SoC02 Ajira mpya Serikalini ziwe ni kwa miaka kumikumi, itasaidia kupunguza tatizo la ajira na ugumu ya maisha

SoC02 Ajira mpya Serikalini ziwe ni kwa miaka kumikumi, itasaidia kupunguza tatizo la ajira na ugumu ya maisha

Stories of Change - 2022 Competition

EzekielEmanuel1997

New Member
Joined
Jul 29, 2022
Posts
4
Reaction score
11
1.0 Ikisiri
Nchi nyingi duniani zinakumbana na changamoto ya ajira kwa vijana. Hii ni kutokana na ongezeko la idadi ya wahitimu katika ngazi mbalimbali za elimu ingali hapajatengenezwa mazingira rafiki kwa ajili ya kuwaajiri au kujiajiri vijana hao. Pamoja na kuonekana madhara makubwa ulimwenguni kote, nchi za Afrika na Asia zimeonekana kukumbwa zaidi na madhara haya ikilinganishwa na nchi za Ulaya. Hivyo mjadala wa makala hii umekitwa zaidi katika nchi za Afrika na Asia, Tanzania ikichukuliwa kama sampuli kifani. Kwa hiyo, katika makala hii, mwandishi analenga kutoa maoni kuhusiana na namna ya kukabiliana na changamoto ya ajira kwa vijana kwa kuzingatia kwamba nchini Tanzania kama ilivyo kwa nchi zingine tatizo hili linazidi kukua na matokeo yake yanatarajiwa kuwa ni mabaya.​

1.2 Utangulizi
Mjadala wa makala hii unazingatia ukweli kwamba, elimu rasmi kwa nchi za Afrika na Asia ni matokeo ya mfumo wa elimu ya kikoloni. Itakumbukwa kwamba adhma ya elimu ya kikoloni ilikuwa ni kuandaa watendaji ambao wangerahisisha ufanyaji wa kazi za uzalishaji mali, shughuli za kiutawala pamoja na kuandaa vibaraka wa kisiasa. Elimu hii haikuwa na lengo la kumuandaa Mwafrika katika kujitegemea kiutawala, kifikra n.k. Hivyo, asilimia kubwa ya wahitimu waliona kuajiriwa ndiyo matokeo ya kupata elimu. Mawazo na tajriba zao zikawa katika mwegamo huo. Kwa hiyo, miongo na miongo mfumo huo ukaendelea mpaka miaka ya leo. Baada ya nchi za nyingi hususani za Afrika kupata uhuru, ziliendeleza mfumo uleule wa elimu huku zikijaribu angalau kuubadili mfumo wa elimu ya kikoloni ingawaje hazikufanikiwa kama ilivyotarajiwa. Mfano mzuri ni Elimu ya Ujamaa na Kujitegemea iliyoanzishwa na Mwl. J.K. Nyerere. Mfumo huu haukufanikiwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo shinikizo kutoka nchi za Magharibi. Hivyo, kwa asilimia kubwa bado tunaogelea katika dimbwi la elimu ya mkoloni ambayo inamuandaa kijana kuajiriwa na si kufikiri katika kutengeneza namna ya kujiajiri. Kwa kuzingatia usuli huu, makala hii inalenga sasa kutoa maoni ya namna ya kukabiliana na hii changamoto.​

2.0 Nini Kifanyike
Waandishi wengi wameandika kuwataka vijana wajiajiri na mapendekezo mengine. Sitarudia kilichosemwa na waandishi bali ninatofautiana nao kidogo kimtazamo kwa kuwa vijana wengi wanajitahidi kujiajiri lakini bado matarajio hayafikiwi na kila siku idadi ya watu wasio na ajira inaongezeka. Mwandishi wa makala hii anaona jambo linalofaa ni:​

2.1 Ajira zote Mpya Serikalini Ziwe za Awamu (Miaka Kumikumi)
Kutokana na sheria za Tanzania, asilimia kubwa ya waajiriwa serikalini wanapaswa kustaafu katika umri miaka 60. Yaani, iwapo mwajiriwa ataajiriwa akiwa na miaka 30 basi ana miaka 30 ya kula keki ya nchi[1] kisha kupatiwa mafao. Hii ni sawa na kusema kwamba, sheria inaruhusu katika miaka yote hii 30 nafasi hii kumilikiwa na mtu mmoja mpaka pale atakapohamishwa kituo, kufa au kufukuzwa kazi. Ni sawa na kusema vilevile kwamba, katika miaka hii 30 kama yupo mwenye sifa ya kuajiriwa atapaswa asubiri mpaka pale mtangulizi wake atakapofikia umri wa miaka 60, atakapokufa au kuhamishwa/ kufukuzwa kazi. Madhara ya sheria hii ni haya yafuatayo.

Kwanza, idadi kubwa ya watu wasio na ajira ilhali wana sifa za kuajiriwa inaongezeka kwa kasi. Hii inachagizwa vilevile na kutokuwapo kwa mikakati ya kuongeza nafasi za ajira ilhali idadi ya wahitimu wa vyuo vikuu inaongezeka kwa kiwango kikubwa kila mwaka. Tafiti za hivi karibuni zinaonesha jumla ya wahitimu zaidi ya laki moja huhitimu kila mwaka.

Pili, waajiriwa wengi wamekuwa wakiridhika na ajira wasiwaze namna ya kuongeza mapato yao nje na ajira. Kutokana na saikolojia kuwafariji waajiriwa serikalini kwamba wana muda mrefu katika ajira, kumefanya waajiriwa wengi waendelee kula keki ya nchi wasijihusishe na shughuli mbalimbali mathalani kilimo bora, ufugaji, biashara n.k ambazo zingekuwa na tija katika maisha yao nje na ajira. Jambo ambalo lingeweza kupunguza ukali wa maisha yao pamoja na wale wasio na ajira

Tatu, hali ya uchumi wa kudumaa. Neema ya kuwapo kwenye ajira mpaka ufikiapo miaka 60 inachangia kwa kiasi kikubwa kufanya uchumi wetu kudumaa. Hii ni kutokana na sababu kwamba mzunguko wa fedha haupo katika uzalishaji bali upo katika matumizi. Hakuna hofu ya mtetereko wa kiuchumi ambayo inawazwa na waajiriwa wengi. Wengi wanafanya matumizi yaliyo nje na bajeti wakijua kwamba mwisho wa mwezi kuna keki ya taifa. Ni rahiri vilevile kujiingiza katika madeni yasiyo na tija kutokana na tu na kuwapo kwa keki itakayotumika kulipa hayo madeni. Hali hii inadhorotesha uchumi wa nchi kwani matokeo ya mwisho kabisa yanamgusa yule asiye na ajira kutokana na mzunguko wa fedha kuwa mgumu kwake ilhali mwepesi kwa wenye keki ya taifa.

Hivyo, kutokana na hali hiyo iko haja ya kuangalia na kuafiki kupunguza miaka ya ajira na kuzifanya ziwe ni za awamu kila baada ya miaka kumi. Yaani iwapo mtu ataajiriwa leo, basi atambue kwamba ana miaka kumi ya kula keki ya taifa kisha ataachia nafasi hiyo kwa mtu mwingine ambaye naye atafanya kwa miaka kumi kisha awamu ya pili inamalizika kwa yule wa kwanza. Kwa hiyo, mwajiriwa serikalini atakuwa na jumla ya miaka 20 pekee ya kula keki ya taifa.

Hii itasaidia mwajiriwa kujiandaa kisaikolojia kwamba anao muda mchache wa kula keki ya nchi. Hivyo, kupitia mshahara wake atafikiri namna ya kujiongezea kipato kabla na baada ya ajira. Mzunguko wa fedha kitaifa utakua hatimaye kupoza makali ya ugumu wa maisha kwa watu wote kwa sababu uzalishaji mali utaongezeka. Kikubwa zaidi, ni kwamba tatizo la ongezeko la vijana wasio na ajira litapunguzwa mara mbili ya hali iliyopo sasa kwani kila baada ya miaka kumi walioko kwenye ajira watapisha wengine. Vivyo hivyo kwa awamu itakayofuata. Mbali na hayo yote mfumo wa namna hii utasaidia kuondoa sononeko la kisaikolojia miongoni mwa wahitimu wa vyuo kwani kwa kufanya hivi kutaleta angalau hali ya usawa katika kula keki ya nchi. Vilevile, bidii ya kujituma ns kuzalisha mali itaongezeka miongoni mwa waajiriwa kutokana na muda mchache walionao katika kuzitumia rasilimali fedha watakazokuwa wakilipwa serikalini.​

3.0 Hitimisho
Mbali na maoni haya, serikali pamoja na wadau inatupasa kuupitia upya mfumo wetu wa elimu kwani huo ndiyo chanzo cha changamoto hii. Hatuna budi kujisahihisha mapema kwani hakuna changamoto isiyo na madhara hasi.

Ezekiel Emanuel
0739828402
ezekielemanue97@gmail.com


[1] Msemo Keki ya nchi una maana “Mshahara”
 
Upvote 30
Ukiwa huna ajira hili wazo unaweza kuliona bora sana lakini siku mtoa wazo akabahatika kuwa hata meneja sehemu hili bandiko lake atakuja kulifuta. Hata aliyesema Urais mwisho miaka kumi alikuwa ni Rais mstaafu na suo rais wa madarani.

