Ajabu sana: Dereva wa basi ahatarisha maisha ya watu 60 kwa kuikwepa bajaj yenye watu watano

Ajabu sana: Dereva wa basi ahatarisha maisha ya watu 60 kwa kuikwepa bajaj yenye watu watano

Down To Earth

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2011
Posts
21,940
Reaction score
16,643
#HABARI Abiria waliokuwa wakisafiri kutoka Dar es salaam kwenda Dodoma kwa kutumia basi la Kampuni ya Shabiby namba T 341 EEU, wamenusurika kifo baada ya basi hilo kuanguka katika eneo la Kihonda Manispaa ya Morogoro na kujeruhi abiria kadhaa.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo wanasema dereva wa basi hilo alikuwa anamkwepa mwendesha bajaji.

Akizungumzia ajali hiyo Afisa Habari na Mahusiano Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Morogoro Betrice Kapoli amesema leo majira ya saa 12 na dakika 45 asubuhi walipokea majeruhi 22 wa ajali ya Shabiby Kati Yao wanaume 5 wanawake 17 ambao wanaendelea kupata matibabu hospitalini hapo.

Credit: #EastAfricaTV
FB_IMG_1716623376664.jpg
 
Kwani hao watano hawastahili kuishi? Kwamba wao ndiyo wanafaa kugongwa kwa sababu wana roho za chuma?

Huyo dereva namsifu. Hakuna kifo hata kimoja. Ila nina uhakika, angeigonga hiyo bajaji basi hao wapendwa watano wangekuwa marehemu.
 
Kwani hao watano hawastahili kuishi? Kwamba wao ndiyo wanafaa kugongwa kwa sababu wana roho za chuma?

Huyo dereva namsifu. Hakuna kifo hata kimoja. Ila nina uhakika, angeigonga hiyo bajaji basi hao wapendwa watano wangekuwa marehemu.
Dr fikilia tena
 
Ameikwepa au aliovetake hiyo bajaji kuikwepa maana yake walikua wanaenda uelekeo tofauti ila mwenye bajaji aliingia upande wa bus kwaiy dereva wa bus akamkwepa,, sasa hapo naomba kueleweshwa alimkwepa au aliovetake?
 
Dr fikilia tena
Sifikrii.

Unachotaka ni kufikiri unavyotaka. Kwamba, ni bora maafa madogo kuliko maafa makubwa.

Lakini hakuna maafa yaliyotokea kwa ukubwa. Kuanza kumlaumu dereva kuikwepa bajaji ni ujuha na upuuzi.

Kwanza kwa taarifa zilizopo, dereva wa bus ndiyo amekosea kuovertake pasiporuhusiwa. Hivyo,bajaji ilikuwa sehemu sahihi kwa wakati sahihi.

Uzembe wa dereva usilete vifo kwa wasiohusika.

Hakuna ambaye angependa kufa kwa uzembe wa mtu yeyote. Mfano, Upo na familia yako, unaendesha zako kistàarabu, dereva kawasha moto huko alafu aje kuivamia gari yenu tu kisa kuokoa roho za watu wengi?
 
Sifikrii.

Unachotaka ni kufikiri unavyotaka. Kwamba, ni bora maafa madogo kuliko maafa makubwa.

Lakini hakuna maafa yaliyotokea kwa ukubwa. Kuanza kumlaumu dereva kuikwepa bajaji ni ujuha na upuuzi.

Kwanza kwa taarifa zilizopo, dereva wa bus ndiyo amekosea kuovertake pasiporuhusiwa. Hivyo,bajaji ilikuwa sehemu sahihi kwa wakati sahihi.

Uzembe wa dereva usilete vifo kwa wasiohusika.
Hapo nimeelewa mkuu...
🙏🙏🙏🙏🙏
Kumbe nilikua nawaza negative kabisa an sasa nimeelewa
 
Back
Top Bottom