Aibu! Aibu! Aibu! National Stadium!!!

MTAZAMO

JF-Expert Member
Joined
Feb 8, 2011
Posts
19,675
Reaction score
33,583
Hivi tumerogwa!,

Toka game ya deby uwanja ni mchafu hadi leo ni hali mbaya! mbaya! mbaya! We can't manage even such tiny thing? Usafi kweli?

Tukubaliane hii nchi yetu kubadili fikra na utendaji wa watu wetu inabidi uwe kichaa kidogo. Tunatia aibu mno tena kwa mambo ambayo hata tungefungia mbuzi mule mwaka wangejiongoza kiusafi.

Inatia hasira sana! Kila jambo mpaka tusukumwe , tufokeane, tuzalilishane! Waziri apige simu! Bagladesh!

Kama vipi huo uwanja mpeni Bakhresa auendeshe kibiashara kuliko hali hii ya sasa. Ni dhahiri public entity zilishafeli kwenye biashara na hazina muono wa kibiashara.

Aibu! Sana!
 
Wafrika akili tunazo ila wapo wasofahamu namna ya kuzitumia.

Ila jukumu la kuhakikisha uwanja upo kwenye viwango vinavyotakiwa ni la meneja wa uwanja.

Na ile fedha ikiingia ya viingilio yaliwa yote au kupotea kusojulikana.

Uwanja kama huo wahitaji matunzo kwa kila kitu nyasi, vyoo sakafu na mazingira kwa ujumla.

Wahitaji kunukia ukiingia wajisikia raha.
 
Mzee wa Lupaso R.I.P alisisitiza sana kuhusu matunzo ya uwanja lakini wapi bongo ni bongo tu bwana hata iweje.
 
Mzee wa Lupaso R.I.P alisisitiza sana kuhusu matunzo ya uwanja lakini wapi bongo ni bongo tu bwana hata iweje.
Kwa mfano ukizungumzia ajira basi hapo kwenye usafi ni kampuni ya usafi, uwanja basi kuna groundswork team.

Halafu viwanja vingi vina mtu wake mmalum kwa jili ya hali ya uwanja kwenye dimba lenyewe yaani zile nyasi huyu aitwa groundsman.

Yaani kwa watu ambao tumezoea kuingia viwanja vya maana vya mpira kila siku twatamani kucopy and Paste ya huko nje.

Ila wahuni hawatakubali.
 
Kinachotutofautisha na wenzetu ni matumizi ya akili tu , tungekuwa kama wao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…