Putin aliwahi kusema kama kuna kitu kitu kinakukera serikalini basi pambana uwe raisi uje kukitoa. Alimanisha kama unaona ni kupoteza fedha rais kuwa na msafara mkubwa basi kuwa wewe Rais afu utmbee pekeyako na pikipiki kusevu pesa au kwa mguu kabisa.
 
Unapowapumzisha wengine baada ya awamu yao ya miaka kumi kutimia si na wao wanakuwa hawana ajira kwa kipindi hicho?

Nadhani nadharia ya keki ya taifa imetumika vibaya hapa. Hivi mshahara wa laki nne na ushee kwa mwezi ndo uite keki ya taifa?

Keki ya taifa nijuavyo mimi ni kwa wale wanaopata mishahara na marupurupu mikubwa. Kwa Bongo pengine waliopo kwenye nafasi za kuteuliwa pamoja na wabunge ndo naweza kuwaweka katika kundi la wala keki ya taifa.
 
Ukiwa huna ajira hili wazo unaweza kuliona bora sana lakini siku mtoa wazo akabahatika kuwa hata meneja sehemu hili bandiko lake atakuja kulifuta. Hata aliyesema Urais mwisho miaka kumi alikuwa ni Rais mstaafu na suo rais wa madarani...
Hahaha
 
Ukiwa huna ajira hili wazo unaweza kuliona bora sana lakini siku mtoa wazo akabahatika kuwa hata meneja sehemu hili bandiko lake atakuja kulifuta. Hata aliyesema Urais mwisho miaka kumi alikuwa ni Rais mstaafu na suo rais wa madarani..
Ni kweli usemayo lakini yote hayo ni kutokana na mtizamo ambao tayari umejengeka miongoni mwa watu wengi. Inaonekana ni vigumu kutekelezeka kwa kuwa ajira imechukuliwa kama ni PUMZIKO na siyo daraja la kujiimarisha zaidi. Hakuna pesa za kuajiri wengi kwa kuwa wale waliopo kwenye ajira silimia kubwa wanajua kwamba wana kipindi kirefu cha Relief.

Mzunguko wa fedha kitaifa unaathiriwa na matumizi zaidi kuliko kuzalisha ili kuongeza pato la taifa. Laiti kama wangekuwa wanajua kwamba nina miaka yangu kumi ya kwanza ya kupata uahueni kisha nitaondoka nirudi tena baadaye basi amini kwamba hali ingekuwa ni tofauti kidogo. Kiwango cha maisha kingekuwa ni afadhali kwa wengi. Matumizi yasiyo ya lazima yangepungua na pato la taifa lingekua.​
 
1.0 Ikisiri
Nchi nyingi duniani zinakumbana na changamoto ya ajira kwa vijana. Hii ni kutokana na ongezeko la idadi ya wahitimu katika ngazi mbalimbali za elimu ingali hapajatengenezwa mazingira rafiki kwa ajili ya kuwaajiri au kujiajiri vijana hao. Pamoja na kuonekana madhara makubwa ulimwenguni kote, nchi za Afrika na Asia zimeonekana kukumbwa zaidi na madhara haya ikilinganishwa na nchi za Ulaya. Hivyo mjadala wa makala hii umekitwa zaidi katika nchi za Afrika na Asia, Tanzania ikichukuliwa kama sampuli kifani. Kwa hiyo, katika makala hii, mwandishi analenga kutoa maoni kuhusiana na namna ya kukabiliana na changamoto ya ajira kwa vijana kwa kuzingatia kwamba nchini Tanzania kama ilivyo kwa nchi zingine tatizo hili linazidi kukua na matokeo yake yanatarajiwa kuwa ni mabaya.​

1.2 Utangulizi
Mjadala wa makala hii unazingatia ukweli kwamba, elimu rasmi kwa nchi za Afrika na Asia ni matokeo ya mfumo wa elimu ya kikoloni. Itakumbukwa kwamba adhma ya elimu ya kikoloni ilikuwa ni kuandaa watendaji ambao wangerahisisha ufanyaji wa kazi za uzalishaji mali, shughuli za kiutawala pamoja na kuandaa vibaraka wa kisiasa. Elimu hii haikuwa na lengo la kumuandaa Mwafrika katika kujitegemea kiutawala, kifikra n.k. Hivyo, asilimia kubwa ya wahitimu waliona kuajiriwa ndiyo matokeo ya kupata elimu. Mawazo na tajriba zao zikawa katika mwegamo huo. Kwa hiyo, miongo na miongo mfumo huo ukaendelea mpaka miaka ya leo. Baada ya nchi za nyingi hususani za Afrika kupata uhuru, ziliendeleza mfumo uleule wa elimu huku zikijaribu angalau kuubadili mfumo wa elimu ya kikoloni ingawaje hazikufanikiwa kama ilivyotarajiwa. Mfano mzuri ni Elimu ya Ujamaa na Kujitegemea iliyoanzishwa na Mwl. J.K. Nyerere. Mfumo huu haukufanikiwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo shinikizo kutoka nchi za Magharibi. Hivyo, kwa asilimia kubwa bado tunaogelea katika dimbwi la elimu ya mkoloni ambayo inamuandaa kijana kuajiriwa na si kufikiri katika kutengeneza namna ya kujiajiri. Kwa kuzingatia usuli huu, makala hii inalenga sasa kutoa maoni ya namna ya kukabiliana na hii changamoto.​

2.0 Nini Kifanyike
Waandishi wengi wameandika kuwataka vijana wajiajiri na mapendekezo mengine. Sitarudia kilichosemwa na waandishi bali ninatofautiana nao kidogo kimtazamo kwa kuwa vijana wengi wanajitahidi kujiajiri lakini bado matarajio hayafikiwi na kila siku idadi ya watu wasio na ajira inaongezeka. Mwandishi wa makala hii anaona jambo linalofaa ni:​

2.1 Ajira zote Mpya Serikalini Ziwe za Awamu (Miaka Kumikumi)
Kutokana na sheria za Tanzania, asilimia kubwa ya waajiriwa serikalini wanapaswa kustaafu katika umri miaka 60. Yaani, iwapo mwajiriwa ataajiriwa akiwa na miaka 30 basi ana miaka 30 ya kula keki ya nchi[1] kisha kupatiwa mafao. Hii ni sawa na kusema kwamba, sheria inaruhusu katika miaka yote hii 30 nafasi hii kumilikiwa na mtu mmoja mpaka pale atakapohamishwa kituo, kufa au kufukuzwa kazi. Ni sawa na kusema vilevile kwamba, katika miaka hii 30 kama yupo mwenye sifa ya kuajiriwa atapaswa asubiri mpaka pale mtangulizi wake atakapofikia umri wa miaka 60, atakapokufa au kuhamishwa/ kufukuzwa kazi. Madhara ya sheria hii ni haya yafuatayo.

Kwanza, idadi kubwa ya watu wasio na ajira ilhali wana sifa za kuajiriwa inaongezeka kwa kasi. Hii inachagizwa vilevile na kutokuwapo kwa mikakati ya kuongeza nafasi za ajira ilhali idadi ya wahitimu wa vyuo vikuu inaongezeka kwa kiwango kikubwa kila mwaka. Tafiti za hivi karibuni zinaonesha jumla ya wahitimu zaidi ya laki moja huhitimu kila mwaka.

Pili, waajiriwa wengi wamekuwa wakiridhika na ajira wasiwaze namna ya kuongeza mapato yao nje na ajira. Kutokana na saikolojia kuwafariji waajiriwa serikalini kwamba wana muda mrefu katika ajira, kumefanya waajiriwa wengi waendelee kula keki ya nchi wasijihusishe na shughuli mbalimbali mathalani kilimo bora, ufugaji, biashara n.k ambazo zingekuwa na tija katika maisha yao nje na ajira. Jambo ambalo lingeweza kupunguza ukali wa maisha yao pamoja na wale wasio na ajira

Tatu, hali ya uchumi wa kudumaa. Neema ya kuwapo kwenye ajira mpaka ufikiapo miaka 60 inachangia kwa kiasi kikubwa kufanya uchumi wetu kudumaa. Hii ni kutokana na sababu kwamba mzunguko wa fedha haupo katika uzalishaji bali upo katika matumizi. Hakuna hofu ya mtetereko wa kiuchumi ambayo inawazwa na waajiriwa wengi. Wengi wanafanya matumizi yaliyo nje na bajeti wakijua kwamba mwisho wa mwezi kuna keki ya taifa. Ni rahiri vilevile kujiingiza katika madeni yasiyo na tija kutokana na tu na kuwapo kwa keki itakayotumika kulipa hayo madeni. Hali hii inadhorotesha uchumi wa nchi kwani matokeo ya mwisho kabisa yanamgusa yule asiye na ajira kutokana na mzunguko wa fedha kuwa mgumu kwake ilhali mwepesi kwa wenye keki ya taifa.

Hivyo, kutokana na hali hiyo iko haja ya kuangalia na kuafiki kupunguza miaka ya ajira na kuzifanya ziwe ni za awamu kila baada ya miaka kumi. Yaani iwapo mtu ataajiriwa leo, basi atambue kwamba ana miaka kumi ya kula keki ya taifa kisha ataachia nafasi hiyo kwa mtu mwingine ambaye naye atafanya kwa miaka kumi kisha awamu ya pili inamalizika kwa yule wa kwanza. Kwa hiyo, mwajiriwa serikalini atakuwa na jumla ya miaka 20 pekee ya kula keki ya taifa.

