Aisee kumbe hadi leo Tabata Chang'ombe barabara kimeo!

Aisee kumbe hadi leo Tabata Chang'ombe barabara kimeo!

Boran Jakutay

Senior Member
Joined
Apr 8, 2023
Posts
110
Reaction score
259
IMG_20230416_151232.jpg

IMG_20230416_151249.jpg
Aisee leo bhana nimepata nafasi ya kupita Barabara ya Tabata Chang'ombe, nilichokutana nacho kimenishangaza sana.

Nilipita njia hiyo kwa dharura kwa sababu daladala niliyopanda ikitokea Mwenge kuja Tabata Segerea ilikwepa foleni, tulipofika Barakuda, tukaingia boda la Chang'ombe.

Huku mwanzomwanzo tumeteleza vizuri, ila kufika mbele, tukakutana na mashimo barabarani, barabara haijakamalika kujengwa hadi mwisho.

Sikuwa nimeenda Tabata Chang'ombe kwa muda mrefu, nilidhani barabara itakuwa imejengwa freshi hadi mwisho kwa sababu nikipita Barakuda naona lami. Kumbe sio.

Bado barabara imekuwa kero sana, mashimo yanaharibu vyombo vya moto.
IMG_20230416_151221.jpg

Kibaya zaidi ni kwamba, hadi leo hakuna stendi ya daladala, magari yanapaki pembezoni mwa barabara kusubiri abiria. Hii ni aibu.
IMG_20230416_150739.jpg

Ukiangalia Tabata Segerea na Tabata Kimanga, kwao safi tu, lakini Tabata Chang'ombe, wapo nyuma sana kimaendeleo unapozungumzia miundombinu ya barabara.

Wahusika oneni aibu, haiwezekani miaka nenda rudi hali ni ileile.
IMG_20230416_151302.jpg
 
Pole mkuu kutoka hapa barakuda kwenda chan'gombe mbele kidogo lami ndio mwisho hapo unachezea dimbwi mpaka basi. Halafu wanasema tabata jina kubwa
 
Back
Top Bottom