African countries by vehicles per capital/ per population (Vehicles per 1000 people). Tanzania 7 and Kenya 70

African countries by vehicles per capital/ per population (Vehicles per 1000 people). Tanzania 7 and Kenya 70

Tabutupu

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2010
Posts
13,206
Reaction score
18,549
AFRICAN COUNTRIES BY VEHICLES PER CAPITA/PER POPULATION (Vehicles per 1000 people)

1. Mauritius [emoji1164] 192
2. Botswana [emoji1052] 177
3. South Africa [emoji1221] 174
4. Algeria [emoji1026] 140
5. Tunisia [emoji1249] 129
6. Egypt [emoji1093] 109
7. Namibia [emoji1176] 106
8. Morocco [emoji1173] 103
9. Cape Verde [emoji1065] 101
10. Eswatini [emoji1235] 89
11. Kenya [emoji1139] 70
12. Nigeria [emoji1184] 64
13. Zimbabwe [emoji1269] 60
14. Senegal [emoji1211] 44
15. Ivory Coast [emoji1132] 41
16. Comoros [emoji1076] 33
17. Guinea [emoji1120] 33
18. Angola [emoji1029] 32
19. Ghana [emoji1110] 32
20. Djibouti [emoji1089] 28
21. Madagascar [emoji1155] 27
22. Congo [emoji1077] 27
23. Sudan [emoji1142] 27
24. Togo [emoji1244] 27
25. Congo [emoji1078] 25
26. Benin [emoji1047] 24
27. Zambia [emoji1268] 23
28. Seychelles [emoji1213] 22
29. Burkina Faso [emoji1059] 16
30. Cameroon [emoji1062] 15
31. Gabon [emoji1107] 14
32. Mozambique [emoji1174] 14
33. Liberia [emoji1148] 14
34. E Guinea [emoji1095] 13
35. Uganda [emoji1254] 12
36. Mali [emoji1159] 12
37. Eritrea [emoji1096] 11
38. Mauritania [emoji1163] 10
39. Ethiopia [emoji1098] 9
40. Malawi [emoji1156] 8
41. Tanzania [emoji1241] 7
42. Gambia [emoji1108] 7
43. Niger [emoji1183] 7
44. Burundi [emoji1060] 6
45. Sierra Leone [emoji1214] 6
46. Chad [emoji1205] 6
47. Guinea [emoji1119] 5
48. Rwanda [emoji1206] 5
49. Central African Republic [emoji1068] 4
50. Lesotho [emoji1147] 4
51. Somalia [emoji1220] 3
52. Sao Tome [emoji1209] 2
Source - Statista
 
Ukiona mtanzania kanunua chombo cha usafiri ,ujue kanunua magari mawili (ushuru huko juu mno) ndo mana bado tunaendesha magari ya hovyo........
Ukiona mkenya akinunua gari, jua amenunua gari nne, ive bought cars in both countries, Tanzania gari ni very cheap
 
TRA inataka kodi kubwa kwenye magari kuliko wale waliotengeneza hayo magari, unadhani watu watamudu kununua magari kweli?

Hii nchi mtu kumiliki gari inaonekana anasa wakati hilo ni hitaji muhimu la binadamu kama yalivyo maji au umeme.

Miaka karibu 100 iliyopita Hitler alitamani kila Mjerumani awe na gari na kuelekeza Wahandisi wa Kijerumani kubuni gari ya bei rahisi na yenye kutumia mafuta kidogo ili kila Mjerumani amudu kuinunua na kuendesha ndipo walibuni Volks Wagen....lakini sisi leo bado tunakomoana hatutataki watu wetu wawe na magari. Ajabu sana hii serikali ya ccm imejaa hila na husda kwa watu wake
 
Oyaa! Mdau tuusan mpaka sasa unataka tuendelee kukushawishi nini umuhimu wa barabara kama ile Expressway inayowapa tabu Watz humu.
 
tuusan natumai kwamba sasa utaelewa point yangu kwamba Kenya watu wengi wanamiliki magari kushinda Tanzania kwa hivyo expressway itapata wateja na wala sio kwamba wanafinywa maana wanalipa toll kwa hiari yao. Yaani tuusan hio statistic hapo juu maana yake ni hivi maana huwa napenda kubreak down vitu into simple language ili hata mama mboga aelewe:

Ukichukua watu elfu moja Tanzania randomly (wengine kutoka Dar, wengine Kigoma, wengine Tanga e.t.c) kisha ukawaambia wanaomiliki gari wainue mkono juu basi kati ya hao watu elfu moja ni watu saba tu watakaoinua mkono. Yaani kwa kila Watanzania elfu moja wasaba tu ndio wanamiliki gari.