Hii itasaidia mwajiriwa kujiandaa kisaikolojia kwamba anao muda mchache wa kula keki ya nchi. Hivyo, kupitia mshahara wake atafikiri namna ya kujiongezea kipato kabla na baada ya ajira. Mzunguko wa fedha kitaifa utakua hatimaye kupoza makali ya ugumu wa maisha kwa watu wote kwa sababu uzalishaji mali utaongezeka. Kikubwa zaidi, ni kwamba tatizo la ongezeko la vijana wasio na ajira litapunguzwa mara mbili ya hali iliyopo sasa kwani kila baada ya miaka kumi walioko kwenye ajira watapisha wengine. Vivyo hivyo kwa awamu itakayofuata. Mbali na hayo yote mfumo wa namna hii utasaidia kuondoa sononeko la kisaikolojia miongoni mwa wahitimu wa vyuo kwani kwa kufanya hivi kutaleta angalau hali ya usawa katika kula keki ya nchi. Vilevile, bidii ya kujituma ns kuzalisha mali itaongezeka miongoni mwa waajiriwa kutokana na muda mchache walionao katika kuzitumia rasilimali fedha watakazokuwa wakilipwa serikalini.​

3.0 Hitimisho
Mbali na maoni haya, serikali pamoja na wadau inatupasa kuupitia upya mfumo wetu wa elimu kwani huo ndiyo chanzo cha changamoto hii. Hatuna budi kujisahihisha mapema kwani hakuna changamoto isiyo na madhara hasi.

Ezekiel Emanuel
0739828402
ezekielemanue97@gmail.com


[1] Msemo Keki ya nchi una maana “Mshahara”
Safi sana Kaka,One of the best article
 
1.0 Ikisiri
Nchi nyingi duniani zinakumbana na changamoto ya ajira kwa vijana. Hii ni kutokana na ongezeko la idadi ya wahitimu katika ngazi mbalimbali za elimu ingali hapajatengenezwa mazingira rafiki kwa ajili ya kuwaajiri au kujiajiri vijana hao. Pamoja na kuonekana madhara makubwa ulimwenguni kote, nchi za Afrika na Asia zimeonekana kukumbwa zaidi na madhara haya ikilinganishwa na nchi za Ulaya. Hivyo mjadala wa makala hii umekitwa zaidi katika nchi za Afrika na Asia, Tanzania ikichukuliwa kama sampuli kifani. Kwa hiyo, katika makala hii, mwandishi analenga kutoa maoni kuhusiana na namna ya kukabiliana na changamoto ya ajira kwa vijana kwa kuzingatia kwamba nchini Tanzania kama ilivyo kwa nchi zingine tatizo hili linazidi kukua na matokeo yake yanatarajiwa kuwa ni mabaya.​

1.2 Utangulizi
Mjadala wa makala hii unazingatia ukweli kwamba, elimu rasmi kwa nchi za Afrika na Asia ni matokeo ya mfumo wa elimu ya kikoloni. Itakumbukwa kwamba adhma ya elimu ya kikoloni ilikuwa ni kuandaa watendaji ambao wangerahisisha ufanyaji wa kazi za uzalishaji mali, shughuli za kiutawala pamoja na kuandaa vibaraka wa kisiasa. Elimu hii haikuwa na lengo la kumuandaa Mwafrika katika kujitegemea kiutawala, kifikra n.k. Hivyo, asilimia kubwa ya wahitimu waliona kuajiriwa ndiyo matokeo ya kupata elimu. Mawazo na tajriba zao zikawa katika mwegamo huo. Kwa hiyo, miongo na miongo mfumo huo ukaendelea mpaka miaka ya leo. Baada ya nchi za nyingi hususani za Afrika kupata uhuru, ziliendeleza mfumo uleule wa elimu huku zikijaribu angalau kuubadili mfumo wa elimu ya kikoloni ingawaje hazikufanikiwa kama ilivyotarajiwa. Mfano mzuri ni Elimu ya Ujamaa na Kujitegemea iliyoanzishwa na Mwl. J.K. Nyerere. Mfumo huu haukufanikiwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo shinikizo kutoka nchi za Magharibi. Hivyo, kwa asilimia kubwa bado tunaogelea katika dimbwi la elimu ya mkoloni ambayo inamuandaa kijana kuajiriwa na si kufikiri katika kutengeneza namna ya kujiajiri. Kwa kuzingatia usuli huu, makala hii inalenga sasa kutoa maoni ya namna ya kukabiliana na hii changamoto.​

2.0 Nini Kifanyike
Waandishi wengi wameandika kuwataka vijana wajiajiri na mapendekezo mengine. Sitarudia kilichosemwa na waandishi bali ninatofautiana nao kidogo kimtazamo kwa kuwa vijana wengi wanajitahidi kujiajiri lakini bado matarajio hayafikiwi na kila siku idadi ya watu wasio na ajira inaongezeka. Mwandishi wa makala hii anaona jambo linalofaa ni:​

2.1 Ajira zote Mpya Serikalini Ziwe za Awamu (Miaka Kumikumi)
Kutokana na sheria za Tanzania, asilimia kubwa ya waajiriwa serikalini wanapaswa kustaafu katika umri miaka 60. Yaani, iwapo mwajiriwa ataajiriwa akiwa na miaka 30 basi ana miaka 30 ya kula keki ya nchi[1] kisha kupatiwa mafao. Hii ni sawa na kusema kwamba, sheria inaruhusu katika miaka yote hii 30 nafasi hii kumilikiwa na mtu mmoja mpaka pale atakapohamishwa kituo, kufa au kufukuzwa kazi. Ni sawa na kusema vilevile kwamba, katika miaka hii 30 kama yupo mwenye sifa ya kuajiriwa atapaswa asubiri mpaka pale mtangulizi wake atakapofikia umri wa miaka 60, atakapokufa au kuhamishwa/ kufukuzwa kazi. Madhara ya sheria hii ni haya yafuatayo.

Kwanza, idadi kubwa ya watu wasio na ajira ilhali wana sifa za kuajiriwa inaongezeka kwa kasi. Hii inachagizwa vilevile na kutokuwapo kwa mikakati ya kuongeza nafasi za ajira ilhali idadi ya wahitimu wa vyuo vikuu inaongezeka kwa kiwango kikubwa kila mwaka. Tafiti za hivi karibuni zinaonesha jumla ya wahitimu zaidi ya laki moja huhitimu kila mwaka.

Pili, waajiriwa wengi wamekuwa wakiridhika na ajira wasiwaze namna ya kuongeza mapato yao nje na ajira. Kutokana na saikolojia kuwafariji waajiriwa serikalini kwamba wana muda mrefu katika ajira, kumefanya waajiriwa wengi waendelee kula keki ya nchi wasijihusishe na shughuli mbalimbali mathalani kilimo bora, ufugaji, biashara n.k ambazo zingekuwa na tija katika maisha yao nje na ajira. Jambo ambalo lingeweza kupunguza ukali wa maisha yao pamoja na wale wasio na ajira

Tatu, hali ya uchumi wa kudumaa. Neema ya kuwapo kwenye ajira mpaka ufikiapo miaka 60 inachangia kwa kiasi kikubwa kufanya uchumi wetu kudumaa. Hii ni kutokana na sababu kwamba mzunguko wa fedha haupo katika uzalishaji bali upo katika matumizi. Hakuna hofu ya mtetereko wa kiuchumi ambayo inawazwa na waajiriwa wengi. Wengi wanafanya matumizi yaliyo nje na bajeti wakijua kwamba mwisho wa mwezi kuna keki ya taifa. Ni rahiri vilevile kujiingiza katika madeni yasiyo na tija kutokana na tu na kuwapo kwa keki itakayotumika kulipa hayo madeni. Hali hii inadhorotesha uchumi wa nchi kwani matokeo ya mwisho kabisa yanamgusa yule asiye na ajira kutokana na mzunguko wa fedha kuwa mgumu kwake ilhali mwepesi kwa wenye keki ya taifa.

Hivyo, kutokana na hali hiyo iko haja ya kuangalia na kuafiki kupunguza miaka ya ajira na kuzifanya ziwe ni za awamu kila baada ya miaka kumi. Yaani iwapo mtu ataajiriwa leo, basi atambue kwamba ana miaka kumi ya kula keki ya taifa kisha ataachia nafasi hiyo kwa mtu mwingine ambaye naye atafanya kwa miaka kumi kisha awamu ya pili inamalizika kwa yule wa kwanza. Kwa hiyo, mwajiriwa serikalini atakuwa na jumla ya miaka 20 pekee ya kula keki ya taifa.

Hii itasaidia mwajiriwa kujiandaa kisaikolojia kwamba anao muda mchache wa kula keki ya nchi. Hivyo, kupitia mshahara wake atafikiri namna ya kujiongezea kipato kabla na baada ya ajira. Mzunguko wa fedha kitaifa utakua hatimaye kupoza makali ya ugumu wa maisha kwa watu wote kwa sababu uzalishaji mali utaongezeka. Kikubwa zaidi, ni kwamba tatizo la ongezeko la vijana wasio na ajira litapunguzwa mara mbili ya hali iliyopo sasa kwani kila baada ya miaka kumi walioko kwenye ajira watapisha wengine. Vivyo hivyo kwa awamu itakayofuata. Mbali na hayo yote mfumo wa namna hii utasaidia kuondoa sononeko la kisaikolojia miongoni mwa wahitimu wa vyuo kwani kwa kufanya hivi kutaleta angalau hali ya usawa katika kula keki ya nchi. Vilevile, bidii ya kujituma ns kuzalisha mali itaongezeka miongoni mwa waajiriwa kutokana na muda mchache walionao katika kuzitumia rasilimali fedha watakazokuwa wakilipwa serikalini.​

3.0 Hitimisho
Mbali na maoni haya, serikali pamoja na wadau inatupasa kuupitia upya mfumo wetu wa elimu kwani huo ndiyo chanzo cha changamoto hii. Hatuna budi kujisahihisha mapema kwani hakuna changamoto isiyo na madhara hasi.

