Afisa Mtumishi Mkuu achana na kulazimisha kutumia nguvu kutumia ESS kama kigezo cha kupanda madaraja watumishi. Kwa sasa nchi iko busy na stationery

Mbona kama umepanic,wewe ni computer iliterate nini.

Ifikie mahali watumishinwa umma mjifunze computer.Mnatia aibu,unakuta mwalimu au nesi.Hata excel hajui kutumia.Word anaina maruerue tu.Kila kazi za mfumo mbio stationery,anaacha credential zake pale.Yaani aibu tupu.

Ujinga huo hukuti private sector.Komputer ni nyenzo muhimu sana.

Ila kwa upande wa pili,mifumo mingi ya serikali ni butu sana.Kazi ya dk 3 kwa mkono kwa mfumo nusu saa.Alafu mfumo una milolongo mingi bila hata sababu za msingi.
 
Pepmis imetusumbua sana!

Unajaza task unakuta zimekaa tofauti na ulivyo arrange!

Stressfull yaani ni maumivu sana!!

Madaraja watupandishe TU!!
 
Nasikia wale waliopanda madaraja tayari kwenye mfumo inaonesha au ndo maruweruwe kama kawaida ya mifumo ya TZ?
 
Mfumo huu ni mzuri kinachotakiwa ni kutoa elimu ya kutosha kwa watumishi pamoja na kuwawezesha kuuzoea mfumo!
Ni mfumo ambao utawezesha mtumishi kupata kile anachostahili bila upendeleo.
Mwanzo ni mgumu lakini mwisho huwa mwepesi.
Mwisho tukubali au tusikubali lazima tuendane na mabadiliko ya sayansi na teknolojia yanayotokea duniani.
 
Ni ujinga ujinga tu.
Kama vipi wakanushe tu ule Waraka..
 
Ifikie mahali watumishinwa umma mjifunze computer.Mnatia aibu,unakuta mwalimu au nesi.Hata excel hajui kutumia.Word anaina maruerue tu.Kila kazi za mfumo mbio stationery,anaacha credential zake pale.Yaani aibu tupu.
Wewe Ni hovyo kweli.

Kwahiyo unamlaumu mtumishi. Miaka yake yote kasoma Kinjekitile war. Excel aijuilie wapi!??
 
Reactions: K11
Ila kwa upande wa pili,mifumo mingi ya serikali ni butu sana.Kazi ya dk 3 kwa mkono kwa mfumo nusu saa.Alafu mfumo una milolongo mingi bila hata sababu za msingi.

Hili ndilo tatizo kubwa zaidi, serikali haijawekeza vya kutosha kwenye software infrastructure. Hiyo PEPMIS hata kwa wanaojua kompyuta vizuri kuna wakati inazingua sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…