Mimi napingana kabisa na Mheshimiwa Mwakyembe. Kwanza kabisa, yeye siyo polisi na siyo subject matter expert katika eneo hilo. Yeye mwenyewe amenukuliwa kwa mara ya kwanza akisema kwamba gari yake ilikuwa inaipita lori halafu akaingia kwenye pot hole tairi ikatoka gari lika anguka na kubiringika. Ya pili alisema kuwa gari yake ilikuwa inaipita lori halafu lori likagonga gari yake kwa nyuma upande wa kushoto gari ikapinduka. Ukiangalia kwa scenario zote mbili zinaonyesha kuwa driver wake hakuwa makini. Kwani kama alikuwa anaipita gari bila kuiscan njia halafu akaingia kwenye pot hole, basi alikuwa na makosa, maana ni mzembe hajapata big picture ya barabara kabla ya kufanya uamuzi wa kuovertake. Hili la pili la kugongwa kwa nyuma, kuna mambo mengi lakini tuangalie mawili, either driver alirudi upande wa lori haraka na mwendo wake ulikuwa mdogo kuliko wa gari kubwa, maana yake atakuwa amekanyaga break au kupunguza mwendo immediately baada ya kuovertake. La pili kama gari kubwa lilimgonga kwa nyuma upande wa kushoto maana yake, driver wa gari kubwa alikata kona haraka sana na alikuwa kwenye mwendo mkali, hivyo nalo gari lingeyumba hata kuanguka ama lingeigonga gari ya Mheshimiwa kwenye ubavu. Na hili kwenye ubavu halipo kwani halijasemwa. Hivyo possibility in kwamba driver wa Mh. Mwakyembe alirudi haraka kabla ya kumaliza kuovertake na kujibamiza kwenye gari kubwa, hapa tena kosa ni la driver wa Mh. Mwakyembe. Ninacho taka kusisitiza hapa ni kwamba madriver wanahitaji kusoma kitu kinachoitwa Defensive Driving, na somo litawasaidia madriver wote kuwa makini barabarani. Madriver wa magari ya serikali na za waheshimiwa wanaendesha rafu sana bila kufuata sheria wakidhani wao wako juu ya sheria maana wako na Mheshimiwa hivyo hata traffic police hawezi kumsimamisha au kupiga faini. Ok, hasimamishwi wala hapigwi faini lakini ajali itampata na tumeshapoteza wakubwa wengi kwa uzembe huu. Hawa madriver wanahitaji defensive driving. TIT inafundisha course hii na haichukui zaidi ya wiki. Uendeshaji wa gari siyo leseni na kunyooshea barabara ni pamoja na kufahamu matumizi sahihi ya barabara kwako wewe na mwingine na kuepuka ajali. Driver mzuri na hodari ni yule anayeanza na kumaliza safari yake vizuri. Mh. Mwakyembe anafanya swala hili kuwa la kisiasa yeye mwenyewe. He is already popular he don't any further cheap popularity. Lazima awe mfano wa kukemea unsafe driving kama iliyoonyeshwa na driver wake. Bongo hii mambo ya wakuu kutetea madriver wavunje sheria ni kawaida, kuna wakati naibu waziri wa wizara inayoshughulikia mambo hayo ya usalama alimripoti police aliyelirudisha gari lake ili lifuate sheria. Kitendo kama ilitakiwa imwajibishe waziri kama huyu ambaye analea uendeshaji mbaya ambao unaweza kupelekea ajali na kugharimu maisha ya watu. Ajali za barabarani zimeshagharimu Watanzania wengi maisha yao. Lazima tubadili tabia ya kuendesha magri. Lets observe Defensive Driving. Asanteni sana. It is possible to reduce road accidents.