Ezekiel Emanuel
0739828402
ezekielemanue97@gmail.com


[1] Msemo Keki ya nchi una maana “Mshahara”
Rushwa na wizi wa fedha utaongezeka kwasabu muajiriwa at a force maisha ili afanikiwe kabla ya miaka 10 afu pia ufanisi wa kazi utapungua mana lengo LA serikali halitatimia ndo mana hamna professor kijana wale wanaujuzi San hata wazungu pia wazee ni hazina ya teknolijia
 
1.0 Ikisiri
Nchi nyingi duniani zinakumbana na changamoto ya ajira kwa vijana. Hii ni kutokana na ongezeko la idadi ya wahitimu katika ngazi mbalimbali za elimu ingali hapajatengenezwa mazingira rafiki kwa ajili ya kuwaajiri au kujiajiri vijana hao. Pamoja na kuonekana madhara makubwa ulimwenguni kote, nchi za Afrika na Asia zimeonekana kukumbwa zaidi na madhara haya ikilinganishwa na nchi za Ulaya. Hivyo mjadala wa makala hii umekitwa zaidi katika nchi za Afrika na Asia, Tanzania ikichukuliwa kama sampuli kifani. Kwa hiyo, katika makala hii, mwandishi analenga kutoa maoni kuhusiana na namna ya kukabiliana na changamoto ya ajira kwa vijana kwa kuzingatia kwamba nchini Tanzania kama ilivyo kwa nchi zingine tatizo hili linazidi kukua na matokeo yake yanatarajiwa kuwa ni mabaya.​

1.2 Utangulizi
Mjadala wa makala hii unazingatia ukweli kwamba, elimu rasmi kwa nchi za Afrika na Asia ni matokeo ya mfumo wa elimu ya kikoloni. Itakumbukwa kwamba adhma ya elimu ya kikoloni ilikuwa ni kuandaa watendaji ambao wangerahisisha ufanyaji wa kazi za uzalishaji mali, shughuli za kiutawala pamoja na kuandaa vibaraka wa kisiasa. Elimu hii haikuwa na lengo la kumuandaa Mwafrika katika kujitegemea kiutawala, kifikra n.k. Hivyo, asilimia kubwa ya wahitimu waliona kuajiriwa ndiyo matokeo ya kupata elimu. Mawazo na tajriba zao zikawa katika mwegamo huo. Kwa hiyo, miongo na miongo mfumo huo ukaendelea mpaka miaka ya leo. Baada ya nchi za nyingi hususani za Afrika kupata uhuru, ziliendeleza mfumo uleule wa elimu huku zikijaribu angalau kuubadili mfumo wa elimu ya kikoloni ingawaje hazikufanikiwa kama ilivyotarajiwa. Mfano mzuri ni Elimu ya Ujamaa na Kujitegemea iliyoanzishwa na Mwl. J.K. Nyerere. Mfumo huu haukufanikiwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo shinikizo kutoka nchi za Magharibi. Hivyo, kwa asilimia kubwa bado tunaogelea katika dimbwi la elimu ya mkoloni ambayo inamuandaa kijana kuajiriwa na si kufikiri katika kutengeneza namna ya kujiajiri. Kwa kuzingatia usuli huu, makala hii inalenga sasa kutoa maoni ya namna ya kukabiliana na hii changamoto.​

2.0 Nini Kifanyike
Waandishi wengi wameandika kuwataka vijana wajiajiri na mapendekezo mengine. Sitarudia kilichosemwa na waandishi bali ninatofautiana nao kidogo kimtazamo kwa kuwa vijana wengi wanajitahidi kujiajiri lakini bado matarajio hayafikiwi na kila siku idadi ya watu wasio na ajira inaongezeka. Mwandishi wa makala hii anaona jambo linalofaa ni:​

2.1 Ajira zote Mpya Serikalini Ziwe za Awamu (Miaka Kumikumi)
Kutokana na sheria za Tanzania, asilimia kubwa ya waajiriwa serikalini wanapaswa kustaafu katika umri miaka 60. Yaani, iwapo mwajiriwa ataajiriwa akiwa na miaka 30 basi ana miaka 30 ya kula keki ya nchi[1] kisha kupatiwa mafao. Hii ni sawa na kusema kwamba, sheria inaruhusu katika miaka yote hii 30 nafasi hii kumilikiwa na mtu mmoja mpaka pale atakapohamishwa kituo, kufa au kufukuzwa kazi. Ni sawa na kusema vilevile kwamba, katika miaka hii 30 kama yupo mwenye sifa ya kuajiriwa atapaswa asubiri mpaka pale mtangulizi wake atakapofikia umri wa miaka 60, atakapokufa au kuhamishwa/ kufukuzwa kazi. Madhara ya sheria hii ni haya yafuatayo.

Kwanza, idadi kubwa ya watu wasio na ajira ilhali wana sifa za kuajiriwa inaongezeka kwa kasi. Hii inachagizwa vilevile na kutokuwapo kwa mikakati ya kuongeza nafasi za ajira ilhali idadi ya wahitimu wa vyuo vikuu inaongezeka kwa kiwango kikubwa kila mwaka. Tafiti za hivi karibuni zinaonesha jumla ya wahitimu zaidi ya laki moja huhitimu kila mwaka.

Pili, waajiriwa wengi wamekuwa wakiridhika na ajira wasiwaze namna ya kuongeza mapato yao nje na ajira. Kutokana na saikolojia kuwafariji waajiriwa serikalini kwamba wana muda mrefu katika ajira, kumefanya waajiriwa wengi waendelee kula keki ya nchi wasijihusishe na shughuli mbalimbali mathalani kilimo bora, ufugaji, biashara n.k ambazo zingekuwa na tija katika maisha yao nje na ajira. Jambo ambalo lingeweza kupunguza ukali wa maisha yao pamoja na wale wasio na ajira

Tatu, hali ya uchumi wa kudumaa. Neema ya kuwapo kwenye ajira mpaka ufikiapo miaka 60 inachangia kwa kiasi kikubwa kufanya uchumi wetu kudumaa. Hii ni kutokana na sababu kwamba mzunguko wa fedha haupo katika uzalishaji bali upo katika matumizi. Hakuna hofu ya mtetereko wa kiuchumi ambayo inawazwa na waajiriwa wengi. Wengi wanafanya matumizi yaliyo nje na bajeti wakijua kwamba mwisho wa mwezi kuna keki ya taifa. Ni rahiri vilevile kujiingiza katika madeni yasiyo na tija kutokana na tu na kuwapo kwa keki itakayotumika kulipa hayo madeni. Hali hii inadhorotesha uchumi wa nchi kwani matokeo ya mwisho kabisa yanamgusa yule asiye na ajira kutokana na mzunguko wa fedha kuwa mgumu kwake ilhali mwepesi kwa wenye keki ya taifa.

Hivyo, kutokana na hali hiyo iko haja ya kuangalia na kuafiki kupunguza miaka ya ajira na kuzifanya ziwe ni za awamu kila baada ya miaka kumi. Yaani iwapo mtu ataajiriwa leo, basi atambue kwamba ana miaka kumi ya kula keki ya taifa kisha ataachia nafasi hiyo kwa mtu mwingine ambaye naye atafanya kwa miaka kumi kisha awamu ya pili inamalizika kwa yule wa kwanza. Kwa hiyo, mwajiriwa serikalini atakuwa na jumla ya miaka 20 pekee ya kula keki ya taifa.

Hii itasaidia mwajiriwa kujiandaa kisaikolojia kwamba anao muda mchache wa kula keki ya nchi. Hivyo, kupitia mshahara wake atafikiri namna ya kujiongezea kipato kabla na baada ya ajira. Mzunguko wa fedha kitaifa utakua hatimaye kupoza makali ya ugumu wa maisha kwa watu wote kwa sababu uzalishaji mali utaongezeka. Kikubwa zaidi, ni kwamba tatizo la ongezeko la vijana wasio na ajira litapunguzwa mara mbili ya hali iliyopo sasa kwani kila baada ya miaka kumi walioko kwenye ajira watapisha wengine. Vivyo hivyo kwa awamu itakayofuata. Mbali na hayo yote mfumo wa namna hii utasaidia kuondoa sononeko la kisaikolojia miongoni mwa wahitimu wa vyuo kwani kwa kufanya hivi kutaleta angalau hali ya usawa katika kula keki ya nchi. Vilevile, bidii ya kujituma ns kuzalisha mali itaongezeka miongoni mwa waajiriwa kutokana na muda mchache walionao katika kuzitumia rasilimali fedha watakazokuwa wakilipwa serikalini.​

3.0 Hitimisho
Mbali na maoni haya, serikali pamoja na wadau inatupasa kuupitia upya mfumo wetu wa elimu kwani huo ndiyo chanzo cha changamoto hii. Hatuna budi kujisahihisha mapema kwani hakuna changamoto isiyo na madhara hasi.

