Afungwa miaka 20 kwa kuwadhalilisha kingono Watoto

Afungwa miaka 20 kwa kuwadhalilisha kingono Watoto

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Hukumu imetolewa na Hakimu Mkazi John Mdoe wa Mahakama ya Wilaya dhidi ya Francis Julius Matiko mkazi wa Isevya kutiwa hatiani kwa makosa mawili ya kuwadhalilisha watoto.

Upande wa Mashtaka uliiambia Mahakama kuwa mshitakiwa kwa nyakati tofauti aliwalaghai watoto wawili wa kike kwa kuwapa Tsh. 500 hadi 1000 na kuwashika maungoni ikiwemo sehemu za siri.

Kwa kuzingatia ushahidi wa waathirika kumtambua mshtakiwa, Mahakama ilmhukumu kutumikia kifungo hicho na kumlipa fidia ya Tsh. 100,000 kila muathirika.

======================

Mkazi wa Isevya, Manispaa ya Tabora, Francis Julius Matiko (19) amehukumiwa kutumikia kifungo cha miaka 40 jela baada ya kutiwa hatiani kwa makosa mawili tofauti ya ukatili wa kingono kwa watoto.

Hukumu hiyo, imetolewa leo Ijumaa Oktoba 28, 2022 na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Tabora, John Mdoe baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na mashahidi watano wa upande wa mashtaka wakiwemo waathirika wa ukatili huo.

Upande wa mashitaka katika shauri hilo ukiongozwa na wakili Joseph Makeno, uliiambia mahakama hiyo kuwa mshtakiwa alitenda makosa hayo mawili, Mei 22, 2021 kinyume na kifungu namba 138 C (1) (a) na Kifungu kidogo (2) (b) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu.

Amesema kuwa siku hiyo katika Kata ya Isevya, Manispaa ya Tabora na kwa nyakati tofauti, mshtakiwa aliwashika maungoni ikiwemo sehemu zao za siri watoto wawili wa kike ambao majina yao yanahifadhiwa.

Wakili Makeno ameiambia mahakama hiyo kuwa ili kufanikisha shambulizi hilo la kingono kwa watoto hao mshtakiwa alikuwa akiwalaghai kwa kuwapatia fedha kati ya Sh500 hadi Sh1,000 au kinywaji aina ya juisi.

Ameongeza kuwa awali alimchukua mtoto wa kwanza mwenye umri wa miaka sita na kumpeleka chumbani mwake na kumlaza kitandani na kuanza kumshika makalio, matiti na sehemu za siri, ukeni.

Upande wa Jamhuri umeongeza kuwa ikiwa haitoshi na bila woga mshtakiwa alimchukua mtoto wa pili na kumpeleka chooni na kuanza kumfanyia vitendo hivyo vya ukatili wa kingono.

Akitoa utetezi wake, Francis Matiko amedai kuwa amefunguliwa kesi hiyo kwa hila kutokana na ugomvi kati yake na shahidi wa kwanza ambaye ni bibi wa mmoja wa wahanga kwamba alikuwa akimtaka kimapenzi bila mafanikio.

Matiko ameongeza katika utetezi wake kuwa bibi huyo alikuwa akimfuata amevaa khanga moja lakini alimkatalia ndipo akamwambia kwamba atamkomesha.

Katika hukumu hiyo hakimu Mdoe, amesema utetezi wa mshtakiwa hauna nguvu kutokana na ukweli kwamba aliyemtaja kwamba alimtaka kimapenzi ni miongoni mwa mashahidi lakini hakuweza kumuuliza swali wakati wa shauri.

Ameongeza kuwa mshitakiwa amewasilisha utetezi wake muda ambao sio mwafaka kwani ameutoa baada ya kujitafakari.

Akitoa uamuzi wa kesi hiyo hakimu Mdoe, amesema kwa kuzingatia ushahidi wa waathirika wa kumtambua mshtakiwa pasipo shaka yoyote, mahakama inamhukumu kutumikia kifungo cha miaka 20 jela kila kosa ambacho ndicho kima cha chini cha adhabu .

Mahakama pia imemtaka mshitakiwa kuwalipa watoto hao wawili fidia ya Sh100,000 kila muathirika, Hata hivyo atatumikia kifungo cha miaka 20 jela kwa vile adhabu hizo, zinaenda pamoja.

MWANANCHI
 
Hukumu imetolewa na Hakimu Mkazi John Mdoe wa Mahakama ya Wilaya dhidi ya Francis Julius Matiko mkazi wa Isevya kutiwa hatiani kwa makosa mawili ya kuwadhalilisha watoto.

