Aishi zaidi ya siku 30 akila wadudu baada ya kupotea msituni

Aishi zaidi ya siku 30 akila wadudu baada ya kupotea msituni

Oldmantz

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2023
Posts
704
Reaction score
1,457
Bolivia. Kisa cha Jhonatan Acosta (30) kimewashangaza wengi baada ya kuishi kwa kula minyoo na wadudu kwa zaidi ya siku 30 tangu alivyopotea katika msitu wa Amazon.

Akifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Unitel alisema, "Ilinibidi kujifunza mbinu mpya za kuishi, nilijilazimu kutumia wadudu, kunywa mkojo wangu, kula minyoo na nilishambuliwa na wanyama."

Acosta aliripotiwa kutoweka na familia yake mwishoni mwa Januari, alipokuwa katika shughuli zake za kuwinda na marafiki zake wanne kwenye msitu wa Amazon lakini akajikuta anapotea kwenye eneo hilo lenye kutisha.
Mwezi mmoja baadaye, alipatikana na timu za utafutaji na uokoaji, maafisa walikuwa wanamtumia mbwa aliyepewa mafunzo maalum (Titan) kusaidia kumtafuta Acosta, kituo hicho kiliripoti.

Acosta aliiambia Unitel kuwa mvua ilinyesha nusu ya muda wote aliopotea, alitumia viatu vyake vya mpira kukinga maji ya mvua, lakini mvua zilipoacha kunyesha alianza kunywa mkojo wake mwenyewe. "Nilimwomba sana Mungu mvua," Acosta alisimulia kwa uchungu.

Anasema wakati wa usiku alikuwa aking’atwa na kila aina ya viumbe na wadudu tofauti tofauti.
Dada yake, Miladde Acosta, aliiambia Unitel TV kwamba kaka yake "ilimbidi kupigana na nguruwe, ambaye ni mnyama wa mwituni na hatari zaidi."

Credit: MWANANCHI
 
Chai hiiiiii
Yaani unywe mkojo ndani ya amazon yenye mito kama yote,matunda,sung ur a,panya,samaki
......
Umeandika kirahisi sana, ukiwa ndani ya msitu unaona miti iliyokuzunguka Hapo tu mita 100 huo mto au ziwa linaweza kuwa mita 200 au 1KM kutoka ulipo na usijue Kama Kuna maji 1KM kutoka ukipo yaani unaweza kuwa KISUTU mto upo pale TPA na ukazungukuuka bila kujua mto ulipo ndio maana ya kupotea msituni

Mto na mazima utaviona Amazon ukiangalia kwa Google map ila tukikutupia humo ndani inaweza pita mwezi unaona miti tu
 
Umeandika kirahisi sana, ukiwa ndani ya msitu unaona miti iliyokuzunguka Hapo tu mita 100 huo mto au ziwa linaweza kuwa mita 200 au 1KM kutoka ulipo na usijue Kama Kuna maji 1KM kutoka ukipo yaani unaweza kuwa KISUTU mto upo pale TPA na ukazungukuuka bila kujua mto ulipo ndio maana ya kupotea msituni

Mto na mazima utaviona Amazon ukiangalia kwa Google map ila tukikutupia humo ndani inaweza pita mwezi unaona miti tu
Unajua mm ni hunter ndo maana nasema jamaa muongo huwez kua msituni ukakosa hivyo vitu kwanza hata ndege na wanyama wadogo unaweza kuwatumia kupata direction ya maji hivyo yaani...
 
Unajua mm ni hunter ndo maana nasema jamaa muongo huwez kua msituni ukakosa hivyo vitu kwanza hata ndege na wanyama wadogo unaweza kuwatumia kupata direction ya maji hivyo yaani...
Jamaa tunazungumzia AMAZON hapa sio msitu wako wa kitonga pia mtu kapotea unaijua SQUARE METER ya Amazon jamaa
 
Huo msitu si ndio una anaconda kama wote! Amewezaje kuishi mwezi mzima humo? Huo msitu pia una wale binadamu wanaokula watu wenzao.duh! Ana bagati sana huyo mwamba.
Kati ya misitu hatari duniani huo msitu ni namba moja.
 
Huo msitu si ndio una anaconda kama wote! Amewezaje kuishi mwezi mzima humo? Huo msitu pia una wale binadamu wanaokula watu wenzao.duh! Ana bagati sana huyo mwamba.
Kati ya misitu hatari duniani huo msitu ni namba moja.
Kile ni kisayari kabisa
 
Umeandika kirahisi sana, ukiwa ndani ya msitu unaona miti iliyokuzunguka Hapo tu mita 100 huo mto au ziwa linaweza kuwa mita 200 au 1KM kutoka ulipo na usijue Kama Kuna maji 1KM kutoka ukipo yaani unaweza kuwa KISUTU mto upo pale TPA na ukazungukuuka bila kujua mto ulipo ndio maana ya kupotea msituni

Mto na mazima utaviona Amazon ukiangalia kwa Google map ila tukikutupia humo ndani inaweza pita mwezi unaona miti tu
Sawa kabisa.
 
Umeandika kirahisi sana, ukiwa ndani ya msitu unaona miti iliyokuzunguka Hapo tu mita 100 huo mto au ziwa linaweza kuwa mita 200 au 1KM kutoka ulipo na usijue Kama Kuna maji 1KM kutoka ukipo yaani unaweza kuwa KISUTU mto upo pale TPA na ukazungukuuka bila kujua mto ulipo ndio maana ya kupotea msituni

Mto na mazima utaviona Amazon ukiangalia kwa Google map ila tukikutupia humo ndani inaweza pita mwezi unaona miti tu
Mwamba angekuwa angalau anafatiliaga zile series za "I Shouldn't Be Alive" walau angepata picha huo mziki unakuagaje ni kisanga na nusu kupotea..
 
Huyo jamaa ni kama ana asili ya uoga na alipopotea hakutaka kuhangaika kuchanja pori.
Alipo potea na siraha nayo ikapotea? Mungu anamletea kitoeo kama nguruwe anashindwa kumuua? ulindi na ulimbombo nayo alishindwa kuapply?

Hata kama amazon ni kubwa na maajabu yake, mi nisingeshindwa kusoma ramani na uelekeo wa mahala mto ulipo na halafu mle pori kuna kambakamba ukikata inatoa pure water sema huyo hakuwa mzoefu tu. Alishindwa hata kukinga umande? hakuna majabari ya mawe yenye kutuamisha maji?

Pia ningetumia mizizi na kambakamba kutengeneza mitego ya kunasa wanyama wadogowadogo.
Mi nikiangushwa Amazon ndani ya wiki 2 tu ningeshakuwa mwenyeji mzuri. Ningemuomba Mungu anitengenezee eva wangu tu niinjoy ma advanture...!
 
Back
Top Bottom