Ezekiel Emanuel
0739828402
ezekielemanue97@gmail.com


[1] Msemo Keki ya nchi una maana “Mshahara”
Serikali kuusuka upya mfumo wa elimu itasaidia sana kupunguza wimbi kubwa la ukosefu wa ajira Nchini.
1.0 Ikisiri
Nchi nyingi duniani zinakumbana na changamoto ya ajira kwa vijana. Hii ni kutokana na ongezeko la idadi ya wahitimu katika ngazi mbalimbali za elimu ingali hapajatengenezwa mazingira rafiki kwa ajili ya kuwaajiri au kujiajiri vijana hao. Pamoja na kuonekana madhara makubwa ulimwenguni kote, nchi za Afrika na Asia zimeonekana kukumbwa zaidi na madhara haya ikilinganishwa na nchi za Ulaya. Hivyo mjadala wa makala hii umekitwa zaidi katika nchi za Afrika na Asia, Tanzania ikichukuliwa kama sampuli kifani. Kwa hiyo, katika makala hii, mwandishi analenga kutoa maoni kuhusiana na namna ya kukabiliana na changamoto ya ajira kwa vijana kwa kuzingatia kwamba nchini Tanzania kama ilivyo kwa nchi zingine tatizo hili linazidi kukua na matokeo yake yanatarajiwa kuwa ni mabaya.​

1.2 Utangulizi
Mjadala wa makala hii unazingatia ukweli kwamba, elimu rasmi kwa nchi za Afrika na Asia ni matokeo ya mfumo wa elimu ya kikoloni. Itakumbukwa kwamba adhma ya elimu ya kikoloni ilikuwa ni kuandaa watendaji ambao wangerahisisha ufanyaji wa kazi za uzalishaji mali, shughuli za kiutawala pamoja na kuandaa vibaraka wa kisiasa. Elimu hii haikuwa na lengo la kumuandaa Mwafrika katika kujitegemea kiutawala, kifikra n.k. Hivyo, asilimia kubwa ya wahitimu waliona kuajiriwa ndiyo matokeo ya kupata elimu. Mawazo na tajriba zao zikawa katika mwegamo huo. Kwa hiyo, miongo na miongo mfumo huo ukaendelea mpaka miaka ya leo. Baada ya nchi za nyingi hususani za Afrika kupata uhuru, ziliendeleza mfumo uleule wa elimu huku zikijaribu angalau kuubadili mfumo wa elimu ya kikoloni ingawaje hazikufanikiwa kama ilivyotarajiwa. Mfano mzuri ni Elimu ya Ujamaa na Kujitegemea iliyoanzishwa na Mwl. J.K. Nyerere. Mfumo huu haukufanikiwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo shinikizo kutoka nchi za Magharibi. Hivyo, kwa asilimia kubwa bado tunaogelea katika dimbwi la elimu ya mkoloni ambayo inamuandaa kijana kuajiriwa na si kufikiri katika kutengeneza namna ya kujiajiri. Kwa kuzingatia usuli huu, makala hii inalenga sasa kutoa maoni ya namna ya kukabiliana na hii changamoto.​

2.0 Nini Kifanyike
Waandishi wengi wameandika kuwataka vijana wajiajiri na mapendekezo mengine. Sitarudia kilichosemwa na waandishi bali ninatofautiana nao kidogo kimtazamo kwa kuwa vijana wengi wanajitahidi kujiajiri lakini bado matarajio hayafikiwi na kila siku idadi ya watu wasio na ajira inaongezeka. Mwandishi wa makala hii anaona jambo linalofaa ni:​

2.1 Ajira zote Mpya Serikalini Ziwe za Awamu (Miaka Kumikumi)
Kutokana na sheria za Tanzania, asilimia kubwa ya waajiriwa serikalini wanapaswa kustaafu katika umri miaka 60. Yaani, iwapo mwajiriwa ataajiriwa akiwa na miaka 30 basi ana miaka 30 ya kula keki ya nchi[1] kisha kupatiwa mafao. Hii ni sawa na kusema kwamba, sheria inaruhusu katika miaka yote hii 30 nafasi hii kumilikiwa na mtu mmoja mpaka pale atakapohamishwa kituo, kufa au kufukuzwa kazi. Ni sawa na kusema vilevile kwamba, katika miaka hii 30 kama yupo mwenye sifa ya kuajiriwa atapaswa asubiri mpaka pale mtangulizi wake atakapofikia umri wa miaka 60, atakapokufa au kuhamishwa/ kufukuzwa kazi. Madhara ya sheria hii ni haya yafuatayo.

Kwanza, idadi kubwa ya watu wasio na ajira ilhali wana sifa za kuajiriwa inaongezeka kwa kasi. Hii inachagizwa vilevile na kutokuwapo kwa mikakati ya kuongeza nafasi za ajira ilhali idadi ya wahitimu wa vyuo vikuu inaongezeka kwa kiwango kikubwa kila mwaka. Tafiti za hivi karibuni zinaonesha jumla ya wahitimu zaidi ya laki moja huhitimu kila mwaka.

Pili, waajiriwa wengi wamekuwa wakiridhika na ajira wasiwaze namna ya kuongeza mapato yao nje na ajira. Kutokana na saikolojia kuwafariji waajiriwa serikalini kwamba wana muda mrefu katika ajira, kumefanya waajiriwa wengi waendelee kula keki ya nchi wasijihusishe na shughuli mbalimbali mathalani kilimo bora, ufugaji, biashara n.k ambazo zingekuwa na tija katika maisha yao nje na ajira. Jambo ambalo lingeweza kupunguza ukali wa maisha yao pamoja na wale wasio na ajira

Tatu, hali ya uchumi wa kudumaa. Neema ya kuwapo kwenye ajira mpaka ufikiapo miaka 60 inachangia kwa kiasi kikubwa kufanya uchumi wetu kudumaa. Hii ni kutokana na sababu kwamba mzunguko wa fedha haupo katika uzalishaji bali upo katika matumizi. Hakuna hofu ya mtetereko wa kiuchumi ambayo inawazwa na waajiriwa wengi. Wengi wanafanya matumizi yaliyo nje na bajeti wakijua kwamba mwisho wa mwezi kuna keki ya taifa. Ni rahiri vilevile kujiingiza katika madeni yasiyo na tija kutokana na tu na kuwapo kwa keki itakayotumika kulipa hayo madeni. Hali hii inadhorotesha uchumi wa nchi kwani matokeo ya mwisho kabisa yanamgusa yule asiye na ajira kutokana na mzunguko wa fedha kuwa mgumu kwake ilhali mwepesi kwa wenye keki ya taifa.

Hivyo, kutokana na hali hiyo iko haja ya kuangalia na kuafiki kupunguza miaka ya ajira na kuzifanya ziwe ni za awamu kila baada ya miaka kumi. Yaani iwapo mtu ataajiriwa leo, basi atambue kwamba ana miaka kumi ya kula keki ya taifa kisha ataachia nafasi hiyo kwa mtu mwingine ambaye naye atafanya kwa miaka kumi kisha awamu ya pili inamalizika kwa yule wa kwanza. Kwa hiyo, mwajiriwa serikalini atakuwa na jumla ya miaka 20 pekee ya kula keki ya taifa.

Hii itasaidia mwajiriwa kujiandaa kisaikolojia kwamba anao muda mchache wa kula keki ya nchi. Hivyo, kupitia mshahara wake atafikiri namna ya kujiongezea kipato kabla na baada ya ajira. Mzunguko wa fedha kitaifa utakua hatimaye kupoza makali ya ugumu wa maisha kwa watu wote kwa sababu uzalishaji mali utaongezeka. Kikubwa zaidi, ni kwamba tatizo la ongezeko la vijana wasio na ajira litapunguzwa mara mbili ya hali iliyopo sasa kwani kila baada ya miaka kumi walioko kwenye ajira watapisha wengine. Vivyo hivyo kwa awamu itakayofuata. Mbali na hayo yote mfumo wa namna hii utasaidia kuondoa sononeko la kisaikolojia miongoni mwa wahitimu wa vyuo kwani kwa kufanya hivi kutaleta angalau hali ya usawa katika kula keki ya nchi. Vilevile, bidii ya kujituma ns kuzalisha mali itaongezeka miongoni mwa waajiriwa kutokana na muda mchache walionao katika kuzitumia rasilimali fedha watakazokuwa wakilipwa serikalini.​

3.0 Hitimisho
Mbali na maoni haya, serikali pamoja na wadau inatupasa kuupitia upya mfumo wetu wa elimu kwani huo ndiyo chanzo cha changamoto hii. Hatuna budi kujisahihisha mapema kwani hakuna changamoto isiyo na madhara hasi.

Ezekiel Emanuel
0739828402
ezekielemanue97@gmail.com


[1] Msemo Keki ya nchi una maana “Mshahara”

Production ya wasomi wanaoweza kujiamini kujiajiri KATIKA shughuli MBALIMBALI za kiuchumi ni ndogo sana.

