Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
AHMED RAJAB, SALIM HIMIDI NA SIMBA WAZIRI
Picha ya kwanza niliyoweka hapa kaniletea rafiki yangu Mohamed Abdul Rahman kutoka Ujerumani.
Picha hii kulia ni Salim Himidi katikati ni Joachim Chisano na kushoto ni Ahmed Rajab.
Joachim Chisano alikuwa rais wa pil wa Msumbuji.
Mohamed kaniletea picha hii kwa makusudi kwani Ahmed Rajab, Salim Himidi ni kaka zetu na tumeingiliananao kwa mengi kwa miaka mingi utotoni.
Picha hii ndiyo ilinifanya niingie Maktaba nitafute picha za zamani sana za hawa kaka zangu za miaka ya mwanzoni 1960.
Picha ya chini ya hiyo alinletea yeye huyo Mohamed kiasi cha miaka miwili iliyopita alipofariki Salim Himid ikimuonyesha Salim Himidi kushoto akiwa na Ahmed Rajab katikati na Simba Waziri kulia.
Maka hiyo mimi ni mdogo sana ndiyo nakua katika mitaa ya Kariakoo na nakumbuka nilikuwa nikienda nyumbani kwao Simba Waziiri, Mtaa wa Tandamti mdogo wake sasa ni marehemu Iddi Waziri alikuwa akinionyesha picha za kaka yake Simba Waziri wakati huo mwanafunzi chuo cha kijeshi Uingereza, Sandhurst.
Nakumbuko moja ya picha ambayo niliona ni hiyo ambayo ilipigwa Trafalgar Square hapo kwenye njiwa wengi akwa na Ahmed Rajab na Salim Himidi.
Haikunipitikia wakati ule hata kwa mbali kuwa ipo siku nitasimama hapo Trafalgar Square nikiwa na Ahmed Rajab na ntapiga picha.
Nakumbuka kama jana vile nina umri wa mika 15 au zaidi kidogo na ilkuwa tukimaliza kutazama picha tunamaliza kwa kuimba nyimbo za Cliff Richard na Iddi Waziri nyimbo yake aliyokuwa akiipenda sana ilikuwa ''High Class Baby.''
Wala haikunipitikia miaka ile ya mwanzoni 1960s kuwa hawa ninaowaangalia katika picha hiyo ya Trafalgar Square nitakuja kukutananao hapa nyumbani Tanzania na Ulaya na kwengineko na watakuwa marafiki na wazungumzaji wangu wakubwa.
Picha ya juu niko na Ahmed Rajab ofisini kwake Barbican, London wakati huo alikuwa Mhariri wa Jarida, Africa Analysis.
Hawa wote watatu kaka zangu nitakuja kukutananao Ulaya, Ahmed Rajab na Simba Waziri London na Simba tukakutana tena Tehran, Iran miaka mingi sana baada ya kukutana London.
Wakati huo Smba Waziri akiwa Mwambata wa Kijeshi katika Ubalozi wa Tanzania.
Nimeweka picha hapo chini ya mwisho nikiwa na Simba Waziri Tehran.
Salim Himidi nimekutananae Tanga kwa mara ya kwanza nkajulishwa kwake na ndugu yake Mohamed Mshangama na tukawa marafiki wakubwa akawa akija Dar es Salaam ananitembelea nyumbani kwangu.
Nilimtembelea Salim Himidi Paris mwaka wa 2011 safari ambayo kwa hakika ndipo nilipomjua Salim Himidi vizuri sana.
Maisha yake yangetosha kwa Steven Spielberg kutengeneza senema ya kusisimua.
Kijana mdogo wa Kizanzibari aliyesafari ''overland,'' akivuka mipaka nchi moja baada ya nyingine hadi Cairo kisha akavuka Bahari ya Mediterranean hadi akaingia Ulaya na kufika Ufaransa akasoma vizuri.
Akarudi nyumbani akajikuta Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje Comoro.
Serikali yake ikapinduliwa na mamluki kutoka Afrika Kusini wakiongozwa na Bob Denard.
Nilikuwa sichoki kumsikiliza Salim Himidi kutwa nzima tukiranda mitaa ya Paris.
Nilikwisha kumwomba kuandika kumbukumbu zake.
Hakuandika.
Moja ya picha nilzopiga na Salim Himid Paris ambayo naipenda sana ni hiyo nimeiweka chini kabisa tuko katika hoteli tunakunywa chai, sambusa na kababu.
Salim Himidi alikuwa akinambia kuwa akiwa katika hoteli hii akinywa chai na sambusa inamkumbusha Zanzibar.
Miaka imekwenda.
