Lady Whistledown
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,147
- 2,008
HOSPITALI ya Aga Khan, Dar es Salaam, imezindua rasmi ujenzi wa Kituo chake cha kisasa cha Tiba ya Saratani kitakachonufaisha hadi watu milioni 1.7 katika mikoa ya Dar es Salaam na Mwanza.
Kituo hicho kitakachojengwa katika hospitali hiyo jijini Dar es Salaam, kitapokea hadi wagonjwa 125 wanaohitaji huduma ya mionzi kwa siku.
Ujenzi huo unakuja wakati data rasmi kutoka kwa Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, zinaonyesha kuwa wagonjwa 68 kati ya 100 wa saratani hufa kila mwaka.
Kutokana na changamoto hiyo, Mradi Kabambe wa Saratani Tanzania (TCCP) uliozinduliwa Januari 2020 na Shirika la Afya la Aga Khan (AKHS), umeamua kujenga kituo hicho kabla ya mradi kumalizika mwaka 2024.
Akizungumza jana wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa kituo hicho kilichogharimu Sh13.8 bilioni, Binti Mfalme Zahra Aga Khan alisema tukio hilo linaashiria dhumuni kubwa la mradi huo ambao ni kuboresha huduma za matibabu ya saratani mipakani nchini.
"Takwimu za Shirika la Utafiti wa Saratani la Umoja wa Mataifa zinaonyesha kuwa Tanzania inapokea wagonjwa 42,000 kila mwaka na wastani wa vifo ni 28,000 kwa mwaka," alisema.
“Takriban asilimia 75 ya wagonjwa hao hugundulika wakiwa katika hatua za mwisho. Hii ni changamoto kubwa inayoathiri uwezekano wa kupona,” aliongeza Princess Zahra.
Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) nchini Tanzania Bi Stephanie Mouen alisema anaamini kuwa hadi mwisho wa mradi wa TCCP huduma bora za uchunguzi zitawafikia walengwa milioni 1.7 katika mikoa ya Dar es Salaam na Mwanza.
Alisema mradi huo pia utasaidia kudhibiti vyema maambukizi ya saratani kwa kuongeza idadi ya wagonjwa wanaogundulika katika hatua za awali kutoka asilimia 20 hadi 50.
"Lakini pia itatoa mafunzo kwa watoa huduma za afya kutoka ngazi ya chini hadi kliniki, pamoja na kuongeza uelewa wa umma kuhusu saratani kupitia vyombo vya habari na njia nyingine za mawasiliano," alisema Bi Mouen.
Hafla hiyo iliyoambatana na maonesho ya makala mbalimbali za utoaji wa huduma za afya katika hospitali hiyo, ilihudhuriwa pia na Mwalimu huyo ambaye aliwashauri Watanzania kuwa na utamaduni wa kwenda kupima afya mara kwa mara.
Chanzo: The Citizen
Kituo hicho kitakachojengwa katika hospitali hiyo jijini Dar es Salaam, kitapokea hadi wagonjwa 125 wanaohitaji huduma ya mionzi kwa siku.
Ujenzi huo unakuja wakati data rasmi kutoka kwa Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, zinaonyesha kuwa wagonjwa 68 kati ya 100 wa saratani hufa kila mwaka.
Kutokana na changamoto hiyo, Mradi Kabambe wa Saratani Tanzania (TCCP) uliozinduliwa Januari 2020 na Shirika la Afya la Aga Khan (AKHS), umeamua kujenga kituo hicho kabla ya mradi kumalizika mwaka 2024.
Akizungumza jana wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa kituo hicho kilichogharimu Sh13.8 bilioni, Binti Mfalme Zahra Aga Khan alisema tukio hilo linaashiria dhumuni kubwa la mradi huo ambao ni kuboresha huduma za matibabu ya saratani mipakani nchini.
"Takwimu za Shirika la Utafiti wa Saratani la Umoja wa Mataifa zinaonyesha kuwa Tanzania inapokea wagonjwa 42,000 kila mwaka na wastani wa vifo ni 28,000 kwa mwaka," alisema.
“Takriban asilimia 75 ya wagonjwa hao hugundulika wakiwa katika hatua za mwisho. Hii ni changamoto kubwa inayoathiri uwezekano wa kupona,” aliongeza Princess Zahra.
Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD) nchini Tanzania Bi Stephanie Mouen alisema anaamini kuwa hadi mwisho wa mradi wa TCCP huduma bora za uchunguzi zitawafikia walengwa milioni 1.7 katika mikoa ya Dar es Salaam na Mwanza.
Alisema mradi huo pia utasaidia kudhibiti vyema maambukizi ya saratani kwa kuongeza idadi ya wagonjwa wanaogundulika katika hatua za awali kutoka asilimia 20 hadi 50.
"Lakini pia itatoa mafunzo kwa watoa huduma za afya kutoka ngazi ya chini hadi kliniki, pamoja na kuongeza uelewa wa umma kuhusu saratani kupitia vyombo vya habari na njia nyingine za mawasiliano," alisema Bi Mouen.
Hafla hiyo iliyoambatana na maonesho ya makala mbalimbali za utoaji wa huduma za afya katika hospitali hiyo, ilihudhuriwa pia na Mwalimu huyo ambaye aliwashauri Watanzania kuwa na utamaduni wa kwenda kupima afya mara kwa mara.
Chanzo: The Citizen