Elimu yetu itupe maarifa (Skills) yatakayotuwezesha kujiajiri kwa fani MBALIMBALI na serikali itoe maeneo ya vipaumbele kwa vijana kujiajiri.
Kilimo
Ufugaji
Uvivu
Viwanda vya kati
Biashara za kimataifa
 
1.0 Ikisiri
Nchi nyingi duniani zinakumbana na changamoto ya ajira kwa vijana. Hii ni kutokana na ongezeko la idadi ya wahitimu katika ngazi mbalimbali za elimu ingali hapajatengenezwa mazingira rafiki kwa ajili ya kuwaajiri au kujiajiri vijana hao. Pamoja na kuonekana madhara makubwa ulimwenguni kote, nchi za Afrika na Asia zimeonekana kukumbwa zaidi na madhara haya ikilinganishwa na nchi za Ulaya. Hivyo mjadala wa makala hii umekitwa zaidi katika nchi za Afrika na Asia, Tanzania ikichukuliwa kama sampuli kifani. Kwa hiyo, katika makala hii, mwandishi analenga kutoa maoni kuhusiana na namna ya kukabiliana na changamoto ya ajira kwa vijana kwa kuzingatia kwamba nchini Tanzania kama ilivyo kwa nchi zingine tatizo hili linazidi kukua na matokeo yake yanatarajiwa kuwa ni mabaya.​

1.2 Utangulizi
Mjadala wa makala hii unazingatia ukweli kwamba, elimu rasmi kwa nchi za Afrika na Asia ni matokeo ya mfumo wa elimu ya kikoloni. Itakumbukwa kwamba adhma ya elimu ya kikoloni ilikuwa ni kuandaa watendaji ambao wangerahisisha ufanyaji wa kazi za uzalishaji mali, shughuli za kiutawala pamoja na kuandaa vibaraka wa kisiasa. Elimu hii haikuwa na lengo la kumuandaa Mwafrika katika kujitegemea kiutawala, kifikra n.k. Hivyo, asilimia kubwa ya wahitimu waliona kuajiriwa ndiyo matokeo ya kupata elimu. Mawazo na tajriba zao zikawa katika mwegamo huo. Kwa hiyo, miongo na miongo mfumo huo ukaendelea mpaka miaka ya leo. Baada ya nchi za nyingi hususani za Afrika kupata uhuru, ziliendeleza mfumo uleule wa elimu huku zikijaribu angalau kuubadili mfumo wa elimu ya kikoloni ingawaje hazikufanikiwa kama ilivyotarajiwa. Mfano mzuri ni Elimu ya Ujamaa na Kujitegemea iliyoanzishwa na Mwl. J.K. Nyerere. Mfumo huu haukufanikiwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo shinikizo kutoka nchi za Magharibi. Hivyo, kwa asilimia kubwa bado tunaogelea katika dimbwi la elimu ya mkoloni ambayo inamuandaa kijana kuajiriwa na si kufikiri katika kutengeneza namna ya kujiajiri. Kwa kuzingatia usuli huu, makala hii inalenga sasa kutoa maoni ya namna ya kukabiliana na hii changamoto.​

2.0 Nini Kifanyike
Waandishi wengi wameandika kuwataka vijana wajiajiri na mapendekezo mengine. Sitarudia kilichosemwa na waandishi bali ninatofautiana nao kidogo kimtazamo kwa kuwa vijana wengi wanajitahidi kujiajiri lakini bado matarajio hayafikiwi na kila siku idadi ya watu wasio na ajira inaongezeka. Mwandishi wa makala hii anaona jambo linalofaa ni:​

2.1 Ajira zote Mpya Serikalini Ziwe za Awamu (Miaka Kumikumi)
Kutokana na sheria za Tanzania, asilimia kubwa ya waajiriwa serikalini wanapaswa kustaafu katika umri miaka 60. Yaani, iwapo mwajiriwa ataajiriwa akiwa na miaka 30 basi ana miaka 30 ya kula keki ya nchi[1] kisha kupatiwa mafao. Hii ni sawa na kusema kwamba, sheria inaruhusu katika miaka yote hii 30 nafasi hii kumilikiwa na mtu mmoja mpaka pale atakapohamishwa kituo, kufa au kufukuzwa kazi. Ni sawa na kusema vilevile kwamba, katika miaka hii 30 kama yupo mwenye sifa ya kuajiriwa atapaswa asubiri mpaka pale mtangulizi wake atakapofikia umri wa miaka 60, atakapokufa au kuhamishwa/ kufukuzwa kazi. Madhara ya sheria hii ni haya yafuatayo.

Kwanza, idadi kubwa ya watu wasio na ajira ilhali wana sifa za kuajiriwa inaongezeka kwa kasi. Hii inachagizwa vilevile na kutokuwapo kwa mikakati ya kuongeza nafasi za ajira ilhali idadi ya wahitimu wa vyuo vikuu inaongezeka kwa kiwango kikubwa kila mwaka. Tafiti za hivi karibuni zinaonesha jumla ya wahitimu zaidi ya laki moja huhitimu kila mwaka.

Pili, waajiriwa wengi wamekuwa wakiridhika na ajira wasiwaze namna ya kuongeza mapato yao nje na ajira. Kutokana na saikolojia kuwafariji waajiriwa serikalini kwamba wana muda mrefu katika ajira, kumefanya waajiriwa wengi waendelee kula keki ya nchi wasijihusishe na shughuli mbalimbali mathalani kilimo bora, ufugaji, biashara n.k ambazo zingekuwa na tija katika maisha yao nje na ajira. Jambo ambalo lingeweza kupunguza ukali wa maisha yao pamoja na wale wasio na ajira

Tatu, hali ya uchumi wa kudumaa. Neema ya kuwapo kwenye ajira mpaka ufikiapo miaka 60 inachangia kwa kiasi kikubwa kufanya uchumi wetu kudumaa. Hii ni kutokana na sababu kwamba mzunguko wa fedha haupo katika uzalishaji bali upo katika matumizi. Hakuna hofu ya mtetereko wa kiuchumi ambayo inawazwa na waajiriwa wengi. Wengi wanafanya matumizi yaliyo nje na bajeti wakijua kwamba mwisho wa mwezi kuna keki ya taifa. Ni rahiri vilevile kujiingiza katika madeni yasiyo na tija kutokana na tu na kuwapo kwa keki itakayotumika kulipa hayo madeni. Hali hii inadhorotesha uchumi wa nchi kwani matokeo ya mwisho kabisa yanamgusa yule asiye na ajira kutokana na mzunguko wa fedha kuwa mgumu kwake ilhali mwepesi kwa wenye keki ya taifa.

Hivyo, kutokana na hali hiyo iko haja ya kuangalia na kuafiki kupunguza miaka ya ajira na kuzifanya ziwe ni za awamu kila baada ya miaka kumi. Yaani iwapo mtu ataajiriwa leo, basi atambue kwamba ana miaka kumi ya kula keki ya taifa kisha ataachia nafasi hiyo kwa mtu mwingine ambaye naye atafanya kwa miaka kumi kisha awamu ya pili inamalizika kwa yule wa kwanza. Kwa hiyo, mwajiriwa serikalini atakuwa na jumla ya miaka 20 pekee ya kula keki ya taifa.

Hii itasaidia mwajiriwa kujiandaa kisaikolojia kwamba anao muda mchache wa kula keki ya nchi. Hivyo, kupitia mshahara wake atafikiri namna ya kujiongezea kipato kabla na baada ya ajira. Mzunguko wa fedha kitaifa utakua hatimaye kupoza makali ya ugumu wa maisha kwa watu wote kwa sababu uzalishaji mali utaongezeka. Kikubwa zaidi, ni kwamba tatizo la ongezeko la vijana wasio na ajira litapunguzwa mara mbili ya hali iliyopo sasa kwani kila baada ya miaka kumi walioko kwenye ajira watapisha wengine. Vivyo hivyo kwa awamu itakayofuata. Mbali na hayo yote mfumo wa namna hii utasaidia kuondoa sononeko la kisaikolojia miongoni mwa wahitimu wa vyuo kwani kwa kufanya hivi kutaleta angalau hali ya usawa katika kula keki ya nchi. Vilevile, bidii ya kujituma ns kuzalisha mali itaongezeka miongoni mwa waajiriwa kutokana na muda mchache walionao katika kuzitumia rasilimali fedha watakazokuwa wakilipwa serikalini.​

3.0 Hitimisho
Mbali na maoni haya, serikali pamoja na wadau inatupasa kuupitia upya mfumo wetu wa elimu kwani huo ndiyo chanzo cha changamoto hii. Hatuna budi kujisahihisha mapema kwani hakuna changamoto isiyo na madhara hasi.

