Ajira ngumu

Joined
Nov 16, 2020
Posts
54
Reaction score
84
Kwa masikitiko makubwa kwa vijana wanaosoma na wazazi kusomesha.

Jana nimeshuhudia wimbi kubwa la Majobless wa Leo na baadae. Ni baada ya kuhudhuria usaili wa kazi za kukusanya taarifa za makazi na postikodi.

Nafasi zilikuwa 415 tu kwa Manispaa ya Morogoro ila idadi ya waombaji ni 5500 hivi.

Sasa kwa uwiano wa waombaji na nafasi hata nusu haijafika, ni hatari mno.

Ushauri kwa vijana Wenzangu. Ni vyema kuondoa mawazo ya kuajiliwa na kupandikiza mawazo ya kujiajiri kwani kwa kutegemea ajira na hali iliyokuwepo unaweza ukakata tamaa ya maisha.

Kwenye elimu, Wazazi ni vyema ukamwambia mwanao mapema juu ya hatari ya kusoma elimu isiyo kuwa na ufundi ndani yake mfano ualimu na kazi nyingine.

Pia ni vizuri kuhamasisha watoto wetu kupenda shughuli halisi za jamii zetu kama kilimo na ufundi licha ya ukweli kwamba huko nako kunachangamoto lakini hutashindwa kuishi kupitia shughuli hizo. Ni Morogoro Manispaa me nimekosa kabisa imani ya kupata kazi yenyewe๐Ÿ™„๐Ÿ™„๐Ÿ™„
 
Wengi wanavishughuli vyao Kama wewe huna Ni wewe. Watu wanazitamani hizo pesa za faster faster kulingana na vijishughuli vyao kuingiza pesa yachini.

Kuna maafisa kilimo na mifugo, walimu, boda boda, mafundi seremala, wafugahi, wakulima, part-timers n.k
 
Ni kweli uelezalo.Lakini,ni lini nafasi za ajira(kuajiriwa hasa na serikali)zilitosha au hata kubaki wazi?Halafu,nimeshuhudia mara nyingi tu,siyo wote waendao kwenye kutahiniwa wanakidhi sifa zitakiwazo.Wengine huenda kama matembezi na kujaribu/kuvizia bahati Ikitokea.Kuwa makini nao.
 
Labda bahati hiyo๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ maana namba niliyoikuta kule kubwa mno mkuu
 
Watu 5000 na ajira 415 ninkukaribisha rushwa tu bora wangechagua tu kule kule bila kuitisha watu kwenye interview... Usumbufu
Walishachagua ila kanuni zinawabana. Ni lazima mchakato na taratibu zizingatiwe ili kuondoa kelele. Huku kwetu Kuna kiongozi wa CCM alikua anakusanya barua za maombi na vyeti wiki moja kabla ya tangazo kutoka.

Tangazo lilipooka ndo nikajua mchakato umekamilika na Kama bado basi nafasi wazi hata 100 hazifiki katika nafasi 400 zilizotangazwa.
 
Watu 5000 na ajira 415 ninkukaribisha rushwa tu bora wangechagua tu kule kule bila kuitisha watu kwenye interview... Usumbufu
Watu hawana shukrani.Wakichujwa kabla watatoa malalamiko ya rushwa.Waache waende wote ili hata wageni wajifunze kutahiniwa huwaje!
 
Hapo kweli maan nilisikia wanampitisha
Mnalipwa kiasi gani mpka mrundikane hivyo?
Siku 30000 mkuu.... Kwa siku kumi hapo..300000 ila ukiipata bila kupitia kwa... Basi wew maisha umeyapatia tayari yaani mungu kakufungulia njia๐Ÿ˜‚
 
Nikurekebishe kidogo.

Utaratibu wa kuajiri madaktari na walimu mara wamalizapo chuo ulipositishwa hata kusomea ualimu imekua ni mzigo mpya.

Kwahiyo unaposema kozi zenye ufundi mfano ualimu jua kuna walimu hawana mbele wala nyuma tangu 2015.
 
Hapo kweli maan nilisikia wanampitisha

Siku 30000 mkuu.... Kwa siku kumi hapo..300000 ila ukiipata bila kupitia kwa... Basi wew maisha umeyapatia tayari yaani mungu kakufungulia njia๐Ÿ˜‚
๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„ Dah kweli mambo magumu
 
Nikurekebishe kidogo.

Utaratibu wa kuajiri madaktari na walimu mara wamalizapo chuo ulipositishwa hata kusomea ualimu imekua ni mzigo mpya.

Kwahiyo unaposema kozi zenye ufundi mfano ualimu jua kuna walimu hawana mbele wala nyuma tangu 2015.
Nimesema zisizo na ufundi kama mwalimu.. Yaani usipoajiliwa ndio badi tena.. Tuanapaswa kutafuta fani nje ya kazi hiyo
 
Tangazo lilzuia Watumishi kuomba cha ajabu nikakuta mstaari wao๐Ÿ˜๐Ÿ˜ Hatari mno
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