Picha tatu zilizobaki ikiwa utapenda kuziona ingia: https://m.facebook.com/story.php?st...W2GCkTLdqAyEbhLf7DpxXwwxEl&id=100022121633704
Picha ya kwanza niliyoweka hapa kaniletea rafiki yangu Mohamed Abdul Rahman kutoka Ujerumani.
Picha hii kulia ni Salim Himidi katikati ni Joachim Chisano na kushoto ni Ahmed Rajab.
Joachim Chisano alikuwa rais wa pil wa Msumbuji.
Mohamed kaniletea picha hii kwa makusudi kwani Ahmed Rajab, Salim Himidi ni kaka zetu na tumeingiliananao kwa mengi kwa miaka mingi utotoni.
Picha hii ndiyo ilinifanya niingie Maktaba nitafute picha za zamani sana za hawa kaka zangu za miaka ya mwanzoni 1960.
Picha ya chini ya hiyo alinletea yeye huyo Mohamed kiasi cha miaka miwili iliyopita alipofariki Salim Himid ikimuonyesha Salim Himidi kushoto akiwa na Ahmed Rajab katikati na Simba Waziri kulia.
Maka hiyo mimi ni mdogo sana ndiyo nakua katika mitaa ya Kariakoo na nakumbuka nilikuwa nikienda nyumbani kwao Simba Waziiri, Mtaa wa Tandamti mdogo wake sasa ni marehemu Iddi Waziri alikuwa akinionyesha picha za kaka yake Simba Waziri wakati huo mwanafunzi chuo cha kijeshi Uingereza, Sandhurst.
Nakumbuko moja ya picha ambayo niliona ni hiyo ambayo ilipigwa Trafalgar Square hapo kwenye njiwa wengi akwa na Ahmed Rajab na Salim Himidi.
Haikunipitikia wakati ule hata kwa mbali kuwa ipo siku nitasimama hapo Trafalgar Square nikiwa na Ahmed Rajab na ntapiga picha.
Nakumbuka kama jana vile nina umri wa mika 15 au zaidi kidogo na ilkuwa tukimaliza kutazama picha tunamaliza kwa kuimba nyimbo za Cliff Richard na Iddi Waziri nyimbo yake aliyokuwa akiipenda sana ilikuwa ''High Class Baby.''
Wala haikunipitikia miaka ile ya mwanzoni 1960s kuwa hawa ninaowaangalia katika picha hiyo ya Trafalgar Square nitakuja kukutananao hapa nyumbani Tanzania na Ulaya na kwengineko na watakuwa marafiki na wazungumzaji wangu wakubwa.
Picha ya juu niko na Ahmed Rajab ofisini kwake Barbican, London wakati huo alikuwa Mhariri wa Jarida, Africa Analysis.
Hawa wote watatu kaka zangu nitakuja kukutananao Ulaya, Ahmed Rajab na Simba Waziri London na Simba tukakutana tena Tehran, Iran miaka mingi sana baada ya kukutana London.
Wakati huo Smba Waziri akiwa Mwambata wa Kijeshi katika Ubalozi wa Tanzania.
Nimeweka picha hapo chini ya mwisho nikiwa na Simba Waziri Tehran.
Salim Himidi nimekutananae Tanga kwa mara ya kwanza nkajulishwa kwake na ndugu yake Mohamed Mshangama na tukawa marafiki wakubwa akawa akija Dar es Salaam ananitembelea nyumbani kwangu.
Nilimtembelea Salim Himidi Paris mwaka wa 2011 safari ambayo kwa hakika ndipo nilipomjua Salim Himidi vizuri sana.
Maisha yake yangetosha kwa Steven Spielberg kutengeneza senema ya kusisimua.
Kijana mdogo wa Kizanzibari aliyesafari ''overland,'' akivuka mipaka nchi moja baada ya nyingine hadi Cairo kisha akavuka Bahari ya Mediterranean hadi akaingia Ulaya na kufika Ufaransa akasoma vizuri.
Akarudi nyumbani akajikuta Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje Comoro.
Serikali yake ikapinduliwa na mamluki kutoka Afrika Kusini wakiongozwa na Bob Denard.
Nilikuwa sichoki kumsikiliza Salim Himidi kutwa nzima tukiranda mitaa ya Paris.
Nilikwisha kumwomba kuandika kumbukumbu zake.
Hakuandika.
Moja ya picha nilzopiga na Salim Himid Paris ambayo naipenda sana ni hiyo nimeiweka chini kabisa tuko katika hoteli tunakunywa chai, sambusa na kababu.
Salim Himidi alikuwa akinambia kuwa akiwa katika hoteli hii akinywa chai na sambusa inamkumbusha Zanzibar.
Miaka imekwenda.
Picha tatu zilizobaki ikiwa utapenda kuziona ingia: https://m.facebook.com/story.php?st...W2GCkTLdqAyEbhLf7DpxXwwxEl&id=100022121633704