Afrika Kusini wameonesha dharau kwa Rais Samia

Kwitogelo

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2023
Posts
310
Reaction score
442
Wakuu habari za humu? Ni matumaini yangu wote hamjambo.

Leo nlikuwa napitia taarifa mbalimbali kwenye kiswaswadu changu nikakutana na taarifa ya mama kwenda kwa Madiba hii leo. Kwakweli mapokezi yale sijayapenda,yaani haiwezeknai Rais wa nchi anapkelewa na balozi wa nchi yetu hukohuko tena bila hata mwenyeji yeyote! .

Kwakweli kama ni dharau wasauzi mmetuonesha na binafsi sijapenda kabisa kwasababu Rais ni mtu mkubwa sana akiwa popote pale kwenye masuala ya kiitifaki na kiutawala.
 
ile ni ziara ya kushtukiza...kwa hiyo kaa kwa kutulia mkuu
 
Write your reply...WAPI SHDA HAPO..mbona jk alishawahi kupokelewa na waziri usa
Mkuu bora huyo alipokelewa na waziri lakini mama yetu amepokelewa na balozi wa Tanzania nchini humo pamoja na waziri wa mambo ya nje wa Tanzania,yaani kiufupi mgeni amepokelewa na mgeni
 
Kiitifaki kuna safari za wakuu wa nchi za aina nyingi.

Kuna state visit (formal, by invitation), kuna working visit. Zote zina itifaki tofauti.

Sasa, kabla ya kuanza kulaumu wa South Africa, inabidi tuulize, hii ni state visit au working visit?

 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ kwahiyo unadhani anaweza kwenda huko bila sababu
Kabisa tena hilo ni swala la kawaida mambo ya hovyo yasiyo na tija kama semina hafla birthday party kwenye awamu hii.Ziara za hovyo zisizokuwa na umuhimu wala tija. Sasa kuhudhuria mikutano ya gesi ya ukaa umesikia Tanzania imekuwa industrial country kwamba ina chafua hewa?! Ndiyo maana kaishia kupokelewa na balozi wake πŸ˜‚
 
Aacha kuwa kiguu na njia Le Madamme Vasco Dagama wa II
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…