Airports: Kenya vs Tanzania

Serikali kununua ndege mpya tano​



WEDNESDAY AUGUST 10 2022​


Summary

Serikali inakusudia kununua ndege mpya tano katika mwaka wa fedha 2022/23 ikiwemo ndege moja ya mizigo, idadi ambayo itaifanya serikali kuwa na jumla ya ndege 16.



By Mwandishi Wetu
More by this Author

Dar es Salaam. Serikali inakusudia kununua ndege mpya tano katika mwaka wa fedha 2022/23 ikiwemo ndege moja ya mizigo, idadi ambayo itaifanya serikali kuwa na jumla ya ndege 16.

Tayari serikali imetenga Sh353 bilioni katika bajeti ya mwaka huu kwa ajili ya kugharamia masuala mbalimbali katika sekta ya usafiri wa anga ikiwemo ununuzi wa ndege hizo.

Akizungumzia utekelezaji wa bajeti katika wizara yake mwishoni mwa wiki, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa alisema hadi kufikia Mei 2022, Serikali ilikamilisha ununuzi wa ndege tatu mpya na kuzikabidhi kwa Shirika la Ndege nchini (ATCL) na kuendelea kutumika.

Alizitaja ndege hizo kuwa ni Dash 8 Q400 moja yenye uwezo wa kubeba abiria 76 na ndege mbili aina ya Airbus A220-300 zenye uwezo wa kubeba abiria 132 kila moja.

Profesa Mbarawa alisema kuongezeka kwa ndege hizo kumeifanya ATCL kuwa na jumla ya ndege mpya 11 ikilinganishwa na ndege nane zilizokuwepo mwaka 2020/2021.

Waziri huyo alisema malengo ya mwaka wa fedha 2022/23 ni malipo ya ununuzi wa ndege tano mpya ambapo ndege moja ni aina ya Boeing 787-8 Dreamliner, ndege mbili aina ya Boeing 737-9, ndege moja ya mizigo aina ya Boeing 767-300F na ndege moja aina ya Dash 8 Q400.

“Tumepanga kugharamia mahitaji ya awali ya uendeshaji wa ndege tano ambazo ni Boeing 787 – 8, Boeing 737- 9 mbili (2), Boeing 767 - 300F na Dash 8 Q400 (1). Pia, kununua vifaa vya kuhudumia ndege na abiria viwanjani,” alisema Profesa Mbarawa.

Aliongeza kwamba wamepanga kuendelea na ukarabati na ununuzi wa vifaa vya karakana za matengenezo ya ndege (Hangar) za Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA) na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Profesa Mbarawa alibainisha Mipango mingine ya wizara yake mwaka huu kuwa ni ukarabati wa jengo la ofisi za makao makuu ya ATCL lililopo kiwanja cha ndege cha JNIA Terminal I.

Alisema serikali itaendelea na ukarabati wa nyumba 38 zilizopo KIA, kujenga eneo la mafunzo ya awali kwa wana anga, kuendelea kulipa madeni ya Shirika na kukarabati na kujenga majengo ya kuhifadhia mizigo katika viwanja vya ndege vya JNIA, KIA na Songwe.

Kuhusu treni ya kisasa, Profesa Mbarawa alisema Septemba mwaka huu itafanyiwa majaribio na baada ya hapo watatoa taarifa rasmi baadaye kuhusu kuanza kutumika kwa usafiri huo katika kipande cha Dar es Salaam - Morogoro.

 
Ila kenya wako vizuri tu
 

Air Tanzania set to launch Central, West Africa and Europe routes​

ESTHER TAKWA
15/08/2022

Tanzania National Carrier Air Tanzania Company is expecting to launch new flights to Central, West and Europe.

The National carrier’s chief executive officer Eng Ladislaus Matindi revealed this in Dar es Salaam on Monday saying the new destinations, which will be launched by next year, are Nigeria, Ghana and Congo-Kinshasa.

The CEO stated that there will also be a direct flight to London.

He said the carrier is strengthening its operations by reviving their flight to China.

By next year, the CEO said, the flights to Goma and Kinshasa in DRC will be operational.

“Trips to South Africa are coming back but now we are starting trips that will attract people to use Air Tanzania to connect their trips, especially to Europe,” ATCL czar said.

 
warudishe kwanza TCH na waitengeneze TCM we are one plane away from dusrupting routes ..they should be serious with maintance
 
Wewe unajua Jomo kenyatta Airpot au unatania tu....Hili dude moja unganisha vya Tz vyote bado hulikuti
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…