Airtel wapandisha vifurushi vya internet

njaakalihatari

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2019
Posts
4,081
Reaction score
8,671
Hakuna waziri anayevutia wawekezaji kupata faida kwenye biashara ya DATA kama Nape nnauye, kijana anapiga kazi aiseeee

Nimeamka nakuta kifurushi cha 1500 nilichokuwa naapata gb1 kwa sasa ni mb 850, hapo ukilalamika utasikia Nape anasema TCRA fatilia hao, utasikia mnalalamika nini wakati Tanzania ni ya 6 afrika kwa kuwa na bei nafuu ya bando na ya 3 kwa speed kali?

Utasikia angalieni simu zenu kuna apps zina run backgrounds zinakula data.
 
Manage your data usage yourself, hakuna wakati sasa hivi na kuendelea vifurushi vitashuka bei! Ni kujibajeti upya mwenyewe!
 
Baada ya Baba kuondoka sasa warina asali wanakamua kwelikweli.

Hata halotel vifurushi vya mwezi kwa internet kama huna elfu kumi hamia Burundi wakati kipindi cha baba hata mwenye kipato kidogo alikuwa anajiunga cha mwezi.
 
hapo bado hao washenzi hawajaiba baada ya dk kadhaa unasikia umetumia asilimia 75 ya mb zako..waziri akisikia malalamiko kama haya anakasirika ni kero kwake anaona raia ni wazenguaji
 
Hahahahahahah huyu jamaa atakuwa anamegewa fungu lake kila quater.

"Nyie pandisheni kifurushi hicho kinachokuwa kinapatikana muweke asilimia kadhaa kwenye account ya chama na asilimia kadhaa muweke kwenye account yangu ya uswizi πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ awamu yetu hii!"
 
anakuwa mkali watu wakilalamika utasikia angalieni apps kwenye simu zenu zinakula data, uatasikia Tz ni nchi ya 6 kwa kuwa na cheap data, jamaa hajali kabisa ana roho mbaya sana
 
anakuwa mkali watu wakilalamika utasikia angalieni apps kwenye simu zenu zinakula data, uatasikia Tz ni nchi ya 6 kwa kuwa na cheap data, jamaa hajali kabisa ana roho mbaya sana
Analamba asali jamani na hio wizara ina namna inamnufaisha sana ndio maana kila wakati anaomba awekwe humo humo. Anakula na Tisiharaeiii
 
Eti waziri.... Kichwa Haina mipango ipo ipo tuπŸ˜‚
 
ok nasikia Tanzania ni ya 6 Afrika kwa kuwa na bei nafuu ya data kwa hiyo malalamiko yetu ni ya kijinga tu
Uliza kwanza source mkuu,ukute huo utafiti wameufanya wenyewe na matokeo wametoa wao wenyewe,kiufupi wamejitafiti.Wabongo wahuni sana aisee ni wazee wa kupika data.
 
Zantel nao wamepandisha...kilichonifurahisha kuhusu zantel no hiki....huku kijijini hakuna wakala wao wa Ezypesa, vocha hakuna hivyo nilikuwa nalazimika kununua bando kupitia Mpesa, sasa kuna haja gani ya kubakia na line yao wakati vifurushi vyao vimepanda sawa na vodacom?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…