Upande wa Mashtaka uliiambia Mahakama kuwa mshitakiwa kwa nyakati tofauti aliwalaghai watoto wawili wa kike kwa kuwapa Tsh. 500 hadi 1000 na kuwashika maungoni ikiwemo sehemu za siri.

Kwa kuzingatia ushahidi wa waathirika kumtambua mshtakiwa, Mahakama ilmhukumu kutumikia kifungo hicho na kumlipa fidia ya Tsh. 100,000 kila muathirika.

======================

Mkazi wa Isevya, Manispaa ya Tabora, Francis Julius Matiko (19) amehukumiwa kutumikia kifungo cha miaka 40 jela baada ya kutiwa hatiani kwa makosa mawili tofauti ya ukatili wa kingono kwa watoto.

Hukumu hiyo, imetolewa leo Ijumaa Oktoba 28, 2022 na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Tabora, John Mdoe baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na mashahidi watano wa upande wa mashtaka wakiwemo waathirika wa ukatili huo.

Upande wa mashitaka katika shauri hilo ukiongozwa na wakili Joseph Makeno, uliiambia mahakama hiyo kuwa mshtakiwa alitenda makosa hayo mawili, Mei 22, 2021 kinyume na kifungu namba 138 C (1) (a) na Kifungu kidogo (2) (b) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu.

Amesema kuwa siku hiyo katika Kata ya Isevya, Manispaa ya Tabora na kwa nyakati tofauti, mshtakiwa aliwashika maungoni ikiwemo sehemu zao za siri watoto wawili wa kike ambao majina yao yanahifadhiwa.

Wakili Makeno ameiambia mahakama hiyo kuwa ili kufanikisha shambulizi hilo la kingono kwa watoto hao mshtakiwa alikuwa akiwalaghai kwa kuwapatia fedha kati ya Sh500 hadi Sh1,000 au kinywaji aina ya juisi.

Ameongeza kuwa awali alimchukua mtoto wa kwanza mwenye umri wa miaka sita na kumpeleka chumbani mwake na kumlaza kitandani na kuanza kumshika makalio, matiti na sehemu za siri, ukeni.

Upande wa Jamhuri umeongeza kuwa ikiwa haitoshi na bila woga mshtakiwa alimchukua mtoto wa pili na kumpeleka chooni na kuanza kumfanyia vitendo hivyo vya ukatili wa kingono.

Akitoa utetezi wake, Francis Matiko amedai kuwa amefunguliwa kesi hiyo kwa hila kutokana na ugomvi kati yake na shahidi wa kwanza ambaye ni bibi wa mmoja wa wahanga kwamba alikuwa akimtaka kimapenzi bila mafanikio.

Matiko ameongeza katika utetezi wake kuwa bibi huyo alikuwa akimfuata amevaa khanga moja lakini alimkatalia ndipo akamwambia kwamba atamkomesha.

Katika hukumu hiyo hakimu Mdoe, amesema utetezi wa mshtakiwa hauna nguvu kutokana na ukweli kwamba aliyemtaja kwamba alimtaka kimapenzi ni miongoni mwa mashahidi lakini hakuweza kumuuliza swali wakati wa shauri.

Ameongeza kuwa mshitakiwa amewasilisha utetezi wake muda ambao sio mwafaka kwani ameutoa baada ya kujitafakari.

Akitoa uamuzi wa kesi hiyo hakimu Mdoe, amesema kwa kuzingatia ushahidi wa waathirika wa kumtambua mshtakiwa pasipo shaka yoyote, mahakama inamhukumu kutumikia kifungo cha miaka 20 jela kila kosa ambacho ndicho kima cha chini cha adhabu .

Mahakama pia imemtaka mshitakiwa kuwalipa watoto hao wawili fidia ya Sh100,000 kila muathirika, Hata hivyo atatumikia kifungo cha miaka 20 jela kwa vile adhabu hizo, zinaenda pamoja.

MWANANCHI
Chuki hizo na kubamkia watu kesi , hata huku uswahilini zipo Sana unabidi ukitaka kuishi nao hakikisha unakaa mbali nao Mita 1000 ukiwazoea utaishia kula Mvua Kama hizo.
 
Chuki hizo na kubamkia watu kesi , hata huku uswahilini zipo Sana unabidi ukitaka kuishi nao hakikisha unakaa mbali nao Mita 1000 ukiwazoea utaishia kula Mvua Kama hizo.
Amebambikiwa?!!! Umejuaje mkuu?!!!
 
