Ahadi ya katiba mpya Jk ameamua kung'atuka

Ahadi ya katiba mpya Jk ameamua kung'atuka

Gsana

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2010
Posts
4,383
Reaction score
1,337
Salaam Jf, tangu jk atoe ahadi ya katiba mpya, nimeanza kukumbuka sana tukio lilitokea zama zilizopita ktk maisha ya kijijini kwetu. Wawindaji 2 walienda kuwinda msitu wa mbali na bahati mbaya walipata sungura peke ake na mbwa aliemkata alikuwa mbwa wa mzee,mzee alimchinja sungura na kumla, akimnyima kijana aliyekuwa naye eti mbwa wake halifanya uzembe. Siku ya nne mwituni njaa ikakaza na mzee kuanza kulia,kijana akamshauri mzee kuwa ili aishi,avue viatu vyake vilivokuwa kama vya maasai yan vpande vya tairi za gari na kukata vipande vidogo na kuvimeza! Mzee akaukwaa ushauri na kula viatu vyote, Mzee alijikokota mpaka kijijini ila maisha yake yakaishia hapo maana tumbo lilivimba na kupasuka kwa viatu alivomeza! Kijana kamumaliza mzee yule kwa ujanja! Sasa naogopa,aliyemtega Jk viatu hivi ni nani?? Akivila itakuwaje!? Baada ya stori hii, leo nahoji uhamuzi wa Jeykey kutoa ahadi ya katiba mpya ndani ya siku 70 za utawala wake kama alivohaidi dr.Slaa kutupa katiba mpya ndani ya siku 100,ama kweli akili za kuambiwa changanya na zako,ila ------ hajazchanganya,ametoa ndo maana siku zimepungua toka 100 za dr.SLAA kuja less 70. Ni tafsiri yangu tu,ila mimi nilitaka Great Thinkers wajadili kama ------ akiamua japo kwa kusoma nyakati kutoa ahadi ya katiba mpya,ambayo pia iko NJE ya ilani ya Ccm si kama kujistaafisha mwenyewe?! Nasema ivi kwa sababu naamini mchakato wa kujenga katiba mpya hakuwezi kuchukua miaka 5 , je ikipatikana mwaka 2012-2013 si itaanza kutumika?na je ikianza kazi si itabidi kila ibara yake ifuatwe?na zikifuatwa si itaruhusu kuhoji utapeli uliofanya ktk kujumlisha kura mwaka 2010?au the past shall be exclusive?! Hapa binafsi naona jk kakubali kwenda Msoga kupumzika endapo kipengele icho kitatambulika mapema,ikumbukwe kuwa bado chadema wanaandaa ushaidi na haijulikani itawachukua muda gani,ambapo wanaweza kuukamilisha siku moja baada ya kupata katiba mpya na kuupeleka Mahakamani hapo ndipo Jk anaweza kujifunga bao mwenyewe au akapigwa goli la kisigino hadharani. Pia itapelekea Viongozi Waandamizi wakiwemo wastaafu kufikishwa mbele ya pilato. Tusichukulie mambo simple simple,yanaweza kutokea na hapo ndo anaweza akapitikana Rais wa wananchi baada ya katiba mpya. Haya matukio si ili mradi wataalam wameshagutuka,------ anataka kusign mwenyewe kuwa sheria mama imtafune mwenyewe na hapo ndo ukweli utajulikana kuwa wananchi walipiga kura. Ktk ili na mengine mengi yatakayojiri, mi kwa maoni yangu,JK HAS DECIDED TO Sow the seed for his own destruction. Hapa hata jk ataelewa kuwa "Haki hainyimwi ila ucheleweshwa tu" ,lets wait n see. I stand 2wait corrections! Nawasilisha!
 
mkuu ungetumia paragraph topic ingevutia zaidi watu kuisoma na kuchangia, fanya editing if possible...
 
Powa mkuu ila leo nko kijijini situmii komputa ndo tatizo ila ntajitahidi soon.
 
No! JK hapa anayo nafasi ya kuenziwa. Kwa kukubali kuandikwa Katiba mpya haina maana kwamba itamgeukia hata yeye mwenyewe. Uamuzi aliouchukuwa kama ni wa kwelikweli ni wa usanii wenye tija kwake. Waliopita watahukumiwa kwa taratibu zilizokuwapo kwa wakati wao, ukisema katiba mpya itumike kuwahoji hata waliopita unamaanisha hata mifupa ya mwalimu JKN ifukuliwe na kusimamishwa mahakamani kwa maamuzi aliyoyafanya na ambayo hata yeye alikujayaona akiwa amekaa pembeni na kuyatubia hata kwa machozi.

