Aina ya watu unaopaswa kuwaepuka kwenye maisha yako. Hawa ni sumu ya mafanikio yako.

Aina ya watu unaopaswa kuwaepuka kwenye maisha yako. Hawa ni sumu ya mafanikio yako.

Kibenje KK

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2016
Posts
270
Reaction score
391
Kuna watu wako maalum KUUA NDOTO YAKO(Dream killer) , Ni aina ya watu wabaya ambao kazi yao ni kuhakikisha wewe hufanyi kitu na hufanikiwi kutimiza ndoto yako.
-
Ni watu gani?
-
1.Mtu mwenye imani ndogo.
Huyu ni mtu anaamini katika udogo, haamini kama unaweza kuwa na biashara kubwa, haamini kama unaweza kufika mbali, haamini kama unaweza kujisimamia mwenyewe ukafika mbali.
( Atakuambia haiwezekani kwenye kila jambo kubwa unalolitaka)

2.Mtu mwenye Wivu mbaya.
Hawa ni watu ata ukinunua gari wataanza '' Gari yenyewe ina rangi mbaya na hizi ajali za siku hizi''
Watasema ''Duh umeona mwanaume aliyeolewa naye? Ndo mwanaume gani?
Hawa hata ufanye zuri la namna gani, kwa sababu ya wivu wao hawawezi kukusifia sana sana watakukatisha tamaa uwe kama wao. (mafanikio yako yanamuhuzunisha) ndo wale nguo nzuri ila shape yako sasa 🤣🤣
__
3.Mtu aliyeumizwa sana na ambaye moyo wake haujapona vizuri. Huyu atakushauri kwa hasira na uchungu. Mara nyingi hawa wako kwenye mahusiano. Atakwambia wanaume wote ni ...., hakuna mwanamke wa kuoa siku hizi, biashara hazilipi, hakuna kazi za maana.
Hawa yaliyowatokea kwao hudhani ni lazima yatokee kwako pia.
_____
4.Mtu anayekukosoa-kosoa.
Hawa wamejaa sana, Binafsi mwanzoni nilikutana nao sana, hawa dawa yao ni kuziba masikio huwa hawaoni lolote jema. wakati mwingine sikiliza na jirekebishe inapobidi lakini nia yao ni kukufanya ujione hujui kitu.
_
5.Mtu asiye na Maono.
Kipofu wa kifikra, Huyu hana ndoto inayomsukuma kufanya kitu, Ni aina ya watu waliokuja Duniani kutembea yaani chochote kinachotokea anaona ni sawa tu. Huyu ukiwa karibu naye atakuharibia ndoto yako.
_
Niambie ni nani umemkutana sana kati ya hawa watano?
#kelvinkibenje
#bego
od
 
Kwa bahati mbaya nimekutana na watu wa hayo makundi yote matano! Na kwakweli wamenirudisha sana nyumba kimaendeleo, kwa sababu ya kuwamini.

Ahueni baada ya kuwagundua, nimeamua kuwapotezea. Na hivyo nimeamua sasa kupambana zidi mwenyewe, na kwa kutumia falsasa zangu. Kati ya wote niliowahi kuwaomba ushauri, kuna boya mmoja huyo ndiyo nina hasira naye mpaka kesho.


Maana nilimuomba ushauri wa kuanzisha biashara fulani hivi ambayo na yeye alikuwa akiifanya kwa wakati huo!! Kiukweli alinikatisha tamaa mpaka nikaahirisha kufanya ile biashara iliyokuwa na faida kubwa ukilinganisha na hii ya kizee ninayoifanya sasa!

Ona sasa leo hii nimebakia tu kujilaumu kwa nini nilimuuliza! Kwa nini nilimsikiliza na kumuamini! Ningefanya maamuzi yangu kimya kimya, huenda leo hii na mimi ningekuwa namiliki kampuni kubwa tu hapa nchini.
 
Amin sana ubongo wako...hata kama haufanyi kaz kwa asilimia kadhaa uamin tuu...kikubwa Mungu ametupa utashi..basi ukiutumia vibaya au vizur...utakupa matokeo tuu...
 
Kwa bahati mbaya nimekutana na watu wa hayo makundi yote matano! Na kwakweli wamenirudisha sana nyumba kimaendeleo, kwa sababu ya kuwamini.

Ahueni baada ya kuwagundua, nimeamua kuwapotezea. Na hivyo nimeamua sasa kupambana zidi mwenyewe, na kwa kutumia falsasa zangu. Kati ya wote niliowahi kuwaomba ushauri, kuna boya mmoja huyo ndiyo nina hasira naye mpaka kesho.


Maana nilimuomba ushauri wa kuanzisha biashara fulani hivi ambayo na yeye alikuwa akiifanya kwa wakati huo!! Kiukweli alinikatisha tamaa mpaka nikaahirisha kufanya ile biashara iliyokuwa na faida kubwa ukilinganisha na hii ya kizee ninayoifanya sasa!