Amebambikiwa?!!! Umejuaje mkuu?!!!
Mkuu hii sio rocket 🚀, soma maelezo hapo juu kwenye mada, hakimu anaonekana ametumia kigezo cha watoto hawa kumtambua mhukumiwa kama ndio ushahidi muhimu, kesi hizi zinatakiwa ziwe na proof without reasonable doubt, je kuna eye witness?,je kuna report kutoka kwa social officer's aliyewahoji watoto hawa?,je kuna DNA test results za kulinks suspect na victims, je finger prints za mtuhumiwa zilipatikana kwenye maungo au kwenye nguo za victims?,Tanzania hadi leo hatuna a single police station yenye rape kits,sasa utakusanya vipi ushahidi bila kits hizi?,yes ni kesi mbaya hasa inayohusisha watoto but suspects ni muhimu wafungwe kwa ushahidi sio blah blah kama hii
 
Mkuu hii sio rocket 🚀, soma maelezo hapo juu kwenye mada, hakimu anaonekana ametumia kigezo cha watoto hawa kumtambua mhukumiwa kama ndio ushahidi muhimu, kesi hizi zinatakiwa ziwe na proof without reasonable doubt, je kuna eye witness?,je kuna report kutoka kwa social officer's aliyewahoji watoto hawa?,je kuna DNA test results za kulinks suspect na victims, je finger prints za mtuhumiwa zilipatikana kwenye maungo au kwenye nguo za victims?,Tanzania hadi leo hatuna a single police station yenye rape kits,sasa utakusanya vipi ushahidi bila kits hizi?,yes ni kesi mbaya hasa inayohusisha watoto but suspects ni muhimu wafungwe kwa ushahidi sio blah blah kama hii
🙏🙏🙏🙏 nimeelewa sasa!
 
🙏🙏🙏🙏 nimeelewa sasa!
Thanks mkuu, mimi ni mzazi pia tena Nina mtoto wa kike, ningekua hakimu hii issue ingenigusa mno ila always mahakimu watoe hukumu kutokanana na ushahidi usio na sitofahamu yeyote, sio kama hukumu hii ambayo inafanana mno na ya Babu seya na wanae, ule ulikua ni ouvu na majaji wale eti nasikia wanaenda kwenye nyumba za ibada, they supposedly to apologize kwa babu seya na wapenda haki wote
 
Aisee miaka 19 +20, atatoka akiwa na miaka 39 network zote hazishiki
 
Mkuu hii sio rocket [emoji573], soma maelezo hapo juu kwenye mada, hakimu anaonekana ametumia kigezo cha watoto hawa kumtambua mhukumiwa kama ndio ushahidi muhimu, kesi hizi zinatakiwa ziwe na proof without reasonable doubt, je kuna eye witness?,je kuna report kutoka kwa social officer's aliyewahoji watoto hawa?,je kuna DNA test results za kulinks suspect na victims, je finger prints za mtuhumiwa zilipatikana kwenye maungo au kwenye nguo za victims?,Tanzania hadi leo hatuna a single police station yenye rape kits,sasa utakusanya vipi ushahidi bila kits hizi?,yes ni kesi mbaya hasa inayohusisha watoto but suspects ni muhimu wafungwe kwa ushahidi sio blah blah kama hii

..kamsaidie kukata rufaa..
 
Pumbavu mkubwa wewe

[emoji1][emoji1] matusi ya nini sasa. Wewe si unajua sheria na unapenda haki? Nenda kaonyeshe utu na umahiri wako mahakama ya rufaa, kama huwezi funga bakuli lako cuz whinning like a little girl hapa JF wont do any justice kwa huyo unayesema ameonewa..
 
Yule baba wa Kenya alihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela. Baada ya kutumikia miaka 17 Binti yake ambaye alishirikiana na mama yake mzazi (mke wa yule baba) kumsingizia ubakaji kwa huyo bintiye kwa lengo la kufaidi mafao yake mara tu baada ya kustaafu, Binti alikwenda police kutolea maelezo ya ukweli wa kisa chote ufuatiliaji ulipofanyika ikagundulika ni kweli yule mzee alifungwa jela kwa kosa la kubambikiwa akafutiwa mashtaka na kuachiliwa huru.

Jambo la ajabu sana mahakama haikumchukulia hatua yyt yule mama na Binti yake kwa maelezo kwamba anayestahili kumfungulia mashtaka ni mume wake ambaye ameachiliwa huru na mahakama na yule mzee hakuwa tyr kufanya hivo badala yake aliishia kulia machozi na kujitenga na mwanamke ambaye wakati huo hakuwa na hela maana mafao yote ya mzee alikuwa ametafuna

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya ndio mambo ya kujifanya anko mixer kuwanunulia vi pipi watoto wa majirani...ukiishi uswahilini bwana piga chini mazoea otherwise mkizinguana tu utaambiwa umerawiti noma sana kijana akipata wafuatiliaji anaweza kupindua meza ila akikosa wafuatiliaji anaolewa tu jela no way.
 
Back
Top Bottom