Airtel ni mtandao wa hovyo kabisa sijawahi kuona

Airtel ni mtandao wa hovyo kabisa sijawahi kuona

Sultani Makenga

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2016
Posts
621
Reaction score
1,039
Nimekuwa mteja wa huu mtandao tangu mwaka 2006 ulipokuwa ukijulikana kwa jina la Celtel mpaka leo. Inasikitisha na inaudhi mno kuona kwamba huu mtandao uliotokea kupendwa sana na watu wa vijijini kwa huduma nzuri kipindi cha nyuma ndio mtandao unaoongoza kwa huduma MBOVU KABISA siku hizi.

Ukipiga simu usikivu ni sifuri, customer care hovyo utadhani wako kwenye klabu ya pombe za kienyeji majibu wanayokupa ni ya uongo. Njoo kwenye huduma za kifedha yaani airtelmoney na Timiza ndio ovyo mno. Nilikuwa na utaratibu wa kujiwekea pesa Timiza, juzi nikawa na shida nikaamua nitoe kiasi kidogo kwa ajili ya matumizi ya nyumbani, ili kutoa pesa ni lazima uitoe hela kutoka Timiza kwenda airtelmoney.

Nimeprocess kutoka juzi jumatano saa 2 usiku mpaka sasa ninavyoandika ijumaa hela haionekani na kila nikiwapigia Airtel huduma kwa wateja wanasema wanarekebisha, huo ni upuuzi na ujinga wa kiwango cha juu, kama walikuwa wanajua kwamba kuna marekebisho si wangetutaarifu wateja tukajipanga.

Hizo pesa tulizoweka kwenye huo mtandao wao wa kipuuzi ni zetu siyo mali zao. Nitavunja hilo li laini lao pumbavu kabisa.
 
Ifike muda wateja wa hii mitandao waunde Clubs na viongozi wao wa kushughulikia changamoto zao. Kubadili laini sio solution maana ni hasara hususani kwa wafanyabiashara.

Ila kukiwa na union za wateja ni rahisi hasa kufile kesi na kwenda TCRA Kama kikundi cha watu kuliko kwenda mtu mmoja mmoja.
 
Pole sana mkuu, usitegemee sana hii mitandao hata benki pindi unahitaji wa pesa wa haraka mkuu. Ni vizuri kuwa na pesa kiasi ndani.
 
Kwenye mtandao ndio hovyoooo! Kabisa..wanakupa mb kabao..lakini muda unaisha bala kutumika yaani Ni ujinga mtupu
 
Wajinga sana eti kurenew laini masharti kibao mpaka ukapange foleni makao makuu.
Unaweka pesa yako airtel una akili au matope? Huo mtandao nishahama kitambo sana kurenew laini tu shida utadhani yana huduma nzuri
 
Nawapenda tu kwenye Internet ..ila siwaelewi na utaratibu wa line moja kutumia watu wawili.
 
Airtel mkoani wana 3G watu wanatafuta 5G shida walikwiba sana hapa awamu hii walitiwa adabu hawezi kununua mitambo ya kisasi.
 
Voda ndio baba lao japo wanagharama ila hawana longolongo za kijinga kama hiyo mitandao mingine. Kwenye internet voda hata mnara ukisoma 'e' bado unachat kama kawaida ila hawa wengine ngoma ikishuka tuu kwishinehi babujii
 
Kiukweli Airtel kwa sasa huduma zake hazipo sawa, unaweza ukampigia mtu hata mara 20 unaambiwa haipatikani au ina-disconnect kabisa wakati anakua hewani kabisa, internet inaweza ikatoka siku nzima mpaka muda wa bando kuisha unafika unakuta haujalitumia kabisa.

Airtel Tanzania kuna tatizo tunaomba mrekebishe urudi kama zamani mtandao wetu pendwa.
 
Back
Top Bottom