababu yoyote ya kumwacha Kapinga pale ofisi ya vifaa na takwimu wakati kuna ushahidi wa wazi kwamba wote ni wezi.
Tunaishukuru JamiiForums, pamekuwa mahali ambapo madudu mengi ya viongozi yanaanikwa hapa na wanaotuhumiwa wanafanyiwa uchunguzi na hatua zinachukuliwa dhidi yao. Kashfa ya escrow zilianzia hapa , kashfa za ajira za Uhamiaji na scandal nyingi tu.