Afrika Kusuni: Rubani atua kwa dharura baada ya kuona nyoka aina ya (cobra) chini ya kiti chake

Afrika Kusuni: Rubani atua kwa dharura baada ya kuona nyoka aina ya (cobra) chini ya kiti chake

Meneja Wa Makampuni

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2020
Posts
7,899
Reaction score
10,415
1680700332666.png

Rubani wa Afrika Kusini anapongezwa kwa kufanikiwa kutua kwa dharura baada ya kuona nyoka aina ya fira ‘Capa cobra’ akiwa amejikunja chini ya kiti chake, ripoti ya vyombo vya habari nchini humo yasema.

Rudolph Erasmus alikuwa akisafirisha abiria wanne kutoka Cape Town kuelekea mji wa kaskazini wa Nelspruit Jumatatu asubuhi lakini alilazimika kukatiza safari baada ya kuhisi kitu cha baridi kwenye mwili wake, aliambia tovuti ya habari ya Times Live.

"Nilipogeuka kushoto kwangu na kutazama chini, niliona nyoka wa aina ya fira ‘Cape’ [cobra] akirudisha kichwa chake chini ya kiti changu," alinukuliwa akisema.

Kuumwa na nyoka aina ya Cape cobra kunaweza kumuua mtu ndani ya dakika 30.

Kamishna wa usafiri wa anga wa Afrika Kusini amemsifu Bw Erasmus kama shujaa, ripoti za tovuti ya news24.

"Rubani hodari ambaye ameokoa maisha ya wote waliokuwa ndani ya ndege," Poppy Khosa alinukuliwa akisema.

Rubani huyo alisema hakuwa na uhakika ikiwa angewaambia abiria wake baada ya kumwona nyoka huyo wakati wa safari ya ndege.

Alisema hakutaka kusababisha hofu.

"Nilisema tu, 'sikiliza, kuna shida. Nyoka yuko ndani ya ndege. Ninahisi kuwa yuko chini ya kiti changu kwa hivyo itabidi tutue ardhini haraka iwezekanavyo,” alinukuliwa akisema. Alifanikiwa kutua kwa dharura huko Welkom.

Wahandisi walioipokea ndege hiyo hawakumpata nyoka huyo, Bw Erasmus alisema.
===

South African pilot is being celebrated for his bravery in making an emergency landing when he discovered a venomous cobra coiled beneath his seat, according to local media reports.

During a routine flight from Cape Town to Nelspruit on Monday morning, pilot Rudolph Erasmus had to abruptly end the journey due to an unexpected and unsettling sensation on his body. Erasmus shared with the Times Live news website that he felt something cold, prompting him to take immediate action.

"As I turned to my left and looked down, I saw the [Cape] cobra putting its head back underneath my seat," he is quoted as saying.

The bite of a Cape cobra can kill a man in 30 minutes.

South African civil aviation commissioner has hailed Mr Erasmus as a hero, news24 website reports.

"Great airmanship indeed which saved all lives on board," Poppy Khosa is quoted as saying.

The pilot said he was unsure if to tell his passengers after spotting the snake during the flight. He said he didn't want to cause panic.

The pilot was hesitant to inform the passengers, as he feared it might cause panic.

“I just said, 'listen, there's a problem. The snake is inside the aircraft. I've got a feeling it's under my seat so we are going to have to get the plane on the ground as soon as possible,” he is quoted as saying.

He managed to make an emergency landing at Welkom.

Engineers who stripped the plane did not find the rogue reptile, Mr Erasmus said.

He hopes to fly the plane again on Wednesday.
 
Duh....aliokula nao cha arusha wenzie walimchanganyia na nya.
 
Back
Top Bottom