Air Tanzania ingeshusha viwango vya nauli, tungesafirisha Watanzania wengi ndani na nje ya nchi

Air Tanzania ingeshusha viwango vya nauli, tungesafirisha Watanzania wengi ndani na nje ya nchi

Bonheur Travels Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2020
Posts
252
Reaction score
499
ATCL.jpg

Salaam Great Thinkers,
Tumeanza kutoa huduma ya kusafirisha abiria wanaotumia ndege kusafiri, iwe ni ndani ya nchi au kimataifa, kwa miaka kadhaa sasa. Uzoefu tulionao umepelekea tuzifahamu changamoto nyingi kupitia feedback tunazozipata kutoka kwa wateja/abiria.

Miongoni mwa changamoto hizo tumejaribu kuzitolea elimu na ufafanuzi kwenye threads zetu zilizopita. Leo tumeona tugusie changamoto ya bei ya nauli.

Bei za Tiketi za #AirTanzania zimekuwa zikilalamikiwa na kufanya usafiri wa anga kuwa anasa badala ya huduma. Ni mara nyingi mno tumelazimika kutumia nguvu ya ziada kushawishi wateja kuona kwamba gharama hizi zinaendana na viwango vya huduma nzuri zitolewazo na ATC. Pia tunatumia kete ya kuwasihi watanzania kutanguliza uzalendo kwani Shirika hili bado linajipanga kibiashara, lakini inafikia hatua tunaishiwa sera!

Baadhi ya threads hapa JF ambazo zimeongelea gharama za ndege za ATCL kuwa sio rafiki na hazivumiliki ni pamoja na;




Kwa utafiti wetu ambao sio rasmi, tumegundua Watanzania wengi wanatamani kutumia usafiri huu lakini wanaogopa bei, hasa wale wenye kipato cha kawaida. Routes mpya za Chato na Arusha zilitia hamasa lakini bei zimewarudisha wengi wao nyuma baada ya kukutana na bei tata. Ni idadi kubwa ya watu ambayo ingeweza kulizalishia shirika faida na kurahisisha safari za masafa marefu zikiwemo za kutoka Dar kwenda Mwanza, Kagera, Kigoma n.k. na kinyume chake.

Tunafahamu, lengo la Serikali na Shirika ni kuhakikisha Ndege hizi zilizonunuliwa kwa wingi zinakuwa affordable kwa watanzania wanaofanya safari (ndani na nje ya nchi). Na sisi kwa uzoefu wetu na tabia za wateja tunaliona hili la bei kuwa kikwazo namba moja kinachosababisha hata rate ya wasafiri ku-book ndege hizi za ndani ikishuka au kushindwa kuongezeka katika kiwango kinachoridhisha.

Imefikia hatua zipo baadhi ya routes za ndani zina gharama ya juu zaidi kulinganisha na gharama za ndege kupitia mashirika mengine kwenda nje ya nchi. Hatuingilii mamlaka, tunajaribu tu kufikisha 'picha halisi' kutoka kwa watumiaji wa huduma na mtazamo wetu wadau wa sekta hii muhimu kwa maendeleo ya taifa.

Ni matarajio yetu wanaofanya maamuzi wataliangalia hili kwa ukaribu na kulifanyia kazi haraka. Wakishusha bei, tutasafirisha watanzania wengi popote pale kwa kweli na ndege hazitasafiri tupu, kwani wengi wapo tayari tatizo ni hilo tu- BEI!

Au abiria wazoefu na watarajiwa mnasemaje?
 
Hongera wadau kwa juhudi na bidii yenu. Lakini nafikiri mzingatia kufikisha ushauri wenu kwa wanasiasa wahusika wa sekta yenu ili kufanikiwa. Tanzania kila kitu ni siasa!

Shukrani kwa pongezi mkuu. Tunazingatia sana. Lengo letu ni kurahisisha huduma hii nzuri na kuchangia maboresho kwa maslahi ya pande zote; sekta na wadau.
 
Shida ni kuwa mashirika yaliyokuwa yanatoa huduma kwa gharama nafuu kama fastjet wameyafigisu mpaka kuyatoa ili wao wapate abiria alafu jambo la ajabu wao wameshindwa kulisha wateja kwa sababu ya bei kubwa kwenye nauli zao. Ninatabiri hili shirika kufa tena jiwe akitoka madarakani.
 
Shida ni kuwa mashirika yaliyokuwa yanatoa huduma kwa gharama nafuu kama fastjet wameyafigisu mpaka kuyatoa ili wao wapate abiria alafu jambo la ajabu wao wameshindwa kulisha wateja kwa sababu ya bei kubwa kwenye nauli zao. Ninatabiri hili shirika kufa tena jiwe akitoka madarakani.

Pengine ni suala la huduma kuwa za viwango vya juu na hadhi ya ndege husika, ndivyo vinapelekea hata bei zake kuwa juu kiasi. Tunatoa wito kwao watazame namna nzuri zaidi ya kuja na bei ambazo zitaendana na hali halisi ya wasafiri. Ushindani tunaokutana nao kwenye zoezi la ukataji tiketi huku ni mkubwa sana.
 
I see fastjet achana nao wale jamaaa. Ndio waliamua kuiua hiyo fastjet vinginevyo ATCL wasingefua dafu kwa fastjet. Utaratibu wao ulikuwa unawafanya hata ambao hawajawahi kusafiri na ndege watamani kusafiri.

Kwanza ilikuwa ukifanya booking mapema mfano huu mwezi wa kwanza unasafiri mwezi wa 3, nauli inakuwa chini tumewahi kusafiri kwa laki 156000,go and return Dar to Mbeya.

Kuna muda walikuwa wanatoa offers nzuri tu. Nyanda za juu kusini kidogo kidogo watu walianza kuachana na usafiri wa mabasi labda upende kipindi cha fastjet. Limekuja shirika letu,watu wanasafiri labda waumwe,wote wamerudi kwenye mabasi.
 
Back
Top Bottom