Ona sasa leo hii nimebakia tu kujilaumu kwa nini nilimuuliza! Kwa nini nilimsikiliza na kumuamini! Ningefanya maamuzi yangu kimya kimya, huenda leo hii na mimi ningekuwa namiliki kampuni kubwa tu hapa nchini.
Mkuu kwema,kumbe ukiachana na mambo ya yanga.kumbe upo vizuri
 
Kuna watu wako maalum KUUA NDOTO YAKO(Dream killer) , Ni aina ya watu wabaya ambao kazi yao ni kuhakikisha wewe hufanyi kitu na hufanikiwi kutimiza ndoto yako.
-
Ni watu gani?
-
1.Mtu mwenye imani ndogo.
Huyu ni mtu anaamini katika udogo, haamini kama unaweza kuwa na biashara kubwa, haamini kama unaweza kufika mbali, haamini kama unaweza kujisimamia mwenyewe ukafika mbali.
( Atakuambia haiwezekani kwenye kila jambo kubwa unalolitaka)

2.Mtu mwenye Wivu mbaya.
Hawa ni watu ata ukinunua gari wataanza '' Gari yenyewe ina rangi mbaya na hizi ajali za siku hizi''
Watasema ''Duh umeona mwanaume aliyeolewa naye? Ndo mwanaume gani?
Hawa hata ufanye zuri la namna gani, kwa sababu ya wivu wao hawawezi kukusifia sana sana watakukatisha tamaa uwe kama wao. (mafanikio yako yanamuhuzunisha) ndo wale nguo nzuri ila shape yako sasa 🤣🤣
__
3.Mtu aliyeumizwa sana na ambaye moyo wake haujapona vizuri. Huyu atakushauri kwa hasira na uchungu. Mara nyingi hawa wako kwenye mahusiano. Atakwambia wanaume wote ni ...., hakuna mwanamke wa kuoa siku hizi, biashara hazilipi, hakuna kazi za maana.
Hawa yaliyowatokea kwao hudhani ni lazima yatokee kwako pia.
_____
4.Mtu anayekukosoa-kosoa.
Hawa wamejaa sana, Binafsi mwanzoni nilikutana nao sana, hawa dawa yao ni kuziba masikio huwa hawaoni lolote jema. wakati mwingine sikiliza na jirekebishe inapobidi lakini nia yao ni kukufanya ujione hujui kitu.
_
5.Mtu asiye na Maono.
Kipofu wa kifikra, Huyu hana ndoto inayomsukuma kufanya kitu, Ni aina ya watu waliokuja Duniani kutembea yaani chochote kinachotokea anaona ni sawa tu. Huyu ukiwa karibu naye atakuharibia ndoto yako.
_
Niambie ni nani umemkutana sana kati ya hawa watano?
#kelvinkibenje
#bego
od
Mimi kwa mtazamo wangu ni kumuepuko mtu yoyote. Binadamu tumekuwa wanafiki huwezi ukamtambua mtu kwa kumuangalia tu
 
Utasikia wanaume wote waongo tu au wanaume hawana maana au wanaume wote washenzi tu,ujuwe hapa iko shida,halafu ukute watoto anaozaa wote wanaume,sasa unajiuliza hao watoto wake nao wako kwenye hilo kundi au wao hawamo...!
 
Mimu kwa mtazamo wangu ni kumueouko mtu yoyote. Binadamu tumekuwa wanafiki huwezi ukamtambua mtu kwa kumuangalia tu

Ndio maana nawaambia watu Mara zote, binadamu wote ni kama tuna asili ya ubinafsi au nitumie neno baya ( roho mbaya). Inahitaji jitihada kubwa sana kujikwamua kwenye hiyo Hali. Yaani Ile uweze kufurahia kabisa mafanikio ya mwenzako kiroho safi, au usaidie wengine kufanikiwa, wachache sana wanaweza.

Watu wakisikia umepata tatizo au mambo yamekuendea vibaya ndio watafurahia, hata kama wataonyesha wako nawewe Kwa maneno lakini ndani kabisa kwenye nafsi zao ni furaha tele.

Ukitaka uwe na furaha ya kweli, jitahidi kuwasaidia au kuwawezesha wengine, hata Kwa mawazo na ushauri. Wape moyo na matumaini.
Haikupunguzii kitu, na sio kwamba mwingine akikosa, unapata wewe.
 
Kwa bahati mbaya nimekutana na watu wa hayo makundi yote matano! Na kwakweli wamenirudisha sana nyumba kimaendeleo, kwa sababu ya kuwamini.

Ahueni baada ya kuwagundua, nimeamua kuwapotezea. Na hivyo nimeamua sasa kupambana zidi mwenyewe, na kwa kutumia falsasa zangu. Kati ya wote niliowahi kuwaomba ushauri, kuna boya mmoja huyo ndiyo nina hasira naye mpaka kesho.


Maana nilimuomba ushauri wa kuanzisha biashara fulani hivi ambayo na yeye alikuwa akiifanya kwa wakati huo!! Kiukweli alinikatisha tamaa mpaka nikaahirisha kufanya ile biashara iliyokuwa na faida kubwa ukilinganisha na hii ya kizee ninayoifanya sasa!

Ona sasa leo hii nimebakia tu kujilaumu kwa nini nilimuuliza! Kwa nini nilimsikiliza na kumuamini! Ningefanya maamuzi yangu kimya kimya, huenda leo hii na mimi ningekuwa namiliki kampuni kubwa tu hapa nchini.
IMG-20220917-WA0037.jpg
 
Lakini Kuna wakati tunawahitaji watu wa namna hii ili kutuimarisha, kutupa elimu na kufanya twende hatua kubwa zaidi mbele. Wanakusaidia usibweteke na kuongeza umakini.
 
Back
Top Bottom