Ikumbukwe kuna mambo mengine ni matokeo ya washauri wabaya, maana uraisi sio mtu bali ni taasisi.Hata wewe kama mwananchi unayo mengi ya kuhukumiwa kama tukiifuata katiba mpya ikufukue hata wewe ulikojichimbia. Katiba mpya haiandikwi ili kujilipiza kisasi bali kujiimarisha kama nchi katika taratibu ambazo tutalazimika kuzifuata baada ya kukubaliana. JK kawazidi kete waliomtangulia kama kweli anakubali katiba iandikwe upya. Haina maana kwamba mambo yaliyomo kwenye katiba ya sasa yote ni mabaya, bali yatakuwa msingi na kioo cha kujua wapi tulikuwa fyongo na tunaandika mpya kwa kujirekebisha na tusahau ya kale na kuganga yaliyopo na yajayo. Vigogo wengine, sikatai kwamba wanapokataa katiba mpya wana wasiwasi kwamba hiyo katiba mpya huenda itawarudi, hayo ni kusutwa kwa dhamira zao kwa uozo wao uliopita, lakini uozo wao ndio msaada wa kuandikwa kwa katiba mpya ambayo itaandikwa ili kudhibiti mianya ya kikatiba iliyotumiwa na hao kujinufaisha pasipo mtu kuruhusiwa kuwauliza.

Bravo JK kwa hapo, lakini kwa kuwa katiba ya sasa inamzuia JK kurudi tena madarakani mara ya tatu na siamini katiba mpya itamruhusu, basi yeye yuko salama, ni kimojawapo kitakachomsababisha JK akumbukwe na historia ya nchi hii kwa miaka mingi ijayo kama Gobavhev wa Tanzania, W. de Clark wa Tanzania. CCM sasa wasome maandiko ukutani maana katiba iliyowaruhusu kufanya chochote kwa kiburi sasa kinaishia ukingoni. Ndio maana kina Makamba et al. wanahaha.

Tukiuweka ushabiki pembani, kunyamaza kwa JK wakati wasaidizi wake wanaropoka mchana kweupe kupinga madai ya wananchi tena wakitukana kwamba wananchi wanadodai katiba mpya ni mabata na wahaini, yeye kuibuka na kuungana na waajiri wake (wananchi) ina maana kubwa kwamba amewaumbua wanafiki wake waliofikiri atawaenzi kwa kuropoka kwao. Hata kina Dowans japo hakuwasemea katika kuukaribisha mwaka mpya inamaanisha ni mlolongo wa ubovu wa katiba tuliyo nayo ambao ikiandikwa upya Dowans na Richmonds wengine hawaji tena kirahisi, kwa sababu mikataba yote italazimika kuanikwa wazi kwa wananchi kabla ya kusainiwa, hata kama ni kupitia wawakilishi wao - wabunge. Labda tuchague wabunge wasio na kitu vichwani au waganga njaa. Anayekutesa anakukomaza akili usilalelale.

Ila najiuliza swali la CCM kuhodhi mali zote zilizotafutwa na watanzania wote wakati wa chama kimoja ambazo sasa wao wanadai ni vyao peke yao kama paka na mnofu. Je, katiba mpya itarudisha mali hizo serikalini isiwe ya chama kwa vile watu wote walizifanya kuwapo mali hizo? Hiyo ingefaa sana ili mchezo wa siasa uwe wa haki sawa kwa vyama vyote, sio mmoja Tyson na mwingine Nchumali wapambane uwanja mmoja wakati hata uwanja na marefa ni mali ya Tyson.
 
No! JK hapa anayo nafasi ya kuenziwa. Kwa kukubali kuandikwa Katiba mpya haina maana kwamba itamgeukia hata yeye mwenyewe. Uamuzi aliouchukuwa kama ni wa kwelikweli ni wa usanii wenye tija kwake. Waliopita watahukumiwa kwa taratibu zilizokuwapo kwa wakati wao, ukisema katiba mpya itumike kuwahoji hata waliopita unamaanisha hata mifupa ya mwalimu JKN ifukuliwe na kusimamishwa mahakamani kwa maamuzi aliyoyafanya na ambayo hata yeye alikujayaona akiwa amekaa pembeni na kuyatubia hata kwa machozi.