Tukija upande wa Kenya, ukichukua Wakenya elfu moja randomly (wengine kutoka Nairobi, wengine Turkana, wengine Mandera, wengine Mombasa) na kuwaambia kwamba wanaomiliki gari wainue mkono juu basi kati ya hao Wakenya elfu moja Wakenya sabini watainua mkono juu.

Yaani nikisema kwamba Mkenya mmoja mmoja ana pesa kushinda Mtanzania mmoja mmoja huwa mnaona kama ni utani. Hata kwenye kumiliki TV au Laptop nipo sure Mkenya mmoja mmoja anamiliki TV au Laptop kwa wingi kushinda Mtanzania mmoja mmoja. Hata umiliki wa baiskeli au pikipiki ni vivyo hivyo tu.

Hata umiliki wa helicopter ni vivyo hivyo maana wakati wa Siasa Uganda na Tanzania huwa mnakuja Kenya kuagiza helicopter za wanasiasa wetu ili mkapige campaign nazo. Nyinyi mnatushinda tu kwa mlo. Yaani Mtanzania mmoja mmoja anashiba kushinda Mkenya mmoja mmoja, hii ni kwa sababu nchi yenu inapokea mvua kwenye 100% ya ardhi yenu ilhali Kenya 75% ya ardhi ni arid or semi-arid.


Cc Geza Ulole joto la jiwe ichoboy01 Shebby01 The best 007
Uhuru n Umoja
 
Ukiona mtanzania kanunua chombo cha usafiri ,ujue kanunua magari mawili (ushuru huko juu mno) ndo mana bado tunaendesha magari ya hovyo........
We ndio hujui kitu kabisa, yaani watanzania mnaolalamikia kodi nchi laiti mngeishi kwenye nchi za jirani ndio mngejua namna Tanzania ilivyo na almost no tax

Anyway hizi statistics ni za uongo mtupu, Hakuna siku hata 1 Kenya inaizidi Tanzania kwa idadi ya magari
 
Na hii Rwanda sijui ni kwa nini watu wanapenda kuisifusifu sana. Inakuanga masikini sana. Huwa wapo nyuma kwa mambo mengi kiuchumi. Hata Gni per capita yao ipo chini ndio maana wao bado ni Ldc.

Hata electricity consumption ipo chini. Gdp yao ni ndogo $10 billion pekee. The only thing wanafanya vizuri ni ease of doing business index ya World bank lakini kwenye mambo mengine wapo nyuma sana hata Tanzania mnawashinda kwenye vigezo vingi vya kiuchumi ikiwemo Gni per capita.

Huwa nikisikia watu wanasifu Rwanda huwa nashangaa wanasifu kwa vigezo gani vya kiuchumi au wanasifu tu bila data, yaani wanasifu tu kwa sababu watu wengine wanasifu. Tujifunze kutathmini mambo kwa undani sio kusifia tu jambo kwa sababu kila mtu anasifia.

Rwanda hata barabara ya lami wamejenga distance kidogo sana, umeme wanaproduce na kuconsume megawatts kidogo. Wana industries chache.

Sasa hio sifa sijaielewa inatokana na nini, pengine ni kwa sababu inamchukua investor mda mfupi sana kuregister a new business. Au pengine wanasifiwa kwa sababu wao ni wasafi wanaosha mji wao mara moja kwa mwezi. Ila vigezo vya kiuchumi vya Rwanda ni mbovu mno. Tuwache kusifia ujinga.

Cc Uhuru n Umoja
 
Una amini Congo isio na barabara za lami na yenyewe inaipita Tanzania? Haha

Tanzania Ina mabus ya mikoani mengi kuliko jumla ya idadi ya magari yote Congo
Western Congo hakuna vita sana na huko ndipo Kinshasa ipo. Kinshasa yenyewe ni megacity na ina watu zaidi ya milioni kumi. Africa ina megacity chache ikiwemo Cairo, Lagos na Kinshasa. Wewe unadhani city ya watu milioni kumi kama Kinshasa itakosa kuwa na magari mengi? Halafu Wakongomani ni watu wanaopenda kujituma na sidhani kama ni Malazy.
 
Back
Top Bottom