Ezekiel Emanuel
0739828402
ezekielemanue97@gmail.com


[1] Msemo Keki ya nchi una maana “Mshahara”
Alafu kam ushajua kwa nchi nyingi zin wasomi hawaja ajirw kaa ukujua muundo wa uongozi w serikali haubebi wananchi wote wajiriwe. Sas kumbe ajir ni maisha hayo unayotafuta kula siku kuw bora MTU mpambaj, biashar n.k SAS elimu ndo unatumia ivo
 
1.0 Ikisiri
Nchi nyingi duniani zinakumbana na changamoto ya ajira kwa vijana. Hii ni kutokana na ongezeko la idadi ya wahitimu katika ngazi mbalimbali za elimu ingali hapajatengenezwa mazingira rafiki kwa ajili ya kuwaajiri au kujiajiri vijana hao. Pamoja na kuonekana madhara makubwa ulimwenguni kote, nchi za Afrika na Asia zimeonekana kukumbwa zaidi na madhara haya ikilinganishwa na nchi za Ulaya. Hivyo mjadala wa makala hii umekitwa zaidi katika nchi za Afrika na Asia, Tanzania ikichukuliwa kama sampuli kifani. Kwa hiyo, katika makala hii, mwandishi analenga kutoa maoni kuhusiana na namna ya kukabiliana na changamoto ya ajira kwa vijana kwa kuzingatia kwamba nchini Tanzania kama ilivyo kwa nchi zingine tatizo hili linazidi kukua na matokeo yake yanatarajiwa kuwa ni mabaya.​

1.2 Utangulizi
Mjadala wa makala hii unazingatia ukweli kwamba, elimu rasmi kwa nchi za Afrika na Asia ni matokeo ya mfumo wa elimu ya kikoloni. Itakumbukwa kwamba adhma ya elimu ya kikoloni ilikuwa ni kuandaa watendaji ambao wangerahisisha ufanyaji wa kazi za uzalishaji mali, shughuli za kiutawala pamoja na kuandaa vibaraka wa kisiasa. Elimu hii haikuwa na lengo la kumuandaa Mwafrika katika kujitegemea kiutawala, kifikra n.k. Hivyo, asilimia kubwa ya wahitimu waliona kuajiriwa ndiyo matokeo ya kupata elimu. Mawazo na tajriba zao zikawa katika mwegamo huo. Kwa hiyo, miongo na miongo mfumo huo ukaendelea mpaka miaka ya leo. Baada ya nchi za nyingi hususani za Afrika kupata uhuru, ziliendeleza mfumo uleule wa elimu huku zikijaribu angalau kuubadili mfumo wa elimu ya kikoloni ingawaje hazikufanikiwa kama ilivyotarajiwa. Mfano mzuri ni Elimu ya Ujamaa na Kujitegemea iliyoanzishwa na Mwl. J.K. Nyerere. Mfumo huu haukufanikiwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo shinikizo kutoka nchi za Magharibi. Hivyo, kwa asilimia kubwa bado tunaogelea katika dimbwi la elimu ya mkoloni ambayo inamuandaa kijana kuajiriwa na si kufikiri katika kutengeneza namna ya kujiajiri. Kwa kuzingatia usuli huu, makala hii inalenga sasa kutoa maoni ya namna ya kukabiliana na hii changamoto.​

2.0 Nini Kifanyike
Waandishi wengi wameandika kuwataka vijana wajiajiri na mapendekezo mengine. Sitarudia kilichosemwa na waandishi bali ninatofautiana nao kidogo kimtazamo kwa kuwa vijana wengi wanajitahidi kujiajiri lakini bado matarajio hayafikiwi na kila siku idadi ya watu wasio na ajira inaongezeka. Mwandishi wa makala hii anaona jambo linalofaa ni:​

2.1 Ajira zote Mpya Serikalini Ziwe za Awamu (Miaka Kumikumi)
Kutokana na sheria za Tanzania, asilimia kubwa ya waajiriwa serikalini wanapaswa kustaafu katika umri miaka 60. Yaani, iwapo mwajiriwa ataajiriwa akiwa na miaka 30 basi ana miaka 30 ya kula keki ya nchi[1] kisha kupatiwa mafao. Hii ni sawa na kusema kwamba, sheria inaruhusu katika miaka yote hii 30 nafasi hii kumilikiwa na mtu mmoja mpaka pale atakapohamishwa kituo, kufa au kufukuzwa kazi. Ni sawa na kusema vilevile kwamba, katika miaka hii 30 kama yupo mwenye sifa ya kuajiriwa atapaswa asubiri mpaka pale mtangulizi wake atakapofikia umri wa miaka 60, atakapokufa au kuhamishwa/ kufukuzwa kazi. Madhara ya sheria hii ni haya yafuatayo.

Kwanza, idadi kubwa ya watu wasio na ajira ilhali wana sifa za kuajiriwa inaongezeka kwa kasi. Hii inachagizwa vilevile na kutokuwapo kwa mikakati ya kuongeza nafasi za ajira ilhali idadi ya wahitimu wa vyuo vikuu inaongezeka kwa kiwango kikubwa kila mwaka. Tafiti za hivi karibuni zinaonesha jumla ya wahitimu zaidi ya laki moja huhitimu kila mwaka.

Pili, waajiriwa wengi wamekuwa wakiridhika na ajira wasiwaze namna ya kuongeza mapato yao nje na ajira. Kutokana na saikolojia kuwafariji waajiriwa serikalini kwamba wana muda mrefu katika ajira, kumefanya waajiriwa wengi waendelee kula keki ya nchi wasijihusishe na shughuli mbalimbali mathalani kilimo bora, ufugaji, biashara n.k ambazo zingekuwa na tija katika maisha yao nje na ajira. Jambo ambalo lingeweza kupunguza ukali wa maisha yao pamoja na wale wasio na ajira

Tatu, hali ya uchumi wa kudumaa. Neema ya kuwapo kwenye ajira mpaka ufikiapo miaka 60 inachangia kwa kiasi kikubwa kufanya uchumi wetu kudumaa. Hii ni kutokana na sababu kwamba mzunguko wa fedha haupo katika uzalishaji bali upo katika matumizi. Hakuna hofu ya mtetereko wa kiuchumi ambayo inawazwa na waajiriwa wengi. Wengi wanafanya matumizi yaliyo nje na bajeti wakijua kwamba mwisho wa mwezi kuna keki ya taifa. Ni rahiri vilevile kujiingiza katika madeni yasiyo na tija kutokana na tu na kuwapo kwa keki itakayotumika kulipa hayo madeni. Hali hii inadhorotesha uchumi wa nchi kwani matokeo ya mwisho kabisa yanamgusa yule asiye na ajira kutokana na mzunguko wa fedha kuwa mgumu kwake ilhali mwepesi kwa wenye keki ya taifa.

Hivyo, kutokana na hali hiyo iko haja ya kuangalia na kuafiki kupunguza miaka ya ajira na kuzifanya ziwe ni za awamu kila baada ya miaka kumi. Yaani iwapo mtu ataajiriwa leo, basi atambue kwamba ana miaka kumi ya kula keki ya taifa kisha ataachia nafasi hiyo kwa mtu mwingine ambaye naye atafanya kwa miaka kumi kisha awamu ya pili inamalizika kwa yule wa kwanza. Kwa hiyo, mwajiriwa serikalini atakuwa na jumla ya miaka 20 pekee ya kula keki ya taifa.

Hii itasaidia mwajiriwa kujiandaa kisaikolojia kwamba anao muda mchache wa kula keki ya nchi. Hivyo, kupitia mshahara wake atafikiri namna ya kujiongezea kipato kabla na baada ya ajira. Mzunguko wa fedha kitaifa utakua hatimaye kupoza makali ya ugumu wa maisha kwa watu wote kwa sababu uzalishaji mali utaongezeka. Kikubwa zaidi, ni kwamba tatizo la ongezeko la vijana wasio na ajira litapunguzwa mara mbili ya hali iliyopo sasa kwani kila baada ya miaka kumi walioko kwenye ajira watapisha wengine. Vivyo hivyo kwa awamu itakayofuata. Mbali na hayo yote mfumo wa namna hii utasaidia kuondoa sononeko la kisaikolojia miongoni mwa wahitimu wa vyuo kwani kwa kufanya hivi kutaleta angalau hali ya usawa katika kula keki ya nchi. Vilevile, bidii ya kujituma ns kuzalisha mali itaongezeka miongoni mwa waajiriwa kutokana na muda mchache walionao katika kuzitumia rasilimali fedha watakazokuwa wakilipwa serikalini.​

3.0 Hitimisho
Mbali na maoni haya, serikali pamoja na wadau inatupasa kuupitia upya mfumo wetu wa elimu kwani huo ndiyo chanzo cha changamoto hii. Hatuna budi kujisahihisha mapema kwani hakuna changamoto isiyo na madhara hasi.

Ezekiel Emanuel
0739828402
ezekielemanue97@gmail.com


[1] Msemo Keki ya nchi una maana “Mshahara”
Very nice article. Issue iliyopo ni kuwafanya watawala wakuelewe na wafanyie kazi.
 
Unapowapumzisha wengine baada ya awamu yao ya miaka kumi kutimia si na wao wanakuwa hawana ajira kwa kipindi hicho?

Nadhani nadharia ya keki ya taifa imetumika vibaya hapa. Hivi mshahara wa laki nne na ushee kwa mwezi ndo uite keki ya taifa?

Keki ya taifa nijuavyo mimi ni kwa wale wanaopata mishahara na marupurupu mikubwa. Kwa Bongo pengine waliopo kwenye nafasi za kuteuliwa pamoja na wabunge ndo naweza kuwaweka katika kundi la wala keki ya taifa.
Ulichokisema ni kweli lakini ukweli huo unapingana na mtazamo na msimamo wa makala hii. Hoja inayosisitizwa katika makala hii ni kwamba, ajira za awamu kwa sababu zifuatazo.

Kwanza, idadi ya wasio na ajira inaongezeka ilhali wana sifa za kuajiriwa. Swali la kujiuliza hatima yao itakuwa ipi?
Pili, kupunguza ukali wa ugumu wa maisha kwa kundi kubwa la watu. Hapa ninamaanisha iwapo atapata nafasi ya kuajiriwa na akajua kwamba ana muda mchache ataishi kwa tahadhari kadri awezavyo. Hii itasaidia kuwawazisha pengine kuanzisha shughuli nyingine kwa kujiandaa dhidi ya miaka kumi ya ukame. Dhen, baada ya miaka 10 mingine atarudi kumalizia awamu yake.

