Aina ya uchezaji wa Kibu Denis na Morrison hauna msaada kwa Simba yenye njaa na mataji

Aina ya uchezaji wa Kibu Denis na Morrison hauna msaada kwa Simba yenye njaa na mataji

SankaraBoukaka

JF-Expert Member
Joined
Jul 2, 2019
Posts
1,213
Reaction score
1,918
Simba kama moja ya klabu kubwa Afrika inahitaji kuwa na wachezaji wenye mwendelezo mzuri wa perfomance kiwanjani ili idumu kwenye hadhi na nafasi yake.

Tokea msimu huu 2021/22 umeanza imeonekana kwamba Kibu Denis na Bernard Morrison wameingia kwenye kikosi cha kwanza. Ni wachezaji wazuri sana kwenye kasi na mara nyingi husababisha faulo nyingi kutokana na hiyo kasi yao.. Na wamefunga na magoli muhimu kwenye mechi walizocheza.

Tatizo walilonalo hawa wachezaji ni ubinafsi uliopitiliza ambao unainyima Simba nafasi ya kufunga magoli mengi kwenye nafasi zilizo wazi.

Hawa wachezaji wanapenda ku-dribble, yaani wao kila muda ni kukaa na mpira sana miguuni wakati wenzao wameshaji-position vizuri kiufungaji au kuelekea kwenye goli pinzani. Ujinga zaidi mwishowe hupoteza kizembe au hulazimisha kupiga mashuti yasiyo na madhara yoyote kwa timu pinzani.

Mechi na JKT Tanzania kijana Mwinuke alifanya mambo ambayo Kibu Denis ni nadra au hayawezi kabisa kufanya, nafkiri kama angeamainiwa basi angkuwa na msaada kuliko Kibu ambaye ni JESHI LA MTU MMOJA.

Mpira wa kisasa unahitaji wachezaji wanaocheza kitimu, kwakuwa ndo mfumo wenye manufaa zaidi kuliko uchezaji wa kibinafsi usio na manufaa.
 
Tukisema wachezaji wengine mmepigwa au mmesajili kukurupuka kimihemuko mnaanza kutuita HATERS. Time will tell

Huko mbeleni naona fyekeo kubwa laja kwa wachezaji wazawa na ma pro..
 
Morrison ni mchezaji mzuri akiachana na show off, alikadhalika kibu

Kibu ni kijamaa fulani hivi chenye ubinafsi na choyo, hua nakivutia picha sijui kinaishije huko mtaani hawa ndo type ya wale watu wanaonyima hata maji ya kunywa ukiomba
 
Ndiyo maana Guardiola alivyotua Man city akabadilisha Aina ya uchezaji wa Aguero [emoji23][emoji23][emoji23]

Kuna mechi licha ya kufunga goli mbili bado Aguero alilaumiwa

Sembuse akina molisoni wanaosubiri free kick
 
Kibu Denis

Ana Vitu karibia vingi Muhimu kwa Mchezaji wa Ushambuliaji anatakiwa awe navyo ila ana shida kidogo katika Kufikiri kwa haraka na hili si jambo geni kwa Wachezaji wengi na naamini kwa Msaada wa Makocha Pablo Martins, Selemani Matola na Hitimana Thierry atabadilika na namuona Mbwana Samatta mwingine ndani ya Kibu Denis kama tu akikubali Kubadilika na Kujifunza zaidi.

Bernard Morrison

Ana Kipaji kikubwa sana, Mbunifu na Mwepesi isipokuwa tu anaangushwa na Nidhamu mbovu, Utoto, Uchoyo, anakamia kwa Kupitiliza na kutaka Kucheza zaidi na Jukwaa. Pia hana Pumzi ya dakika 90 ila anayo tu ya dakika 45.

Kibu Denis kwa Simba SC ya miaka Mitatu ijayo atakuwa na Msaada Kwetu hivyo asiachwe, ila Bernard Morrison namuona ana Msaada kwa mwaka ( msimu ) huu tu ila kwa mwakani ( Msimu ujao ) hatokuwa na Umahiri sana sana atakuwa anachezea tu Jina lake na siyo Ufanisi wake Kimechezo na Kiuchezaji.

Yangu ni haya tu kwa sasa Mkuu wangu.
 
Kibu Denis

Ana Vitu karibia vingi Muhimu kwa Mchezaji wa Ushambuliaji anatakiwa awe navyo ila ana shida kidogo katika Kufikiri kwa haraka na hili si jambo geni kwa Wachezaji wengi na naamini kwa Msaada wa Makocha Pablo Martins, Selemani Matola na Hitimana Thierry atabadilika na namuona Mbwana Samatta mwingine ndani ya Kibu Denis kama tu akikubali Kubadilika na Kujifunza zaidi.

Bernard Morrison

Ana Kipaji kikubwa sana, Mbunifu na Mwepesi isipokuwa tu anaangushwa na Nidhamu mbovu, Utoto, Uchoyo, anakamia kwa Kupitiliza na kutaka Kucheza zaidi na Jukwaa. Pia hana Pumzi ya dakika 90 ila anayo tu ya dakika 45.