Ikumbukwe kuna mambo mengine ni matokeo ya washauri wabaya, maana uraisi sio mtu bali ni taasisi.Hata wewe kama mwananchi unayo mengi ya kuhukumiwa kama tukiifuata katiba mpya ikufukue hata wewe ulikojichimbia. Katiba mpya haiandikwi ili kujilipiza kisasi bali kujiimarisha kama nchi katika taratibu ambazo tutalazimika kuzifuata baada ya kukubaliana. JK kawazidi kete waliomtangulia kama kweli anakubali katiba iandikwe upya. Haina maana kwamba mambo yaliyomo kwenye katiba ya sasa yote ni mabaya, bali yatakuwa msingi na kioo cha kujua wapi tulikuwa fyongo na tunaandika mpya kwa kujirekebisha na tusahau ya kale na kuganga yaliyopo na yajayo. Vigogo wengine, sikatai kwamba wanapokataa katiba mpya wana wasiwasi kwamba hiyo katiba mpya huenda itawarudi, hayo ni kusutwa kwa dhamira zao kwa uozo wao uliopita, lakini uozo wao ndio msaada wa kuandikwa kwa katiba mpya ambayo itaandikwa ili kudhibiti mianya ya kikatiba iliyotumiwa na hao kujinufaisha pasipo mtu kuruhusiwa kuwauliza.

Bravo JK kwa hapo, lakini kwa kuwa katiba ya sasa inamzuia JK kurudi tena madarakani mara ya tatu na siamini katiba mpya itamruhusu, basi yeye yuko salama, ni kimojawapo kitakachomsababisha JK akumbukwe na historia ya nchi hii kwa miaka mingi ijayo kama Gobavhev wa Tanzania, W. de Clark wa Tanzania. CCM sasa wasome maandiko ukutani maana katiba iliyowaruhusu kufanya chochote kwa kiburi sasa kinaishia ukingoni. Ndio maana kina Makamba et al. ... Mkuu utaniwia radhi kwa kufupisha mchango wako ili niweze kuchangia kwa urahisi ila si kitu kwani bado mchango wako uko hapo juu. Mkuu umeanza kwa kuniondoa hofu kuwa Jk atakuwa salama pia sheria haiwezigusa mambo ya zamani ila mwishoni ukapata kigugumizi kama changu kwamba endapo tutapata msingi wa sheria yan katiba mpya si kuna mambo yatahojiwa kama mali za ccm zilizokuwa mali ya Serikali,pia ujue hapa kuna watu walijichukulia mali za umma. Kumbuka Molinge Sokoine kabla ya kupata ajali ambayo iliwagusa wengi,alikuwa amehaidi kuwakamata wahujumu uchumi waandamizi wa serikali na wafanyabiashara wakubwa! Inaonekana dhairi kuna mali yetu walibaki nazo watu wachache ambao Sokoine alitaka awalete mbele za Pilato. Bado naamini kuwa sheria halipi fadhila,yaweza kumkuta hata aliyeipitisha,rejea A.Chenge aliyeisimamia sheria kama A.G lakini ile ile ilitaka kumweka kolokoloni kama si visenti vyake. Upande wa pili nakubali kuwa Jk kaingia moja kwa moja ktk vitabu vya historia kwa kuleta katiba mpya lakini haimaanishi kwamba kama kesi au matatizo yaliyokuwapo yanafutwa kutokana na katiba mpya,hapana ila hapa yatapewa ufumbuzi kwa ujumla wake,na ufumbuzi huu waweza kumtia wavuni uyu mkulu! Ikumbukwe nchi moja kusini mwa Tanzania ambako rais alipitisha katiba mpya iliyompelekea kuhojiwa mtangulizi wake kwa maela aliyokomba serikalini. Ila kwetu kwa jambo lililonipa wasiwasi ni kwamba mkwere anashutuma ya kuongoza kipindi cha pili kwa kulazimisha au kulazimishwa na Nec,sasa kama tatizo litapata dawa kabla ilo tatizo alija expire,pia ata mlalamikaji ajaamua kuleta lalamiko lake kwa kuwa alidai anakusanya ushaidi,si itakuwa tafrani kama akishapata ruhusa ya kuhoji kwa katiba mpya? Mi naona kuna kamba mbele ya mkwere sijui atikwepaje hapa! Naomba unipe uhakika kama katiba mpya itaweza kumfanyia hisani kwa dhambi zake kwa kuwa kaiasisi yeye. Ikumbukwe kila mtu anafurahi kwa hoja ya mkwere ya kutoa katiba tegemeo la wengi,ila je ataruka ivyo viunzi? Remember Law is inclusive and has no time limit,zipo hata kesi za mwaka 70 ambazo hadi leo zinatolewa hukumu! Nakushukuru!
 
