Afrika Kusini, Kenya, Nigeria na Tunisia leo kuna maandamano. Hawa ni vinara wa uchumi wa Afrika wanadai maisha bora zaidi na demokrasia

Afrika Kusini, Kenya, Nigeria na Tunisia leo kuna maandamano. Hawa ni vinara wa uchumi wa Afrika wanadai maisha bora zaidi na demokrasia

fazili

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2011
Posts
16,427
Reaction score
22,418
Leo nchi vinara wa uchumi wa Afrika wanaandamana kudai maisha bora, demokrasia na utawala bora. Inashangaza nchi hizi ambazo zina unafuu ukilinganisha na Tanzania katika masuala ya maendeleo wapo barabarani wanadai mambo bora zaidi.

Maandamano ya amani ni njia mojawapo nzuri sana ya kudai yote yale tunayohitaji serikali yetu itufanyie. Ni njia nzuri ya kufikisha ujumbe kwa viongozi wetu endapo njia za kawaida zimeshindikana. Huu ni wakati wa vuguvugu la ukombozi wa Afrika dhidi ya serikali zisizojali matakwa ya raia wake.

Naelewa kuwa JPM aliwaogofya watanzania kwa staili ya uongozi wake uliojaa ukatili kiasi kwamba miaka miwili baada ya kifo chake bado tumeendelea kufikiri tupo chini ya mfumo wake.

Je watanzania tuna haja ya kuandamana kudai unafuu katika kodi, tozo, pembejeo za kilimo na hata katiba mpya na tume huru ya uchaguzi? Pengine huu ndio wakati mzuri wa kuleta mabadiliko hayo kwa mshikamano wetu.
 
Usisahau historia lakini, maandamano ya amani hayakumto Kaburu, ni mwili na damu ya Watanzania kwa uongozi TANU ikawagomboa. Kenya wana matatizo ya ukabila, na kuwahiana kuiba hela big time. Nigeria ni Nigeria, Tunisia ni Nji ya Ulaya mwakani wanahost World Cup na Spain na Portugal. If you go there, hawana Nyerere wala Karume wa Nnauye wala Asha Bakari, hawana uzalendo hata chembe. Usitulinganishe na mafala.
 
Usisahau historia lakini, maandamano ya amani hayakumto Kaburu, ni mwili na damu ya Watanzania kwa uongozi TANU ikawagomboa. Kenya wana matatizo ya ukabila, na kuwahiana kuiba hela big time. Nigeria ni Nigeria, Tunisia ni Nji ya Ulaya mwakani wanahost World Cup na Spain na Portugal. If you go there, hawana Nyerere wala Karume wa Nnauye wala Asha Bakari, hawana uzalendo hata chembe. Usitulinganishe na mafala.
Watu wasio na uzalendo hawajali lolote katika nchi yao, inyeshe isinyeshe wao huona heri tu. Ni watu kama wewe.
 
Back
Top Bottom