Kibu Denis kwa Simba SC ya miaka Mitatu ijayo atakuwa na Msaada Kwetu hivyo asiachwe, ila Bernard Morrison namuona ana Msaada kwa mwaka ( msimu ) huu tu ila kwa mwakani ( Msimu ujao ) hatokuwa na Umahiri sana sana atakuwa anachezea tu Jina lake na siyo Ufanisi wake Kimechezo na Kiuchezaji.

Yangu ni haya tu kwa sasa Mkuu wangu.
I think Chikwende (sijui kama bado ni mchezaji wa Simba au la) anafit sana kwa huu mfumo wa sasa wa Pablo wa kucheza wide, angepewa Wing moja things would have been different kidogo kuliko matumizi ya Morrison...
Ndo maana Sven na Gomez walikuwa wanampa Morrison mara nyingi dakika 15 za mwisho tena haswa haswa anapohitajika mchezaji wa kubadilisha mchezo mambo yanapokuwa magumu,,, ila siyo mchezaji wa kucheza dakika 90, anakera to the maximum...
 
Kibu ni mchezaji mzuri ana pumzi, kasi, nguvu, anatembea na mpira. Mapungufu yake makubwa ni kukosa mbinu za ufungaji na kukosa utulivu mbele ya goli. Yeye ana staili moja tu ya kufunga nayo ni kupiga mashuti tu. Iwapo benchi la ufundi la Simba litaweza kumfundisha namna mbalimbali za kufunga kama kupress mpira, kucurve, kuchop n.k. basi Simba itakuwa na bonge la mshambuliaji.

Kuhusu Morison kwa kweli huyu jamaa tukubali tukatae jamaa ana akili sana ya mpira na anaujua na kuuweza mpira vizuri sana. Tatizo lake kubwa ni mizaha uwanjani na utovu wa nidhamu na ubinafsi kidogo anao . Siku Morison akiamua kwa dhati ya moyo wake kuwa anaacha kabisa mizaha na utovu wa nidhamu na kupunguza ubinafsi basi ataisaidia sana Simba kuliko msaada anautoa sasa hivi. Na zaidi ajifunze kukaba kwani mara nyingi anapiga chenga zisizo na faida badala ya kutoa pasi kwa haraka halafu akinyangánywa mpira anatembea anawaachia msala viungo na mabeki wake.

Wote wawili wasipojirekebisha kwa wakati shauri zao kwani jinsi ninavyoona sajili za Simba zinavyoenda basi baada ya msimu mmoja au miwili watakuja kuwa historia.
 
Mimi nishaongea hapa kuhudu kibu kuwa Ana papara nyingi sana

Morrison mzee wasifa sna kutaka kucheza na jukwaa pia Ana tabia ya kulazimisha kupiga chenga hata sehem ambayo alipaswa atoe pass ,hapa sasa ndio unaona umuhimu wa chama kwenye jicho la kugawa pass kwa haraka
 
Hii ni kweli. Tena huyo Morrison ndo kabisa hana consistency. This time atacheza vzr next mechi hatoonekana. Anaperfom vzr kwa timu isiyomjua but kwa ligi ya ndani hawezi kabisa..
mechi moja akifanya vizuri akasifiwa inayofuata anaanza show off
 
Kibu denis ni mchezaji mzuli sana ila tatizo lake ni kwenye kumalizia kwenye umaliziaji hawez anatakiwa agawe mpira mana hana maamuz,wala mbinu za haraka katika ufungaji namuona kama ni mchoyo katika ugawaji mpira .
 
Mimi nishaongea hapa kuhudu kibu kuwa Ana papara nyingi sana

Morrison mzee wasifa sna kutaka kucheza na jukwaa pia Ana tabia ya kulazimisha kupiga chenga hata sehem ambayo alipaswa atoe pass ,hapa sasa ndio unaona umuhimu wa chama kwenye jicho la kugawa pass kwa haraka
Huyo Chama mtaendelea kumuota tu
 
Wakimbizi tangu lini wakacheza soka.
Huyo mvuta bange wa Ghana simba tumepigwa pazito
 
Wakimbizi tangu lini wakacheza soka.
Huyo mvuta bange wa Ghana simba tumepigwa pazito
We bwege itakuwa unaishi kwa shemeji yako,, lkn endapo ungekuwa ushawahi japo kuvuka boda hata nchi moja kisha ubaguliwe kwa utaifa wako ndo utajua ubaya wa ubaguzi,,
 
Ndo hao hao Wameiingiza Simba Makundi hivyo....!
Wakati Utopolo Wanaendelea Kuugulia Kipigo cha Nje ndani Cha Rivers.
Ndugu makundi mmeingia kwa tiketi ya viti maalum! Kumbukumbu zinaonesha mlidhalilishwa kwa Mkapa na wale Makilikili!
 
Back
Top Bottom