Mkuu utaniwia radhi kwa kufupisha mchango wako ili niweze kuchangia kwa urahisi ila si kitu kwani bado mchango wako uko hapo juu. Mkuu umeanza kwa kuniondoa hofu kuwa Jk atakuwa salama pia sheria haiwezigusa mambo ya zamani ila mwishoni ukapata kigugumizi kama changu kwamba endapo tutapata msingi wa sheria yan katiba mpya si kuna mambo yatahojiwa kama mali za ccm zilizokuwa mali ya Serikali,pia ujue hapa kuna watu walijichukulia mali za umma. Kumbuka Molinge Sokoine kabla ya kupata ajali ambayo iliwagusa wengi,alikuwa amehaidi kuwakamata wahujumu uchumi waandamizi wa serikali na wafanyabiashara wakubwa! Inaonekana dhairi kuna mali yetu walibaki nazo watu wachache ambao Sokoine alitaka awalete mbele za Pilato. Bado naamini kuwa sheria halipi fadhila,yaweza kumkuta hata aliyeipitisha,rejea A.Chenge aliyeisimamia sheria kama A.G lakini ile ile ilitaka kumweka kolokoloni kama si visenti vyake. Upande wa pili nakubali kuwa Jk kaingia moja kwa moja ktk vitabu vya historia kwa kuleta katiba mpya lakini haimaanishi kwamba kama kesi au matatizo yaliyokuwapo yanafutwa kutokana na katiba mpya,hapana ila hapa yatapewa ufumbuzi kwa ujumla wake,na ufumbuzi huu waweza kumtia wavuni uyu mkulu! Ikumbukwe nchi moja kusini mwa Tanzania ambako rais alipitisha katiba mpya iliyompelekea kuhojiwa mtangulizi wake kwa maela aliyokomba serikalini. Ila kwetu kwa jambo lililonipa wasiwasi ni kwamba mkwere anashutuma ya kuongoza kipindi cha pili kwa kulazimisha au kulazimishwa na Nec,sasa kama tatizo litapata dawa kabla ilo tatizo alija expire,pia ata mlalamikaji ajaamua kuleta lalamiko lake kwa kuwa alidai anakusanya ushaidi,si itakuwa tafrani kama akishapata ruhusa ya kuhoji kwa katiba mpya? Mi naona kuna kamba mbele ya mkwere sijui atikwepaje hapa! Naomba unipe uhakika kama katiba mpya itaweza kumfanyia hisani kwa dhambi zake kwa kuwa kaiasisi yeye. Ikumbukwe kila mtu anafurahi kwa hoja ya mkwere ya kutoa katiba tegemeo la wengi,ila je ataruka ivyo viunzi? Remember Law is inclusive and has no time limit,zipo hata kesi za mwaka 70 ambazo hadi leo zinatolewa hukumu! Nakushukuru!

Mkuu, kwanza ujue kwamba ili katiba hiyo ipate kuanza kufanya kazi ni lazima yeye JK kama rais wa wakati huu asaini maamuzi ya Bunge ili iwe sheria kamili na ianze kung'ata. Kama ataanza kuingiwa hofu na kipengele chochote hataruhusu kamba hiyo imnyonge mwenyewe. Kadhalika, anao wapambe kibao ambao lazima watauchambua mswada wa katiba mpya hiyo kujua usalama wake kuondoa vipengele ambavyo vinaweza kutumika kwa visasi. Usisahau kwamba hata kama ataipitisha, katiba hiyo mpya haitawaondoaa wateule wake aliowaweka kwenye sehemu nyeti kama mwanasheria mkuu na majaji na prosecutor. Ili kesi iwe kesi ni lazima prosecutor akubali kwamba kesi ipo na majaji wakubaliane naye. Mwanasheria mkuu wa serikali atakuwa pale kuhakikisha bosi wake haumizwi, na hivyo usitegemee kukwea ulingoni kwa ajili ya makosa ambayo JK hakuhusika moja kwa moja kama JK. Nilikuambia kwamba uraisi ni taasisi. Uchakachuaji hakufanywa na JK bali waateule wake ambao SIO MMOJA bali ni system. Utawala ni system ambayo daima inajiwekea kinga wasijerudiwa. Sio wajinga wale.

