Ajira ngumu

Ajira ngumu

Sawa mkuu.. Lakin duuh kama hali ndo ilivyo nikisikia hata sitaenda tena
Kutoenda kwenye usaili kwa hiyari ni sawa lakini siyo sahihi sana.Haina tofauti na kuzira kupiga kura ya kuchagua viongozi kwa sababu hukupendezwa na yaliyopita.Au,kugoma kuishi katika ndoa(kuwa katika mahusiano ya mahaba)kwa sababu tu kuna mtu alikuudhi siku zilizopita.Yote hayo ni kujipoka haki halali uliyoishika mkononi.
 
Kwa masikitiko makubwa kwa vijana wanaosoma na wazazi kusomesha.

Jana nimeshuhudia wimbi kubwa la Majobless wa Leo na baadae. Ni baada ya kuhudhuria usaili wa kazi za kukusanya taarifa za makazi na postikodi.

Nafasi zilikuwa 415 tu kwa Manispaa ya Morogoro ila idadi ya waombaji ni 5500 hivi.

Sasa kwa uwiano wa waombaji na nafasi hata nusu haijafika, ni hatari mno.

Ushauri kwa vijana Wenzangu. Ni vyema kuondoa mawazo ya kuajiliwa na kupandikiza mawazo ya kujiajiri kwani kwa kutegemea ajira na hali iliyokuwepo unaweza ukakata tamaa ya maisha.

Kwenye elimu, Wazazi ni vyema ukamwambia mwanao mapema juu ya hatari ya kusoma elimu isiyo kuwa na ufundi ndani yake mfano ualimu na kazi nyingine.

Pia ni vizuri kuhamasisha watoto wetu kupenda shughuli halisi za jamii zetu kama kilimo na ufundi licha ya ukweli kwamba huko nako kunachangamoto lakini hutashindwa kuishi kupitia shughuli hizo. Ni Morogoro Manispaa me nimekosa kabisa imani ya kupata kazi yenyewe🙄🙄🙄
Tutajiajiri vipi na huku hatuna mtaji, mbaya Zaidi serikali haimtambui mwenye kipaji.

~kala Jeremiah
 
Nipo Dodoma hapa. Tangu ju?I naona vimwana wengi mno na makaka wamejaa nyumba za wageni kusubiri ajira ya tra sijusi usaili j3? Yaani wadada aanaruhusiwa kulala hata 3 Lodge na wakaka wanazuiliwa. Noma sana. Sijui tusomeshe nini wanetu
 
Nenda mtaani Kama utakuta mtu amekaa idle tu. Sema Vijana tunahisi ajira ndo kazi rasmi pekee. Yaani mtu akiajiriwa alipwe laki 3 anaona ndo mwisho wa matatizo kuliko kujiajiri apate zaidi.

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Kujiajiri kuna liability na kupata zaidi maana yake ni kujiongeza zaidi. Kumbuka kwenye kujiajiri jua na mvua vyote ni halali yako😅!

Ukiambiwa utafute 1.5M kwa mwezi kwa kujiajiri ukiwa kama Jobless ambaye huna hata tsh.100 ya mtaji unafikiri itakuchukua muda kiasi gani? Siku hufungui biashara jua sikuhio huingizi hata tsh.100

Ila kuajiriwa jua na mvua ni juu ya boss wako wewe alimradi umesaini siku jua utapata 1.5M yako bila kelele kila ifikapo kati ya tarehe 27-30!

Ajira tamu mkuu hasa ikiwa na maslahi mazuri. Its less stressing kama biashara kwa mtazamo wangu. Biashara inakuwa relaxed ukiwa na mtaji mkubwa yani ndio utafaidi biashara ila kwa hii mitaji yetu ya laki 1 na nusu tutaishia kuuza pweza barabarani tu mwisho utimuliwe na migambo wavunje meza.
 
Kujiajiri kuna liability na kupata zaidi maana yake ni kujiongeza zaidi. Kumbuka kwenye kujiajiri jua na mvua vyote ni halali yako[emoji28]!

Ukiambiwa utafute 1.5M kwa mwezi kwa kujiajiri ukiwa kama Jobless ambaye huna hata tsh.100 ya mtaji unafikiri itakuchukua muda kiasi gani? Siku hufungui biashara jua sikuhio huingizi hata tsh.100

Ila kuajiriwa jua na mvua ni juu ya boss wako wewe alimradi umesaini siku jua utapata 1.5M yako bila kelele kila ifikapo kati ya tarehe 27-30!

Ajira tamu mkuu hasa ikiwa na maslahi mazuri. Its less stressing kama biashara kwa mtazamo wangu. Biashara inakuwa relaxed ukiwa na mtaji mkubwa yani ndio utafaidi biashara ila kwa hii mitaji yetu ya laki 1 na nusu tutaishia kuuza pweza barabarani tu mwisho utimuliwe na migambo wavunje meza.
Bora waishie meza kuliko wavunje na miguu kabisa

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Tutajiajiri vipi na huku hatuna mtaji, mbaya Zaidi serikali haimtambui mwenye kipaji.

~kala Jeremiah
Anaongelea kuganga njaa sio kujiajiri huyo😅

Kujiajiri ina involve either Trading, Entrepreneruship ama Industrialization. Kwa scale ya mtaji ili ufanye kitu chenye tija ni pesa ndefu lazma uwekeze. Kwa Trading maybe 30M walau unaweza kutengeneza mazingira kuanza ku realize faida za kueleweka kila siku na biashara ikakuwa kwa kasi.
 
Back
Top Bottom