TANZIA Ahmed Yahya Abdulwakil, mbunge wa Kwahani afariki dunia

TANZIA Ahmed Yahya Abdulwakil, mbunge wa Kwahani afariki dunia

LUS0MYA

JF-Expert Member
Joined
Aug 4, 2011
Posts
866
Reaction score
1,109
Tanzia.jpg

Spika wa Bunge la Tanzania Dkt. Tulia Ackson ametangaza kifo cha mbunge wa Jimbo la Kwahani, Zanzibar Ahmed Yahya Abdulwakil ambaye amefariki ghafla kwa shinikizo la damu.

Dkt. Tulia amelazimika kuahirisha shughuli za Bunge hadi Aprili 15, 2024.

Kwahani.JPG

Ahmed Yahya Abdul-wakil enzi za uhai wake
---
Mwili wa Mbunge wa Kwahani (CCM), Ahmed Yahya Abdulwakil (65) unatarajiwa kuzikwa leo Jumanne, Aprili 9, 2024 kijijini kwao Buyuni Zanzibar.

Taarifa za kifo chake zilitangazwa jana Jumatatu Aprili 8, 2024 na Spika wa Bunge Dk Tulia Ackson kuwa kifo hicho kilichotokana na shinikizo la damu, kilitokea Zanzibar.

“Amefariki ghafla kwa shinikizo la damu. Mazishi ya marehemu yanatarajiwa kufanyika kesho (leo) Aprili 9, 2024 kijijini kwao Buyuni Zanzibar.”

Amesema kwa mujibu wa kanuni za Uendeshaji wa Bunge ya 173 kufuatia msiba huo, leo Jumanne Aprili 9 hakuna kikao cha Bunge ili kutoa fursa ya wabunge kushiriki katika msiba huo.

Abdulwakil alizaliwa Mei 19, 1958. Enzi za uhai wake amekuwa kuwa Mwakilishi katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar 2017/2020 na katika uchaguzi mkuu 2020 aligombea uvunge katika Jimbo la Kwahani na kuibuka mshindi.

Jimbo hilo awali lilikuwa linaongozwa na Dk Hussein Mwinyi ambaye mwaka 2020 alipitishwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) kugombea urais wa Zanzibar na kushinda.

Abdulwakil ni mbunge wa nane kufariki dunia katika Bunge la 12, kati yao watano ni wabunge wa majimbo na wawili wa viti maalumu.

Wabunge wengine waliofariki dunia ni Atashasta Nditiye (Muhambwe), Elias Kwandikwa (Ushetu), William Ole Nasha (Ngorongoro), Said Khatibu Haji (Konde), Martha Umbula na Irene Ndyamukama waliokuwa wabunge wa viti maalumu.
 
Pole kwa familia na Mungu aiweke mahali pema peponi roho ya Mbunge.
 
Taarifa ya Spika...Ahmed Yahya Abdulwakil mbunge wa Kwahani Zanzibar afariki ghafla kwa shinikizo la damu.
R.I.P Mh. Ahmed Y. Abdulwakili

Mwenyezi Mungu akuweke mahali unapostahili..
Amen...
 
RIP Mh. Mbunge. Kwa hakika Mwenyezi Mungu akujalie pepo iliyo njema kwa kutwaliwa mwezi huu wa neema.
 
Vifo vya ghafla vinataka kuwa vingi kwa sasa!
 
Back
Top Bottom