Hata hivyo vitu walivyohodhi CCM watatafuta lugha ili wapate kutopoteza uhodhi huo, wakishinikizwa sana watatoa vichache, maana mashirika mengi walishayaua kwa uroho wao kitambo kwa jina la chama kushika hatamu. Sana sana viwanja vya mpira ambavyo wanaweza kuviachia iwe mali ya serikali, ambayo mpaka hapo mtawala wa serikali hiyo atakuwa ccm wenyewe. Wakiwa bado madarakani watachakachua mali hizo hata yabaki maghofu tu ambayo itakuwa aghali kuyarudisha kwenye hali ya kawaida.

Kumbuka mifano ya karibuni ya wabunge wa CHADEMA Mbeya na Mwanza ambako wabunge wa ccm walipokataliwa na wananchi waliamua kufilisi ofisi za majimbo yao kwa visingizio kwamba samani zilizokuwamo zilinunuliwa na pesa zao kutoka mifukoni mwao wakati hata wao wanajua kwamba wananchi wanaelewaa kulikuwako pesa ambazo wabunge walipewa kuendeshea ofisi hizo. Roho ya ufilisi ni msingi wa CCM pata picha mwenyewe. Hata hizo mali zitakazoanza kupigiwa kelele kwamba ziende serikalini wanaccm watazichakachua kiasi cha kutotamanika maana ni mafundi wa kuchakachua hao na huwezi kuwashinda kwa kuongea tu.

Kaatiba mpya itaanza kuonyesha makucha yake hasa wakati wa kuingia awamu ya Tano ya utawala, waliopo sasa watatukuzwa tu,la vilaza ambao hawakuchukuwa vyao mapema ndio watakaoathirika. Kipindi hiki hujaona vingunge wa ccm wanavyojitayarishia maisha bora baada ya 2015? Miradi mingi inagawanywa kwao. Angalia Kingunge na mradi wa packing system, angalia ante plates writing wanaosema wa Masasi uliza walioko ni nani huko; vipingamizi kwao watu hao ni wale wanaoogopa ufisadi wa mchana kama kina Maghufuli ambao wanaonekana kama maadui kwa ccm conservatives ambao wanatafutiwa dawa kila kukicha.

Siamini kwamba watanzania watakengeuka na kuanza kuchokonoa mambo ya Kikwete ya zamani, maana wanaelewa kwamba hakuna msafi hata kwa watangulizi wake. Hata JKN anayo mapungufu mengi lakini ubaba wa Taifa ndio kinga pekee. Kama leo ingeruhusiwa ashitakiwe mtu yeyote mahakamani pasingetosha kwa viongozzi wote. Angalia watu walivyohamishwa kwa nguvu wakati wa operation vijiji vipya na wakapoteza mali zao na hata maisha wengine enzi za JKN, bado watu kibao wana donge na hilo. Mrema aliposhika dhahabu Airport na kusababisha atimuliwe kazi unajua zilikuwa mali za nani enzi za mzee Ruksa? Kiwira coal mine aliyeifilisi wakati wa Mr Clean ni nani? Sasa tunasumbuliwa na bei za umeme, unafikiri lili matatizo haya yalianza kubambikizwa deni la wageni wa Nskanska kama sio tangia JK akiwa waziri wa madini na nguvu ya umeme? Maukurutu ya benki kuu Kagoda enzi za Mkapa na Meremeta huoni viunganishi hapo?

Bado naamini kwamba katiba mpya kazi yake itakuwa kuziba mianya na sio kuchokonioa yaliyopita ambayo ni visasi, watanzania hatuwezi kulinganishwa na malawi na Zambia, maana JKN alijitahidi sana kutufanya kuwa wapole tunaoweza kuchunwa huku tukigugumia kimyakimya. Angalau JK na katiba mpya atazuia machafuko ambayo yalikuwa dhahir kutokea kama angeiachia ccm ishupae shingo na virakla vyake.
 
Back
Top Bottom