Malaika wa Misukosuko
JF-Expert Member
- Jul 16, 2021
- 2,470
- 7,376
Ps4 Flat dukani 500k linakuwa na pads mbili na games kadhaa inategemea na muuzaji uliyenunua.Vip gharama zake huwa zina range bei gan console+games?
Ahsante bro ngoja nijipange nidake hyo ps4 slim🙏Ps4 Flat dukani 500k linakuwa na pads mbili na games kadhaa inategemea na muuzaji uliyenunua.
Ps4 Slim dukani 680k + pads mbili na games ngapi inategemea na muuzaji,
Ps4 pro bei kuanzia 850k + pads mbili na games kadhaa
Pads za Ps4 original unapata kuanzia bei ya 100k kwa pad moja ila pads za kawaida tu unapata kuanzia 50k kwa pad moja .
Ppoa kaka ila hizi ni bei za mwanzo tu kwa wauzaji wengi ila kiufupi huwa wanashusha mpaka hadi 600k mfano kwa hiyo Ps4 slim, na ukinunua kwa mtu hata kwa 500k Ps4 slim unapata.Ahsante bro ngoja nijipange nidake hyo ps4 slim🙏
Mkuu Off-Topic kidogo, Ni website zipi ziko njema kwa ku download magemu ya PC, mfano Farcry 6 na kadhalika yenye GB za kutosha, ukiachia Torrents.Fat na slim ni za mwanzo zinafanana perfomance ila kiumbo kama unavyoona majina yake moja inakuwa nene na kubwa na nyengine inakuwa nyembamba na ndogo
Ps4 pro ilikuja baadae perfomance wise ipo vizuri, ps4 zote zitacheza games sawa ila pro itacheza hizo games kwa quality kubwa.
Mtu anaposema version 9 hii ni version ya mwisho ya ps4 ambayo inachakachulika na kuweka games bure
So ili ps4 iweze kuchipiwa unahitaji hii version
Ps4 iliochipiwa itacheza games bure ila huchezi online, isiochipiwa utanunua games ama account za magumashi ila utacheza online angalia matumizi yako.
Dod repack,fit girl repackMkuu Off-Topic kidogo, Ni website zipi ziko njema kwa ku download magemu ya PC, mfano Farcry 6 na kadhalika yenye GB za kutosha, ukiachia Torrents.
Kama mdau alivyo jibu fitgirl wanaweka direct link, sema kama una hela nunua/Tafuta real debrid account, utadownload kitu chochote kilicho kwenye internet direct na kwa speed kubwa.Mkuu Off-Topic kidogo, Ni website zipi ziko njema kwa ku download magemu ya PC, mfano Farcry 6 na kadhalika yenye GB za kutosha, ukiachia Torrents.
P1 bruh💪Chukua Ps4 Slim Version ya 9.00. Ni mashine ya kazi haina changamoto za mara kwa mara. Ps4 Fat zinazingua sana hasa ukichezesha mda mrefu mfululizo bila kuzipumzisha.
Kwa huduma za Kuingiza Games,
Tuwasiliane.
Mkuu, real debrid ndio kitu gani. Tufafanulie kidogo.Kama mdau alivyo jibu fitgirl wanaweka direct link, sema kama una hela nunua/Tafuta real debrid account, utadownload kitu chochote kilicho kwenye internet direct na kwa speed kubwa.
Unakumbuka zamani kulikua na premium link generator na torrent to IDm ambazo unaweka link ya torrent ina convert kuwa ya IDm?Mkuu, real debrid ndio kitu gani. Tufafanulie kidogo.
Mkuu naomba kujua kuhusu PS5 , nataka kununua ila sijajua ninunue lipi maana nataka kwaajili ya nyumbani tu sio kwa biashara, ufafanuzi wako pleaseNgoja nikupe muongozo kidogo tu maana mi mwenyewe nina Ps4 kwahyo sibahatishi huu ushauri naokupa,
Sifa za Ps4 Flat(FAT) ni kwamba yenyewe inakuwa pana kidogo na ina ngazi ila hii kwa matumizi ya nyumbani inafaa na inakula umeme mdogo, udhaifu wake ni kwamba ikitumika muda mrefu huanza kuleta matatizo ya kuchemka kupitiliza na ikichezewa masaa 7 mfululizo hujizima ghafla.
Pia hizi ni bei rahisi kidogo ila kama unataka kufungua biashara sikushauri ununue hizi maan zikishatumika muda mrefu zinaanza matatizo.
Ps4 Slim hili nalijua nje ndan maana nalimiliki, kiufupi hili linaweza tumika hata miaka na halina tatizo lolote,
kwenye upande wa umeme linatumia unit 1.4 likitumika kwa masaa 6 mfululizo bila kuzima hapo ni kama unachezea kwenye Tv isiyo na 4K HD ila kama utatumia TV ya 4K unit zitazidi kidogo mpaka 2 unit hivi 6/hrs.
Ps4 pro hili ni bomba sana kama unapenda Good and smooth graphic ila ukitaka kulienjoy hili inabidi uwe na TV ya 4K ndo utafaidi hili game tofauti na hapo ina view kama Ps slim na Fat tu, udhaifu wake yenyewe ni kwenye umeme tu hili linakula sana umeme ila kwenye ubora ni zuri sana.
Kuhusu upande wa Chipped na non-chipped kuanzia version 9 linaweza kuwa chipped ila kuanzia version 11 kwenda juu haiwezekani kuwa chipped, kwa ushauri tu nakushauri bora upate lililo chipped maan sio gharama kupata magemu yake ila ukiwa na non chipped game lake moja ni mpka 65k wakati chipped kwa 25k unaweza kupata game.
Ps non chipped uzuri wake ni kwamba utaweza kuingia online na kuangalia hata Netflix na inaingia internet kama Pc tu na kama upo vzuri kifedha unaweza kuwa unadownload magemu mwenyew tu,
Ps chipped hili kinachofanyika ni kuvunja software isiwe na access ya internet yani sawa na kuiondoa kwenye server za internet kwahyo games zake zitaingizwa kwa mfumo kama wa (Apk + obb ya kwenye simu) hasara yake ni kwamba tu hutopata access ya internet na hutoweza kudownlod games online, na pia hutoweza ku update version ya Ps lako kama itatoka.
So kwa upande wangu mimi ninalo (Ps4 Slim non-chipped) ila changamoto nayopata ni kupata games tu maan ni bei ghali kidogo, kila kitu unacheza offline ila ukitaka kucheza na watu wengine Duniani ndo utawasha Data ili ucheze nao,
Kwa ushauri mi nakushauri tu ununue Ps4 slim na hili ndo pendekezo kubwa linalotolewa na watu wengi wenye Ps maan kwanza ni imara unaweza kulitumia miaka na pia linatumia umeme mdogo usinunue Flat(FAT) na kwakuwa unataka kuchezesha pia sikushauri ununue Ps4 pro maana linakula sana umeme, kama una swali niulize.
Kama uwezo unao nunua ps 5 slim disk versionMkuu naomba kujua kuhusu PS5 , nataka kununua ila sijajua ninunue lipi maana nataka kwaajili ya nyumbani tu sio kwa biashara, ufafanuzi wako please
Chukua Ps5 slim lipo vizuri sanaMkuu naomba kujua kuhusu PS5 , nataka kununua ila sijajua ninunue lipi maana nataka kwaajili ya nyumbani tu sio kwa biashara, ufafanuzi wako please