Afrika inarejea katika zama za mapinduzi?

Afrika inarejea katika zama za mapinduzi?

Ngongo

Platinum Member
Joined
Sep 20, 2008
Posts
20,654
Reaction score
35,887
1622979760346.png

Afrika ya zama za Mwl Nyerere, Nkrumah, Jomo Kenyatta, Mobutu Seseseko, Augustino Neto. Tulishuhudia mapinduzi kila uchao sababu kubwa ilikuwa pengine uchanga wa nchi husika, maslahi ya wakoloni, upendeleo katika ugawaji wa rasilimali na nk.

Kidogo Afrika ilipumzika katika zama za mapinduzi ya kijeshi, nchi kama Nigeria, Mali na Uganda zilitia aibu na doa kubwa katika bara letu na kuonekana kama bado tuka katika zama za mawe.

Hivi karibuni hali ya mapinduzi imerejea kwa kasi kubwa sijui kwanini nchi za Kaskazini zimekuwa zikinyemelewa na mapinduzi ya mara kwa mara.
 
Shida yetu kama Afrika tumekaa kuendekeza upuuzi, kwa wenye mamlaka hasa wale wanaoamua kuyatumia Vibaya.Kwa namna hiyo huchochea yanayotokea kwingineko Barani.
 
Nchi za huko watu wanajielewa....Sisi Nyerere alituroga , kimsingi hii nchi ilitakiwa ziwe nchi tano tofaut , tutaendelea kulaumiana Tu
Ha haaaaaaaaaaa haaaaaaaaaaa jamaaa nenda kanywe Pepsi naja kulipa

Yaaan paaap Tit for Tat
 
Watawala wengi wanaendekeza sana ubinafsi na kuwatelekeza wananchi wanaowaweka madarakani. Ni sawa na wabunge wengi wanavyotuacha solemba mara baada ya kuwachagua.

Siku hizi hata chaguzi za kidemokrasia zimeisha, tumekuwa na chaguzi za kimapinduzi au za kifisadi. Tunapinduana kwa kutumia tume za uchaguzi na kuwakaba koo washindani wa ukweli kupitia vyombo vya ulinzi na usalama.
 
Watawala wengi wanaendekeza sana ubinafsi na kuwatelekeza wananchi wanaowaweka madarakani. Siku hizi hata chaguzi za kidemokrasia zimeisha, tumekuwa na chaguzi za kimapinduzi au za kifisadi.

Tunapinduana kwa kutumia tume za uchaguzi na kuwakaba koo washindani wa ukweli kupitia vyombo vya ulinzi na usalama. Ni sawa na wabunge wengi wanavyotuacha solemba mara baada ya kuwachagua!
Nikweli
 
Afrika tuna asili ya fikra ya utawala wa kitemi ambapo watawaliwa walifahamu Mtemi ndio mungu wao.

Sasa kwa mazingira ya leo ambapo watu wanasoma na kutembea nje ya Afrika wanaondokana na fikra hizo za kijinga za kumuabudu rais kama Magufuli alivyolazimisha watu wamuabudu.

Ktk hali hiyo matukio kama ya mapinduzi ya kijeshi lazima tu yatakuwepo hayawezi kuepukika.
 
Watawala wengi wanaendekeza sana ubinafsi na kuwatelekeza wananchi wanaowaweka madarakani. Ni sawa na wabunge wengi wanavyotuacha solemba mara baada ya kuwachagua.

Siku hizi hata chaguzi za kidemokrasia zimeisha, tumekuwa na chaguzi za kimapinduzi au za kifisadi. Tunapinduana kwa kutumia tume za uchaguzi na kuwakaba koo washindani wa ukweli kupitia vyombo vya ulinzi na usalama.
Taifa likipata wanajeshi wazalendo kama Rawlings kwakweli bora kutawaliwa kijeshi.
 

Afrika ya zama za Mwl Nyerere, Nkrumah, Jomo Kenyatta, Mobutu Seseseko, Augustino Neto. Tulishuhudia mapinduzi kila uchao sababu kubwa ilikuwa pengine uchanga wa nchi husika, maslahi ya wakoloni, upendeleo katika ugawaji wa rasilimali na nk.

Kidogo Afrika ilipumzika katika zama za mapinduzi ya kijeshi, nchi kama Nigeria, Mali na Uganda zilitia aibu na doa kubwa katika bara letu na kuonekana kama bado tuka katika zama za mawe.

Hivi karibuni hali ya mapinduzi imerejea kwa kasi kubwa sijui kwanini nchi za Kaskazini zimekuwa zikinyemelewa na mapinduzi ya mara kwa mara.
Niseme kiufupi:

Sijawahi kushangilia mapinduzi ya kijeshi katika nchi yoyote; lakini kwa tawala dhalimu niliyoishuhudia hivi karibuni, wazo la kuwepo mapinduzi ya kijeshi lilionekana kuwa pengine ni 'option' nzuri!

Watawala kama M7, hata kama unefanya mambo mazuri, hayo mazuri yako mwishowe yataonekana sio mazuri tena kwa kujifanya kama nchi ni mali yako binafsi na hakuna wengine wanaoweza kuendeleza tokea hapo ulipofikia.
Hata kama wataharibu, achia wananchi waamue kuhusu hilo.

Kwa hiyo, nadhani siyo kila aina ya mapinduzi ya kijeshi ni mabaya; maana mapinduzi hayo ni kuondoa viongozi wakorofi; na kama wapinduaji hawana nia ya kuwa watawala wa kudumu, mapinduzi huwa ni ukombozi.
 
Back
Top Bottom