Suala la ufisadi silipongi kwani hata sasa upo. Hoja kuu ni kuleta relief kubwa kwa watu wengi
 
Rushwa na wizi wa fedha utaongezeka kwasabu muajiriwa at a force maisha ili afanikiwe kabla ya miaka 10 afu pia ufanisi wa kazi utapungua mana lengo LA serikali halitatimia ndo mana hamna professor kijana wale wanaujuzi San hata wazungu pia wazee ni hazina ya teknolijia
Wizi na rushwa hata sasa vimekithiri, je tutasemaje hapo. Ninafikiri hilo ni janga ambalo lipo na pengine lipo kwa sababu watu wanatumia nguvu nyingi kwenye kuzitafuta hizo ajira au sababu nyingine. Ajira zikiwa ni za muda mfupimfupi inasaidia kuleta matumaini na relief ya maisha kwa wengi. Ninafikiri pia inaweza kupunguza wizi na rushwa
 
1.0 Ikisiri
Nchi nyingi duniani zinakumbana na changamoto ya ajira kwa vijana. Hii ni kutokana na ongezeko la idadi ya wahitimu katika ngazi mbalimbali za elimu ingali hapajatengenezwa mazingira rafiki kwa ajili ya kuwaajiri au kujiajiri vijana hao. Pamoja na kuonekana madhara makubwa ulimwenguni kote, nchi za Afrika na Asia zimeonekana kukumbwa zaidi na madhara haya ikilinganishwa na nchi za Ulaya. Hivyo mjadala wa makala hii umekitwa zaidi katika nchi za Afrika na Asia, Tanzania ikichukuliwa kama sampuli kifani. Kwa hiyo, katika makala hii, mwandishi analenga kutoa maoni kuhusiana na namna ya kukabiliana na changamoto ya ajira kwa vijana kwa kuzingatia kwamba nchini Tanzania kama ilivyo kwa nchi zingine tatizo hili linazidi kukua na matokeo yake yanatarajiwa kuwa ni mabaya.​

1.2 Utangulizi
Mjadala wa makala hii unazingatia ukweli kwamba, elimu rasmi kwa nchi za Afrika na Asia ni matokeo ya mfumo wa elimu ya kikoloni. Itakumbukwa kwamba adhma ya elimu ya kikoloni ilikuwa ni kuandaa watendaji ambao wangerahisisha ufanyaji wa kazi za uzalishaji mali, shughuli za kiutawala pamoja na kuandaa vibaraka wa kisiasa. Elimu hii haikuwa na lengo la kumuandaa Mwafrika katika kujitegemea kiutawala, kifikra n.k. Hivyo, asilimia kubwa ya wahitimu waliona kuajiriwa ndiyo matokeo ya kupata elimu. Mawazo na tajriba zao zikawa katika mwegamo huo. Kwa hiyo, miongo na miongo mfumo huo ukaendelea mpaka miaka ya leo. Baada ya nchi za nyingi hususani za Afrika kupata uhuru, ziliendeleza mfumo uleule wa elimu huku zikijaribu angalau kuubadili mfumo wa elimu ya kikoloni ingawaje hazikufanikiwa kama ilivyotarajiwa. Mfano mzuri ni Elimu ya Ujamaa na Kujitegemea iliyoanzishwa na Mwl. J.K. Nyerere. Mfumo huu haukufanikiwa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo shinikizo kutoka nchi za Magharibi. Hivyo, kwa asilimia kubwa bado tunaogelea katika dimbwi la elimu ya mkoloni ambayo inamuandaa kijana kuajiriwa na si kufikiri katika kutengeneza namna ya kujiajiri. Kwa kuzingatia usuli huu, makala hii inalenga sasa kutoa maoni ya namna ya kukabiliana na hii changamoto.​

2.0 Nini Kifanyike
Waandishi wengi wameandika kuwataka vijana wajiajiri na mapendekezo mengine. Sitarudia kilichosemwa na waandishi bali ninatofautiana nao kidogo kimtazamo kwa kuwa vijana wengi wanajitahidi kujiajiri lakini bado matarajio hayafikiwi na kila siku idadi ya watu wasio na ajira inaongezeka. Mwandishi wa makala hii anaona jambo linalofaa ni:​

2.1 Ajira zote Mpya Serikalini Ziwe za Awamu (Miaka Kumikumi)
Kutokana na sheria za Tanzania, asilimia kubwa ya waajiriwa serikalini wanapaswa kustaafu katika umri miaka 60. Yaani, iwapo mwajiriwa ataajiriwa akiwa na miaka 30 basi ana miaka 30 ya kula keki ya nchi[1] kisha kupatiwa mafao. Hii ni sawa na kusema kwamba, sheria inaruhusu katika miaka yote hii 30 nafasi hii kumilikiwa na mtu mmoja mpaka pale atakapohamishwa kituo, kufa au kufukuzwa kazi. Ni sawa na kusema vilevile kwamba, katika miaka hii 30 kama yupo mwenye sifa ya kuajiriwa atapaswa asubiri mpaka pale mtangulizi wake atakapofikia umri wa miaka 60, atakapokufa au kuhamishwa/ kufukuzwa kazi. Madhara ya sheria hii ni haya yafuatayo.

Kwanza, idadi kubwa ya watu wasio na ajira ilhali wana sifa za kuajiriwa inaongezeka kwa kasi. Hii inachagizwa vilevile na kutokuwapo kwa mikakati ya kuongeza nafasi za ajira ilhali idadi ya wahitimu wa vyuo vikuu inaongezeka kwa kiwango kikubwa kila mwaka. Tafiti za hivi karibuni zinaonesha jumla ya wahitimu zaidi ya laki moja huhitimu kila mwaka.

Pili, waajiriwa wengi wamekuwa wakiridhika na ajira wasiwaze namna ya kuongeza mapato yao nje na ajira. Kutokana na saikolojia kuwafariji waajiriwa serikalini kwamba wana muda mrefu katika ajira, kumefanya waajiriwa wengi waendelee kula keki ya nchi wasijihusishe na shughuli mbalimbali mathalani kilimo bora, ufugaji, biashara n.k ambazo zingekuwa na tija katika maisha yao nje na ajira. Jambo ambalo lingeweza kupunguza ukali wa maisha yao pamoja na wale wasio na ajira

Tatu, hali ya uchumi wa kudumaa. Neema ya kuwapo kwenye ajira mpaka ufikiapo miaka 60 inachangia kwa kiasi kikubwa kufanya uchumi wetu kudumaa. Hii ni kutokana na sababu kwamba mzunguko wa fedha haupo katika uzalishaji bali upo katika matumizi. Hakuna hofu ya mtetereko wa kiuchumi ambayo inawazwa na waajiriwa wengi. Wengi wanafanya matumizi yaliyo nje na bajeti wakijua kwamba mwisho wa mwezi kuna keki ya taifa. Ni rahiri vilevile kujiingiza katika madeni yasiyo na tija kutokana na tu na kuwapo kwa keki itakayotumika kulipa hayo madeni. Hali hii inadhorotesha uchumi wa nchi kwani matokeo ya mwisho kabisa yanamgusa yule asiye na ajira kutokana na mzunguko wa fedha kuwa mgumu kwake ilhali mwepesi kwa wenye keki ya taifa.

Hivyo, kutokana na hali hiyo iko haja ya kuangalia na kuafiki kupunguza miaka ya ajira na kuzifanya ziwe ni za awamu kila baada ya miaka kumi. Yaani iwapo mtu ataajiriwa leo, basi atambue kwamba ana miaka kumi ya kula keki ya taifa kisha ataachia nafasi hiyo kwa mtu mwingine ambaye naye atafanya kwa miaka kumi kisha awamu ya pili inamalizika kwa yule wa kwanza. Kwa hiyo, mwajiriwa serikalini atakuwa na jumla ya miaka 20 pekee ya kula keki ya taifa.

Hii itasaidia mwajiriwa kujiandaa kisaikolojia kwamba anao muda mchache wa kula keki ya nchi. Hivyo, kupitia mshahara wake atafikiri namna ya kujiongezea kipato kabla na baada ya ajira. Mzunguko wa fedha kitaifa utakua hatimaye kupoza makali ya ugumu wa maisha kwa watu wote kwa sababu uzalishaji mali utaongezeka. Kikubwa zaidi, ni kwamba tatizo la ongezeko la vijana wasio na ajira litapunguzwa mara mbili ya hali iliyopo sasa kwani kila baada ya miaka kumi walioko kwenye ajira watapisha wengine. Vivyo hivyo kwa awamu itakayofuata. Mbali na hayo yote mfumo wa namna hii utasaidia kuondoa sononeko la kisaikolojia miongoni mwa wahitimu wa vyuo kwani kwa kufanya hivi kutaleta angalau hali ya usawa katika kula keki ya nchi. Vilevile, bidii ya kujituma ns kuzalisha mali itaongezeka miongoni mwa waajiriwa kutokana na muda mchache walionao katika kuzitumia rasilimali fedha watakazokuwa wakilipwa serikalini.​

3.0 Hitimisho
Mbali na maoni haya, serikali pamoja na wadau inatupasa kuupitia upya mfumo wetu wa elimu kwani huo ndiyo chanzo cha changamoto hii. Hatuna budi kujisahihisha mapema kwani hakuna changamoto isiyo na madhara hasi.

Ezekiel Emanuel
0739828402
ezekielemanue97@gmail.com


Hongeraa Sana hii idea niliandika chapisho kabla yako Ila kwa sababu ya kutokidhi chapisho Hilo halikuruhusiwa nimefurahi kuona tumewa kitu kimoja
 
Back
Top Bottom