Tetesi: Ajali ya magari daraja la Kibamba

Tetesi: Ajali ya magari daraja la Kibamba

Kumbe kukosea jukwaa nalo ni kosaaa!?????? R.I.P walofariki
 
Mkuu Petro Mselewa poleni kwa hiyo foleni na pia pole kwa wote ambao wamepata madhara katika ajali hiyo.Nakukumbusha tu wakili msomi na wadau wengine humu,hakuna ajali mbaya wala ajali nzuri japo kuna ajali zinazosababisha madhara makubwa ikiwemo vifo na nyingine zisizosababisha vifo wala majeruhi.
 
Tarehe kama hizi kila mtu ni dereva wa highway ...itatugharimu kushika usukani bila uzoefu...chondechonde
 
Kuna ajali ya magari mawili yaliyogongana katikati ya Daraja la Kibamba. Kuna foleni kubwa mno. Nami nipo kwenye foleni hiyo nikielekea Kibaha. Naambiwa kuwa kuna waliopoteza maisha na waliojeruhiwa katika ajali hiyo.

Vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vipo hapa kuhakikisha kuwa mambo yanakwenda vyema. Taarifa zaidi zitafuata...
Wewe ni Law philosopher, achana na petty news kama hizi. Weka legal issue/nondo watu waelimike!
 
Yaa hyo ajali imetokea kweli inasadikiwa watu watatu wamepoteza maisha, ni ajali kati ya double keabin na gari la taka. Kibamba darajani.
 
IMG-20171218-WA0002.jpg
 
Swala la ajali hapo kibamba darajan sio la kushangaaa kwani ni kawaida sana.

Zaman watu walikuwa wanasema ni majini ya rose, Sasa Leo hii rose ni marehem sijui watasingizia nani.

Iyo hata bara imekaa mteremko, Kona na kuna kilima pia madereva hu under estimate wepesi wa ajali kutokea
 
Back
Top Bottom