babalao 2
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 5,423
- 3,297
Habari za muda huu.
Habari za kusikitisha kabisa ni kwamba mmoja wa wakaguzi wa ELIMU wilayani Rombo ametoa kauli chafu na ya kuudhi kama si kudhalilisha kwa kundi la Walemavu.
Mkaguzi huyo amesema ya kwamba WALEMAVU hawana UMUHIMU kwa taifa hili. Aliyasema hayo alipokuwa akikagua darasa la WALEMAVU lililojengwa na wafadhili.
Hatua hiyo imepelekea Walemavu wilayani humo kugomea darasa hilo kufuatia kukasirishwa na kauli hiyo ila wafadhili hao waliwafariji walemavu hao ya kwamba wako nao kwa kila jambo kwani kila mmoja wetu ni MLEMAVU MTARAJIWA.
Juhudi za kumpata Afsa Elimu Wilaya kuzungumzia kadhia hiyo zinaendelea.
Source: ITV HABARI ZA MCHANA
Hivi huu ubaguzi unaolelewa taratibu hapa nchini dhidi ya baadhi ya makundi katika jamii kwa nini wanaobainika kuwatenga na kuwadharau wengine wasichukuliwe hatua kali ili iwe mfano kwa wengine?
Habari za kusikitisha kabisa ni kwamba mmoja wa wakaguzi wa ELIMU wilayani Rombo ametoa kauli chafu na ya kuudhi kama si kudhalilisha kwa kundi la Walemavu.
Mkaguzi huyo amesema ya kwamba WALEMAVU hawana UMUHIMU kwa taifa hili. Aliyasema hayo alipokuwa akikagua darasa la WALEMAVU lililojengwa na wafadhili.
Hatua hiyo imepelekea Walemavu wilayani humo kugomea darasa hilo kufuatia kukasirishwa na kauli hiyo ila wafadhili hao waliwafariji walemavu hao ya kwamba wako nao kwa kila jambo kwani kila mmoja wetu ni MLEMAVU MTARAJIWA.
Juhudi za kumpata Afsa Elimu Wilaya kuzungumzia kadhia hiyo zinaendelea.
Source: ITV HABARI ZA MCHANA
Hivi huu ubaguzi unaolelewa taratibu hapa nchini dhidi ya baadhi ya makundi katika jamii kwa nini wanaobainika kuwatenga na kuwadharau wengine wasichukuliwe hatua kali ili iwe mfano kwa wengine?