Agizo la Rais Samia kuhusu utozaji wa Ushuru wa Mazao lapuuzwa Wilaya ya Sumbawanga

Agizo la Rais Samia kuhusu utozaji wa Ushuru wa Mazao lapuuzwa Wilaya ya Sumbawanga

Lobapula

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2011
Posts
2,389
Reaction score
1,584
Rais SAMIA SULUHU alitoa agizo kuwa wakulima wasitozwe Ushuru wa mazao kwa magunia yasiyozidi tani moja akiwa Tabora.

Jambo la ajabu hapa Mkoa wa Rukwa wilaya Sumbawanga kuna kizuizi cha Mazao njia ya kwenda Tunduma kinaitwa Laela wananchi wanatozwa ushuru wa mazao mfano leo tarehe 24/05/2022 majira ya saa nne na nusu asubuhi wamesimamisha bus na kuanza kukagua walikuta gunia 5 za alizeti wametozwa ushuru, kuna dada alikua na gunia moja la mahindi ametozwa ushuru pia kuna kijana alikua amebeba maharage debe tatu katozwa ushuru.

Hapa tunajiuliza tamko la rais huko tabora lilikua la kufurahisha genge na watendaji wamegoma kulitekeleza na kulisimamia?? Au watendaji wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa Mkirikiti,Mkuu wa wilaya Sumbawanga na Mkurugenzi wa Sumbawanga Vijijini wameamua kuwaumiza wananchi kwa makusudi?

Au ndio dhana ya Kazi iendelee?
 
Google maana ya msemo wa kuleni kulingana na urefu wa kamba zenu,halafu rudi hapa.
 
Hilo ni agizo la kisiasa halijawahi kuja kwenye maandishi toka alitamke Mwendazake na utozaji ushuru wa Mazao uko pale pale..

Muwe mnawaambia wanaleta maandishi
 
Subiri watumbuliwe uone BAVICHA wakija juu kuwatetea.

Kama kweli imetokea kuna sehemu hakupo sawa hata Rais Samia alisema "hata Kama hamnipendi basi ipendeni nchi yenu", katika hili mbona wasaidizi wake wanafanya nchi ichukiwe?

Tunahitaji tiba ya kudumu ya matatizo yetu
 
Hilo ni agizo la kisiasa halijawahi kuja kwenye maandishi toka alitamke Mwendazake na utozaji ushuru wa Mazao uko pale pale..

Muwe mnawaambia wanaleta maandishi
Unajua maana ya "Presidential decrees", agizo na amri ya Rais ni sheria na mtaalamu wa sheria Afrika, Prof.Kabudi aliwahi kusema Kuna sheria zisizoandikwa na zinafanya kazi.

Wakianza kutumbuliwa msije kusema wanaonewa
 
Unajua maana ya "Presidential decrees", agizo na amri ya Rais ni sheria na mtaalamu wa sheria Afrika, Prof.Kabudi aliwahi kusema Kuna sheria zisizoandikwa na zinafanya kazi.

Wakianza kutumbuliwa msije kusema wanaonewa
Huku sio Marekeni,toka agizo limetolewa na Magufuli uliwahi ona mageti ya Mazao yameondolewa ? Au watu hawatozwi?
 
Nakumbuka marehemu Magufuli aliwahi kusema na kuwaambia watendaji wake waache mara moja kutoza ushuru ama kuwapangia bei wakulima, akasema mtu anayetaka kukupangia bei na wewe mwambie akalime zao lake aweke bei yake na kweli lile agizo lake maeneo mengi yalitiliwa maanani.
 
Huku sio Marekeni,toka agizo limetolewa na Magufuli uliwahi ona mageti ya Mazao yameondolewa ? Au watu hawatozwi?
Kupuuzia kwa maagizo haimaanishi kwamba kilichosemwa hakitakiwi kutekelezwa, wote tupo humu wakitumbuliwa inawezekana ukawa mmoja wao kutetea na kudai wanaonewa
 
Mtoa tamko mwenyewe ameshasema anataka "heshima ya kutoka moyoni" hataki nidhamu ya uoga.😁.

Unategemea nini?
Heshima kutoka moyoni kwenye njaa?!!
 
Hao watu wa Sumbawanga huwa wana mambo yao ya ajabu sana. Ukikata leseni ya biashara ya mazao katika Mkoa wa Mbeya, ukienda kwao wanakwambia hawaitambui. Mtu unajiuliza Mbeya ipo Nchi gani na Rukwa ipo Nchi gani?

Je, Ada za leseni huwa zinaingia kwenye mfuko wa mikoa husika ama ni makusanyo yanayoingia kwenye mfuko wa hazina ya Nchi?

Hili la kuwatoza watu ushuru kwa kuwa na mazao yanayobebeka kwenye bus, ni uonevu usiokubalika kwa RAIA.
 
Huku sio Marekeni,toka agizo limetolewa na Magufuli uliwahi ona mageti ya Mazao yameondolewa ? Au watu hawatozwi?
Kuna sehemu unachanganya, agizo lilikua ni kwa. Mazao chini ya tani 1(Kama gunia 10 hivi). Ila juu ya hapo ndio Kuna ushuru. Sasa mageti yataondolewaje?
 
Kuna sehemu unachanganya, agizo lilikua ni kwa. Mazao chini ya tani 1(Kama gunia 10 hivi). Ila juu ya hapo ndio Kuna ushuru. Sasa mageti yataondolewaje?
Hakuna napochanganya,hakuna Halmashauri iliwahi tekeleza hilo agizo kwa sababu serikali inafahamu kwamba Halmashauri zinategemea mapato huko.
 
Back
Top Bottom